Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 94,296
- 122,540
Wanasema eti kuuliza si ujinga! Wakati ujinga ni hali ya kutojua kitu au jambo fulani.
Sasa kama kitu unakijua au jambo unalijua, unauliza ili iweje sasa?
Baadhi ya hii misemo ya Kiswahili ukiichambua kwa undani utabaini haina mantiki kabisa.
Ah! Hayo ya misemo ya Kiswahili tuyaache kwa leo maana nina ujinga wa mambo kadha wa kadha na ningependa niufute.
Haya twende kazi:
Hivi, hili suala la katiba mpya ni suala la fadhila ya Rais aliyepo madarakani au?
Nauliza hivyo kwa sababu tokea hili vuguvugu lianze tena baada ya kifo cha Rais Magufuli, kumekuwepo na maombi kwa Rais Samia kuwa aurejeshe tena mchakato wa katiba mpya.
Mara kadhaa sasa yeye Rais Samia keshasema suala hilo lisubiri [kidogo/ kwanza] maana anataka aisimamishe kwanza nchi kiuchumi.
Ni kama sielewi elewi vile inakuwaje suala muhimu kama hilo kuhusu mustabali wa taifa liwe ni suala la hisani ya mtu mmoja ilhali taifa linakadiriwa kuwa idadi ya watu takriban milioni 60.
Jingine ambalo silielewi elewi ni hili suala la huyu jamaa wa CHADEMA aitwaye Mdude Nyagali.
Hivi hilo ‘Mdude’ ni jina lake kweli? 🤔
Baada ya kutoa kauli yake ya hivi karibuni kwamba kimsingi ataendelea kuanzia palepale alipoishia kabla ya kwenda jela kipindi Rais Magufuli akiwa hai, kumekuwepo na maneno maneno ya kwamba auchunge mdomo wake kuhusu anayoyasema dhidi ya Rais Samia kwa sababu yeye Mama Samia ndo kamtoa huko jela alikokuwa.
Ina maana Tanzania mtu kuwa jela au kuwa huru kunaweza kutegemea hila ama fadhila za Rais aliyepo madarakani na si sheria za nchi?
Madai ni kwamba Mdude alibambikiwa kesi na utawala wa Magufuli. Lakini utawala wa Samia umeamua kumwachia huru 🤦♂️.
Rais Magufuli alipiga marufuku wanasiasa kufanya shughuli za kisiasa nchini. Akasema eti wanaruhusiwa tu kufanya shughuli hizo kwenye majimbo yao.
Ajabu kweli kweli maana Tanzania ni nchi iliyo huru na nijuavyo Mtanzania yeyote yule ana haki ya kufanya kazi sehemu yoyote iliyo nchini mwake.
Kaja Rais Samia naye anaendelea na uamuzi huo huo wa kupiga marufuku shughuli za kisiasa kwa wanasiasa nje ya majimbo yao isipokuwa kwa CCM tu.
Ni wazi kabisa kuwa hii amri ni ukiukwaji wa katiba maana shughuli za kisiasa ni haki kwa mujibu wa katiba.
Sielewi kwa nini wanasiasa wa upinzani hawaikaidi hiyo amri maana sheria ipo upande wao.
Kwani kwa mfano wakiamua kuzifanya hizo shughuli za kisiasa nchi nzima, nini kitawatokea?
Watakamatwa na polisi na kufungwa jela? Watashitakiwa na serikali kwa kosa/ makosa gani?
Watafikishwa mahakamani na kushitakiwa kutenda kosa/ makosa gani?
Kama wanachokifanya ni haki yao kikatiba, ni mahakama gani itayowapata na hatia ya kuitumia haki yao ya kikatiba?
Hii nchi bana…imejaa watu wa ajabu kweli!
Sasa kama kitu unakijua au jambo unalijua, unauliza ili iweje sasa?
Baadhi ya hii misemo ya Kiswahili ukiichambua kwa undani utabaini haina mantiki kabisa.
Ah! Hayo ya misemo ya Kiswahili tuyaache kwa leo maana nina ujinga wa mambo kadha wa kadha na ningependa niufute.
Haya twende kazi:
Hivi, hili suala la katiba mpya ni suala la fadhila ya Rais aliyepo madarakani au?
Nauliza hivyo kwa sababu tokea hili vuguvugu lianze tena baada ya kifo cha Rais Magufuli, kumekuwepo na maombi kwa Rais Samia kuwa aurejeshe tena mchakato wa katiba mpya.
Mara kadhaa sasa yeye Rais Samia keshasema suala hilo lisubiri [kidogo/ kwanza] maana anataka aisimamishe kwanza nchi kiuchumi.
Ni kama sielewi elewi vile inakuwaje suala muhimu kama hilo kuhusu mustabali wa taifa liwe ni suala la hisani ya mtu mmoja ilhali taifa linakadiriwa kuwa idadi ya watu takriban milioni 60.
Jingine ambalo silielewi elewi ni hili suala la huyu jamaa wa CHADEMA aitwaye Mdude Nyagali.
Hivi hilo ‘Mdude’ ni jina lake kweli? 🤔
Baada ya kutoa kauli yake ya hivi karibuni kwamba kimsingi ataendelea kuanzia palepale alipoishia kabla ya kwenda jela kipindi Rais Magufuli akiwa hai, kumekuwepo na maneno maneno ya kwamba auchunge mdomo wake kuhusu anayoyasema dhidi ya Rais Samia kwa sababu yeye Mama Samia ndo kamtoa huko jela alikokuwa.
Ina maana Tanzania mtu kuwa jela au kuwa huru kunaweza kutegemea hila ama fadhila za Rais aliyepo madarakani na si sheria za nchi?
Madai ni kwamba Mdude alibambikiwa kesi na utawala wa Magufuli. Lakini utawala wa Samia umeamua kumwachia huru 🤦♂️.
Rais Magufuli alipiga marufuku wanasiasa kufanya shughuli za kisiasa nchini. Akasema eti wanaruhusiwa tu kufanya shughuli hizo kwenye majimbo yao.
Ajabu kweli kweli maana Tanzania ni nchi iliyo huru na nijuavyo Mtanzania yeyote yule ana haki ya kufanya kazi sehemu yoyote iliyo nchini mwake.
Kaja Rais Samia naye anaendelea na uamuzi huo huo wa kupiga marufuku shughuli za kisiasa kwa wanasiasa nje ya majimbo yao isipokuwa kwa CCM tu.
Ni wazi kabisa kuwa hii amri ni ukiukwaji wa katiba maana shughuli za kisiasa ni haki kwa mujibu wa katiba.
Sielewi kwa nini wanasiasa wa upinzani hawaikaidi hiyo amri maana sheria ipo upande wao.
Kwani kwa mfano wakiamua kuzifanya hizo shughuli za kisiasa nchi nzima, nini kitawatokea?
Watakamatwa na polisi na kufungwa jela? Watashitakiwa na serikali kwa kosa/ makosa gani?
Watafikishwa mahakamani na kushitakiwa kutenda kosa/ makosa gani?
Kama wanachokifanya ni haki yao kikatiba, ni mahakama gani itayowapata na hatia ya kuitumia haki yao ya kikatiba?
Hii nchi bana…imejaa watu wa ajabu kweli!