Nini kina sababisha siku za hedhi kupitiliza kama huna mimba?

Nini kina sababisha siku za hedhi kupitiliza kama huna mimba?

pole sana ndugu, hl tatizo sio geni masikioni mwangu, kwani lilishawapata marafiki zangu kama watatu hv, nilisikia linatokana na kula chakula cha aina moja ila cjawah fanya uchunguz kuprove, we nenda hospital ukapime uone nini tatizo.
 
Mi mzima mamii, naona unamtisha mdada wa watu, katembea na mume wa mtu so wameshamtengeneze ahahahah

hahaaahahahahah shost wangu hujambo ni moja ya diagnosisi na troubleshooting za kwanza
 
kama unatumia dawa za uzazi wa mpango madhara yake ndio hayo. nakama hautumii muone daktari atakupa ushauri
 




Mwanamke 1 katika wanawake 3 hupatwa na tatizo la kuvuja damu nyingi wakati za siku zao. Hata hivyo, mara nyingi ni vigumu kujua kama mwanamke anatoka damu nyingi au kawaida ikilinganishwa na wanawake wengine wakati wa hedhi. Baadhi ya wanawake ambao wanahisi kuwa huvuja damu nyingi wakati wa siku zao hakika wanapoteza damu kiasi cha wastani.Baadhi ya wanawake ambao wanaona kuwa wanapoteza kiasi cha kawaida huwa wanapoteza damu nyingi.



Ufafanuzi
mzunguko wa kawaida - upotevu wa damu hukadiriwa kuwa kati ya mls 20 na 60 (vijiko vya chai 4-12 ). Kutokwa na damu inaweza kudumu hadi siku nane, lakini wastani ni siku tano .
Kutoka damu nyingi - upotevu wa damu ni kati ya mls 60-80 au zaidi. Hii ni kama nusu kikombe au zaidi. Hata hivyo, ni vigumu kupima kiasi cha damu ambacho kinapotea wakati wa mzunguko. Lakini unaweza kutambua kama unavuja damu nyingi iwapo :
-Damu zinafurika na kulowanisha nguo au matandiko.
-Unahitaji kubadilisha mara kwa mara kitambaa au pedi.
-Unahitaji vitambaa au pedi mbili au zaidi.
-Unapata damu zenye mabonge .

Menorrhagia ni hali ya kuvuja damu nyingi kila mwezi mwanamke anapokuwa kwenye hedhi. Pia, damu inayovuja inaweza kuathiri ubora wa maisha . Kwa mfano,hufanya mwanamke kushindwa kufanya shughuli zake za kawaida kama vile kufanya kazi au kwenda shuleni.


Sababu.
Mara nyingi sababu haijulikani. Lakini magonjwa yafutayo yanaweza kusababisha mwanamke kuvuja damu nyingi
-Dysfunctional uterine bleeding-katika tatizo hili mwanamke huvuja damu bila kuwepo ugonjwa wowote katika

mfuko wa mayai. Inadhaniwa kuwa chemikali iitwayo prostaglandin inaweza kuchangia tatizo hili. Linatokea katika miaka ya mwanzo baada ya kuvunja ungo.
-Uvimbe kwenye mfuko wa uzazi
-maambukizi kwenye kizazi
-matatizo ya hormoni
-saratani ya kizazi hasa kwa wanawake wenye umri mkubwa.
-kitanzi(IUD)-hiki ni kifaa kinachowekwa kwa utaalamu kwenye mfuko wa kizazi.
-Dawa mfano dawa za kutogandisha damu,matibabu ya saratani nk


Uchunguzi
Vipimo mbalimbali vinaweza kuhitajika ili kujua sababu ya kuvuja damu nyingi wakati wa hedhi mfano ultrasound,kipimo cha hormoni na wakati mwingine uchunguzi hufanywa kuangalia kama kuna tatizo lolote wakati mwanamke amepewa dawa za usingizi.

Matibabu
Matibabu ya msingi hutegemea dalili na chanzo cha tatizo. Hata hivyo daktari anaweza kuanza kutibu dalili wakati akiendelea na uchunguzi.

 
Kuna jamaa mmoja Uingereza alifanya majaribio ya uchungu wanaopata wanawake wakati wa kujifungua,hakufika hata nusu ya uchungu akazimika,ukifikiria sana kuhusu mwanamke sidhani kama kuna ambaye anaweza kuwadharau.

dah! najaribu kuimagine mwanaume apite first, second na third stage ya labour.
hasa apitie 1st and 2nd dah!

lakini hivi mwanume akiekewa oxytocin IV hatapata haya maumivu?? eti MziziMkavu na Dr Riwa??
 
Last edited by a moderator:
Kuna jamaa mmoja Uingereza alifanya majaribio ya uchungu wanaopata wanawake wakati wa kujifungua,hakufika hata nusu ya uchungu akazimika,ukifikiria sana kuhusu mwanamke sidhani kama kuna ambaye anaweza kuwadharau.


Kwa mwanamme anayedharau na kupiga mwanamke atakuwa tu amewehuka.
 
jaman wanajamvi naomba mnisaidie shemeji yenu amekumbwa na tatizo yaan toka ameanza bleeding mwenzi wa tano amekuwa akivuja damu mara kwa mara yani kila baada ya wk moja anatoka damu nyingi amejaribu kwenda kwa dokta kapewa dawa bt tatizo bado lipo naomba msaada tafadhari suluhu ya hili kwa wataalamu wanao jua plz plz plzjaman wanajamvi naomba mnisaidie shemeji yenu amekumbwa na tatizo yaan toka ameanza bleeding mwenzi wa tano amekuwa akivuja damu mara kwa mara yani kila baada ya wk moja anatoka damu nyingi amejaribu kwenda kwa dokta kapewa dawa bt tatizo bado lipo naomba msaada tafadhari suluhu ya hili kwa wataalamu wanao jua plz plz plz


Ajaribu kutumia Flaxseeds zinapatikana kariakoo au Kisutu. Pia anywe sana juice ya nanasi. Pitia hapa kisha tuwasiliane: Mafanikio Na Afya Njema: Maumivu ya Tumbo ya Wanawake - Natural Home Remedies for Endometriosis
 
Anaweza kuwa ametumia vizuia mimba kama sindani/vipandikizi ambavyo vimemkataa.Atumie vidonge vya uzazi kurekebisha mzunguko.
Mke wangu aliwahi kupata tatizo hili na kuhangaika mahospitalini lakini alikuja kusaidiwa na mkunga mmoja mzoefu kwa kumpa ushauri niliokuandikia hapo juu na imemsaidia hadi sasa yupo fiti.Sasa ameacha kabisa hayo madawa na tuna tumia kalenda.
 
Jamani ni husababisha kwa baadhi ya watu damu ya hedhi kutoka kwa kipindi kirefu,kwa mfano kuna mtu ana breed kuanzia tarehe tatu septemba mpaka leo bado dalili ya breed kuisha haionekani.Je nini tiba yake kama ni ugonjwa.Eti madaktari wamemwambia azae na yeye hana mpango wa kuzaa je kweli kuzaa ndio suluhisho
 
ina maana ovulation inafanyika kila kukicha kwake...azae tu hali itaondoka ingawa itarudi pale mtoto atakua amekaa mda bila kupata mdogo wake.
 
Back
Top Bottom