Nina uhakika kwa hili la 'Freeman' hivi sasa wana CHADEMA wote wanampenda 'Mama' na 2025 wote watampigia 'Kura' zao aendelee kuwa Rais wa Kusamehe TZ

Kwa Hili tukio, score card ya mama Ina pointi nyingi, Chadema walitarajia Mbowe akitoka atakuja na confrontational politics zaidi, wanashangaa Mbowe kaenda kupiga goti kwa mama.

Akina mdude na martin Maranja Masese wanavuja damu moyoni, wamekesha twitta halafu waliyemkeshea kaamkia kwa mama kula ugali
 
Chadema is "technically dead"..siku za Mbowe kuvurumishiwa matusi zinahesabika.Tundu hawezi kuongea sababu ataambiwa mbona na wewe uliomba kuteta na Rais Samia huko ughaibuni?
Naona mmegeuka kuwa wasemaji wa Chadema. Poleni sana
 
Vipi umeamkaje?
 
Unataka kusema wale active members milion12 wote watakuwa na mama uchaguzi ujao[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tunataka katiba mpya ili tuchague viongozi tuwatakao, na kila mtu atii sheria. Sio rais kupewa kinga ya kutoshtakiwa, matokeo yake tunajikuta tunaoongozwa kama na lile dubwasha la chattle. Hilo la Mbowe kukutana na rais sio jambo kubwa kwetu,bali walichoongea kina maslahi gani kwetu sisi.

Tumechoka kutawaliwa kwa shuruti na chama chakavu, tunataka mshindi halali. Mbowe aangalie asije akatujia na zile swagga za kumsifia mama kwa style ya chawa wa ccm. Hatuna muda na siasa za kinafiki maana hata yeye tutampotezea.
 
Huyu mama nchi ilishamshinda kitambo... haya maigizo ya kina Mbowe ni mwendelezo wa kuwadhoofisha wanaotishia kiti chake.... yaani mpaka sasa kamuunda Mbowe awe kibaraka wake... Lissu nae keshamfinyanga baada ya Nairobi na Ubelgiji ... Zitto hana meno alishatulizwa kitambo amevimbewa Zanzibar. Ndani ya chama chake kawakata Kidafu wote wenye midomo... ila ninachokiona this time Mbowe akichanga karata zate vyema kwa ile gia ya Angani anaweza kuleta mabadiliko makubwa sana ya kiuongozi.
 
Cdm ndio wt wenye uelewa na akili kuliko wanachama wa chama chochote cha siasa subiri mbowe aje azungumze ndio utawaelewa cdm
 
Chadema hakuna kitu

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Hakuna mtu amesamehewa. Serikali imekwepa kudhalilishwa na kina kibatala kwenye utetezi. Period!
 
M
Mbowe alituma viongozi wa dini kumbembereza Samia, mwenyewe Samia kakubari kumsamehe,la sivyo Mbowe angekula mvua za kitosha, Ndio Maana baada ya kuachiwa ameahaidi kufanya siasa za kistarabu Ili kumpa nafasi Samia kitawala vizuri 🤣🤣🤣inamaana tokea mwanzo walikuwa wakifanya siasa za fujo
 
Huwa
Huwa nasema kila siku shule za kata zimeharibu vijana wa kizazi hiki

Ona Sasa akili za huyu popoma

Wakati wenye akili tunapigania katiba yeye anawaza kumpenda sijui! ujinga gani! eti uchaguzi 2025
 
Labda wanachadema feki wa lumumba
 
Mtoa post anasema: "Kwa furaha niliyoiona kwa Wana Chadema... Swali, ina maana yeye hakufurahi? Hali ya kisiasa kwa miaka sita Tanzania ilikuwa mbaya sana, akifa wa CCM, upinzani wanasema haiwahusu , akifa wa upinzani, CCM wanasema haiwahusu. Hali hii ya hovyo haikuwa na afya kama Taifa. Wapo chawa wa CCM Kama mtoa post wangependa hali hii iendelee, na Jana hawakulala usingizini walipoona Rais Samia anamaliza hili la Mbowe japokuwa watasema Rais hahusiki na masuala ya mahakama, lakini DPP aliyetoa hiyo Nolle proseque ni mteule wa Rais.
 
Tetetetee
 
Akili duni hizi. Busara ya kukutana na watesi wake haijaanza leo. Mandela alipotoka jela aliendelea kucheka na watesi wake, Mzee Jomo Kenyatta alipotoka jela aliendelea kucheka na watesi wake, kinachotolewa watesi ndio huteseka baadaye. Mbowe ametumia busara kukutana na mtesi wake, mtesi wake atateseka baadaye. Busara hii hutumiwa na wachache wenye akili
. Wale chawa wa CCM wameteseka Jana hawakulala usingizi.
 
Huwezi kupenda nnya eti kwa sababu imewekwa kwenye sahani.
 
Chadema is "technically dead"..siku za Mbowe kuvurumishiwa matusi zinahesabika.Tundu hawezi kuongea sababu ataambiwa mbona na wewe uliomba kuteta na Rais Samia huko ughaibuni?
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] sijui umeandika vitu gani hata havielewiki ndio kupagawa huko au [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…