Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapo sasa..!!Duh, si sngekwambia tu ukweli
NakuchekiYupo sahihi maana mwanamke alitaka ndoa na siyo kutumika kama mchepuko
Mm urafiki ulikufa na mshikaji wangu baada ya kujifanya demu na akaanza kunitongoza akajua ninashobokea mademu.nilikuwq na chati nae kwa namba ngeni ambyo nilimwambia ni wrong namba ila aliendelea zoezi lilienda kama wiki hivi mwisho wa siku akaja kusema yeye ni fulani.nilimkataa mazima hadi leo haamini macho yakeKwema team MMU?
Marafiki ni watu muhimu na wenye manufaa makubwa kwetu, japokuwa wakati mwingine anaweza kuwa kichomi akavuruga maisha yako?
Mimi na rafiki yangu mmoja urafiki ulikufa sababu hakulipa deni langu, kila nikimdai anatafuta vijisababu vya kunikwepa, jamaa ananikwepa mpaka kesho.
Kwa upande wako nini kilisababisha urafiki wako na besti yako/mshkaji wako kufa?
SawaNakucheki
Hatumissian wanaumeSasa kuna ubaya gani wa kukumiss Mkuu, au ulitaka akwambie kibishi.... "We mjinga (au tusi kubwa zaidi) kitambo sana.... hapo ingekuwa freshi?
Dah 🤔 huyo kweli ni falaDaaah ni stori ndefu, siku nikiipata wasaa nitashusha kisa kizima, ila Kwa ufupi fala kaoa shemeji yake (mchepuko wangu) ilihali alikuwa anajua kila kitu.
Fala namchukia kila siku, kibaya zaidi nilimtumia pesa ya kuchukulia mzigo wa biashara jamaa ndo akafanya ya kuolea.
Sent from my Infinix X6516 using JamiiForums mobile app
Ah basi sawaa, ndio ukawe mke wa 3?Yupo sahihi maana mwanamke alitaka ndoa na siyo kutumika kama mchepuko
Nakumbuka kipindi hicho Mimi ni fundiKwa upande wako nini kilisababisha urafiki wako na besti yako/mshkaji wako kufa?
Mkuu huyo rafiki yako anaependa mashindano mbona siyo vibaya, kama kaja kwako kakuta una TV ya laki tano na yeye kaenda kununua TV ya milioni hapo hakuna shida, hiyo inaitwa wivu wa maendeleo.1.Huyu ni rafiki wa kike alikuwa mbinafsi sana.Nimewahi kumsaidia vitu vingi tu wakati mwingine alikuwa anaumwa nkirudi safari kutoka mkoani hata sipumziki naenda moja kwa moja kumuona na kumpelekea matunda na kumuachia cash kidogo ya kupambana,akiwa down/hopeless naenda namtoa out tunakula then stori namsindikiza mpaka home kwake then naondoka.Akiwa na shida kuna watu nawanyima ila yeye nampa.Siku moja tu nilikuwa sina na alikuwa anajua hali yangu nikamwambia sina akaanza kununa akanitumia na voice note ananilalamikia nikamwambia sina hela na unajua changamoto zangu,mwisho nikamuuliza why unanifanya niwe responsible kwa ishu zako kwa lazima hivyo? Akaanza kuwaka nikampigia simu nimchane kwamba hakuna urafiki wa kipuuzi kama huu ambao tunao yani yeye ni mbinafsi 200% hajawahi kunisaidia hata 100 yake mbovu na hata urafiki wa kushauri hajawahi kuwa na ushauri wa msaada kwenye maisha yangu,akanikatia simu nikamtext akiwa free anipigie akakataa akasema hapana.Nikajisemea sawa yani mimi kosa afanye yeye nikitaka nimwambie ukweli ili tukae sawa anaona kama nafosi urafiki ambao in fact hauna faida yoyote kwangu maana mara nyingi ukiona simu au text yake ni ya shida tu naomba hela ,naomba hela.Nikasema hapa dawa moja tu namba sifuti ila simu sipigi,txt situmi.Mpaka leo kutoka mwaka jana kajipigisha simu kama mara 4 anajisalimisha anauliza maswali ya kijinga namjibu simple tu maana nishaona hata akili ya kawaida hana hata kuomba samahani kwa ujinga wake hawezi nkasema this kind of pride/ego itampeleka pabaya sana unless marafiki alio nao wamshauri vyema.
2.Mwingine ni high school friend..Ni mtu wa mashindano sana kila kitu mkifanya anataka kuoutshine/kuonekana yupo superior sana kuwazidi.Sio vibaya kuwa best lakini kushindana na watu ili kujionesha ndio tatizo hapa.Hiyo tabia hadi chuo tumekutana ndio nikajua kumbe haijapoa.Yupo vilevile.atataka kuja gheto kwako aangalie ni kitu gani unacho alafu aende anunue cha bei zaidi ya cha kwako.Yan full mashindano ambayo hayana msingi na hayajengi.nilipoa chuo na yeye mra moja moja tunawasiliana ila ni salamu tu hakuna jipya sana.
2.Wengine walienda jeshi tukawa tunawasiliana vizuri.baadae nikwatafuta tuonane kama watapata nafasi,hawakupata.By the way ubize wao at least una sababu.jamaa mmoja akawa hata hapokei simu tena na ni homeboy kabisa na tulikuwa marafiki.ni kama kuignore hivi kwa mbali na sababu sijui ni nini maana nilikuwa nawatafuta sana kuliko wao ila nikaona kama sasa huku ni kujiprndekeza ngoja na mimi nimute maana pia niko busy mambo ni mengi.Mpaka sasa bila bila🤣.Kila mtu anashinda mechi zake.
3.Wote ambao nilikuwa nawapigia sana simu nikaona wamejisahau nikaona ngoja niache kupiga simu kabisa.Nilipoacha kuwatafuta nikaanza kuona txt/simu zao kwamba nimepoa nikajisemea wajinga sana hawa wandhani mtu anapowatafuta hana kazi ya kufanya sahivi ndio wanaona kama mimi nina jukumu la kuwatafuta wao lakini wao hawawezi/hawana muda?
Nkatulia kimyaa na nikabaki na list yangu ndogo lakini ya watu ambao niko comfortable kushare nao vitu vyangu kwa amani kabisa japo sio wote.
Nikagundua pia mimi ndio nlikuwa nashikilia mahusiano yangu na marafiki kwa nguvu sana kuliko wao na nlipoachia kamba wote chini🤣.
Nkasema hawa ndio ntaenda nao atakayepata time ntamkumbuka pia,asiye na muda pia hata mimi sina mambo mengi hii dunia bado inazunguka.
MWISHO:Kuna watu ambao watakua marafiki wa karibu regardless una hela/hauna wengine ni watakua wa kushauri mambo mazuri sana ya kimaisha hata kama hawatakusaidia kifedha.Hao ndio marafiki wa kufa na kuzikana.Wengine tunasogezeana siku tu.
Sijasema ni vibaya ila anajitesa yeye mwenyewe hayuko comfortable na watu wengine wakimzidi vingine anajipush nje ya uwezo wake kabisa unaona..Ishu sio yeye kunizidi ishu ni kwamba anateseka yeye sana..Mkuu huyo rafiki yako anaependa mashindano mbona siyo vibaya, kama kaja kwako kakuta una TV ya laki tano na yeye kaenda kununua TV ya milioni hapo hakuna shida, hiyo inaitwa wivu wa maendeleo.