Nini kifanyike ili kiongozi asipendelee kwao kama Hayati Dkt. Magufuli alivyoipendelea Chato?

Nini kifanyike ili kiongozi asipendelee kwao kama Hayati Dkt. Magufuli alivyoipendelea Chato?

Ugatuzi wa madaraka. Magufuli alikuwa anafanya kazi iliyokuwa ifanywe na local government institutions, ila tu yeye alipendelea eneo/wilaya moja. Kungekuwa na serikali za mitaa/mikoa ambazo ziko huru kujiamulia mambo yake na kutekeleza mipango yake mwenyewe, Magufuli asingekuwa na haja ya kufanya aliyoyafanya.

Ugatuzi wa madaraka unasaidia kukuza na kukomaza demokrasia, kugawanya na kupunguzia majukumu central government, na kusogeza maendeleo na huduma kwa wananchi, kwasababu wao ndo wanajua nini hasa wanataka kwenye maeneo wanayoishi.

Serikali iko too centralized, ndo maana hata unakuta ili kujenga zahanati, madarasa, barabara za mitaa, hata choo tu, lazima idhini itoke serikali kuu. Wakati hizo kazi na zingine nyingi zingeweza kufanyika na serikali na serikali za mitaa/mikoa.

Ni vile CCM wana-allergy na kushare madaraka kwa mfumo wa aina wowote ule ndo maana ukiwaambia waziimarishe na kuziacha huru serikali za mitaa, na kuanzisha utawala wa majimbo, wanapinga kwa nguvu zote. Wakati ni faida kwa wote.
Hii ni nzuri sana. Serikali kuu inashughulika na miradi na mambo ya kitaifa yaliyopitishwa na bunge tu. Hili suala lingekuwa na faida sana kwa nchi na kuharakisha maendeleo. Bahati mbaya, kama ulivyosema kuna watu mfumo huu unawafaidisha, hawawezi kubadilika hata kama gharama ni maendeleo ya nchi.
 
Zanzibar kujengwa hotel za kitalii za bilions of dollar, kiwete kipindi anapendelea pwani kwenye uwekezaji wa viwanda pamoja na mashule hamkuona? Acheni ngebe
Inaonekana ni ugonjwa wa siku nyingi. Membe alipokuwa wizara ya maji, alipelekaga karibu bajeti nzima ya maji kwao, watu walipiga mno kelele.

Mifano kama hii ni mingi, unafikiri ni coincidence kwa maduka ya MSD kuanzishwa Chato na Ruangwa? Kumekuwa na utaratibu kuwa mkipata Rais au Waziri basi mmeula, maana mnajua atapendelea kwenu. Ndiyo tunajadili tiba ya hilo.
 
Ninyi mliopewa madaraka sasa hivi chuki zenu ambazo mnashindwa kuzidhibiti zitawatokea puani huko mbeleni. Ofisi ya Tanesco inayojengwa ni ya kwake binafsi au kwa matumizi ya umma? Bajeti ya fedha hizo aliidhinisha nani wakati viongozi wasimamizi wake walikuwepo na bado wako madarakani? Mnataka kuonesha chuki zenu dhidi ya JPM kwa kuonesha ni kwa jinsi gani watu wanatakiwa wahudumiwe? Mradi kama huo haupo mahali pengine Tanzania? Kwanini mnaendelea kumzonga mtu asiyekuwepo kujitetea na mnatishia kushitaki wasaidizi wake?

Anzeni kwanza na walioko juu kwa sasa kwa sababu ndio walishiriki moja kwa moja kuidhinisha mradi kama huo.

Chato ni sehemu ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kama ilivyo Kizimkazi, Kiwengwa, Mkokotoni nk

Mbona Msoga kuna makazi ya rais mstaafu yenye hadhi ya Ikulu ikiwa na hospitali kubwa ambayo hata Chalinze hawana lakini hakuna kinachosemwa?

Ifike pahala chuki hizi zikome mara moja kwa sababu mnatengeneza VISASI ambavyo havitakoma. Msijidai kwamba mtabaki madarakani, mnasubiriwa chini ili muadabishwe vizuri.

Mnaachia wezi mnafungulia mashitaki feki watu wasio na hatia kwa sababu ya chuki zilizokubuhu, inda na nongwa zinazonuka uvundo wa uharifu ndani yake.

Kumbe wakati JPM analalamika hujuma kufanyika ninyi ndio mnaziongoza kwa kuzipitia kwa wapinzania ambao kimsingi hawakuwa na nia ya kukwamisha maendeleo.

Achaneni na kesi feki ya Mbowe na Sabaya ili kurejesha mstakbali huko mbeleni
Mkuu miradi mingi ya Chato haikujadiliwa kabisa bungeni. Ni kama Rais mwenyewe aliamua kuitekeleza. Na si Magufuli tu. Huu utaratibu wa Marais kupendelea kwao upo siku nyingi, sema tu Magufuli aliupeleka next level, hadi uvumilivu wa watu ukavunjika.
 
Ni wazi kuwa rais Magufuli aliipendelea sana wilaya ya Chato katika kupeleka maendeleo. Alijenga uwanja wa ndege wa kimataifa, alijenga hospitali kubwa ya rufaa ya kanda, alijenga chuo cha Veta, alianza kujenga hoteli ya nyota tatu, mipango ya kujenga uwanja wa mpira. Na mambo mengine mengi sana.

Haya mambo hayakuanza na Rais Magufuli, ni vile tu yeye aliyafanya kwa kiwango cha kushangaza.

Sasa siku nyingine atatokea kiongozi atafanya zaidi ya Magufuli alivyofanya. Nini kifanyike ili kuzuia Rais au kiongozi yoyote asiweze kufanya kitu kama hicho?
Hakuna cha kufanya mkuu,hata wewe mwenye vihela vyako mbuzi huwezi kuacha kujenga kwenu,sembuse Rais...
 
Ni wazi kuwa rais Magufuli aliipendelea sana wilaya ya Chato katika kupeleka maendeleo. Alijenga uwanja wa ndege wa kimataifa, alijenga hospitali kubwa ya rufaa ya kanda, alijenga chuo cha Veta, alianza kujenga hoteli ya nyota tatu, mipango ya kujenga uwanja wa mpira. Na mambo mengine mengi sana.

Haya mambo hayakuanza na Rais Magufuli, ni vile tu yeye aliyafanya kwa kiwango cha kushangaza.

Sasa siku nyingine atatokea kiongozi atafanya zaidi ya Magufuli alivyofanya. Nini kifanyike ili kuzuia Rais au kiongozi yoyote asiweze kufanya kitu kama hicho?
Sema nini kifanyike kiongozi mzalendo kama Dkt Magufuli asije kuuawa? Maana furaha yenu ya kumuua Dkt Magufuli sasa hamfichi, mnajiachia kama vile watanzania ni vilaza hawajui, just wait 2025!
 
Ni wazi kuwa rais Magufuli aliipendelea sana wilaya ya Chato katika kupeleka maendeleo. Alijenga uwanja wa ndege wa kimataifa, alijenga hospitali kubwa ya rufaa ya kanda, alijenga chuo cha Veta, alianza kujenga hoteli ya nyota tatu, mipango ya kujenga uwanja wa mpira. Na mambo mengine mengi sana.

Haya mambo hayakuanza na Rais Magufuli, ni vile tu yeye aliyafanya kwa kiwango cha kushangaza.

Sasa siku nyingine atatokea kiongozi atafanya zaidi ya Magufuli alivyofanya. Nini kifanyike ili kuzuia Rais au kiongozi yoyote asiweze kufanya kitu kama hicho?

Katiba mpya.
 
Acheni Nongwa na Uswahili Kiongozi asipopendelea Kwao apendelee wapi? Kupendelea Kwao ni Dhambi?

Hivi siyo nyie nyie ambao leo mnamcheka Hayati Nyerere kuwa hakupajenga Kwao Butiama?

Watanzania tuna PhD's nzuri za Unafiki.
Kwani chato kuna nn cha ajabu ambacho unaweza sema alipendelea?
 
Kwa katiba hii hata aje nani mambo yatakuwa yale yale tu maana katiba ina mpa nguvu nyingi sana kiongozi na hapo hapo inampa hakikisho la ulinzi(kutoshtakiwa).kwa katiba hii kukitoa chama tawala madarakani ni ngumu sana,labda tuombe msaada wa jeshi kukitoa chama tawala.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwa katiba hii hakuna wa kumgusa Rais. Rais wa Tanzania ni mtu mkubwa mno baada ya Muumba mbingu na nchi. ushahdi huo upo waziwazi.

Ili kuepusha chochoko zote hizo watanzania wanatakiwa kwa mara ya kwanza kupewa katiba yao waliyoiandika kupitia kwa Tume ya Jaji Warioba.
 
Sema nini kifanyike kiongozi mzalendo kama Dkt Magufuli asije kuuawa? Maana furaha yenu ya kumuua Dkt Magufuli sasa hamfichi, mnajiachia kama vile watanzania ni vilaza hawajui, just wait 2025!
Kwa hatua aliyofikia ilibidi tu watu watengeneze mipango ya kifo maana alitaka kutawala milele

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna cha kufanya mkuu,hata wewe mwenye vihela vyako mbuzi huwezi kuacha kujenga kwenu,sembuse Rais...
Rais pesa siyo zake. Mimi nikitaka kujenga kwetu ni pesa zangu.
 
Ni wazi kuwa rais Magufuli aliipendelea sana wilaya ya Chato katika kupeleka maendeleo. Alijenga uwanja wa ndege wa kimataifa, alijenga hospitali kubwa ya rufaa ya kanda, alijenga chuo cha Veta, alianza kujenga hoteli ya nyota tatu, mipango ya kujenga uwanja wa mpira. Na mambo mengine mengi sana.

Haya mambo hayakuanza na Rais Magufuli, ni vile tu yeye aliyafanya kwa kiwango cha kushangaza.

Sasa siku nyingine atatokea kiongozi atafanya zaidi ya Magufuli alivyofanya. Nini kifanyike ili kuzuia Rais au kiongozi yoyote asiweze kufanya kitu kama hicho?
Wewe ni mpumbavu kwelikweli,huyu mzee hakika alikuwa mwamba Tanzania Africa na duniani
 
Inaonekana ni ugonjwa wa siku nyingi. Membe alipokuwa wizara ya maji, alipelekaga karibu bajeti nzima ya maji kwao, watu walipiga mno kelele.

Mifano kama hii ni mingi, unafikiri ni coincidence kwa maduka ya MSD kuanzishwa Chato na Ruangwa? Kumekuwa na utaratibu kuwa mkipata Rais au Waziri basi mmeula, maana mnajua atapendelea kwenu. Ndiyo tunajadili tiba ya hilo.
Hii nchi huwa inaongozwa na vichaa na hawana uzalendo wa kweli maeneo potential yanaachwa kwasababu ya chuki wakikimbilia kuwekeza sehemu ambazo hazichangii kwa chochote kwenye pato la taifa tunapoelekea kutakuwa na matigray mengi hapa nchini.
 
Mkuu miradi mingi ya Chato haikujadiliwa kabisa bungeni. Ni kama Rais mwenyewe aliamua kuitekeleza. Na si Magufuli tu. Huu utaratibu wa Marais kupendelea kwao upo siku nyingi, sema tu Magufuli aliupeleka next level, hadi uvumilivu wa watu ukavunjika.
Hapana tembelea Msoga uone maajabu yaliyopo pale hutarudia kusemea wengine ovyo

Maraisi wengine walipendelea kuishi mijini hasa DSM na kutelekelza walikotokea, kwahiyo hilo ni takwa la wananchi sio rais kama mtu binafsi.

Mbona ujenzi huo upo maeneo yote.

Mtwara kuna soko la kisasa pale Chuno karibu na kituo cha mabasi ya mikoani lakini wafanyabiashara ni kama wamegoma kuhamia sokoni huko
 
Ni katiba mpya, kuwajibisha viongozi wakikiuka katiba na pia kupatikana bunge lenye wabunge waliochaguliwa na wananchi kidemokrasia ili wawe na uwezo wa kuidhibiti serikali.
 
Back
Top Bottom