Mgaa gaa upwa
Senior Member
- Jan 11, 2024
- 180
- 281
- Thread starter
-
- #81
Nashukuru Mimi dhamana yangu kuwa ajira yangu la sivyo sijui tungefikishana wapi.Ndugu yangu mkopo wa bank una walakini, hakuna aliyekopa akabaki salama
Jirani zangu hapa wengi na Watanzania wengi wameuzishwa nyumba zao kila mtu mtaani analaani
Huwezi Amin kwa muda uliobakia nawaza kuchukua maamuzi magumu itakapofika JanuaryPambania haki yako, asikutishe au yeye ndio anaiba
Hawa jamaa wananiudhi sana
Nilishatukana benk kwa wizi wao wa kutupa elfu 10 chini halafu wanasema zimepungua
Usiwape heshima kama wao wameshindwa kujiheshimu
Kwani sio halali hizo pesa?
Kuna bank za kiswahili kuweni nazo makini,bank za maana si zipo,kila siku tu bank inapewa lawama bado mnaing'angnia tu,aisee poleniPoleni na majukumu ya Kila siku.
Mwezi wa tano nilimfungulia biashara ya uwakala mke wangu, nikajenga duka na lilipokamilika nikawa nimebakiwa na fedha kidogo Kama mtaji, baada ya biashara kuanza nikaona Umuhimu wa kupanua biashara.
Nikawahi Benki ya NMB na kupata mkopo wa fedha kidogo ili kukuza biashara nilichukua kidogo ili kuendana na upepo.
Upepo ukakubali hivyo nikaamua kuongeza mkopo (top up).
Hilo lilikuwa kosa kubwa kwani Mara baada ya fedha za top up kuingia tu matatizo yakaanza..
1:-Akaunti yangu ikafungiwa na kiasi changu Cha fedha zangu za akiba, matumizi binafsi na mkopo wenyewe zikafungiwa.
2:- Nikaanza kukatwa mkopo Mara mbili yaani nakatwa mkopo wa Kwanza ule mdogo nilioulipa (kwenye top up) na mkopo wa pili (mkopo mkuu uliobeba Deni lote) nakatwa pia.
3:- Mkopo wa Kwanza haujafutwa (Maana nimeulipia kwenye top up)
Nimefuatilia Sana tatizo langu hapa tawini Hadi branch manager akanichukia na kuanza kunitisha kuwa atanishtaki kwa mkurugenzi ili nifukuzwe kazi.
Nikaamua kuingia kwenye emails (NMB makao makuu,huduma kwa wateja na BOT huduma kwa wateja) nikatembelea tawi la NMB mkoani Ila tatizo lipo pale pale.
Kuanzia mwezi wa Tisa Hadi mwezi wa kumi na mbili bado namekatwa makato zaidi na fedha zangu zimezuiliwa.
Msaada wanajf maana mwaka unaelekea ukingoni na Mimi sijatimiza adhima ya kumuwezesha mke.
Nitumie mbinu gani, watu gani na njia gani kuchukua pesa zangu.
Nimeweka ushahidi wa emails hapo chini.
Fata huu ushauri mkuu,washtaki hao !Pole kwa kukatwa mara mbili!
Nakushauri nenda mahakama ya kibiashara ukafungue madai yako!
Hakikisha una vielelezo vyako mhimu!
Shitaki na claim fidia na usumbufu wa hasara walizokuingizia!
Ukikosa wakili weka namba mawakili wazuri wapo waliobebea kwenye kesi kama hizo.
Ifahamike hata kucheleweshewa pesa kwa wakati ni kosa taasisi inatakiwa ishitakiwe!
Kama wao walivyo na haki yankukutoza riba ukichelewa na wao unaweza kuwashitaki kwa kukucheleweshea malipo!
Mimi maishani mwangu sitambui samahani! Nachojua ni kusudi na uzembe!
Tumia mwanasheria,watakulipa fidia na kila kitu haoHiyo ndiyo changamoto kubwa inayonikabil mbele yangu, sijui nitumie mbinu gani maana ya maridhiano Kama imefika ukingoni.
Ipo hivyiKwanza naomba kuuliza wakati unapewa mkopo wa top up, ulipewa hela yote uliyoomba au ulipewa balance baada ya kufuta mkopo wa awali.
(i) Kama ulipewa hela zote ulizoomba kwenye mkopo wa pili maana yake mkopo wa kwanza haukufutwa hivyo benki wako sahihi kukukata mikopo yote 2 unless urudishe hela zilizotakiwa kufuta mkopo wa kwanza
(ii) Kama ulipewa balance baada ya kukata hela za kufuta mkopo wa kwanza then benki wamekosea kuendelea kukukata mkopo wa kwanza ambao ulishakatwa hela kuulipa na hivyo wewe una haki
Yaan pesa zako wao wanajichukulia tu, alafu ukienda kuomba waache kuzichukua wanakutishia kukufukuza kazi, na wewe hujui ufanye nini?Uliza chochote kuhusu taarifa hii kinacho kutia Shaka nitakujibu.
Umeona jinsi nchi hii ilipotufikisha?, Na huyu Ni mtumishi wa umma, vipi kwa mwananchi wa kawaida?Yaan pesa zako wao wanajichukulia tu, alafu ukienda kuomba waache kuzichukua wanakutishia kukufukuza kazi, na wewe hujui ufanye nini?
Afisa utumishi aliishasema wamuone awasaidie Nini Cha kufanya Ila wao wakajifanya Ukuaji, maana Hadi alirejea Benki ya CRDB napo walikutana na changamoto Kama yangu ikatatuliwa Ila wao wakajifanya wajuaji.Wakati wa top up ilitakiwa deni liwekwe pamoja.
Kufikia kufungiwa account ni kuwa hakuna kitu unachoweka kwenye account yako, hivyo wanai hold kiknachoingia kinamezwa.
NMB walitakiwa wakuite kupitia mwajiri wako ili mrekebishe hilo.
Sasa hilo la kumfungulia mke wangu biashara ujiweke sawa, hakuna mia atakayolipia deni.
Itaje Benki ya maanaKuna bank za kiswahili kuweni nazo makini,bank za maana si zipo,kila siku tu bank inapewa lawama bado mnaing'angnia tu,aisee poleni
NMB wengi hawana customer care language.Afisa utumishi aliishasema wamuone awasaidie Nini Cha kufanya Ila wao wakajifanya Ukuaji, maana Hadi alirejea Benki ya CRDB napo walikutana na changamoto Kama yangu ikatatuliwa Ila wao wakajifanya wajuaji.
Tena ulitaka Benki nyingine wanakua wakali mno, kwamba nawafundisha kazi.
Bado haujakua, ukikua utaelewa.Kuna uzi huzielewi...
Ukisoma comments ndo unachanganyikiwa kabsaa...
๐๐
๐ฎ๐ฎ
Ntakuwa nawapigia promo za bureItaje Benki ya maana
Kwa taarifa yako, ndani ya Tanzania yetu hii na chini ya BOT hakuna Benki ya maana.Ntakuwa nawapigia promo za bure
Asante
Hakuna cha taasisi kubwa kwenye swala la hakiIla kumbuka napambana na taasisi kubwa inayopitisha mishahara asilimia kubwa ya watumishi wa serikali.
Yani wewe hueleweki,hata kusiidiwa ni ngumu sana.Ipo hivyi
Walikuwa wananidai Milioni mbili na nikaongeza Deni la Milioni Saba jumla Milioni Tisa.
Hivyo Basi kwenye Deni jipya nikaandikiwa Milioni 9 na nikapewa Milioni 7 cash Ila wakati pesa zinaingia akaunti ikafungiwa na pesa sikuzipokea mkononi na salio lilokuwepo kwenye akaunti pia likajumlishwa na mkopo huo kufungiwa.
2:- Mkopo wa awali kwenye ESS haujatolewa na huku kwenye makato mapya ya mkopo wa Milioni Tisa wanakata pia......Aiseeeeh