Ninavyomkumbuka Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mwalimu mtu wa watu (6)

Ninavyomkumbuka Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mwalimu mtu wa watu (6)

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
NINAVYOMKUMBUKA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE
MWALIMU MTU WA WATU 6

Mwalimu alikuwa anazungumza na Profesa Malima nyumbani kwake na katika mazungumzo Mwalimu akamsikitikia Profesa Malima kuwa kuna watu wanamshutumu yeye yeye kuwa hawapendi Waislam.

Mwalimu akanyanyuka alipokuwa amekaa na kwenda chumbani kwake, akatoka na moja ya picha za wakati wa kudai uhuru, akamwonyesha Malima.

Mwalimu akasema, ''Profesa unaona picha hii, Waislam watupu, Mkristo ni mimi peke yangu, vipi mimi leo niwachukie watu walionifikisha hapa?''

Mwalimu amefariki dunia wakati nchi yetu ipo katika hofu ya kuvunjika amani.

Waislam ambao walikuwa mstari wa mbele katika kumpokea Mwalimu na kumuunga mkono na kudai uhuru wanaichagiza serikali iwafanyie uadilifu kwa kuwa wanadai kuna watu ndani ya serikali wameweka maslahi ya dini zao dhidi ya maslahi ya taifa.

Waislam wanadai kuwa CCM kimekuwa chama cha kanisa kikifanya maamuzi kwa maslahi ya Ukristo.
Waislam wameshapambana na askari mara kadhaa na damu imemwagika.

Hii ni hatari ya wazi na inatishia uhai wa taifa letu.

Waislam walioshiriki katika kuleta uhuru wa nchi hii wanashangaa wanaposoma magazeti na kuambiwa na wanasiasa kuwa wao wanataka kuvuruga amani.

Kinachowashangaza ni kuwa vipi wao wapiganie uhuru wa nchi hii kisha wao waanze kuuvuruga.

Lakini kinachowashangaza Waislam zaidi na hasa marafiki wa zamani wa Mwalimu ni ukimya wake Mwalimu katika tatizo hili zito linalotishia uhai wa taifa hili.

Nafasi za mbele katika mazishi na maombolezo watachukua wale waliokuja kumkumbatia na kujidai kumpenda Mwalimu kwa kuwa kwa kufanya hivyo kuna maslahi makubwa kwao.

Lakini kama Mwalimu angeliweza kufunua macho na kuangalia umma unaoomboleza kifo chake kwa hakika kabisa akili yake ingelirudi nyuma zaidi ya miaka 40 na kuwakumbuka rafiki zake waliompokea Dar es Salaam na katika TANU katika miaka ya 1950.

Katika marafiki zake hawa, wengi wametangulia na kumuacha Mwalimu nyuma.

Kwa bahati mbaya wale walio hai kama Mzee Shaaban Gonga, Mzee Juma Mlevi na Mzee Rashid Sisso, historia imekataa kuwatambua.

Kwa ajili hii basi wataomboleza kifo cha rafiki yao kimya kimya na katika upweke.

Mwalimu hatunae tena na kwa hakika ameacha historia ambayo itazungumzwa kwa muda mrefu baada ya yeye kutoweka.

(Kutoka taazia iliyochapwa na Mtanzania, Jumatatu, Oktoba 18, 1999).
 

Attachments

  • BARAZA LA WAZEE WA TANU.jpg
    BARAZA LA WAZEE WA TANU.jpg
    36.8 KB · Views: 5
  • TATU BITI MZEE.JPG
    TATU BITI MZEE.JPG
    53.3 KB · Views: 5
  • SHEIKH SULEIMAN TAKADIR NA BANTU GROUP.jpg
    SHEIKH SULEIMAN TAKADIR NA BANTU GROUP.jpg
    20.1 KB · Views: 5
  • ALI MSHAM.jpg
    ALI MSHAM.jpg
    45 KB · Views: 5
  • Prof._Kighoma_Malima.jpg
    Prof._Kighoma_Malima.jpg
    17 KB · Views: 5
Naona umri umeenda sasa ni wakati wa kupumzika maana udini umekukaa sana! Jitafakari
 
Acha udini mkuu.....TZ haina dini....Uhuni ni tabia ya mtu wala haiangalii dini na ndio maana tumeona mapadre wanalawitiwa na pia tumeona mwalimu wa madrasa amerekodi video za ngono akitikisha makalio.
 
Acha udini mkuu.....TZ haina dini....Uhuni ni tabia ya mtu wala haiangalii dini na ndio maana tumeona mapadre wanalawitiwa na pia tumeona mwalimu wa madrasa amerekodi video za ngono akitikisha makalio.
Hayo uliyoandika yanahusiana nini na hii mada?

Wewe hauna dini?
 
Hayo uliyoandika yanahusiana nini na hii mada?

Wewe hauna dini?
Yes yanahusiana kwasababu mtoa mada anasisitiza kwamba tuwatambue waislamu katika kutupatia uhuru wetu wa TZ.,mambo ya kupigania uhuru hauna dini,ile sio jihad ya kuuana,ukiona mtu anaua kwa kutumia dini huyo ni MUHUNI tu na ndio maana kuna mapadre mashoga na "maostazi" wanabaka watoto kwenye madrasa.
 
Hivi waislamu mmebaguliwa wapi mbona lawama nyingi sana maana kuanzia awamu ya nne mpk hii mna viongozi wakubwa kwenye uongozi wa juu, awamu ya nne 3 Rais, makamu wa Rais walikuwa waislamu achia mbali wengine na huko Zanzibar wakristo walikuwa na waziri Mkuu tu lkn hatukusikia malalamiko ya wakristo. Awamu hii ambayo Makamu wa Rais, Waziri Mkuu wote ni waislamu lkn bado mnalia sasa shida nini

Mnataka nchi yote viongozi muwe nyie ndiyo nyoyo zenu zifurahi mbona huko Zanzibar viongozi karibia wote ni waislamu japo wakristo wapo lkn hatusikii wakilalamikia hilo na mnawaminya kweli lkn wametulia lkn huku kila siku malalamiko mnabaguliwa acheni zenu sote ni wamoja tuishi kwa amani
 
Yes yanahusiana kwasababu mtoa mada anasisitiza kwamba tuwatambue waislamu katika kutupatia uhuru wetu wa TZ.,mambo ya kupigania uhuru hauna dini,ile sio jihad ya kuuana,ukiona mtu anaua kwa kutumia dini huyo ni MUHUNI tu na ndio maana kuna mapadre mashoga na "maostazi" wanabaka watoto kwenye madrasa.
Naona unajitahidi kuibadili mada. Inakuuma?

Wapi umeyaona yote uliyoandika?

Nimekuuliza wewe hauna dini?
 
Hivi waislamu mmebaguliwa wapi mbona lawama nyingi sana maana kuanzia awamu ya nne mpk hii mna viongozi wakubwa kwenye uongozi wa juu, awamu ya nne 3 Rais, makamu wa Rais walikuwa waislamu achia mbali wengine na huko Zanzibar wakristo walikuwa na waziri Mkuu tu lkn hatukusikia malalamiko ya wakristo. Awamu hii ambayo Makamu wa Rais, Waziri Mkuu wote ni waislamu lkn bado mnalia sasa shida nini

Mnataka nchi yote viongozi muwe nyie ndiyo nyoyo zenu zifurahi mbona huko Zanzibar viongozi karibia wote ni waislamu japo wakristo wapo lkn hatusikii wakilalamikia hilo na mnawaminya kweli lkn wametulia lkn huku kila siku malalamiko mnabaguliwa acheni zenu sote ni wamoja tuishi kwa amani
Zanzibar huifahamu dada. Ni heri uongee unayoyafahamu.
 
Naina unajitahidi kuibadili mada. Inakuuma?

Wapi umeyaona yote uliyoandika?

Nimekuuliza wewe hauna dini?
Dini tumeletewa mkuu,kama waarabu wasingekuja au "wamishionari" kusingekuwa na dini,tungeendelea kuabudu mizimu(mibuyu etc)....Kwa mantiki hiyo mie sina dini ila nina amini Mungu yupo.
 
Zanzibar huifahamu dada. Ni heri uongee unayoyafahamu.
Jibu hoja mbona mnapenda kulalamika sana mnaonewa? Mnataka nchi yote viongozi wawe waislamu? Mwalimu alisema kama unawaza hivyo basi ni "UJINGA".
 
Jibu hoja mbona mnapenda kulalamika sana mnaonewa? Mnataka nchi yote viongozi wawe waislamu? Mwalimu alisema kama unawaza hivyo basi ni "UJINGA".
Nimekuuliza swali. Wewe una dini? Naona hujajibu. Raha ya mjadala nawe ukiulizwa ujibu maswali.

Umeisoma mada? umesoma nani aliyelalamika mpaka akaingia ndani kutoa picha?

Mbona unakuja na lugha chafu? Nini kilichokufanya hivyo? Kilichokufanya utoe povu ni nini?
 
Orodha ya viongozi wetu Tanzania

1. Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere

Mkristo

2. Ndugu Ally Hassan Mwinyi (mzee Ruksa)

Mwislam

3. Benjamin William Mkapa (mzee wa uwazi na ukweli)

Mkristu

4. Jakaya Mrisho Kikwete (mzee wa anga)

Mwislam

5. John Pombe Magufuli (mzee wa pushapu)

Mkristo

Hatujapata ajaye rais wa 6 na kwa trend hii atakuwa mwislam lazima....by induction method

Mzee Mwinyi na mzee Kikwete walipaswa kurekebisha mapungufu unayoyaona endapo yapo.

Mwilinyi aliwapiga mwembe chai

Benjamin aliwapiga zanzibar mpaka shimoni Mombasa

Kikwete na mashekhe wa uamsho zanzibar, kawasweka nakuwaacha ndani mpaka leo kama sijakosea sidhani kama ni Pombe

Hapa tunamlaum nani

Mwinyi, Benjamin au Kikwete?
 
Dini tumeletewa mkuu,kama waarabu wasingekuja au "wamishionari" kusingekuwa na dini,tungeendelea kuabudu mizimu(mibuyu etc)....Kwa mantiki hiyo mie sina dini ila nina amini Mungu yupo.
Nani kakuuliza yote hayo?

Nimekuuliza wewe hauna dini?

Mbona swali jepesi sana hilo.
 
Orodha ya viongozi wetu Tanzania

1. Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere

Mkristo

2. Ndugu Ally Hassan Mwinyi (mzee Ruksa)

Mwislam

3. Benjamin William Mkapa (mzee wa uwazi na ukweli)

Mkristu

4. Jakaya Mrisho Kikwete (mzee wa anga)

Mwislam

5. John Pombe Magufuli (mzee wa pushapu)

Mkristo

Hatujapata ajaye rais wa 6 na kwa trend hii atakuwa mwislam lazima....by induction method

Mzee Mwinyi na mzee Kikwete walipaswa kurekebisha mapungufu unayoyaona endapo yapo.

Mwilinyi aliwapiga mwembe chai

Benjamin aliwapiga zanzibar mpaka shimoni Mombasa

Kikwete na mashekhe wa uamsho zanzibar, kawasweka nakuwaacha ndani mpaka leo kama sijakosea sidhani kama ni Pombe

Hapa tunamlaum nani

Mwinyi, Benjamin au Kikwete?
Umeusoma mstari huu juu hapo...

Nafasi za mbele katika mazishi na maombolezo watachukua wale waliokuja kumkumbatia na kujidai kumpenda Mwalimu kwa kuwa kwa kufanya hivyo kuna maslahi makubwa kwao.
 
Umeusoma mstari huu juu hapo...

Nafasi za mbele katika mazishi na maombolezo watachukua wale waliokuja kumkumbatia na kujidai kumpenda Mwalimu kwa kuwa kwa kufanya hivyo kuna maslahi makubwa kwao.

Mwinyi na kikwete hawajawa mstari wa mbele?

Walifanya nini
 
Hivi "udini" maana yake nini?
Udini ni pale unaposhadidia makala zinazoangukia dini fulani kila wakati. Mfano wewe hata ulikonfuzi na kumshabikia waziri mkuu wa Ethiopia ukikengenyuka kuwa ni mwislam ilhal ni mlokole. By the way mimi ni muislam lakini sipendi udini.
 
Back
Top Bottom