Nina Tshs. 300,000, Naweza kuifanyia nini ili mpaka July niwe nimepata ada ya Tshs. 1,114,400?

Nina Tshs. 300,000, Naweza kuifanyia nini ili mpaka July niwe nimepata ada ya Tshs. 1,114,400?

Angalia website ya NACTE omba diplonma ya ualimu ada nadhani laki mbili kwa mwaka ukimaliza utapata kazi hata serekalini then tumia mshahara kufanya mitihani ya form six then utajaenda kusomea UDACTARI WAKO.
AU nrenda wizara ya afya omba MA yaani medical assistant au narsinng au mahabara au ufamasia diploma utajajiendeleza huko mbele ya safari
.
 
pole sana ndugu, kwaharaka nashndwa kufkri ni kitu gani unaweza fanya na hcho kiasi cha laki 3 kwa miezi takribani miwili ili upate 1200000, naomba wadau waje wakusaidie, ila usikate tamaa. Naamin kamwe ndoto yako haiwez kupotea, inaweza kuchelewa tu, one day yes!

Asante sana mkuu kwa kujali.
 
Pole sana ndugu. Watanzania, japokuwa si wote hatupendi kuchangia vitu kama hivi. Lakini kwenye mambo ya starehe, tuko mbele.

Ndugu yetu kaomba ushauri tu, lakini watu tunakosa utu. Maandiko yanasema..."Maskini na afurahi kwa kuwa ametukuzwa, na tajiri kwa kuwa ameshushwa maana anaweza kutoweka muda wowote."

Nije kwenye point. Nilisoma Muhas ila kwa upande wa Bachelor. Nafikiri pia serikali inawafadhili wanafunzi wa diploma hasa wenye matatizo fulani (mfano: walemavu, yatima etc)..jaribu kufuatilia utapata exemption. Kuna mdada nilisoma nae primary & alifiwa na baba yake udogoni, alisoma hapo. Nilipomuuliza alisema alikuwa analipiwa na serikali.

So, usikate tamaa kwa sababu Mungu anasema, "Yeye ni baba wa yatima..." Naamini atagusa mioyo ya watu ili awatumie kukusaidia. All the best & stay blessed.

Umenitia nguvu kaka yangu.
 
Mi nakushauri hivi Tafuta Mikoba Ya Kike kwa Bei ya Jumla Jumla halafu tafuta Wateja Katika Maofisi uwatembezee.. Najua Ukipata Mikoba Ya 10000 ukauza 30 utapata hela ya Ada
 
IZAMA
Hicho kiasi cha 300,00×4=1,200,000 chenji itabaki itakua poketi money utakua unafanya hivyo kila mwaka .
 
Last edited by a moderator:
Mmh hapana hii mbinu ya kubeti ni mbaya na hatari, ni bahati nasibu ya hatari sana, wasi wasi wangu huenda hata hiyo laki tatu akaipoteza, pesa ikiliwa usishangae mtu akataka kujiyonga.
Ni kweli imekaa kibahati zaidi, kuna jamaa alitoa ushuuda humu alikuwa anasoma ud, zilibaki siku 3 deadline ya kulipa ada na mfukoni alikuwa na elfu 10 tu, akajitoa mhanga akabetia yote, mkeka ulitoa mil.2
 
Mmmh!! Wenye majanga tuko wengi~ kaka uko vizur paffomance yako nimeiipenda~ sasa cha kufanya tembelea media na dhani utashauriwa ukafungua account ~ benki kama ss ambae tuko mbali tukusaidie~ hata mm nahitaji kwenda college nimemaliza kidato cha NNE mwaka 2012, nilipata div 4 points 26 , Tatizo kubwa linalo tukumba ni uwezo2, lakin mwaka Jana mwez wa tatu iv nilipata kazi ~ usambazaji wa Lain za mtandao wa tigo~ namshuru mingu saiv naweza pata Milion 1 iv binafs, ombA mungu atakusaidia ndg
 
Mmmh!! Wenye majanga tuko wengi~ kaka uko vizur paffomance yako nimeiipenda~ sasa cha kufanya tembelea media na dhani utashauriwa ukafungua account ~ benki kama ss ambae tuko mbali tukusaidie~ hata mm nahitaji kwenda college nimemaliza kidato cha NNE mwaka 2012, nilipata div 4 points 26 , Tatizo kubwa linalo tukumba ni uwezo2, lakin mwaka Jana mwez wa tatu iv nilipata kazi ~ usambazaji wa Lain za mtandao wa tigo~ namshuru mingu saiv naweza pata Milion 1 iv binafs, ombA mungu atakusaidia ndg

Nifahamishe hapo kwenye media.
 
Pole ndugu yangu, Kwa Ufaulu Wako Tena Wa Sayansi unaweza Pata msaada wa haraka sana kutoka kwa Wamisionary Wa Kikatoliki wajulikanao kama Order Of St. Benedict(O.S.B), wanapatikana Ndanda Mtwara na peramiho Songea, ila nina hofu na mambo mawili umemaliza zamani na pia upo dar ambako asilimia kubwa watu wake hawaaminiki. Hawa Wamishenari Wana shule za sekondari za advance na Vyuo vya Afya (cheti na diploma). Nimeshuhudia watu wenye matatizo na uwezo darasan wanasaidiwa kusoma bure ila wakihitimu unatumikia kwenye taasisi zao (hasa hospitali) kwa mkataba then wanakuruhusu uingie serikalin baada ya miaka mitatu, ingawa wanakulipa salary scale ileile kama serikalini.
 
Pole sana ndugu lakini usikate tamaa kwa hapo ulipo.
Mimi nakushauri na kukupa msaada wangu kupitia kitu ninachokifanya mimi,mimi ni mfugaji wa kware nauza mayai na vifaranga pia.Ungekuwa unahitaji uweke hiyo hera ianze kijizalisha after 8 weeks ningekwambia nunua vifaranga wa kware then ufuge,sasa kwa kuwa unataka hera hiyo ijizalishe within a short time anza hivi njoo nikuuzie mayai ya kware tray 1@10,000 hii ni kwako tu kama msaada coz sio bei yake hata kwa jumla.so ukinunua tray 10 itakucost 100,000 then ukaenda kuuza 20,000-30,000 depend on your market utajikuta inapata 100,000 nyingine as a profit so the more you sale you +profit.
Soko la mayai ya kware nila uhakika kwa sasa.
Huu ndo msaada wangu kwako kama utaupenda njoo pm
NOTE: BEI HIYO NI KWAKO TU
 
junior
Nimekuelewa xna junior bora boy aende teachng 2
 
Last edited by a moderator:
1. pole sana,
2. tafuta nafasi za sponsorship, search kwenye mtandao.
3. au fungua biashara upate pesa uje usome mwakani, mwaka huu hapo ni ngumu.
4. Vipi kuhusu ndugu zako?
5. vumilia na mwombe Mungu, usilazimishe kusoma mwaka huu.
 
Back
Top Bottom