Maisha ni ushindani, binadamu tumeumbwa na kaushindani fulani hivi ndo asili. Upinzani wakisusa, wananchi wakisusa, CVM watakosa radha, watapoa - huna mtu wa kumwamwia sera zako na uongo, yaan nobody cares- automatically nao wataanza kukata moto - nao wataona havina maana - watasusa bila kujitambua, haijalishi hata mtu akapata uongozi fake, akaiba, akajilimbikizia mali - maisha na raha ya siasa na ubinadamu ni hekaheka - Angalia US watu wanavyopashana - watu wanaongea - watu wanasemana - wanaongea sera zao - wanaenda kwenye midahalo - watu wanashindana - inaleta utamu fulani hivi na ukamikifu wa kibinadamu.
Angalia kwetu sasa - kwanza hakuna kinachofanyika cha maendeleo mtaani huku ( ni hili sio kosa lao) waani viongozi wa serikali ya mtaa hata barabara kidogo tu ikaharibiwa na mvua - hawana uwezo wa kurekebisha, usafi chali, yaani hawana influence ya moja kwa moja, mazingira mabovu, ujenzi holela - HAWA viongozi wa serikali za mitaa hawasaidii moja kwa moja wananchi kikubwa wanakuwa ni kama extension ya executive tu: Kuwa mashushu na wambea, kuandikisha zile barua za kwenda kufungua akaunti, kuchukua 10% za mauzo ya ardhi - kusainisha mikataba ambalo sio hata jukumu lao, kuwa madalali, kuwa mahakama ndogo - kusuruhisha ikishindikana wanapiga kimya, ofisi zao wenyewe zinatia huruma, unaenda ofisi ya serikali ya mtaa unakuta mara mibendera ya vyama vya siasa hasahasa CCM, viti na meza vilovyojichokea, watu waliochoka kuanzia taswira mpaka uhalisia wa maisha n.k.
Mtu anaweza maliza miaka 5 hajawahi kumuona na hamjui hata kiongozi wa serikali ya mtaa na hana.Hivi kwa mzingira hayo hawa vijana wa siku hizi wataheshimu kweli uchaguzi wa kuwaweka hao madarakani, na tunakoelekea na uchaguzi huu utaendelea kudharaulija mpaka ujifie kabisa.
Na ndo maana huwezi ona vijana wenye mawazo mapya wanapambana et awe mteule wa mtaa - watu wanapambana waingie bungeni - wapige perdiem, wanapambana waingie serikali kuu - wapate mav8 n.k.
Mpaka pale tutakapopata katiba itakayoempower watu wa chini ndo na hizi chaguzi zitakuwa na maana.
Nchi yetu inasikitisha sana - inauma sana - viongozi wetu hawajali na ni kama hawajui kusolve matatizo au sijui ni uelewa?? Ni kama wao wanaulimwengu wao na wananchi wanaulimwengu wao.
Pale ambapo tutawezs kuepower watu huku chini kabisa, watu wafanye na wawe na uwezo wa kujifanyia maendeleo yao madogo madogo ndo tutapata maendeleo kama taifa na uzalendo, otherwise kila mtu aendelee kugombania goli- ale alipo mpaka siku akili zitukae sawa.