Nini kilisababisha urafiki na Besti/ Mshkaji wako kufa?

Nini kilisababisha urafiki na Besti/ Mshkaji wako kufa?

Kila tukikutana badala ya kufurahi yeye ni kuelezea matatizo kila siku ana matatizo yeye tu hana hela yeye tu kukopa kopa nikakaa mbali nae maana alikuwa hanipi furaha
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwema team MMU?

Marafiki ni watu muhimu na wenye manufaa makubwa kwetu, japokuwa wakati mwingine anaweza kuwa kichomi akavuruga maisha yako?

Mimi na rafiki yangu mmoja urafiki ulikufa sababu hakulipa deni langu, kila nikimdai anatafuta vijisababu vya kunikwepa, jamaa ananikwepa mpaka kesho:pepeLaughing:.

Kwa upande wako nini kilisababisha urafiki wako na besti yako/mshkaji wako kufa?
Nilitembea na mama yake,akajua urafiki ukafia hapo[emoji23]
 
Zipo sababu nyingi za kutengana na marafiki ila kwa upande wangu ni

Ubinafsi na dharau plus kujisikia flani hivi....

Yani mshikaji wako anajali mambo yako yaende wewe ukwame.


kuna mmoja huyo toka alivojipatia kazi sehemu akaanza kujikuta busy nikampunguza.
 
Ubinafsi,yan kwenye shida zake unapambania kadiri ya uwezo wako ila zako hazimuhusu,unamshirikisha mambo yako ila yeye yake ni siri,mwisho wa siku kuna changamoto ilitokea kazin kwangu,so utaratibu ikawa ni upate mdhamini au uende rumande,jamaa nikamwelekeza akanambia nakuja fasta halafu akazima kabisa simu,uzuri kuna jamaa alikuwa nae mda huo ndio akanijuza kuhusu mpango wa jamaa,Mungu mwema,ndani ya saa moja nililopewa nitafute mtu anidhamini nikakutana na bro mmoja aliwaipata shida halafu mfukoni hana kitu nilimsaidia tu kama mwanaume mwenzangu,yule bro ndio akaja kuniwekea dhamana,police wakamaliza uchunguzi wao,wakawapata waarifu wao wengine kazini maisha yakaendelea fresh,ukaribu ulifia hapo,lakini nilipata somo kuwa unapokuwa na nafasi we saidia tu hata kama mtu humjuwi maana hujuwi kesho yako itakuwaje,yule jamaa huwa tunaonana mara chache sana,ila Mungu ni fundi sana kudadeki
 
Kwa upande wangu, mshikaji wangu tulikuwa tunaishi maeneo yanayokaribiana. Tulikuwa na utaratibu wa kuambiana kuwa nakuja maeneo ya kwenu utanikuta baa fulani. Sasa siku moja nikamwambia hivyo kuwa nipo mitaa yake hivyo atanikuta baa fulani. Mwenzangu alikuwa anajenga mahala pengine ili baada ya kumaliza ujenzi ahamie huko (sikuwa nalijua hili). Kumbe siku namwambia nipo mitaa yake, mwenzangu amehama kama wiki imepita. Ila akaniambia nimsubiri anakuja. Nilikaa hapo mpaka usiku mkubwa. Nikaondoka. Siku za baadaye nikaja sikia kuwa alihama na siku ile aliyoniweka mitaa aliyohama hakuwa mitaa hiyo. Umbali ulitusaidia kuuvunja ushikaji.
Duh, si sngekwambia tu ukweli
 
Ubinafsi,yan kwenye shida zake unapambania kadiri ya uwezo wako ila zako hazimuhusu,unamshirikisha mambo yako ila yeye yake ni siri,mwisho wa siku kuna changamoto ilitokea kazin kwangu,so utaratibu ikawa ni upate mdhamini au uende rumande,jamaa nikamwelekeza akanambia nakuja fasta halafu akazima kabisa simu,uzuri kuna jamaa alikuwa nae mda huo ndio akanijuza kuhusu mpango wa jamaa,Mungu mwema,ndani ya saa moja nililopewa nitafute mtu anidhamini nikakutana na bro mmoja aliwaipata shida halafu mfukoni hana kitu nilimsaidia tu kama mwanaume mwenzangu,yule bro ndio akaja kuniwekea dhamana,police wakamaliza uchunguzi wao,wakawapata waarifu wao wengine kazini maisha yakaendelea fresh,ukaribu ulifia hapo,lakini nilipata somo kuwa unapokuwa na nafasi we saidia tu hata kama mtu humjuwi maana hujuwi kesho yako itakuwaje,yule jamaa huwa tunaonana mara chache sana,ila Mungu ni fundi sana kudadeki
Japokuwa mwabmba alizingua, ila amekupa somo kubwa sana Mkuu na wengine tuchukue notes
 
Wakati mwingine tunapaswa kuvumiliana kwenye madhaifu ili kumantain urafiki wetu.
Ingekua mimi ndio wewe ningemtafuta huyo rafiki hadi nimpate, kisha nikaongea nae mambo mengine kabisa tofauti na deni langu na baada ya hapo naamini urafiki wetu ungedumu.
Unamtafutaje mtu anayekukwepa Mkuu, ukipiga simu haishikwi?
 
Nliua nilipoona jamaa kantumia message KANIMISS
Sasa kuna ubaya gani wa kukumiss Mkuu, au ulitaka akwambie kibishi.... "We mjinga (au tusi kubwa zaidi) kitambo sana.... hapo ingekuwa freshi?
 
Alikuwa haeleweki. Mtu hana malengo ya kimaisha yeye ni bata tu umri umeenda bado ana akili kama yupo foolish age.

Anaweza pata laki 5 hapa akapigia simu washkaji ikachakazwa ikaisha yote akaamka asubuhi ana 30,000 tu.

Ukiwa na shida ukimwambia anataka ujielezee kama unaomba mkopo wakati yeye akiwa na shida hata simuulizi nampa kile anachoomba.

Alikuwa anatabia anakuja na gari yake anaipaki anaomba yangu aendee mtaa wa nyuma sababu anasema yake ipo chini sana halafu inatoa mlio hauelewi ila nikajua anafanya kusudi tu ila nikawa nampa tu ufunguo afanye anachotaka sijui alikuwa anaenda gongea mademu zake kwenye gari. Maana anaweza ondoka saa kumi na moja jioni anarudi saa tano au saa nne za usiku. Nikamwambia nataka nisepe gari ipo wapi ananiambia niende na yake atakuja home kuichukua me huwa namkatalia namwambia niambie ulipo unikuletee gari yako me naenda home basi hapo ataogopa utashangaa huyo hapo baada ya nusu saa.

Nilipopitia kipindi kigumu kidogo ndipo nikajua tabia zake halisi. Kwanza alikata mguu, simu zangu akawa hapokei, nishamuomba sana hizi hela ndogo ndogo hajawahi nitoa hata 10. Kuna siku mshikaji wetu mwingine akasema mbona jana nilikuwa na fulani nikamwambia nikupigie simu uje akasema nisikuite, mnashida gani? Nikatabasamu tu na kutikisa kichwa nikamwambia acha tu ubinadamu kazi ndugu yangu. Nikamuelezea jamaa akasikitika sana na yeye akaanza muepuka. Akawa akienda kiwanja ananipigia ananitumia boda boda tunaenda kula bata kimya kimya.

Kuna siku akatukuta kwa bahati mbaya kiwanja kinaitwa small planet pale tabata. Akawa ananionyesha sura ya dharau kabisa yaani utasema kuna kitu nimemfanyia, aisee nilipatwa na hasira nusu nimfyatukie sema nikajikaza. Akaondoka na demu alikutana nae pale pale akaenda zake.

Fast-forward leo mimi niliendelea jikongoja nikakaa sawa hali si mbaya, aliniona wapi sijui naendesha gari ya mshikaji wangu mwingine akajua sijui yangu nashangaa simu ananipigia ananichangamkia sana. Nikajisemea "ona jinga hili".

Akawa anataka sana tuonane namkwepa hadi leo. Nasubiria kwa hamu sana nipate usafiri wangu tena nitahakikisha anajua halafu ajaribu kuniletea mazoea aisee ntamlipua dry na nitampa makavu yote hadi ajue kuwa kazingua.
Umenikumbusha rafiki yangu mmoja, huyu jamaa atakucheki muda wa kula bata tu, yuko radhi hata akutumie usafiri ukaungane nae, ila ukiwa na shida uombe msaada hata wa elf 10 humuoni. Kuna muda alikwama sehemu akata hela ya mafuta kwa wakati huo sikuwa nayo ila kulikuwa na hela yafanyia jambo lingine nikamwambia naichomoa huku ila unirudishie kesho, maana alidai mtandao umemsumbua ameshindwa kutoa hela, alikausha mazima hakurudisha ile hela mpaka kesho, na ilinihangaisha kidogo sababu nilichomoa sehemu ambako ilikuwa na kazi nyingine. Nikasema freshi atapata tu shida siku nyingine

Baada muda kupita siku akarudi na pigo zile zile, this time nilikuwa nayo ila nikakausha, akalalama wee ndio ikawa imetoka hiyo!
 
kwa umbea wangu tu yani full kumteta na siri zake natangaza alinisuuuuta akamalizia i love you but i cant keep you jaman alikua ana roho nzuri msafi mtoaji mtu wa kumtegemea nililia niliomba msamaha nilituma watu akasema tupendane mbali mbali kila nilivojipendekeza waapi ananichangamkia vizuri ila hataki ukarib kabisaaa nammis ampenda kanivumilia megi sana na hii ni stori ya kutunga asanteni.
Jinga kabisa 😂😂
 
Back
Top Bottom