Ninawaogopa sana viumbe wa kuitwa binadamu

Ninawaogopa sana viumbe wa kuitwa binadamu

Una uwezo wa kuishi na kila binadamu, ila uwe makini na yule unayemsogeza kwenye maisha yako.

Wengine wanastaili uishi nao kwa mbali na wachache sana wanapaswa uwe nao karibu.
Kosa ni kufanya vise versa ama kuwakataa watu.

Kumbuka hata huyo unayemuona mbaya kuna namna moja ama nyingine anamsaada na wewe.

Kumkataa mtu ni sawa na kujikataa mwenyewe, cha msingi tumia akili kuishi na watu.
Asante sana. Nimezingatia maneno haya🙏🏾
 
Watu ndiyo maisha.

Ukikata uepukane na watu, basi unahitaji pumziko la milele. Kufa.

Na huko huna hakika kama hawapo. Unaweza kuwakimbia huku, alafu unaelekezwa Jehanamu.
Huko ni vilio, vijambo, machozi, ukunga, harufu ya kuungua, aaagh kubabake.

Au ukimbilie Paradiso huko ni kelele za kusifu, shangwe, kuabudu, kugigida mito ya pombe, kufanyana, eee bhanah weee.

Bakia tu humu ulipotuzoea Mkuu.
Wakikuumiza wapo watakaokufariji. Wakikuzomea wapo watakushangilia. Wakikuchukia wapo watakaokupenda.

Hakunaga upande mmoja tu.
 
Nimejikuta ninawaogopa sana binadamu kutokana na visa mbalimbali nilivyowahi kupitia kwenye maisha yangu.

Asili yangu ni ukimya na utaratibu lakini kuna wakati maisha yanahitaji ujichanganye na watu mbalimbali kutokana na mifumo yetu.
Na ndicho kipindi nilichojifunza kuwa binadamu ni kiumbe hatari mno.

Ninaogopa watu, ninaogopa miunganisho mipya, hata katika mahusiano ya kimapenzi inachukua muda mno kujiunganisha na mtu kihisia.

Sina imani na kiumbe binadamu kwenye nyanja zote za kimaisha! Japokuwa haiwezekani, lakini ninatamani niishi mahali nisiyoweza kukutana na binadamu.😔😔😔
Wakati nasoma heading, nikadhani aliyeandika post hii labda ni mamba au kiboko au mbwa..!! Kumbe naye ni binadamu lakini hajiogopi yeye..!!

Embu mamdogo Amehlo njoo nisaidie kuelewa hii makitu. Dada To yeye na wewe unajiogopa? Shemela Evelyn Salt kwani huyu kapigapigaje hapo?
 
Ni kweli lakini ikifikia hatua ya kuwaogopa watu hadi utamani kuishi kipweke ni hatari kwako.
Jichanganye nao hivyohivyo sababu ukishindwa utaishia kuyachukia maisha yako pia... Wao ni watu, na wewe ni mtu.
Ukituona sisi sote ni wabaya lazima ufikie kujiua sababu wewe na mimi tunafanana. Ukiona watu wote hawafai hata wewe utajiona hufai na utaanza kutafuta maisha ya kipekeepekee ambayo hawezi kuyapata ukiwa hai.

Kwa kifupi wewe unahitaji daktari wa akili au unaweza kupona mwenyewe kwa kuanza kuyatazama maisha tofauti kadogo
Asante, sijawahi kufikiria kujitoa uhai.
Nipo sawa kwa sasa.
 
Watu ndiyo maisha.

Ukikata uepukane na watu, basi unahitaji pumziko la milele. Kufa.

Na huko huna hakika kama hawapo. Unaweza kuwakimbia huku, alafu unaelekezwa Jehanamu.
Huko ni vilio, vijambo, machozi, ukunga, harufu ya kuungua, aaagh kubabake.

Au ukimbilie Paradiso huko ni kelele za kusifu, shangwe, kuabudu, kugigida mito ya pombe, kufanyana, eee bhanah weee.

Bakia tu humu ulipotuzoea Mkuu.
Wakikuumiza wapo watakaokufariji. Wakikuzomea wapo watakushangilia. Wakikuchukia wapo watakaokupenda.

Hakunaga upande mmoja tu.
Upo sahihi.
 
Wakati nasoma heading, nikadhani aliyeandika post hii labda ni mamba au kiboko au mbwa..!! Kumbe naye ni binadamu lakini hajiogopi yeye..!!

Embu mamdogo Amehlo njoo nisaidie kuelewa hii makitu. Dada To yeye na wewe unajiogopa? Shemela Evelyn Salt kwani huyu kapigapigaje hapo?
Binadamu katika level tofauti tofauti za wanyama😂
 
Nimejikuta ninawaogopa sana binadamu kutokana na visa mbalimbali nilivyowahi kupitia kwenye maisha yangu.

Asili yangu ni ukimya na utaratibu lakini kuna wakati maisha yanahitaji ujichanganye na watu mbalimbali kutokana na mifumo yetu.
Na ndicho kipindi nilichojifunza kuwa binadamu ni kiumbe hatari mno.

Ninaogopa watu, ninaogopa miunganisho mipya, hata katika mahusiano ya kimapenzi inachukua muda mno kujiunganisha na mtu kihisia.

Sina imani na kiumbe binadamu kwenye nyanja zote za kimaisha! Japokuwa haiwezekani, lakini ninatamani niishi mahali nisiyoweza kukutana na binadamu.😔😔😔
Mimi nadhani wewe tutaendana. Mimi pia nipo hivo hivo..natamani ningeenda kuishi kwenye kisiwa changu peke yangu.Binadamu ni hatari sana sio wa kuwachukulia poa kabisa.
 
Back
Top Bottom