Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Impongo,
Usinikumbushe.

Wanasema haujapata kutokea mnakasha kama ule.
Ulidumu miezi 6.

Abdul Sykes mzalendo mwana TANU kadi np 3.
Baba yake muasisi wa African Association 1929.

Abdul Sykes aliyeona ofisi ya African Association ikijengwa yeye ana umri wa miaka 5.
Abdul Sykes mfadhili wa TAA na TANU rafiki ya Nyerere na mwenyeji wake Dar es Salaam.

Abdul Sykes aliyekuwa Katibu toka 1950 na 1951 akawa Katibu na Kaimu Rais.
Abdul Sykes aliyegombea nafasi ya urais wa TAA na Nyerere mwaka wa 1953.

Chuo Cha CCM Kivukoni wanakataa kupokea ''notes'' za historia ya TANU zilizoletwa na mwanajopo wa uandishi wa historia ya TANU Hassan Upeka.

Mwenyekiti wa jopo Dr. Mayanja Kiwanuka anasema historia inayoandikwa ya TANU haimuhusu Abdul Sykes.
JF bila khiyana wananipa ukumbi nimzungumze Abdul Sykes kwa miezi 6 bila kupumzika.

Nilikuwa kila nikiandika namuona baba yangu Abdul Sykes anazungumza na mimi kutoka kaburini.

Impongo ndugu yangu usinikumbushe mnakasha ule.
Chuo cha pale kivukoni hakiwezi kupokea Mashudu na Uongo ulioandikwa na Wavaa vipedo na kobasi
 
Hadithi za kale hizi hazina maana yoyote.

Watu wanahitaji maji safi, makazi bora, chakula, ajira, elimu safi, miundombinu na huduma zote muhimu!

Mambo ya Tanu sijui abdul sykes yananisaidia nini mimi?
Huyu Mzee sijui nani alimlaani mpaka kuandika Mashudu na Uongo humu jamvini
 
May Day,
Ikiwa unataka mimi nifanye mjadala kwa namna utakavyo wewe utanipa shida.
Moja ya namna yangu ya mjadala ni kukwepa ubishi kwani ubishi hauongezi elimu wala kusomesha.

Nimefurahi sana umeniwekea historia ya Wachagga.

Hivi sasa naandika kitabu cha Rajab Ibrahim Kirama (1843 -1962) naamini hili jina hujapata kulisikia katika historia ya Wachagga.

Huyu ndiye aliyeingiaza Uislam Uchaggani na historia ya ukoo huu wake wa Njau kama Majemadari wa Vita inarudi nyuma miaka 300 na imehifadhiwa kwa kumbukumbu za kichwa na kwa ushahidi wa nyaraka zinazokwenda nyuma kiasi cha miaka 100.

Sasa kwa kuwa unasema sina jipya naona nikupe kitu kipya na ni katika haya haya tunayojadili hapa.

Nakuunga mkono katika historia ya Mangi Meli na nakuonyesha kitu kutoka kitabu ninachoandika.
Nimempa Mangi Meli jina kwa utanashati wake na jinsi alivyojaliwa sura jamili.

Nimempa jina ''Handsome Boy.''

Hivi nahangaika kutafuta jina kama hili kwa Kichagga.

Karibu:

''Mwaka wa 1890 Herman von Wissman baada ya kumaliza vita na Abushiri na kumnyonga alielekeza jeshi lake kaskazini na akamshambulia Mangi Sina katika vita vikali ambavyo jeshi la Sina lilionyesha uhodari mkubwa wa mapambano.

Vita hivi vilinyanyua haiba ya Sina na Wajerumani wakanyoosha mkono wa urafiki na huo ndiyo ukawa mwisho wa uhasama baina ya Mangi Sina na Wajerumani.

Juu ya haya Rindi aliungana na Hermann von Wissman dhidi ya Sina na na hii ikapelekea kwa Sina kushindwa vita mwaka wa 1891.

Fitna na usaliti ukawa sasa ni moja ya silaha zilizowapa Wajerumani ushindi.

Sina alifariki mwaka wa 1899 akiwa kaacha sifa ya ushujaa wa vita mbele ya Wajerumani kwani peke yao hawakuweza kumshinda hadi ulipopitika usaliti dhidi yake.

Kunyongwa kwa Mangi Meli Old Moshi mwaka wa 1900 pengine yeye Muro Mboyo akiwa shahidi wa mauaji yale ulikuwa ujumbe tosha kuwa nyakati zimebadika.

Meli kama ilivyokuwa kwa Abushiri na yeye alisalitiwa pia na wale aliokuwa akiwapigania.

Kadhalika kama ilivyokuwa kwa Abushiri kuwa adui wa kweli hakuwa Mjerumani peke yake bali pia nduguze katika ukanda wote wa pwani ambao walikuwa tayari kujiuza kwa Wajerumani.

Haikuwa tabu sana pia kwa baadhi ya watawala wa Uchagani kutambua kuwa adui wa kweli pia hakuwa mtawala jirani yake aliye Kibosho au Machame chini ya Mlima Kilimanjaro bali Mjerumani kutoka mbali.

Hali hii ilikuwa na manufaa makubwa kwa Wajerumani.

Lakini usaliti huu haukuwa uko katika siasa za Wachagga peke yao kwa watawala kufitiana na kusalitiana.

Wajerunani na wao waliucheza mchezo huu kwa mafanikio makubwa kwa kuwaghilibu askari wa Kinubi kutoka Sudan na Wazulu waliowachukua kutoka kijiji kinachojulikana kama Kwa Likunyi, Imhambane Mozambique.

Wissmann alipofika katika kijiji hiki alifanya mazungunguzo na Chifu Shangaan kiongozi wa Wazulu waliokimbia vita vya Chaka na kuingia Mozambique kutafuta hifadhi.

Mkataba alioweka Wissmann na Chifu Shangaan ambae baada ya kufika Tanganyika akajulikana kwa jina la Affande Plantan ilikuwa baada ya kushinda vita Wajerumani na Wazulu wataitawala Tanganyika kwa pamoja.

Jeshi hili la mamluki chini ya Wissmann walipigana dhidi ya Waafrika wenzao kwa tamaa kuwa na wao watakuja kuwa watawala kama Wajerumani baada ya ushindi.

Lakini baada ya Ujermani kushinda vita vyake na kuanza kutawala kwa utulivu hawakutimiza ahadi waliyoweka ingawa walirejesha hisani kwa kuunda jeshi waliloliita Germany Constabulary na mkuu wa jeshi hili alikuwa Affande Plantan.

Hili jeshi liliwekwa ndani ya kambi Dar es Salaam hadi mwaka wa 1918 baada ya Ujerumani kushindwa katika Vita Vya Kwanza Vya Dunia huu ndiyo ukawa mwisho wa jeshi hili Tanganyika.

Wakati wa utawala wao Wajerumani walijenga shule na wakawasomesha watoto wa hawa askari kwa kiwango ambacho watoto wa raia wa kawaida hawakukipata na baada ya kumaliza shule darasa la sita walitoka shule wakiwa wanakisema Kijerumani vizuri na wakiwa na ujuzi mbalimbali na wengi wao waliingizwa jeshini kama askari katika Germany Constabulary.''

(Shule hizi za Wajerumani iliyojengwa Dar es Salaam na shule nyingine zilizojengwa kwengineko huko bara na wamishionari ndizo zilizokuja kuwatoa Waafrika ambao waliacha alama katika historia ya Tanganyika watu kama Joseph Merinyo, Paul Njau kutoka Kilimanjaro, Kleist Sykes, Schneider Plantan, Mashado Plantan kutoka Dar es Salaam, Martin Kayamba kutoka Tanga na wengine wengi ambao walikuja kuutumikia utawala wa Mfalme George wakati wa utawala wa Waingereza na ghilba waliyofanyiwa baba zao na Wissmann ni sehemu ya historia ya wazazi wao.

Hii leo haya ni sehemu ya simuliza katika historia ya Tanganyika vipi wazee wao walifika Tanganyika zaidi ya miaka 100 iliyopita na kuwa sehemu ya utawala wa kikoloni na pia baadae kuwa sehemu ya msingi ya kudai uhuru wa Tanganyika).

Tanbihi: Muro Mboyo ndiye baba yake Rajab Ibrahim Kirama.

View attachment 1526065
Unalazimisha kupost mada ulizojitungia na kupost picha mlizoedit wenyewe huko misikitini.
 
Unalazimisha kupost mada ulizojitungia na kupost picha mlizoedit wenyewe huko misikitini.
Azarel, mambo ni hivi...babu zake huyo Abdulwahid Sykes walikuwa ni miongoni wa askari wa kukodi walioletwa kutoka sehemu mbali mbali ulimwenguni na wakoloni wa Kijerumani kuja kudumisha himaya yao Tanganyika. Nyakati hizo wakoloni kutoka nchi mbali mbali za Ulaya walikuwa katika vita vyao vya kunyang'anyana ardhi ya babu zetu katika vita vya wao kwa wao.

Awali hao babu zake Abdulwahid Sykes walipigana upande wa Wajerumani lakini Wajerumani waliposhindwa wengi wa hawa mamluki walirudi walikotoka sehemu mbali mbali Afrika. Hata hivyo wapo wachache, pamoja na babu zake Abdulwahid Sykes, walioamua kulowea kwenye ardhi yetu ya Tanganyika na kujiunga na jeshi la Malkia wa Uingereza.

Kama ilivyotokea kwa babu zake, Abdulwahid Sykes naye alikuja kujiunga na askari wa Kiingereza na hivyo akapelekwa Burma kuwasaidia Waingereza nao kudumisha himaya yao huko. Vita ilipokwisha, tofauti na babu zake, yeye hakubaki nchini Burma kama walivyofanya bali yeye aliamua kurudi nchini Tanganyika ambako babu zake wamelowea.

Hebu tufikirie kama angebaki Burma na kuamua kulowea huko, je ingekuwa halali kwake kudai kutambuliwa nchini Burma kama mpigania uhuru wa Burma kama Mohamed Said anavyodai kwa Tanganyika? Hiyo hali ingekuwa na tofauti gani na Makaburu, wale walowezi wa Afrika Kusini kudai walikuwa ndio wapigania uhuru wa Afrika Kusini?

Hizi ngano za Mohamed Said tulizimaliza katika thread hii hapa chini na zingine nyingi lakini kila baada ya muda anakuja na madai yale yale, santuri zile zile, ngano zile zile na hadithi zile zile. Kwaherini ndugu zangu na Mkuu Nguruvi3 samahani sana, sikutaka kuchangia humu kabisa ila nililazimika baada ya wewe kunitag. Usiku mwema!

Swali...Kwa nini anataka hawa Wazulu ndio watambulike kama mashujaa wa kupigania uhuru wa Watanganyika na si wazawa ambao walikuwepo?

Bonyeza hapa...

 
"
Mohamed Said, post: 36218778, member: 12431"]
Hili la katiba huwa kila nikisoma si kwako tu hata katika Wasifu wa Julius Nyerere hujiambia Mwingereza atapitisha katiba gani ya maana kwa chama cha Waafrika.
Ni hawa Waingereza ambao chini ya governor , kama sitakosea DC Cameron walichangia ujenzi wa ofisi(Narudia kama kumbu kumbu zangu zipo sawa)

Lakini pia ni kweli ilikuwa ngumu kwa Waingereza kwasababu chama kilikuwa cha Ukoo wa Sykes na kilijieneza maeno ya Tandamti, Kidongo chekundu. Hakuna shaka Mwingereza hakuona tishio lolote.
Yote haya yanatokana na ukweli kuwa mbinu, weledi na elimu havikuipa nafasi familia ya Sykes kujipambanua.
Wengi hawajui kuwa hata hiyo TANU katiba yake ilinakiliwa kutoka katiba ya Convention People's Party (CPP)ya Kwame Nkrumah...Earle Seaton huyo.Na hii katiba si kama ilimsubiri Nyerere afike ndiyo itafutwe.
Lakini kinachonifariji ni kuwa Abdul Sykes aliyefutwa katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika leo karudi anazungumzwa.
Ni kweli kuwa katiba nyingi si ya TANU tu bali za nchi zinazoendelea ni matokeo ya kusoma na hata kunakili katiba za mataifa yaliyotangulia kama Marekani n.k. Hakuna ubaya katika hilo.

Hoja iliyopo hapa ni ile inayoshadidiwa na msemo kuwa ''the end justifies the means''.
Hivyo kama Nyerere alinakili, si hoja tena. Hoja ni TANU ilipata katiba baada ya ujio wake kama muongozo.

Sioni mahali ambapo Kleist Sykes au Abdul Sykes walijaribu hata kunakili katiba.
Kuanzia 1929 hadi 1953 trakribani miaka 24 ya Tawala za Familia ya Sykes, hakuna nyaraka iliyoitwa katiba.

Kuna hoja ya Earle Seaton, hapa tunarudi kule kule ipo wapi draft ya hiyo katiba na upi ni ushiriki wa Abdul Sykes katika kufanikisha hilo? Well, kama hiyo ya Seaton ndiyo ile ya Nyerere ambayo iligeuka kuwa muongozo wa chama bado credit ni za Nyerere. Hivyo katiba ya kwanza ya TANU ilipataikana chini ya Mwl Nyerere, period.

Kuhusu Abdul kuzungumzwa, nadhani unashindwa kuangalia kwa kina.
Ni kweli anazungumzwa leo kuliko huko nyuma na historia inamtendea haki kama ambavyo inamtendea haki kwa kuonyesha udhaifu na madhaifu yake na Baba yake.

Hivyo kwa siasa za Tanganyika, ukiachilia mbali kazi za Umamluki wa Jeshi la Ujerumani kama alivyobainisha Mag3 hapo juu, na ukiachilia hoja kwamba Abdul Sykes aliwafumusha wazee wake kwa makonde ili kurudisha utawala wa Sykes, na ukiachilia kumhifadhi Nyerere, kisiasa hakuwa na jipya au la maana na alifutika haraka kisiasa kwasababu hiyo, alikuwa overrated tu .

Lakini pia Abdul anazungumzwa kwasababu jina lake linatumika kutaka '' kumpa Nyerere jina baya''
Kwamba huwezi kumdunisha Nyerere bila kumtaja Abdul, si kwamba Abdul analingana na Nyerere kwa sifa, la hasha, bali anatumiwa tu kumdhalilisha Nyerere kama tunavyoona Nyerere akielezwa kupikiwa mayai kwa Abdul
 
Kama mtu hajaelewa ulichoandika hapa atakuwa na makusudi yake.

Atakuwa kaamua kufanya ubishi wa simba na Yanga.

Mtoto wa Abdul anathibitisha Nyerere kukaa kwao. Mtu ambaye kaja Dar miaka ya Themanini na Tisini anabisha.
Hakuna anayebisha Nyerere kukaa nyumbani kwa Abdul Sykes,mzee said kasema Sykes ndie aliempokea Nyerere dar ndio tunauliza ilikuwaje
 
Sir...
Natambua hii historia jinsi inavyowachoma baadhi ya watu.

Ikiwa unaona kuwa kuishi Pugu ni sawa mtu kaishi Dar es Salaam Mtaa wa Stanley kwangu ni sawa.
Duuh mzee,historia inawachoma labda wajinga wasiojua kusoma nakuelewa uongo ni upi na ukweli ni upi,kumbe pugu sio dar Ila kwako enzi hizo kariakoo ndio dar!!! Sasa pugu ilikuwa pwani sasa imehamishiwa dar?bora ungesema Sykes alipokea Nyerere kariakoo,sasa naamini una kitu cha ziada unachotaka watu wako waelewe
 
Kaka nilikwambia na nitaendelea kukwambia wewe una tatizo la kutokuwa makini, sasa sijui tatizo hili linasababishwa na pupa hasi au ufahamu wako kuwa mdogo au vipi ? Jaribu kulitatua hili tatizo kinyume chake utazidi kuonekana kituko.

Hivi nani alikwambia kutumia tamko fulani la lugha fulani baada ya kuoholewa ndiyo kuonfea lugha hiyo ? Angalia wewe ulivyotumia msamiati wa Kiarabu, lakini ukweli ni kuwa huongei Kiarabu. Hapo mzee amekukumbusha au kugusia tamko "Taazia" hapo kabla na sasa kwamba ni la asili ya Kiarabu. Ona wewe umatumia matamko "Tafadhali, Tafakari" na mfano wa hayo na huambiwi unaongea au kuandika Kiarabu.

Bali hata hilo tamko la huko kwenu "Bara",tamko Bara ni la asili ya Kiarabu, lakini hatukwambii unaandika Kiarabu au unaongea Kiarabu.
Mbona Kiswahili kina maneno mengi tu ya mataifa mengine Kama ujerumani lakini hatuoni tatizo na tunajua kiarabu kimechangia maneno mengi tu kwenye Kiswahili na lugha nyingi duniani zipo hivyo,kiarabu ndio mnaona pepo au
 
Ngoja nikuulize swali kiongozi, kwani kumpokea mtu anapo ingia mji fulani sharti huyo mtu awe ndiyo anaingia katika mji huo kwa mara kwanza au kinyume chake ?

Je hayo marejeo ya Mzee Muhammed Said kwa kina mzee Shivji na Said, kuhusu kupokelewa si ushahidi au ni uongo pia ?

Wewe unao ushahidi unao onyesha ya kuwa mzee Nyerere hakupokelewa na mzee Abdul ?
Kwa hiyo ukweli ni kuwa Nyerere alipokewa kariakoo na Sykes maana dar Nyerere alikujua kabla ya kumjua Sykes
 
Hii mzee wangu katika elimu ya uhakiki wa habari "si sawa" hao wanao ona hivyo wanatakiwa kutupa ushahidi pia.

Ila mzee wangu wewe una busara sana navumilivu,ningekuwa mimi hapa ningekuwa nishamjeruhi mtu, sasa sijui tatizo mimi ni kijana bado au nina maarifa machache, maana naona kuna watu hata misingi ya kuhakiki habari hawana na wanaendekeza ujinga mno.
Kumbe we mfuasi
 
Nyerere kaja Dar na kafikia kwa Abdul Sykes na wapo walioishi nae ndani ya nyumba moja.

Hivi ili kupata ushahidi wa Nyerere alivyofika Dar tumfuate aliyeishi Tandahimba? Na sio aliyemkaribisha kwenye Nyumba yake?

Ikiwa harakati za Uhuru zilianzia Dar kwa nini iwe vibaya kuwauliza watu wa Dar?

Kama nawe una taarifa za harakati za eneo lako tuwekee tusome. Sio kubisha tu.

Mzee Mohamed Said anazungumzia harakati za Uhuru zilizokuwepo Dar na kwa wazee wake.

Kama na ninyi mna historia za harakati za Uhuru za wazee wenu sehemu zingine tuleteeni tusome tujue.

Lakini hamleti isipokuwa kupinga tu na mkipinga hamleti zilizo sahihi.
Tunaweza kuuliza hata wa butiama maana walimuona Nyerere akija dar ili aende masomoni uingereza na walimuona akitua dar kurudi kwao huko
 
Mbona Kiswahili kina maneno mengi tu ya mataifa mengine Kama ujerumani lakini hatuoni tatizo na tunajua kiarabu kimechangia maneno mengi tu kwenye Kiswahili na lugha nyingi duniani zipo hivyo,kiarabu ndio mnaona pepo au
Hahaha, wana upuuzi sana hawa
 
Mbona Kiswahili kina maneno mengi tu ya mataifa mengine Kama ujerumani lakini hatuoni tatizo na tunajua kiarabu kimechangia maneno mengi tu kwenye Kiswahili na lugha nyingi duniani zipo hivyo,kiarabu ndio mnaona pepo au
Jikite kwenye hoja, naona unaandika ambalo hatulijadili sidi. Acha hisia na usizitangulize bali tanguliza elimu mbele, usizidi kuwa kipofu.
 
Kwa hiyo ukweli ni kuwa Nyerere alipokewa kariakoo na Sykes maana dar Nyerere alikujua kabla ya kumjua Sykes
Mwenzako nilimuuliza swali huko juu, ila matokeo yake akarauka na kuwa na jazba hasi, nilimuuliza hivi "Kwani kupokewa sharti ni awe mtu ameingia sehemu husika kwa mara ya kwanza au hata akiwepo ila hutegemea muktadha ?" ,unaweza kulijibu hili swali pia.
 
"Ni hawa Waingereza ambao chini ya governor , kama sitakosea DC Cameron walichangia ujenzi wa ofisi(Narudia kama kumbu kumbu zangu zipo sawa)

Lakini pia ni kweli ilikuwa ngumu kwa Waingereza kwasababu chama kilikuwa cha Ukoo wa Sykes na kilijieneza maeno ya Tandamti, Kidongo chekundu. Hakuna shaka Mwingereza hakuona tishio lolote.
Yote haya yanatokana na ukweli kuwa mbinu, weledi na elimu havikuipa nafasi familia ya Sykes kujipambanua.
Ni kweli kuwa katiba nyingi si ya TANU tu bali za nchi zinazoendelea ni matokeo ya kusoma na hata kunakili katiba za mataifa yaliyotangulia kama Marekani n.k. Hakuna ubaya katika hilo.

Hoja iliyopo hapa ni ile inayoshadidiwa na msemo kuwa ''the end justifies the means''.
Hivyo kama Nyerere alinakili, si hoja tena. Hoja ni TANU ilipata katiba baada ya ujio wake kama muongozo.

Sioni mahali ambapo Kleist Sykes au Abdul Sykes walijaribu hata kunakili katiba.
Kuanzia 1929 hadi 1953 trakribani miaka 24 ya Tawala za Familia ya Sykes, hakuna nyaraka iliyoitwa katiba.

Kuna hoja ya Earle Seaton, hapa tunarudi kule kule ipo wapi draft ya hiyo katiba na upi ni ushiriki wa Abdul Sykes katika kufanikisha hilo? Well, kama hiyo ya Seaton ndiyo ile ya Nyerere ambayo iligeuka kuwa muongozo wa chama bado credit ni za Nyerere. Hivyo katiba ya kwanza ya TANU ilipataikana chini ya Mwl Nyerere, period.

Kuhusu Abdul kuzungumzwa, nadhani unashindwa kuangalia kwa kina.
Ni kweli anazungumzwa leo kuliko huko nyuma na historia inamtendea haki kama ambavyo inamtendea haki kwa kuonyesha udhaifu na madhaifu yake na Baba yake.

Hivyo kwa siasa za Tanganyika, ukiachilia mbali kazi za Umamluki wa Jeshi la Ujerumani kama alivyobainisha Mag3 hapo juu, na ukiachilia hoja kwamba Abdul Sykes aliwafumusha wazee wake kwa makonde ili kurudisha utawala wa Sykes, na ukiachilia kumhifadhi Nyerere, kisiasa hakuwa na jipya au la maana na alifutika haraka kisiasa kwasababu hiyo, alikuwa overrated tu .

Lakini pia Abdul anazungumzwa kwasababu jina lake linatumika kutaka '' kumpa Nyerere jina baya''
Kwamba huwezi kumdunisha Nyerere bila kumtaja Abdul, si kwamba Abdul analingana na Nyerere kwa sifa, la hasha, bali anatumiwa tu kumdhalilisha Nyerere kama tunavyoona Nyerere akielezwa kupikiwa mayai kwa Abdul
Nguruvi3,
Mimi ningethubutu kumdunisha Mwalimu katika kitabu changu basi ningekiua hiki kitabu.

Mimi siwezi kuingia katika ubishi wowote kwani ubisho unakaribisha mizozo na tukizozana tutaharibu huu mjadala.

Bahati mbaya sana na hili naliona sana kwenu.

Hamjui kabisa ile "life style," waliokuwanayo wazee wetu na ndiyo maana kwa Daisy kueleza kuwa alikuwa kila Mwalimu akija kwao yeye kazi yake ilikuwa kumtayarishia chai na mayai mnahisi haikustahili.

Hizi ni kumbukumbu za Daisy wakati huo msichana mdogo wa miaka saba.

Baba yangu Said Salum ana kumbukumbu za Nyerere akimuona pale kwa Abdul na sijapata kumsikia akimkejeli hata siku moja.

Hata pale baba yake Salum Abdallah yaani babu yangu alipokamatwa na kuwekwa kizuizini sikupata kusikia akimsema vibaya Nyerere.

Kilichokuwa kikimuhangaisha ni zile tetesi kuwa babu alikuwa mmoja wa watu waliokula njama kumuua Nyerere na kupindua serikali.

Lakini baba alipoelezwa na Rashid Kheri Baghdelleh sababu ya babu kuwekwa kizuizini kuwa Nyerere anataka kuunda chama kimoja tu cha wafanyakazi na kiwe chini ya TANU, baba aliondokewa na hofu.

Baghdelleh alimuhakikishia baba kuwa hicho chama kikishaundwa viongozi wote wa wafanyakazi waliokuwa jela wataachiwa.

Hivi ndivyo ilivyokuwa.

Baghdelleh wakati ule alikuwa Regional Commissioner wa Tabora na akimjua babu toka utoto wake.

Muhimu narudia kusema ni kuwa leo wengi wanatambua kuwa kulikuwa na kitu kilichokuwa kinafichwa kuhusu mchango wa Abdul Sykes katika TANU.

Mimi nimeishi ndani ya historia kwa hiyo naihisi ndani ya mifupa yangu.

Nyinyi mnaandika nyuma yangu baada ya mimi kukuelezeni yale mliyofichwa kwa miaka mingi.

Kuwa leo unakaa na kupiga "critique," hili ni jambo la faraja kwangu kuwa sikukosea pale nilipoamua kuandika historia ya wazee wangu.

Historia hii hakuna atakaeweza kuifuta tena.
 
Duuh mzee,historia inawachoma labda wajinga wasiojua kusoma nakuelewa uongo ni upi na ukweli ni upi,kumbe pugu sio dar Ila kwako enzi hizo kariakoo ndio dar!!! Sasa pugu ilikuwa pwani sasa imehamishiwa dar?bora ungesema Sykes alipokea Nyerere kariakoo,sasa naamini una kitu cha ziada unachotaka watu wako waelewe
One...
Tatizo katika haya liko kwenye msingi uliokwishajengwa kwenye akili za wengi.

Hili la kupokewa si kitu muhimu sana cha kuwashughulisha watu kwa kiwango hiki.

Yapo ya kuwashughulisha lakini tayari tupo katika taharuki ya ala kumbe ndivyo hivi?

Mbona miaka yote hii haya hatukuyasikia?

Nini sababa yake?

Ndiyo maana hata magazeti ya TANU hayakuthubutu kumwandika Abdul Sykes.

Hili ndilo lingetuhangaisha si kuwa Abdul alikuwa au hakuwa mwenyeji wa Nyerere Dar es Salaam.
 
May Day,
Sasa ungekuwa umesoma kitabu cha Abdul Sykes ndiyo ungeshangaa.

Safari ya kwanza ya Nyerere nje ya Dar es Salaam ilikuwa Morogoro na aliongozana na Zuberi Mtemvu.

Bahati mbaya Nyerere mwenyewe katika hotuba ya kuaga Ukumbi wa Diamond anasema safari yake ya kwanza ilikuwa Mbeya.

Inawezekana Mwalimu kasahau maana kutoka 1954 hadi 1985 ni miaka mingi sana.

Hii safari ya Morogoro haikuwa na mafanikio.
(Taarifa hizi zipo katika barua ya Mtemvu kwa Ally Sykes ya tarehe 15 August, 1954).

Safari ya pili ilikuwa 1955 alikwenda Lindi na alifatwa Dar es Salaam na Salum Mpunga na Ali Mnjale.

Umepata kuwasikia wazalendo hawa wakitajwa popote kama walipigania uhuru bega kwa bega na Mwalimu Nyerere?

Nimeandika historia ya Salum Mpunga (2018) kitabu kipo sokoni.
Kama mimi sikuwataja hawa wazalendo hakuna wa kuwataja na historia ya kweli ya TANU itapotea.

Yako mengi tena kwa ushahidi.
Mzee Said umekuwa Mtu wa kupoteza muelekeo wa ubishani kwa kuibua mambo mapya bila kujibu hoja za msingi zinazoibuka.

Sidhani kama kuna Mtu ana tatizo na nia yako njema ya kuwataja walioshiriki harakati za kuleta uhuru....unachpingwa nacho ni kutumia nafasi hiyo ya kuwafahamisha wasio fahamu kupenyeza ajenda zako.

Kwani huwezi kuwataja Mashujaa hao bila kuhangaika kumdogosha Mwalimu?.

Hakuna yeyote mwenye nia njema atakubali kuona ushujaa wa Mtu kama Mwalimu unafifishwa na Watu wenye ajenda zao.

Kuhusu kitabu cha Abdul Sykes nitafurahi nikikipata na kukisoma ila sioni kwa nini utake kuilazimisha jamii kuwa kila alichokisema au kuandika Abdul kina ukweli wa 100%.

Karibu Watu wote walioshiriki wakati huo hawasemi suala la kuanzishwa kwa chama 1954, nadhani ni wewe na Abdul pekee ndio mnasema hilo...hata Waikela anasema "kubadilishwa kwa TAA kuwa TANU"

Umepata kuwasikia wazalendo hawa wakitajwa popote kama walipigania uhuru bega kwa bega na Mwalimu Nyerere?

Na je kwani umeshawataja Wazalendo wote, na unadhani unaweza kuwataja wote?,.....waweza kujitahidi sana lakini bado hutoweza kuwataja wote na michango yao kuwezesha kufikia uhuru...mathalan umewahi kumtaja Mtu kama Fundi Muhindi, Shabani Kichwa wa Tabora?.

Je wajua kuwa kwenye harakati hizi walikuwepo Wahindi na Wazungu pia, sasa unadhani waweza kuwataja wote?.

Safari ya pili ilikuwa 1955 alikwenda Lindi na alifatwa Dar es Salaam na Salum Mpunga na Ali Mnjale.

Na je Mwalimu alikwenda Lindi mara ngapi kabla ya Uhuru, 1954-1961?
 
Mzee Said umekuwa Mtu wa kupoteza muelekeo wa ubishani kwa kuibua mambo mapya bila kujibu hoja za msingi zinazoibuka.

Sidhani kama kuna Mtu ana tatizo na nia yako njema ya kuwataja walioshiriki harakati za kuleta uhuru....unachpingwa nacho ni kutumia nafasi hiyo ya kuwafahamisha wasio fahamu kupenyeza ajenda zako.

Kwani huwezi kuwataja Mashujaa hao bila kuhangaika kumdogosha Mwalimu?.

Hakuna yeyote mwenye nia njema atakubali kuona ushujaa wa Mtu kama Mwalimu unafifishwa na Watu wenye ajenda zao.

Kuhusu kitabu cha Abdul Sykes nitafurahi nikikipata na kukisoma ila sioni kwa nini utake kuilazimisha jamii kuwa kila alichokisema au kuandika Abdul kina ukweli wa 100%.

Karibu Watu wote walioshiriki wakati huo hawasemi suala la kuanzishwa kwa chama 1954, nadhani ni wewe na Abdul pekee ndio mnasema hilo...hata Waikela anasema "kubadilishwa kwa TAA kuwa TANU"

Umepata kuwasikia wazalendo hawa wakitajwa popote kama walipigania uhuru bega kwa bega na Mwalimu Nyerere?

Na je kwani umeshawataja Wazalendo wote, na unadhani unaweza kuwataja wote?,.....waweza kujitahidi sana lakini bado hutoweza kuwataja wote na michango yao kuwezesha kufikia uhuru...mathalan umewahi kumtaja Mtu kama Fundi Muhindi, Shabani Kichwa wa Tabora?.

Je wajua kuwa kwenye harakati hizi walikuwepo Wahindi na Wazungu pia, sasa unadhani waweza kuwataja wote?.

Safari ya pili ilikuwa 1955 alikwenda Lindi na alifatwa Dar es Salaam na Salum Mpunga na Ali Mnjale.

Na je Mwalimu alikwenda Lindi mara ngapi kabla ya Uhuru, 1954-1961?

May Day,
Mimi siko hapa kubishana na yeyote niko hapa kujaribu kueleza yale ambayo si wengi wanayafahamu.

Ningekuwa mjinga na nikaandika kitabu changu kwa nia ya kumdogosha Mwalimu Nyerere ningekiua kitabu changu na kisingefika kuchapwa mara tatu.

Narejea kwako tena soma kitabu cha Abdul Sykes kitakuongezea maarifa.
Haya maswali unayouliza usingeuliza.

Angalia hapo chini:

''Kamati kama hiyo iliundwa vilevile Tabora mwaka wa 1956, na Mzee Fundi Muhindi mwanasiasa mkongwe, muasisi wa African Association Tabora mwaka wa 1945 na muasisi wa TANU mwaka wa 1954 Jimbo la Magharibi alichaguliwa mwenyekiti wake wa kwanza.

Baada ya kuundwa kwa TANU uongozi ulianza kushughulikia mpango wa kupeleka madai yake mbele ya Baraza la Udhamini la umoja Mataifa kudai uhuru wa Tanganyika kutoka kwa Waingereza.

Hii ilikuwa mara ya pili Waafrika wa Tanganyika kufikisha madai yao Umoja wa Mataifa.

Mara ya kwanza ilikuwa mwaka wa 1952 wakati Japhet Kirilo alipokwenda Umoja wa Mataifa kuwakilisha madai ya mgogoro wa ardhi ya Wameru.

TANU ilikuja kutambua kuwa taarifa za ujumbe za Umoja wa Mataifa zilikuwa na athari ndogo sana kwa Uingereza.

Ikijifunza kutokana na ujuzi iliopata wa Japhet Kirilo katika Umoja wa Mataifa, kuanzia mwaka wa 1952 TAA ikawa inashughulikia kumpeleka mjumbe wake mwenyewe kwenda Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa kudai uhuru wa Tanganyika.''


''Chama kilipata msukumo mwingine na kuongezeka nguvu wakati Sadik Ali Patwa Muasia tajiri alipoingia TANU.''
 
Back
Top Bottom