Nina swali kwenu Wachungaji wenye ujuzi na Biblia (Imani)

Nina swali kwenu Wachungaji wenye ujuzi na Biblia (Imani)

kidonto

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2014
Posts
1,961
Reaction score
2,918
Shalom!
Nataka tu kujifunza na kuongeza Imani yangu!

Nimekua nikishuhudia Watu wengi wakifunguliwa Makanisani kwa Macho yangu!

Nimeshuhudia Baadhi ya watu wakifunguliwa kwa namna tofauti, katika kisa kimoja, mwanaume wa Makamo alikua Mgonjwa akiamini Kalogwa, alihangaika kutafuta Tiba toka kwa Mganga mmoja mpaka mwingine, Ndugu za yule Mgonjwa walikua hawaamini Nguvu ya Yesu Kristo katika Uponyaji, ila mmoja baada ya mwingine miongoni mwa Wanafamilia wakaanza kupokea Uponyaji, kwa mujibu wa Ushuhuda wa Ndugu na Mgonjwa, hata siku hiyo Jumapili wao wanajiandaa kwenda Kanisani, Ndugu yao anajiandaa kwenda kwa Mganga!

Ndugu wakamkamata kwa Nguvu na kwenda nae Kanisani, baada ya maombi akapona, sasa wakati anatoa Ushuhuda anasema, Nanukuu..

"Sikua hata na Mpango wa kuja hapa, nilikua nataka kwenda kwa Mganga coz alinambia nirudi leo nikachukue Dawa, mimi sikujui wewe Mchungaji wala simwamini Yesu, ila nashangaa tu baada ya maombi, nimejikuta Mwili kama unapigwa Shoti ya Umeme, nikaanguka, baada ya kuinuka, sasa najiona Mzima"

Mwisho wa kunukuu.

Nimekuwa nikibarikiwa sana na Mafundisho na Maombi ya Mtumishi mmoja Mkubwa ambaye hayupo Tanzania, huwa nafatilia Ibada zake live Youtube kila Jumapili.

Kuna siku akiwa anaendelea na Maombi, baadaye akaanza kusema Mungu anamwambia amuombee mtu mmoja mwenye shida ambaye hayupo Kanisa, akasema, Nanukuu.....

"Mungu ananambia nimuombee Mtu mmoja anaitwa Flani, anatatizo hili na hili, hapa naongea amevaa hivi na hivi, anakunywa Chai na ananitizama sasa hivi"

Mwisho wa kunukuu
basi akaanza kumuombea, baadaye Mchungaji akasema Mungu amemfungua kule alipo.

Dakika chache Misa haijaisha tangazo linatolewa Kanisani kwamba yule mtu ambaye sio member wa kanisa na Pastor aliyemuombea kabla amekuja Kanisani.

Anaingia Mwanaume wa Makamo, kashika Kikombe Mkononi, Kikombe, aina ya nguo mpaka Soksi vyote Pastor alivizungumzia wakati akimwelezea huyo mtu, akapewa nafasi ya kuongea akasema hivi, nanukuu....

"Mimi nina miaka sasa naumwa, nasumbuliwa na Maumivu Mgongoni kwa ndani upande mmoja, nimeacha kazi nimekua mtu wa kulala na kukaa ndani, mke kaniacha, leo wakati nakunywa Chai, nikwasha TV wakati natafuta Channel ya kuangalia nikajikuta nimewasha hii Channel, nasikia Pastor anataja jina langu na kuzungumza kuhusu Mimi na Ugonjwa wangu.... Mimi sio Mkristu, sina hata jina la Kikristo, mimi nimekulia katika jamii ambapo ikitokea shida tunaenda kwa Sangoma, nashangaa leo Pastor kaomba baada ya Muda nikaona nimekua Mzima, baada ya kufatilia location nikaamua nije hapa Kumuona huyu Pastor aliyeniombea"

Mwisho wa kunukuhu.

Kama Wakristo tunafundishwa juu ya Imani, kwamba Mungu hu deal na watu wenye Imani, wanaoamini 200%

Na tunaambiwa ukikosa Imani hakuna Jambo ambalo Mungu atahusika na wewe....!

Swali.
Kwa nini baadhi ya Watu Mungu anawafungua wakiwa hawana Imani kwake kabisa, yani hawana hata 10% ya Imani, na wengine wanaambiwa wakuze Imani yao ili Mungu aweze kuwasikia na kuwafungua.....!???

NB.
Kama hii mada unaona haikuhusu pita zako kimya kimya!
 
Sijatulia vizuri ila jioni nitakujibu kwa vifungu vya Biblia. Nifahamuvyo, Uponyaji wa kimungu umejengwa katika imani za namna 3.
1. Imani ya Muombeaji. Wewe unayeombea mtu una imani ya namna gani mbele za Mungu. Lazaro alilala mauti ila Yesu alimfufua. Petro na Yohana walimuombea yule Mlemavu pale kwenye lango la Hekalu katika kitabu cha Matendo ya Mitume. Kilichofanyika pale ni uponyaji wa kimungu pitia imani waliyokuwa nayo akina Petro.
2. Imani ya muombewaji. Yesu alikuwa anawauliza sana wale aliokuwa anataka waombea kama unaamini. Inawezekana wewe muombeaji una imani ya kuhamisha milima ila muombewaji hana imani hata chembe. Na hii ndio maana hata wakati Yesu akiwa duniani hakuwa anajisumbukia kufuata wagonjwa mahospitalini au majumbani mwao.
3. Imani ya Tatu ni ya Mungu mwenyewe hapa namaana ni yeye kutaka kujitwalia utukufu. Sisi Wakristo imani hii ya Mungu tumepewa sisi pitia mamlaka ya Yesu kristo.

Bali kwa ushuhuda wako, binafsi ni mkristo na nimeokoka maswali TAG ila katika kitu ambacho siamini na binafsi nakwenda nacho taratibu ni shuhuda za Mungu kaniambia moja mbili tatu. Ukiangalia shuhuda hizi nyingi hazina msingi wa Neno la Mungu. Leo unatabiri eti Mungu kanionesha nimuombee mtu kavaa nguo fulani, soksi fulani n.k then huyo mtu anakuja kanisani kwa kuvaa kama ulivyosema. Hilo halina msingi wa Kibiblia.

Naweza hitimisha kuwa, Matendo ya uponyaji na miujiza ni Karama za Roho Mtakatifu naye humpa amtakaye lakini Karama hizi zina Lengo moja tu. Kulijenga kanisa la Yesu na sio Kujijengea heshima binafsi ya Nabii/Mtumishi kama ilivyo sasa.
 
Swali zuri sana japo umeweka Maelezo Mengi sana.

Nitakujibu vizuri baadaye.
Nikimrefeer Ayubu na watumishi Wengine wengi walioteseka, waliumia walionyongwa kwa kuubeba msalaba wa Yesu.
 
Sijatulia vizuri ila jioni nitakujibu kwa vifungu vya Biblia. Nifahamuvyo, Uponyaji wa kimungu umejengwa katika imani za namna 3.
1. Imani ya Muombeaji. Wewe unayeombea mtu una imani ya namna gani mbele za Mungu. Lazaro alilala mauti ila Yesu alimfufua. Petro na Yohana walimuombea yule Mlemavu pale kwenye lango la Hekalu katika kitabu cha Matendo ya Mitume. Kilichofanyika pale ni uponyaji wa kimungu pitia imani waliyokuwa nayo akina Petro.
2. Imani ya muombewaji. Yesu alikuwa anawauliza sana wale aliokuwa anataka waombea kama unaamini. Inawezekana wewe muombeaji una imani ya kuhamisha milima ila muombewaji hana imani hata chembe. Na hii ndio maana hata wakati Yesu akiwa duniani hakuwa anajisumbukia kufuata wagonjwa mahospitalini au majumbani mwao.
3. Imani ya Tatu ni ya Mungu mwenyewe hapa namaana ni yeye kutaka kujitwalia utukufu. Sisi Wakristo imani hii ya Mungu tumepewa sisi pitia mamlaka ya Yesu kristo.

Bali kwa ushuhuda wako, binafsi ni mkristo na nimeokoka maswali TAG ila katika kitu ambacho siamini na binafsi nakwenda nacho taratibu ni shuhuda za Mungu kaniambia moja mbili tatu. Ukiangalia shuhuda hizi nyingi hazina msingi wa Neno la Mungu. Leo unatabiri eti Mungu kanionesha nimuombee mtu kavaa nguo fulani, soksi fulani n.k then huyo mtu anakuja kanisani kwa kuvaa kama ulivyosema. Hilo halina msingi wa Kibiblia.

Naweza hitimisha kuwa, Matendo ya uponyaji na miujiza ni Karama za Roho Mtakatifu naye humpa amtakaye lakini Karama hizi zina Lengo moja tu. Kulijenga kanisa la Yesu na sio Kujijengea heshima binafsi ya Nabii/Mtumishi kama ilivyo sasa.
Tena kwa kuongezea ni vyema kujiongeza na maandiko Mungu anaweza kufanya muujiza kwa mtu asiyeamini ili aanze kuamini kwake ila kwa sasa ni tofauti jamani tunapigwa mnoooo kuwa makini na hao manabiii ndugu yangu
 
Kuponywa mara nyingi ni mchongo kwenye ulimwengu wa roho. Kama mtu umezunguka kwa waganga wengi, basi huyo anaekuponya ni zaidi ya waganga uliopita. Kwa maneno mengine huyo mponyaji alipikwa kwenye kilenge kikali na cha gharama.
 
wali.
Kwa nini baadhi ya Watu Mungu anawafungua wakiwa hawana Imani kwake kabisa, yani hawana hata 10% ya Imani, na wengine wanaambiwa wakuze Imani yao ili Mungu aweze kuwasikia na kuwafungua.....!???
Baada yaa Yesu kufa msalabani, uponyaji ukawa umekusudiwa kwa kila mtu kupitia jina la Yesu. Nadhani neema hii ndiyo inayowagusa hata wale ambao hawana imani na wala hawamwani Yesu.

Tuseme kwa mfano mtoto mdogo huwa hajui kama kaa la moto huwa linaunguza, lakini haaimanishi kuwa akilishika hataungua kisa tu hajui kuwa kaa la moto huwa linaunguza. Ukishaingia anga za Yesu, haijalishi unamfahamu au humfahamu
 
Ndugu swala lakupona Ni vile Mungu anaamua kuachilia hyo neema kwa mtu,binafsi nimeombea watu wengi wamepona Ila si kila anayeombewa atapona ,Kupokea uponyaji Ni mapenzi ya Mungu vile atakavyo kwa ajili ya utukufu wa jina Lake.Jambo jingine Ni kuwa nyakati hizi wapo watu wanatengeneza mazingira ili waonekane kuwa wao wanatokana na Mungu,hao nao ujiepushe nao,Wapo matapeli wengi sana ,Mungu akusaidie upate kufahamu
 
Kitendo tu cha mgonjwa kusikiliza maombi au kukubali kuombewa tu tayari anakuwa ameifungulia ile nguvu ya kiMungu ipenye ndani yake na kuleta uponyaji.
Hivi hawa manabii, makuhani n.k. wakienda mahospitalini walikojazana wagonjwa wa kila aina na kutaka kuwaombea wapone kuna atakaekataa kweli kuombewa?
 
Shalom!
Nataka tu kujifunza na kuongeza Imani yangu!

Nimekua nikishuhudia Watu wengi wakifunguliwa Makanisani kwa Macho yangu!

Nimeshuhudia Baadhi ya watu wakifunguliwa kwa namna tofauti, katika kisa kimoja, mwanaume wa Makamo alikua Mgonjwa akiamini Kalogwa, alihangaika kutafuta Tiba toka kwa Mganga mmoja mpaka mwingine, Ndugu za yule Mgonjwa walikua hawaamini Nguvu ya Yesu Kristo katika Uponyaji, ila mmoja baada ya mwingine miongoni mwa Wanafamilia wakaanza kupokea Uponyaji, kwa mujibu wa Ushuhuda wa Ndugu na Mgonjwa, hata siku hiyo Jumapili wao wanajiandaa kwenda Kanisani, Ndugu yao anajiandaa kwenda kwa Mganga!

Ndugu wakamkamata kwa Nguvu na kwenda nae Kanisani, baada ya maombi akapona, sasa wakati anatoa Ushuhuda anasema, Nanukuu..

"Sikua hata na Mpango wa kuja hapa, nilikua nataka kwenda kwa Mganga coz alinambia nirudi leo nikachukue Dawa, mimi sikujui wewe Mchungaji wala simwamini Yesu, ila nashangaa tu baada ya maombi, nimejikuta Mwili kama unapigwa Shoti ya Umeme, nikaanguka, baada ya kuinuka, sasa najiona Mzima"

Mwisho wa kunukuu.

Nimekuwa nikibarikiwa sana na Mafundisho na Maombi ya Mtumishi mmoja Mkubwa ambaye hayupo Tanzania, huwa nafatilia Ibada zake live Youtube kila Jumapili.

Kuna siku akiwa anaendelea na Maombi, baadaye akaanza kusema Mungu anamwambia amuombee mtu mmoja mwenye shida ambaye hayupo Kanisa, akasema, Nanukuu.....

"Mungu ananambia nimuombee Mtu mmoja anaitwa Flani, anatatizo hili na hili, hapa naongea amevaa hivi na hivi, anakunywa Chai na ananitizama sasa hivi"

Mwisho wa kunukuu
basi akaanza kumuombea, baadaye Mchungaji akasema Mungu amemfungua kule alipo.

Dakika chache Misa haijaisha tangazo linatolewa Kanisani kwamba yule mtu ambaye sio member wa kanisa na Pastor aliyemuombea kabla amekuja Kanisani.

Anaingia Mwanaume wa Makamo, kashika Kikombe Mkononi, Kikombe, aina ya nguo mpaka Soksi vyote Pastor alivizungumzia wakati akimwelezea huyo mtu, akapewa nafasi ya kuongea akasema hivi, nanukuu....

"Mimi nina miaka sasa naumwa, nasumbuliwa na Maumivu Mgongoni kwa ndani upande mmoja, nimeacha kazi nimekua mtu wa kulala na kukaa ndani, mke kaniacha, leo wakati nakunywa Chai, nikwasha TV wakati natafuta Channel ya kuangalia nikajikuta nimewasha hii Channel, nasikia Pastor anataja jina langu na kuzungumza kuhusu Mimi na Ugonjwa wangu.... Mimi sio Mkristu, sina hata jina la Kikristo, mimi nimekulia katika jamii ambapo ikitokea shida tunaenda kwa Sangoma, nashangaa leo Pastor kaomba baada ya Muda nikaona nimekua Mzima, baada ya kufatilia location nikaamua nije hapa Kumuona huyu Pastor aliyeniombea"

Mwisho wa kunukuhu.

Kama Wakristo tunafundishwa juu ya Imani, kwamba Mungu hu deal na watu wenye Imani, wanaoamini 200%

Na tunaambiwa ukikosa Imani hakuna Jambo ambalo Mungu atahusika na wewe....!

Swali.
Kwa nini baadhi ya Watu Mungu anawafungua wakiwa hawana Imani kwake kabisa, yani hawana hata 10% ya Imani, na wengine wanaambiwa wakuze Imani yao ili Mungu aweze kuwasikia na kuwafungua.....!???

NB.
Kama hii mada unaona haikuhusu pita zako kimya kimya!
mponyanji ni Mungu, watumishi au wanadamu wowote wanaoomba kwa Jina la Yesu hata mtu akafunguliwa wanatumiwa kama chombo tu, ila nguvu ni za Mungu. katika Zaburi 62:11 imeandika, Mara moja amenena Mungu; Mara mbili nimeyasikia haya, Ya kuwa nguvu zina Mungu.

vilevile, kuna watu wengine wanapitia mateso makubwa, magonjwa shida n.k kwasababu Mungu ameamua wayapitie hayo aidha kama majaribu kupima au kuimarisha imani yao, au kama adhabu kwasababu ya kiburi chao ila ni adhabu ya upendo ili wabadilike manake angekuwa hawapendi angewauwa kwasababu uwezo huo anao.

kuna wakati fulani, na hii inatokea kwa watu wote wa Mungu, ambapo unaweza kupita kwenye jangwa/kipindi kigumu ukaomba hadi ukachoka na unaona kama Mungu hakusikii kumbe anakusikia ila kuna kitu anatengeneza kwako. hii inatokana na asili ya kila mtu aliyo nayo kwasababu Mungu anatujua kila mtu alivyo.

hivyo hata ukiwa unaombea watu sio wote wakija kwako watapona, kuna wengine hawajamalizana kibarua na Mungu, pengine Mungu ameandaa muujiza fulani mbele yao au anakatakata matawi ya kiburi dharau n.k maishani mwao, yakiisha wanapona hata bila kuombewa, ila pale kwenye mkutano hawatapona kwasababu Mungu ndio anaamua wapone au wasipone.

kwa wale wanaopitia magumu sana ya magonjwa shida n.k kwasababu ya kipigo cha Mungu, hao nao hawawezi kupona hadi watubu dhambi na wamrudie yeye. Zaburi 103:3 imeandikwa " akusamehe dhambi zako zote, akuponya magonjwa yako yote". wasipotubu,kibano kitaendelea na wanaweza kuangamia, ila wakitubu Mungu anawasamehe na kuwasikia.

hapa duniani sisi sote tu viumbe wa Mungu, na tunapendwa na Mungu. ila kuna baadhi ya watu wengine wameingia agano na Mungu, au ni watumishi ambao Mungu anawaangalia kwa jicho la pekee. hao ni wale walioyatoa maisha yao yote kwa Mungu, na Mungu ndio kimbilio lao. hawa ukiwagusa umegusa mboni ya jicho la Mungu, lazima upigwe viboko, ndio maana unashauriwa unapoishi ishi kwa haki na kila mtu ukionea mtu wengine ni mboni za macho ya Mungu, utapotezwa.

generally, naweza kusema, kupona au kutopona ni maamuzi ya Mungu ambaye ndiye mponyaji, lakini hata asipopona mtu haimaaanishi kwamba Mungu hana uwezo kuponya. hajaponya kwa sababu, ingekuwa kila anayeombewa anaponya pasingekuwepo na hospitali, na mwanadamu angekuwa na kiburi sana, au pengine angefanya biashara kama hao manabii wa mafuta na chumvi, na angechukua hata utukufu wa Mungu. yeye Mungu ameamua iwe hivyo, na ni sahihi kuwa hivyo.
 
Swali zuri sana japo umeweka Maelezo Mengi sana.

Nitakujibu vizuri baadaye.
Nikimrefeer Ayubu na watumishi Wengine wengi walioteseka, waliumia walionyongwa kwa kuubeba msalaba wa Yesu.
Ilibidi niweke maelezo mengi ili nieleweke moja kwa moja!
 
Kitendo tu cha mgonjwa kusikiliza maombi au kukubali kuombewa tu tayari anakuwa ameifungulia ile nguvu ya kiMungu ipenye ndani yake na kuleta uponyaji.
Yeah!
Umeongea jambo ambalo nimemsikia Pastor mmoja akiliongelea!

Anasema yeye siku hizi kaacha kuwaambia Waumini wake kwamba hawana imani ndo maana hawapokei, anasema Kitendo cha mtu kuacha Shughuri zake, na kuamua kuja Kanisani basi tayari yeye anayo Imani!

Swali linakuja kwa nini hawapokei!?
 
Shida ya kimwili ni matokeo ya shida ya kiroho kwanza.
Naamini hili pia, but binafsi naamini Imani pekee haikufanyi ukapokea Uponyaji, nadhani kuna vitu baadhi Pastors hawatufundishi, kama kuomba nini na kwa wakati gani, wakati gani unatakiwa kuomba, wakati gani unatakiwa kuabudu, pia tunawezaje kuomba kupitia Vifungu vya Biblia!

Ni juzi tu ndo nimejua kumbe kuna Utofauti kati ya kuomba, ku sali na kuabudu, ni juzi tu ndo nimejua kumbe mimi nilikua nasoma Biblia kama Kitabu cha Hadithi, baada ya kumsikiliza Pastor Bushiri, nikajua kuna vingi hatukuwahi kufundishwa hasa kina sisi ambao Mizizi ya Ukristo wetu ulianzia Ukatoliki.
 
Ni hadi uwe na imani
Na wenye imani ni wale tu wenye uwezo wa kuwafata hao manabii/mitume/makuhani huko makanisani kwao? Maana sijawahi sikia hao manabii wakienda mahospitalini kujitafutia wenye kuwaamini ili wawaponye huko huko. Au kwa vile idadi kubwa kama siyo wote wa wale "wenye imani" wanaoonekana kuponywa huko makanisani kwao ni wa mchongo?
 
Kuponywa mara nyingi ni mchongo kwenye ulimwengu wa roho. Kama mtu umezunguka kwa waganga wengi, basi huyo anaekuponya ni zaidi ya waganga uliopita. Kwa maneno mengine huyo mponyaji alipikwa kwenye kilenge kikali na cha gharama.
Source ya Nguvu za Giza ni moja, na Source ya Nguvu za Mungu pia ni moja!

Kila njia ina njia zake za Uponyaji, hazichangamani!

Rejea habari ya Mussa na Nyoka kwa Pharao, Hata Shetani ana Miujiza pia lakini haiwezi kutokana na Mungu.
 
Naomba niendelee kupitia comments maana nikitia neno nitaaribu uzi wa watu na uzuri mtoa mada alishatoa onyo...
 
Back
Top Bottom