Nini kimechochea wimbi la wanawake wa kisasa kuwa na vitambi?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Vitambi kwa wanaume ni jambo ambalo linajulikana limekuwepo karne zote lakini wimbi la wanawake kuwa na vitambi kote duniani lilianza takribani miaka ya 2000's. Nini hasa imechochea wimbi kubwa la wanawake kuwa na vitambi mijini na vijijini?
 
Vitambi kwa wanaume ni jambo ambalo linajulikana limekuwepo karne zote lakini wimbi la wanawake kuwa na vitambi kote duniani lilianza takribani miaka ya 2000's. Nini hasa imechochea wimbi kubwa la wanawake kuwa na vitambi mijini na vijijini?
Life style mkuu, hakuna jibu jingine zaidi ya hilo.

Mavitambi wengine yanawapendeza, lakini hawajui kuwa wamebeba viriba vya magonjwa hatarishi yasiyo ya kuambukiza.
 
Wanawake dizaini hii kutoboa miaka sabini ni shughuli pevu, kisukari, kansa, presha, TB za aina mbalimbali, magonjwa ya figo, moyo, maini, mapafu na mifupa wanayakaribisha bila kujua. Wanapaswa kupewa elimu ya lishe haraka sana wasije kufa chini ya miaka sitini
 
Vitambi kwa wanaume ni jambo ambalo linajulikana limekuwepo karne zote lakini wimbi la wanawake kuwa na vitambi kote duniani lilianza takribani miaka ya 2000's. Nini hasa imechochea wimbi kubwa la wanawake kuwa na vitambi mijini na vijijini?
Kuna mmoja nilikutana nae she was uncomfortable!, maana alifikia mpaka akaanza kunionyesha picha zake za zamani alivyokuwa hana kitambi!.
ni kama mtu anakwambia "usiniache zamani sikuwa na kitambi!"..🤣

Okay ipo hivi, life style ndo imekuwa changamoto kubwa sana watu tunakula kwa ratiba kwasababu ndo umeshakuwa mfumo!, yani asubuhi unakula, mchana unakula na usiku unakula! haijalishi umesikia njaa ama hujasikia!. hiyo sio tabu sana japo ni mchawi pia, mchawi mkubwa ni huyu "Tunakula sana vyakula vya wanga!".

Asubuhi
chapati na supu

Mchana
Ugali, maharage,mboga ya majani,nyama na coca baridi..😅

Usiku
Wali na broiler ama biriani au tambi na minyamanyama!.

Tuje kwenye kazi, huyu mtu kazi anayofanya sio ya purukushani yakumtoa jasho na hana ratiba ya mazoezi, unategemea hizo sukari zilizoingia hapo zitaenda wapi..??
ulaji unatakiwa utegemee na kazi na ndio maana ni ngumu kukuta mtu anaefanya kazi ngumu kuwa na likitambi!.
watu tibadilishe life style zetu.
 
Vitambi kwa wanaume ni jambo ambalo linajulikana limekuwepo karne zote lakini wimbi la wanawake kuwa na vitambi kote duniani lilianza takribani miaka ya 2000's. Nini hasa imechochea wimbi kubwa la wanawake kuwa na vitambi mijini na vijijini?
Kuna wanawake wanapikia msosi au bia.
Yani mtu anamalizia sijui kisinia cha biliani au chips na kuku mzima.
Kuna wale wa kupenda michemsho na makange.
kuna wale yani anakunywa kreti nzima ya bia au jagi kubwa la juice.
 
Umero/uroho uliokithiri. Toto la kike linafuta kilo nzima ya kitimoto peke yake huku likishushia na safari kadhaa.
Zamani watoto wa kike walikuwa wanakula kwa staha. Siku hizi wana matonge kama makuli.

Kufakamia pombe hasa za ofa.

Uvivu wa kufanya shughuli hata za nyumbani. Hata kitandani ni wavivu, jitu linalala kama gogo mawazo yote yapo kwenye VICOBA na upatu.

Kujishindilia midonge ya majira ili isishike mimba ikinjunjana ovyo wakati wa kutafuta pesa za VICOBA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…