Nini Hatma ya MCC na AGOA baada ya Trump kuwa Rais wa Marekani?

Nini Hatma ya MCC na AGOA baada ya Trump kuwa Rais wa Marekani?

Naona mmeanza kulialia kabla ajaapishwa.

Operation ya kwanza ni kwa wale wote waliojibakisha madarakani kwa nguvu ya Dola.

Mimi nadhani tujiulize hivi....
NINI HATMA YA VISIWANI BAADA YA UJIO WA TRUMP?"
Swali zito sana hilo
 
Msiwe na haraka.tumuombe mungu tu.atupe uzima.tuisome namba ya trump.
 
AGOA na MCC ni nyenzo mbili kuu zinazotumiwa na Marekani katika kuzisaidia nchi za Afrika kukabiliana na changamoto za ndani ya nchi ikiwa ni pamoja na masuala ya kiuchumi, kisiasa na hata utamaduni. Kupitia AGOA na MCC, nchi nyingi za Afrika zimenufaika kupitia miradi mingi ya maendeleo na kijamii kwa njia ya msaada na mikopo ya masharti nafuu.

Niwaulize wabobezi wa masuala ya siasa za Marekani, je Ujio wa Trump utaathiri vipi AGOA na MCC hasa ikizingatiwa matamshi aliyotoa hapo awali juu ya Afrika na watu wake?
nchi hii ni tajiri.wasiwasi wa nin liz
 
Liz naona unajitekenya na kucheka kwa nini umeuliza if kweli halituhusu.Naipenda sana ile nyimbo yenu mliforecast mambo mengi mno.
lizaboni kaleta huu uzi,lakini umegeuka kaa la moto kwake,kawa kama kuku aliyekatwa kichwa
 
ule mchezo wakuongilia mikataba ya wawekezaji wa marekani kwa gia eti uzalendo umetukolea sasa umefikia mwisho.

yale magwangala ya geita,mchanga wa buzwagi......

the man is a businessperson anajua maana ya mkataba
Vipi atawasaidia na chadema pia kuingia madarakani ama vipi?
 
AGOA na MCC ni nyenzo mbili kuu zinazotumiwa na Marekani katika kuzisaidia nchi za Afrika kukabiliana na changamoto za ndani ya nchi ikiwa ni pamoja na masuala ya kiuchumi, kisiasa na hata utamaduni. Kupitia AGOA na MCC, nchi nyingi za Afrika zimenufaika kupitia miradi mingi ya maendeleo na kijamii kwa njia ya msaada na mikopo ya masharti nafuu.

Niwaulize wabobezi wa masuala ya siasa za Marekani, je Ujio wa Trump utaathiri vipi AGOA na MCC hasa ikizingatiwa matamshi aliyotoa hapo awali juu ya Afrika na watu wake?
Nadhani kutakuwa na uhakiki wa wanaonufaika na Agoa. Nyepesi nyepesi kunà vitu vinavyotengenezwa na wachina vinanufaika.
 
M
Hizo hela za MCC waliinyima Tanzania baada ya kuchakachua uchaguzi wa Zanzibar.

Trump ni simba aliyejeruhiwa,alikuwa anaongelea uchakachuaji wa uchaguzi Marekani,na akaonya wasimchakachue.

Najua briefing kubwa atakayoipata kuhusu afrika mashariki,baada ya al shaabab,mafaili ambayo yatamchukiza sana ni la zanzibar,nkurunzinza,na baadae CongoDR.

Hayo yako mezani kwake kabisa tayari kwa hat
Mnavyomuabudu sasa, ptuuuu!!
 
Sidhani kama ni pigo maana Rais wetu alishajiandaa mapema kisaikolojia.
Na utashangaa atatengeneza partnership naye maana ni reliable na atapunguza costs za investments zao...Mafisadi wajiandaye mikataba kuwa reviewed...
Ninajiandaa kwa winwin negotiation na huyo mteule...We mean business hatuwezi kuwa watazamaji tu duniani...
 
Halafu huyo Jamaa Muamerikano Nikimwangalia Sana, Maamuzi yake Anafanana Na Mze, hapendi Ujinga Kabisa, Nadhani na yeye Ni Mchaka Mchaka wa Kazi tu.
Yeye siye kazi tu! Hakuna Raisi mwenye akili anaweza kusema watu wafanye kazi tu. Yy anataka to Make America great again. Watu wengi wanafanya kazi tu, lakni maisha hayabadidiki. We need to be more strategic
 
AGOA na MCC ni nyenzo mbili kuu zinazotumiwa na Marekani katika kuzisaidia nchi za Afrika kukabiliana na changamoto za ndani ya nchi ikiwa ni pamoja na masuala ya kiuchumi, kisiasa na hata utamaduni. Kupitia AGOA na MCC, nchi nyingi za Afrika zimenufaika kupitia miradi mingi ya maendeleo na kijamii kwa njia ya msaada na mikopo ya masharti nafuu.

Niwaulize wabobezi wa masuala ya siasa za Marekani, je Ujio wa Trump utaathiri vipi AGOA na MCC hasa ikizingatiwa matamshi aliyotoa hapo awali juu ya Afrika na watu wake?
Sahau hata salamu au hisani toaka marekani. Nakukumbusha Richmond baadae Dowans ni ya familia ya Clinton. JK amelishwa limbwata la ufeemason ya akina Clinton nchi itayumba hadi CCM iondoke madarakani,

Hamna mpango wa kujirekebisha na ufisadi wa kisiasa na ukandamizaji wa kidemokrasia wa chama chenu dola ccm, hakuna atayekuwa na mpango na ninyi.

USAID watafanya policy review ya misaada kwa nchi zinayo sustain udikteta hasa Tanzania na kupunguza au kufuta kabisa fungu hilo.

Hospitali ya akina mama Arusha ilikuwa inafadhiliwa na Gates foundation mmeihujumu kupitia Gambo tarajieni mrejesho.

Uchumi mlioamumua kuunyea kwa kukurupuka kwenu tarajieni kuzikwa kabisa. Na kwa vile uchwara ana allegy ya diplomasia uhusiano na Marekani na Tanzania ni bye bye maana amediriki kushikamana na magaidi wa Morroco wanayoitesa Marekani.

Kafungua ubalozi wa Israel ina maana yanaowapata wapalestina Tanzania imejitoa tusubiri shubiri ya wapigania haki kimataifa.

Naamini serikali ya Trump ina mikakati chungu kwa dikteta uchwara.
 
AGOA na MCC ni nyenzo mbili kuu zinazotumiwa na Marekani katika kuzisaidia nchi za Afrika kukabiliana na changamoto za ndani ya nchi ikiwa ni pamoja na masuala ya kiuchumi, kisiasa na hata utamaduni. Kupitia AGOA na MCC, nchi nyingi za Afrika zimenufaika kupitia miradi mingi ya maendeleo na kijamii kwa njia ya msaada na mikopo ya masharti nafuu.

Niwaulize wabobezi wa masuala ya siasa za Marekani, je Ujio wa Trump utaathiri vipi AGOA na MCC hasa ikizingatiwa matamshi aliyotoa hapo awali juu ya Afrika na watu wake?
MCC hujui kuwa imeshakuwa suspended kwa sababu ya wizi wa kura Zanzibar na ile sheria ya makosa ya kimtandao?
 
Pamoja ya gagari zote za Trump,sioni mabadiliko yoyte katika sera ya nje ya marekani.Trump ni kama Magufuli ameahidi kujenga na kuimarisha miundombinu ya nchi na kuongeza ajira

Hayo mambo ya utemi ni kawaida kwa kila Rais,lazima akaue tushazoea
 
Back
Top Bottom