Pre GE2025 Ninawapongeza CHADEMA kwa maoni yao ila hoja namba 5 ni ya ovyo

Pre GE2025 Ninawapongeza CHADEMA kwa maoni yao ila hoja namba 5 ni ya ovyo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Unaamini kwenye vyama kwani?
Hoja nyingine ya hovyo ni kuhusu mgombea binafsi asiwe mwanachama wa chama chochote kwa miezi sita. Sarawat yule muasisi wa ugombea binafsi nchini alikuwa mwana TANU. Sasa hawa hiyo hoja sijui wameitoa kwa misingi gani?
 
Ni vipi kama wabunge watakuwa wengi kwa maana ya kuhudumia wananchi, kisha mishahara Yao ikapunguzwa zaidi ya nusu ya Sasa? Je wakipunguza posho za Sasa za wabunge, sambamba na kupunguza vikao vya bunge, huoni kama suala la gharama halitakiwepo. Tatizo ni hiyo kuongelea mapendekezo ya cdm, katika mtazamo wa kiccm.

Kwa taarifa yako huko uwanjani wachezaji huwa 11 Kila upande, lakini Kila team huwa na mbinu au mfumo wake wa kiuchezaji.
UMEUA KABISA;
Kuzungumzia mapendekezo ya Chadema kwa mawazo ya kiccm.
Hiyo haina tofauti na ile mihadhara ya kidini kujadili Agano Jipya kwa kutumia Quran au kuijadili Quran kwa kutumia Biblia.

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Ambacho hujaelewa nini? Hatutaki wanawake waingie bungeni kwa viti maalum ila ni lazima wapigiwe kura majimboni sasa whether ni wagombea wawili kila jimbo kama ilivyo Uganda is another issue ila hoja nzima ya equal footing ni sababu women are majority in Tanzania thus it has to be reflected in legislative representation.

As simple as that
Ambayo ni hoja ya Kijinga.......
Kuna utafauti gani na Viti maalamu hicho kinachofanyika?
Women Vs Women
Men vs Men
Huoni shida shida hapo? Mnataka kuashiria nini ? Kwamba wanawake ni dhaifu hawawezi shindana na wanaume?
Kwani saiv wanawake wanazuiliwa kugombea?
Kuna equal footing tayari, hicho mnachotaka kucreate nyie ni nini?

Hamtaki waingie kwa Viti maalumu na kwa chini yake mnazungumzia wabunge wa kuteuliwa wasiopungua asilimia 30 ya wabunge wote, hawa ni kina nani?
Hakutakuwa na wanawake kwenye hizi asilimia 30?
 
Leo nimeamua kuwapongeza CHADEMA kwa kuonyesha weledi wa kisiasa kwa kutoa maoni yao kuhusu muswada wa sheria ya uchaguzi. Safari hii ufipa wamejitahidi tofauti na wakati mwingine.

Hata kama sikubaliani na maoni yao yote ila nakubaliana na namna walivyojitahidi kupanga hoja zao.

Nawapongeza pia kutoruhusu kila kada wa Ufipa na kupost maoni kwenye social media hali inayofanya CHADEMA ionekane kama familia ya kambale kila mwanafamilia ana ndevu.

Imezoeleka huko UFIPA kila mtu ni msemaji wa chama. Pia nakipongeza ACT kwa kuwafundisha CHADEMA siasa za kisomi. ACT wao hutoa matamko yao kisomi na sio kila mwanachama kuropoka mitandaoni.

Maoni mengi sio mabaya kwa kutolewa na chama cha siasa kinachotaka kushika dola ingawa maoni mengi ni copy & paste toka kwenye rasimu ya Warioba. Mimi nimeshangazwa sana na hoja namba 5 inayosomeka hivi:

"Kuwe na wabunge wawili wa kuchaguliwa kwa kila Jimbo la uchaguzi, moja Mwanaume na Mmoja mwanamke ambao kila mmoja atachaguliwa kwa kura zake kwenye kundi analogombea".

Hii ni hoja ambayo haikutakiwa kutolewa na chama kinachojinadi kuguswa na mzigo wa kodi walio nao wananchi kugharamia uendeshaji wa serikali. Yaani kwenye hizi zama tunazotaka wabunge wapungue kutoka 393 hadi labda 100 wao CHADEMA ndo wanataka waongezeke wengine? inashangaza na kutia hasira mno.

Wabunge wa kuchaguliwa mwaka 2020 walikuwa 264 kwahiyo kwa hesabu za hovyo za Ufipa wanataka waongezeke wengine 264. Hoja yao hii ikipita tutakuwa na wabunge zaidi ya 528 kwenye bunge lijalo. INAKERA SANA kuwa na upinzani unaowaza jinsi gani waingie madarakani na kutafuna kodi za wananchi.

Ninashauri hoja za CHADEMA zisomwe kwa utulivu mkubwa kwasababu kuna hoja zina nia ovu kwa mwananchi mlipa kodi. Hoja zao zimejikita kushika dola zaidi bila kujali maumivu atakayopata mtanzania.

Pia wanaCCM na wazalendo tusichoke kukiadhibu hiki chama cha Mbowe kila fursa ya sanduku la kura inapojitokeza. Kuanzia ngazi ya kitongoji lazima tukiadhibu CHADEMA.
Pasiwepo na viti maalum,

ELIMU inatokewa sawa Kwa makundi yote, hivyo DEMOKRASIA ichukue mkondo wake.
 
Mkuu pendekezo hilo wala halina shida kwa upande wa gharama. Kwa kuwa marupurupu ya sasa ya mbunge wa jimbo na stahili zake nyingine zote, vinaweza kugawanywa mara mbili ili viendane na mahitaji ya wabunge hao wawili.

Mathalani, kama mbunge wa sasa analipwa mshahara wa Tsh 12Mn, basi kupitia mapendekezo hayo wabunge hao wawili wa jimbo husika watalipwa kila mmoja Ths. 6Mn. Kwa upande wa posho z vikao kila mmoja itapaswa alipwe nusu ya kile anacholipwa mbunge wa sasa, n.k..

Kuliko kuwa na nafasi za wabunge wanawake wa viti maalum na tena wasiokuwa na majimbo ya uwakilishi wa moja kwa moja. Ni heri wapitie mchakato wa kupigiwa kura majimboni mwao ili kuweza kupima kukubalika kwao majimboni kuliko kutokana na utashi wa kukubalika kwao ndani ya vyama vyao vya kisiasa.

Ukichunguza kwa undani zaidi ubora wa pendekezo hili lenye mantiki, utaona dhahiri kuwa gharama kwa ujumla za uendeshaji wa bunge zitapungua sana, kwa kuwa hakutakuwepo tena na gharama za wabunge wa viti maalum, bali zile za wabunge wa jimbo zitabakia kuwa ni zile zile.
Nani kasema viti maalumu inaondoka?
Ukisoma kwa chini wanasema Wabunge wa kuteuliwa wasipungue asilimia 30 ya wabunge wote.
Je hii sio viti maalumu?
 
Ambayo ni hoja ya Kijinga.......
Kuna utafauti gani na Viti maalamu hicho kinachofanyika?
Women Vs Women
Men vs Men
Huoni shida shida hapo? Mnataka kuashiria nini ? Kwamba wanawake ni dhaifu hawawezi shindana na wanaume?
Kwani saiv wanawake wanazuiliwa kugombea?
Kuna equal footing tayari, hicho mnachotaka kucreate nyie ni nini?

Hamtaki waingie kwa Viti maalumu na kwa chini yake mnazungumzia wabunge wa kuteuliwa wasiopungua asilimia 30 ya wabunge wote, hawa ni kina nani?
Hakutakuwa na wanawake kwenye hizi asilimia 30?
Huu ubishi unaoleta hapa ni uhuru wako wa maoni na tunauheshimu, je ni kwanini usihoji kwenye public places Kuwa na vyoo vya me na ke kuwa wanaleta ubaguzi wa kijinsia, wakati huko majumbani hakuna vyoo vya me na ke?
 
Nasema mleta mada ni mpumbavu sana, siwezi kukosoa upumbavu ni Sawa na kumpigia mbuzi gitaa ukiamini atacheza. Ni mpumbavu sana! I mean it. Full stop 🛑
Ndugu najua una hasira za kuachwa na mumeo. Relax kila kitu kitakuwa sawa. Wewe sio wa kwanza kuachika kwa tuhuma za kuchepuka.
 
Hakuna asiylipa Kodi nchi hii, kumbuka usipolipa direct, utalipa indirect. Kama hujui sema ueleweshwe kuhusu Kodi. Mfano mdogo tu, kitendo Cha kuwa online, vifurushi umeshalipia Kodi tayari.
Acha ujanja wa Mbuzi kujambia mdomo. Ninauliza kama wewe una biashara ambayo unalipa Corporate tax? Kama huna kaa kimya.
 
Nani kasema viti maalumu inaondoka?
Ukisoma kwa chini wanasema Wabunge wa kuteuliwa wasipungue asilimia 30 ya wabunge wote.
Je hii sio viti maalumu?
Mkuu uwepo wa viti maalumu ni upuuzi mtupu. Labda pendekezo lingekuwa watokane na makundi maalum, kwa mfano watu wenye mahitaji maañum, vyama vya wafanyakazi, vyama vya ushirika, vyama vya wamiliki wa biashara, masoko, uvuvi, wafugaji, wakulima, n.k.

Uwepo wa viti maalum kwa ajili ya wanawake tu ni ubaguzi kwa wanaume maskini na makundi ya vijana wa kiume ambao hawana ajira. Yaani mwanamke apendelewe kwa kuwa tu yeye ni mwanamke, na mwanaume apigike kisa kazaliwa mwanaume. Kama suala ni usawa wa jinsia, basi fursa ziwekwe kwa usawa bila ya kujali jinsi ya mtu.
 
Ningeshauri kila Wilaya iwe na mbunge mmoja tu n viti maalum kil mkoa atoke mmoja tu badala ya baadhi ya Wilaya kuwa na wabunge zaidi ya mmoja
 
Leo nimeamua kuwapongeza CHADEMA kwa kuonyesha weledi wa kisiasa kwa kutoa maoni yao kuhusu muswada wa sheria ya uchaguzi. Safari hii ufipa wamejitahidi tofauti na wakati mwingine.

Hata kama sikubaliani na maoni yao yote ila nakubaliana na namna walivyojitahidi kupanga hoja zao.

Nawapongeza pia kutoruhusu kila kada wa Ufipa na kupost maoni kwenye social media hali inayofanya CHADEMA ionekane kama familia ya kambale kila mwanafamilia ana ndevu.

Imezoeleka huko UFIPA kila mtu ni msemaji wa chama. Pia nakipongeza ACT kwa kuwafundisha CHADEMA siasa za kisomi. ACT wao hutoa matamko yao kisomi na sio kila mwanachama kuropoka mitandaoni.

Maoni mengi sio mabaya kwa kutolewa na chama cha siasa kinachotaka kushika dola ingawa maoni mengi ni copy & paste toka kwenye rasimu ya Warioba. Mimi nimeshangazwa sana na hoja namba 5 inayosomeka hivi:

"Kuwe na wabunge wawili wa kuchaguliwa kwa kila Jimbo la uchaguzi, moja Mwanaume na Mmoja mwanamke ambao kila mmoja atachaguliwa kwa kura zake kwenye kundi analogombea".

Hii ni hoja ambayo haikutakiwa kutolewa na chama kinachojinadi kuguswa na mzigo wa kodi walio nao wananchi kugharamia uendeshaji wa serikali. Yaani kwenye hizi zama tunazotaka wabunge wapungue kutoka 393 hadi labda 100 wao CHADEMA ndo wanataka waongezeke wengine? inashangaza na kutia hasira mno.

Wabunge wa kuchaguliwa mwaka 2020 walikuwa 264 kwahiyo kwa hesabu za hovyo za Ufipa wanataka waongezeke wengine 264. Hoja yao hii ikipita tutakuwa na wabunge zaidi ya 528 kwenye bunge lijalo. INAKERA SANA kuwa na upinzani unaowaza jinsi gani waingie madarakani na kutafuna kodi za wananchi.

Ninashauri hoja za CHADEMA zisomwe kwa utulivu mkubwa kwasababu kuna hoja zina nia ovu kwa mwananchi mlipa kodi. Hoja zao zimejikita kushika dola zaidi bila kujali maumivu atakayopata mtanzania.

Pia wanaCCM na wazalendo tusichoke kukiadhibu hiki chama cha Mbowe kila fursa ya sanduku la kura inapojitokeza. Kuanzia ngazi ya kitongoji lazima tukiadhibu CHADEMA.
Nadhani wao hawakulenga kuwa na idadi kubwa zaidi ya wabunge, bali kutoa fursa sawa kwa wabunge wanaume na wanawake na huenda mantiki yao ni kwamba kura ziamue nani atakuwa mshindi na ikitokea (kama kuna huo muujiza) wakashinda wote wawili, sawa. Pendekezo hili halina maana kwamba majimbo ya uchaguzi hayawezi kupunguzwa ili tuwe na idadi ndogo ya wanaochaguliwa kama shida iko kwenye idadi ya wabunge watakaochaguliwa na Chadema siyo wanaoongeza hayo majimbo.
 
Acha ujanja wa Mbuzi kujambia mdomo. Ninauliza kama wewe una biashara ambayo unalipa Corporate tax? Kama huna kaa kimya.
Kwamba Kila mtanzania analazimika kulipa corporate Tax? Au umeishiwa na hoja Sasa unaanza kutumia mabavu hoja yako ipite?
 
Ni vipi kama wabunge watakuwa wengi kwa maana ya kuhudumia wananchi, kisha mishahara Yao ikapunguzwa zaidi ya nusu ya Sasa? Je wakipunguza posho za Sasa za wabunge, sambamba na kupunguza vikao vya bunge, huoni kama suala la gharama halitakiwepo. Tatizo ni hiyo kuongelea mapendekezo ya cdm, katika mtazamo wa kiccm.

Kwa taarifa yako huko uwanjani wachezaji huwa 11 Kila upande, lakini Kila team huwa na mbinu au mfumo wake wa kiuchezaji.
Magari na mafuta navyo hawatapewa?
 
Ni vipi kama wabunge watakuwa wengi kwa maana ya kuhudumia wananchi, kisha mishahara Yao ikapunguzwa zaidi ya nusu ya Sasa? Je wakipunguza posho za Sasa za wabunge, sambamba na kupunguza vikao vya bunge, huoni kama suala la gharama halitakiwepo. Tatizo ni hiyo kuongelea mapendekezo ya cdm, katika mtazamo wa kiccm.

Kwa taarifa yako huko uwanjani wachezaji huwa 11 Kila upande, lakini Kila team huwa na mbinu au mfumo wake wa kiuchezaji.
Naam zitapunguzwa kwa miezi kadhaa alafu kuongezwa maradufu baada ya miezi kadhaa..., Hata walivyoongeza hizi posho za sasa sidhani kama walikushirikisha wewe kama mwananchi ?

Duniani hizi Political Parties zimeshageuka kama platforms za watu kupata kura ili waende kura...,
 
Back
Top Bottom