Ninahisi nimebugi, nataka tuandikishiane nimpe milioni 5 ya msingi. Anipe mwanangu atakapofikisha umri

[emoji2][emoji2][emoji2][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kumbe msukuma!!! Wasukuma sijui huwa wanakwama wapi? Wako lainilaini sana kwa wanawake
 

Laana ya mkeo 9months unaanza mahusiano serious na majukumu ya kulea, una uhakika gani mimba ni yako, mpige chini komaa na kumhudumia Mama, baharia unakwama wapi uguza mama achana na mikosi, mke wako wa ukweli yupo. Ukitumia pesa kwa mvuto na wewe utavutwa kindezi na shetani.
 
Dah pole kiongozi ,Kuna kitu nimejifunza sana kwenye maisha ,
Kuwa makini sana na watu hawa japo sio wote wako hivyo ,ila baadhi wanamatatizo hasa .
waangalie sana wanawake walioachika ,kabla ya kutaka kumuoa chunguza kwa makini ,kipi kilimshinda kwenye ndoa ya mwanzo ,huwenda ukapata cha kujifunza maana sio wote wanayoyazungumza kama walinyanyasika au kutendwa na wanaume ,wengine wao ndio sababu na mwanaume ameamuwa kubwaga manyanga.
pili mwanamke Alozaa bila kuolewa ,,hapa napo nieleweke sio wote ,ila wapo baadhi wenye kushindikana kuolewa kwa tavia zao ,mpaka mtu akamzalisha na kusepa,na wapo ambao wao walikuwa wazuri tu ila hawakupata mtu sahihi .
Tatu Mwanamke kama atafikisha umri mkubwa na bado hajaolewa au anapata wa mwanaume ila hamuowi ,

Dizaini ya hawa watu kabla hujafanya maamuzi ya kuwa na mahusiano nao ya kina ,kwanza fanya uchunguzi wa kina na ujiridhishe ,huyo unayetaka kuanzisha nae mahusiano ya kweli ,yuko katika hali gani ,
je amekumbwa tu na bahati mbaya za kilimwengu ikapelekea kujikuta mikononi ,mwa wanaume ambao si sahihi ? Au yeye chanzo cha tatizo ,

Pana kisa kimoja ,pana dada mmoja wa mjini hasa na maarufu ,Alitokea kunipenda hasa na paka kutamani nimuowe hata mke wa pili ,
Ila nilichomwambia. dunia yako na yangu ni tofauti,Ila akalazimisha kuwa anaweza kuishi hali yeyote ,na akawa analalamika hakupata mwanaume sahihi n.k ,kwa jinsi anavyongea unaweza ona kweli ,huyu hajapata mwanaume wa kweli ,lkn kwa kadri nilivyomsoma tabia na kuwa nae karibu tu kama rafiki ,nikagundua huyu mtu why hawezi olewa na kuwekwa ndani ,au kwann wanaume huchemka kumweka ndani kama mke ,zaidi ya kumchezea ,
Tatizo lao wengi huwa hawajitathmini na kupitia baadhi ya kasoro zao na kujirekebisha ,badala yake ,ni watu wa kutupa lawama tu ,na kujiona kila siku wao wanaonewa au kila mwanaume anayempata si sahihi ,Ila wanajisahau kuwa wakati unaona mwanaume si sahihi je wewe uko sahahi?.
. Ajabu wanawake wengi atakwambia anataka mwanaume mwenye hofu ya mungu ,ila cha kujiuliza wao wanayo iyo hofu ?
Na je akimpata atakubali kufata misingi ya mungu au atakubali kuongozwa katika kumjua mungu?
jibu wengi wao wanahubiri wasioyatenda ama kuyataka ,


MWISHO NI KUSHAURI NDGU YANGU ,Fanya maamuzi sahihi na kwa wakati sahihi ,Na hakikisha linapokuja swala la maamuzi tumia akili kuamua ,na kamwe usiuwache moyo wako ukafanya maamuzi
 
Pole sana kwa kuuguza mama .
 
Wamegundua wewe unazo na ni mwepesi wa kutoa
 
Ila kudate na single mom inahitaji moyo sana.
 
Be a man, mueleze siwezi kuoa mpaka afya ya mama yangu ikae sawa na hayo ndio maamuzi yangu. Kama unaona afya ya mama yangu sio muhimu kwako basi nitatafuta mtu mwingine wa kumuoa muda ukifika na nitakapokuwa huru. Mnachokosea vijana ni kutosimamam katika nafasi ya mwanaume ndio maana unapelekeshwa.

Mimi ndio muoaji halafu wajinga wengine wanipangie lakufanya labda niwe nimezaliwa na jinsia tofauti na hii niliyonayo
 
We jamaa ni mlalamishi tu usiye na gut ya kumueleza mtu unachotaka ndo maana demu anakuendesha.
- Amekupangua umlipie ada mwanaye,umekubali.
- Amekupangia tarehe za mahari, umekubali.
Sasa unalalamika hapa ili iweje? Kama hutaki si umwambie?
- Mama yako anaumwa demu anakuambia "pole" unakuja kulalamika..Sasa unataka afanyaje? Akamuuguze?
Na kama ndivyo si umwambie. Boresha mawasiliano ndani ya mahusiano yako bhana.
 
Hebu muuguze mama yako

Ujasiri wa kuoa unautoa wapi???

Mbona alomzalisha hakumuoa???

Jitulize kwanza. Asikupangie kwenda kwao. Utaenda kwa wakati wako
Kweli.kamuona jamaa ni kitonga,
Huyo mwanamke. Sio wa kuoa utajuta.Huyo Ana pepo LA kuzalishwa
 
Kitakachofuata demu atampiga jamaa mikwaju
 
Hakika ulikosea kuingia kwny mahusiano mapya baada ya kufiwa na mweñza, siñgle mumy mpangie utaratibu unaotaka wewe km hataki mwache
 
Usikute hata mimba sio yake.
Ukiona mwanamke anakukimbiza kimbiza kumuoa jua Kuna lililofichama.
Mama hawezi kuwa mgonjwa aafu yeye yuko mbio kutaka ukalipe mahari.
Kwani ndio nguzo pekee inakuja kumuuguza mama?
 
Akili yako nadhani kuna switch imezima. Mamaako mgonjwa, na hapo hapo unaambiwa ukatoe mahari yenye vikorombwezo vya kutosha tu halafu unakuja kuomba ushauri huku!? Ndio maana wanawake wanazidi kutudharau kadri siku zinavyozidi kwenda
 
Baba mkubwa ndo anayekuja kupanua mapaja??? Hela inamuhusu nini hiyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…