Nini kimeifanya Rwanda ipunguze kupitishia mizigo Tanzania na kugeukia Kenya?

Nini kimeifanya Rwanda ipunguze kupitishia mizigo Tanzania na kugeukia Kenya?

Yaani tuko bize kujadili uingizwaji wa goods ambazo hatujui zimetengenezwa wapi! BADALA ya kuhoji uhalali wa WanyaRwanda waliopenyezwa kwenye idara nyeti za nchi hii
Kila jambo hujadiliwa Kwa wakati wake. Hizo 30.16% zilizopungua Tanzania na kuingia kupitia Kenya ni Hela hizo.

Au hatujaelewana?
 
Hizo porojo. Rushwa iko TRA ndio maana wafanyabiashara wa Kariakoo hadi sasa wanalia. Ili mzigo utoke kazime uwe na TRA clearance. Sio DP WORLD

Pili Kabla ya kuja hao DP World kuna uwekezaji mkubwa ulifanyika kwa mkopo wa World Bank na kwa kawaida kabla ya investment huwa tunafanya economic analysis ya projected income kwa miaka kadhaa, sasa kabla hujawasifia tafuta data kwa ule mkopo tuliokopa mapato yangekuwa kiasi gani ( net income) ambayo yote yalikuwa yanaingia hazina kwa asilimia 100. Kisha chukua baada ya kuja DP World mapato ni kiasi gani then ondoa kile wanachochukua DP World na tazama kile kunachoingia Hazina baada ya kugawana na DO World kisha ltoa kile tunacholipa mkopo wa Workd bank then lnganisha kinachobaki na kile ambacho tungepata kutokana na ule mkopo wa Works bank kama tungebaki pwke yetu
Baada,ya hapo ndio useme kama tunanufaika au la.
Hizo ni porojo ndefu umeandika. Mojawapo wa vipengele vya mkataba wa DPW ni kuwapa elimu wa wafanyakazi pale bandarini, maana yake ufanisi unakuwa mdogo kwa sababu wafanyakazi hawana viwango vya kisasa vya elimu za bandari.

Kuchukua mkopo haina maana kwamba kiuendeshaji tupo vizuri, malalamiko yalikuwa ni mengi sana pale bandarini katika suala zima la ucheleweshaji wa mizigo ya wateja, ikafikia hatua raia wa mataifa jirani ya Burundi na DRC wakaikimbia bandari na kuanza kutoa mizigo yao pale Mombasa.

Ukipunguza hizi negativity utagundua kwamba bandari ya TPA kwa sasa inaongoza katika suaka la utoaji huduma katika eneo hili la afrika mashariki.
 
Hii hoja inahitaji majibu sahihi na njia sahihi yakuboresha bandari yetu na hizi Taasisi zetu za kodi,ushuru na tozo.

Hili ni tatizo linalohitaji solution sio majibu yakisiasa.
Wakati bado tunaendelea kuomboleza kifo cha mfanyakazi wa TRA, Marehemu Amani Simbayao, Kuna jambo limenishangaza kidogo.

Kumbe Mwigulu Nchemba yupo. Maana zaidi ya kumkumbuka ninaposafiri na kuona mamia ya mawe huko kwenye barabara ninazopita, yameandikwa "Mwigulu Rais 2015", huwa simsikii akijibu hoja na maswali mbali mbali kwa namna ya uharaka aliouonesha kwenye jambo hili.

Rwanda ni nchi ambayo kijografia, inaifanya kutegemea nchi nyingine ili kupata mizigo yake inayopitia baharini.

Kwa kifupi Rwanda haina bahari na kwa ivo haina bandari ya bahari. Bandari za Rwanda ni zile zilizoko kwenye ziwa Viktoria.

Siku za nyuma Rwanda baada ya DRC ndiyo ilikuwa nchi inayoitegemea Bandari ya Dar es salaam kusafirishia mizigo yake kutoka na kwenda Rwanda.

Lakini baadae Rwanda ikaleta sera kwamba nchi hiyo isiwe tegemezi wa kupitishia mizigo kwenye nchi moja. Hivyo ikaanza kupitishia mizigo yake na Kenya pia.

Lakini ndani ya mwaka mmoja mambo haya yametokea. Kwanza shehena ya mizigo kupitia Kenya imeongezeka na mizigo inayopitia Tanzania imepungua.

Mizigo yenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 121.45 sawa ongezeko la asilimia 361.43 (361.43%) imepitia Kenya ukilinganisha na Oktoba Mwaka jana 2023.

Idadi hiyo ya mizigo kupitia Kenya unaifanya nchi hiyo kuwa ya pili nyuma ya China ambayo imeingiza Rwanda mizigo yenye thamani ya Dola za Kimarekani 142.08 sawa na ongezeko la 34.95% .

Kwa Tanzania uingizaji wa mizigo Rwanda kupitia Tanzania umekuwa ukipungua kwa karibia 39.04% kwa msingi wa mwezi kwa mwezi na kwa mwaka mzima uingizaji mizigo Rwanda kupitia Tanzania umepungua kwa 30.16%.

Ukilinganisha Mwezi Oktoba 2023, Rwanda imepitishia Tanzania Mizigo yenye thamani ya Dola za kimarekani milioni 57.38 pekee.

Wazee wa kushinda 99% nini kinaendelea hapa.
 
Kuna shida bandarini na hasa utaratibu wa kutoa mzigo tena kwa gharama kubwa. Kingine ni ubovu wa barabara zetu hasa kipande cha kutoka Nyakanazi hadi kuipata border ya Rusumo. Barabara ile iko kwenye hali mbaya kwa zaidi ya miaka 6 sasa.
Japo kuna umbali mrefu kwa mzigo wa Rwanda kuingizwa kutokea Kenya na Uganda, unafuu uko kwenye ubora wa barabara za nchi hizo tatu ukilinganisha na barabara zetu. Ukiritimba na janja janja ya bandari na border post zetu inaweza kuwa sababu ya wanyarwanda kuamua kutumia bandari ya Mombasa.
Huko kusini pia hakuko salama, Malawi wako kwenye mchakato wa kuangalia uwezekano wa kuitumia bandari ya Beira zaidi na kwa mbali naona wakijaribu kufanya window shopping kwenye bandari ya Mtwara. Zambia huenda wakajiunga na Malawi kwenye mpango huo. Burundi pia wakati wa Nkurunziza walikuwa na mpango wa kujenga barabara na reli kwenye mwambao wa magharibi ya ziwa Tanganyika ili mizigo yao ipitie Kapirimposhi na Lubumbashi.
Tuendelee tu kutekana na kuuana wakati wengine wakipanga mipango imara ya kunusuru nchi zao kiuchumi.
 
Tuendelee tu kutekana na kuuana wakati wengine wakipanga mipango imara ya kunusuru nchi zao kiuchumi.
Umeongea mambo mengi sana ya maana. Hili la mwisho linafikirisha Sana.

Yaani kipaumbele kiko kwenye kushinda chaguzi bila ya kuwa na mpango wa nini Cha kufanya wakiwa madarakani.

Hivi hili jambo wanaona liko sawa kweli?
 
Pamoja na Dp world kusemekana kuongeza ufanisi lakini bado utokaji wa mzigo kwenda kwa muagizaji unachelewa sababu ya broken CFS au ICD ambazo hazina vifaa. Malori na wafanyakazi wanaojua wajibu wao. Ucheleweshaji bado ni mkubwa sana
 
Katika hizi takwimu, Kwa nini Rwanda ipike hizi takwimu na inafaidika vipi?

Jee takwimu sahihi ni zipi tofauti na hizi?
Deal la nchi tatu za afrika mashariki na DPW ni kubwa na lilipangwa miaka kadhaa iliyopita.

Rwanda kupitisha mizigo yao bandari ya Kenya ni maamuzi yao na hayawezi kuifanya Tanzania ikaingiwa na hofu yoyote.
 
Sababu ni kwamba baada ya bandari yetu kuuzwa Kwa dp world ufanisi imepungua sana japo vichaa wa mama wanakataa.mizigo inachelewa sana kuondolewa na ushuru umepanda maradufu ndiyo maana wanyarwanda wameihama bandari ya dar.hata Zambia Kwa Sasa wanapitoshia mizigo Yao nyingi beira
 
Wakati bado tunaendelea kuomboleza kifo cha mfanyakazi wa TRA, Marehemu Amani Simbayao, Kuna jambo limenishangaza kidogo.

Kumbe Mwigulu Nchemba yupo. Maana zaidi ya kumkumbuka ninaposafiri na kuona mamia ya mawe huko kwenye barabara ninazopita, yameandikwa "Mwigulu Rais 2015", huwa simsikii akijibu hoja na maswali mbali mbali kwa namna ya uharaka aliouonesha kwenye jambo hili.

Rwanda ni nchi ambayo kijografia, inaifanya kutegemea nchi nyingine ili kupata mizigo yake inayopitia baharini.

Kwa kifupi Rwanda haina bahari na kwa ivo haina bandari ya baharini. Bandari za Rwanda ni zile zilizoko kwenye ziwa Viktoria.

Siku za nyuma Rwanda baada ya DRC ndiyo ilikuwa nchi inayoitegemea Bandari ya Dar es salaam kusafirishia mizigo yake kutoka na kwenda Rwanda.

Lakini baadae Rwanda ikaleta sera kwamba nchi hiyo isiwe tegemezi wa kupitishia mizigo kwenye nchi moja. Hivyo ikaanza kupitishia mizigo yake na Kenya pia.

Lakini ndani ya mwaka mmoja mambo haya yametokea. Kwanza shehena ya mizigo kupitia Kenya imeongezeka na mizigo inayopitia Tanzania imepungua.

Mizigo yenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 121.45 sawa ongezeko la asilimia 361.43 (361.43%) imepitia Kenya ukilinganisha na Oktoba Mwaka jana 2023.

Idadi hiyo ya mizigo kupitia Kenya unaifanya nchi hiyo kuwa ya pili nyuma ya China ambayo imeingiza Rwanda mizigo yenye thamani ya Dola za Kimarekani 142.08 sawa na ongezeko la 34.95% .

Kwa Tanzania uingizaji wa mizigo Rwanda kupitia Tanzania umekuwa ukipungua kwa karibia 39.04% kwa msingi wa mwezi kwa mwezi na kwa mwaka mzima uingizaji mizigo Rwanda kupitia Tanzania umepungua kwa 30.16%.

Ukilinganisha Mwezi Oktoba 2023, Rwanda imepitishia Tanzania Mizigo yenye thamani ya Dola za kimarekani milioni 57.38 pekee.

Wazee wa kushinda 99% nini kinaendelea hapa.
Tanzania hawafanyi utafiti shindani wa masoko, wao wanaamimini wateja watakuja tu, hata kama wana tozo za ajabu ama mapungufu, pia wanadhani wateja ni wajinga na wapumbavu

Lack of competitive analysis and taking customers for granted, in reality though these days customers need to be treated like queens even help to solve their family problems, in this case help solve their National burning issues, thus, create partnership in business

Simple answer, they do not know how to handle customers, similarly to, no entrepreneurship skills there will be no business growth, in actual fact in entrepreneurship we learn how to do business not about business

Kwenye elimu ya ujasiriamali tunajifunza jinsi ya kufanya biashara na siyo kuhusu biashara walio wengi waliopewa dhamana wamesoma kuhusu biashara, watakwambia kuhusu "demand and supply", hahahaa!
 
Rwanda has made a surprising shift in its trading preferences, with Kenya overtaking Tanzania to become the country’s second-largest source of imports after China.

This marks a significant change in the regional trade dynamics, as Tanzania had long been Rwanda’s primary partner due to its geographical proximity and the role of the Dar es Salaam port.


According to the October 2024 Formal External Trade in Goods report by the National Institute of Statistics of Rwanda (NISR), imports from Kenya reached $121.45 million, representing a 361.43% increase compared to October 2023.

This places Kenya behind only China, which accounted for $142.08 million in imports, a 34.95% rise over the same period. In contrast, imports from Tanzania fell to $57.38 million, marking a 39.04% month-to-month decline and a 30.16% year-on-year decrease.


Several factors appear to be driving Rwanda’s growing preference for Kenya as an import partner.


Rwanda and Kenya have strengthened ties, influenced by improved relations and efforts to reduce trade barriers. In contrast, tensions in the region may have reduced Rwanda’s reliance on Tanzania as a transit route.

Rwanda’s government has encouraged diversification of trade routes to mitigate risks associated with over-reliance on a single country. The Northern Corridor, which runs through Kenya, is increasingly being utilized for imports.

The shift in Rwanda’s trade dynamics with Tanzania is further complicated by rising trade tensions, particularly surrounding Rwanda’s dairy exports. Tanzania has recently imposed various Non-Tariff Barriers (NTBs) on Rwandan milk, disrupting a historically vital trade relationship.

Tanzania has reportedly blocked the entry of Rwandan milk under the guise of meeting local regulatory and quality standards. These barriers have effectively shut out Rwandan dairy products from Tanzanian markets, despite Rwanda meeting East African Community (EAC) standards.
Source kt rwanda
 
Yaani tuko bize kujadili uingizwaji wa goods ambazo hatujui zimetengenezwa wapi! BADALA ya kuhoji uhalali wa WanyaRwanda waliopenyezwa kwenye idara nyeti za nchi hii

Taja wawili tu kwa mfano ambao wapo serikalini na sio watz?

Mkuu wenu wa majeshi aliropoka hadi Leo hajataja hata mmoja ili achukuliwe hatua. Mnapenda sana story za vijiweni.
 
Back
Top Bottom