Nini kinachotuongoza? Sheria na Katiba au hila na fadhila za Rais?

Nini kinachotuongoza? Sheria na Katiba au hila na fadhila za Rais?

Rais anafurahia sana ujinga wa wananchi, maana hata kilicho chao wanaenda kumwomba Rais.

Kuna siku tutaenda kumwulizavRais, kama tuvae suruali au misuli!

Huu utukufu wa Rais, ni sisi ndio tunampa kutokana na uwoga, ujinga, na unafiki wetu. Katiba inasema vyama vina haki ya kufanya siasa wakati wowote, svyama vinasubiri mpaka Rais aseme, nendeni mkafanye siasa.

Mbowe alikuwa sahihi sana kusema wataanza kufanya mikutano ya hadhara. Hakuwa hata na haja ya kumtaja Rais. Alitakiwa tu kutoa maelekezo kwa viongozi na wanachama, maana ni haki ya kikatiba. Tutamshangaa atakayezuia, tutamwuliza ni kwa sheria ipi anazuia.
Mimi naombea waanze hiyo mikutano.
 
Tumejawa na watu tunaopenda hisani siyo haki, watu haki zetu za msingi tunahisi tunapaswa kuwabembeleza wakubwa watupatie.

Cha kushangaza tunafurahia hili jambo na ajabu zaidi ukionekana unadai haki Watanzania wenzako huanza kukusuta na unaonekana huitakii mema nchi yako.
Mkuu watanzania nima-snitch yaani mtu anavunja kitu muhimu kwa ustawi wa taifa alafu Kuna kundi la mazwazwa linaona ni sawa
 
Sawa haki sio hisani naelewa ila kuna namna ya kuidai hio haki! Angalia nani anapaswa akupatie hio haki? Personality traits zake zikoje? Kuna watu wanataka kuwa pleased ili upate unachotaka na ambao ndio wengi kuliko wale ambao wanajua kukupatia haki ni wajibu wao so hutenda bila kuombwa!

Shida ya hawa ndugu zetu wao wanataka haki kwa kupush kauli za kibabe! Ukikutana na mtu mwenye roho ngumu anakufyekelea mbali and the rest is history! Tuwe na adabu kidogo...tunadai haki ila tuwe na adabu kidogo huwezi kuvunja vipengele vya katiba kwa makusudi hii ni nchi yenye utawala wa sheria sio kijiwe cha kahawa kwamba lugha za chooni ni ruksa kwa yeyote yule!

Ombeni kibali fateni taratibu mkinyimwa lalamikeni na mtoe hoja zenu mama personality yake ni rahisi kusikiliza watu. She is not a harsh person kama mtangulizi wake so mambo yanaweza kwenda smooth watu wakitumia akili vizuri. Wakitaka ubabe vijana wenye kazi ya kuwatuliza wapo!

Ningependa hao wanaojitia wana uchungu sana na katiba wapeleke matumbo yao mbele na familia zao kisha wakifanikiwa kwenye hio vurugu watanzania wengine watafuata!

Mie nimesema ntashiriki mchakato wa hio katiba mpya kama kutakuwa na kipengele cha wananchi kupewa hela ya maendeleo 5M cash kwenye account zao kila mwanzo wa mwaka mpya wa serikali. Kama hilo litakuwepo ntawaunga mkono ila kama ni lile la kuwaingiza akina Mbowe Ikulu tu basi sihusiki na shughuli hio!
Kumbe na wewe unajuwaga kuandika hivi!??? 🙂 Huwa nadhani unachofahamu tu ni kulaiki 🙂
 
Kama katiba ya sasa inavunjwa ni vipi hiyo mpya itaheshimiwa?

Nadhani ungeanza usimamizi thabiti wa katiba ya sasa kabla ya kudai mpya.

Aidha CHADEMA wanadai katiba mpya ili iwasaidie kushika dola ila sio kumsaidia mwananchi wa kawaida katika shughuli zake za kila siku.
 
Mkuu umejikita katika kulinda maslahi ya muda mfupi na yanayo umiza. Kudai haki yako siyo kumshurutisha mtu ni kitu ambacho unadeserve kupata siyo kuwa unahurumiwa.

Harafu ukidai haki yako kwa huyo boss hata usipodumu katika hiyo kazi naamini siyo vibaya cha msingi hujataka haki yako kusiginwa.

| tunapalilia dhuluma hivyo uvinjifu wa haki unamea na kustawi katika jamii zetu|
Hivi unajua hio haki mnayotaka kuidai kwa ubabe itaambatana na mkong’oto wa FFU?

Hakuna asiyetaka kudai haki ya katiba ila je umejiandaaje na kichapo hicho maana lazma utata utakuwa mkubwa! Kama ulikuwepo zama za Mwembechai 1996 basi kile kilichotokea ndio hasa kitatokea maeneo mengi ya nchi katika kizazi hiki mayai mayai nani yupo tayari kwa ule uharibifu?

Nikiangalia hio katiba haininufaishi moja kwa moja bado! Nimesema ntapambania katiba kama kuna kipengele cha mwananchi kupewa gawio lisilopungua 5M kila mwaka wa serikali unapoanza ili kupunguza makali ya maisha! Siwezi kupambania ndoto za wanasiasa wao wakabunye zao Burj Khalifa kila December wakati mie naganga njaa!
 
Na wakati ni katiba hiyo hiyo ndo iliyo mpa madaraka akisha pata oath basi katiba ni takataka kwake ila mawazo yake ndo yafuate utadhani Mungu ndo kamuweka
Hahahahah raisi akifata kila mnachotaka nchi itatawalikaje? Halafu mnataka katiba ambayo nyie mnachofikiri ndio raisi afanye huyo atakuwa raisi au mdoli!? 😅 Mfano mwepesi tu wewe ndio baba mjengoni kwako ila mtoto wako wa darasa la 4 ndio akupangie utaratibu wa kuendesha nyumba we uliskia wapi? Eti baba usioe nimesema hatutaki mama wa kambo humu 😂😂😂 na we mzee unakubali unaanza kupiga nyeto! We uliskia wapi hilo???

Acheni kuota hata huyo Mbowe akipewa nchi pamoja na katiba mpya hamna kitu atafanya ambacho kitampa ugumu kuwatawala! Mkileta ujinga atatumia polisi na majeshi kama kawa!!!
 
Wanasema eti kuuliza si ujinga! Wakati ujinga ni hali ya kutojua kitu au jambo fulani.

Sasa kama kitu unakijua au jambo unalijua, unauliza ili iweje sasa?

Baadhi ya hii misemo ya Kiswahili ukiichambua kwa undani utabaini haina mantiki kabisa.

Ah! Hayo ya misemo ya Kiswahili tuyaache kwa leo maana nina ujinga wa mambo kadha wa kadha na ningependa niufute.

Haya twende kazi:

Hivi, hili suala la katiba mpya ni suala la fadhila ya Rais aliyepo madarakani au?

Nauliza hivyo kwa sababu tokea hili vuguvugu lianze tena baada ya kifo cha Rais Magufuli, kumekuwepo na maombi kwa Rais Samia kuwa aurejeshe tena mchakato wa katiba mpya.

Mara kadhaa sasa yeye Rais Samia keshasema suala hilo lisubiri [kidogo/ kwanza] maana anataka aisimamishe kwanza nchi kiuchumi.

Ni kama sielewi elewi vile inakuwaje suala muhimu kama hilo kuhusu mustabali wa taifa liwe ni suala la hisani ya mtu mmoja ilhali taifa linakadiriwa kuwa idadi ya watu takriban milioni 60.

Jingine ambalo silielewi elewi ni hili suala la huyu jamaa wa CHADEMA aitwaye Mdude Nyagali.

Hivi hilo ‘Mdude’ ni jina lake kweli? 🤔

Baada ya kutoa kauli yake ya hivi karibuni kwamba kimsingi ataendelea kuanzia palepale alipoishia kabla ya kwenda jela kipindi Rais Magufuli akiwa hai, kumekuwepo na maneno maneno ya kwamba auchunge mdomo wake kuhusu anayoyasema dhidi ya Rais Samia kwa sababu yeye Mama Samia ndo kamtoa huko jela alikokuwa.

Ina maana Tanzania mtu kuwa jela au kuwa huru kunaweza kutegemea hila ama fadhila za Rais aliyepo madarakani na si sheria za nchi?

Madai ni kwamba Mdude alibambikiwa kesi na utawala wa Magufuli. Lakini utawala wa Samia umeamua kumwachia huru 🤦‍♂️.

Rais Magufuli alipiga marufuku wanasiasa kufanya shughuli za kisiasa nchini. Akasema eti wanaruhusiwa tu kufanya shughuli hizo kwenye majimbo yao.

Ajabu kweli kweli maana Tanzania ni nchi iliyo huru na nijuavyo Mtanzania yeyote yule ana haki ya kufanya kazi sehemu yoyote iliyo nchini mwake.

Kaja Rais Samia naye anaendelea na uamuzi huo huo wa kupiga marufuku shughuli za kisiasa kwa wanasiasa nje ya majimbo yao isipokuwa kwa CCM tu.

Ni wazi kabisa kuwa hii amri ni ukiukwaji wa katiba maana shughuli za kisiasa ni haki kwa mujibu wa katiba.

Sielewi kwa nini wanasiasa wa upinzani hawaikaidi hiyo amri maana sheria ipo upande wao.

Kwani kwa mfano wakiamua kuzifanya hizo shughuli za kisiasa nchi nzima, nini kitawatokea?

Watakamatwa na polisi na kufungwa jela? Watashitakiwa na serikali kwa kosa/ makosa gani?

Watafikishwa mahakamani na kushitakiwa kutenda kosa/ makosa gani?

Kama wanachokifanya ni haki yao kikatiba, ni mahakama gani itayowapata na hatia ya kuitumia haki yao ya kikatiba?

Hii nchi bana…imejaa watu wa ajabu kweli!
Wakati was msukuma mwenzio JPM ulikuwa unasifu na kuabudu
 
Hahahahah raisi akifata kila mnachotaka nchi itatawalikaje? Halafu mnataka katiba ambayo nyie mnachofikiri ndio raisi afanye huyo atakuwa raisi au mdoli!? 😅 Mfano mwepesi tu wewe ndio baba mjengoni kwako ila mtoto wako wa darasa la 4 ndio akupangie utaratibu wa kuendesha nyumba we uliskia wapi? Eti baba usioe nimesema hatutaki mama wa kambo humu 😂😂😂 na we mzee unakubali unaanza kupiga nyeto! We uliskia wapi hilo???

Acheni kuota hata huyo Mbowe akipewa nchi pamoja na katiba mpya hamna kitu atafanya ambacho kitampa ugumu kuwatawala! Mkileta ujinga atatumia polisi na majeshi kama kawa!!!
Leo naona umewaamkia; umewachomolea koki kabisa!!! Hatari na nusu!!! Bi Mkubwa anaweza kukupatia cheo hata leo au kesho, ngoja tungojee siye 🙂 🙂 🙂
 
Kunapokuwa na mushkeri kwenye mfumo wa maisha hasa uminywaji wa fursa na haki ndipo vuguvugu hujitokeza.
Mifano ni mingi, wanawake wanadai 50/50, walemavu wana madai yao, wapinzani nk. Nk.
Ni nani hasa anayedaiwa? Je, wanaona hayo mapungufu? Ni kwa nini wanagugumia kama wanayaona.
Ni hivi, mwenye shibe hamjui mwenye njaa.
Watawala duniani wamejitwalia haki zote hawana cha kudai zaidi ya utii na heshima na warudishe hisani ikiwapendeza.
Eti raia wanakiri, neno la mfalme ni amri wakati la raia ni ombi.
Kwa jinsi hii dunia itachelewa sana kuendelea. NENO LA MFALME LIWE OMBI NA NENO LA RAIA LIWE AMRI hapo watawala watageukia haki na nchi itaendelea.
Iweje kilicho haki kitafutwe kwa maombi ilhali kisicho haki chatendwa kwa amri?
 
Sawa haki sio hisani naelewa ila kuna namna ya kuidai hio haki! Angalia nani anapaswa akupatie hio haki? Personality traits zake zikoje? Kuna watu wanataka kuwa pleased ili upate unachotaka na ambao ndio wengi kuliko wale ambao wanajua kukupatia haki ni wajibu wao so hutenda bila kuombwa!

Shida ya hawa ndugu zetu wao wanataka haki kwa kupush kauli za kibabe! Ukikutana na mtu mwenye roho ngumu anakufyekelea mbali and the rest is history! Tuwe na adabu kidogo...tunadai haki ila tuwe na adabu kidogo huwezi kuvunja vipengele vya katiba kwa makusudi hii ni nchi yenye utawala wa sheria sio kijiwe cha kahawa kwamba lugha za chooni ni ruksa kwa yeyote yule!

Ombeni kibali fateni taratibu mkinyimwa lalamikeni na mtoe hoja zenu mama personality yake ni rahisi kusikiliza watu. She is not a harsh person kama mtangulizi wake so mambo yanaweza kwenda smooth watu wakitumia akili vizuri. Wakitaka ubabe vijana wenye kazi ya kuwatuliza wapo!

Ningependa hao wanaojitia wana uchungu sana na katiba wapeleke matumbo yao mbele na familia zao kisha wakifanikiwa kwenye hio vurugu watanzania wengine watafuata!

Mie nimesema ntashiriki mchakato wa hio katiba mpya kama kutakuwa na kipengele cha wananchi kupewa hela ya maendeleo 5M cash kwenye account zao kila mwanzo wa mwaka mpya wa serikali. Kama hilo litakuwepo ntawaunga mkono ila kama ni lile la kuwaingiza akina Mbowe Ikulu tu basi sihusiki na shughuli hio!
Wewe ni Mpuuzi unayedhani Katiba ni Takwa la CHADEMA
 
Waongee kwa hekima na staha! Kutumia lugha kali za vitisho havijawahi kurahisisha mchakato wa kupata unachotaka toka kwa mtu mwenye mamlaka ya kukuzidi. Kama huamini mshurutishe boss wako hapo ofisini juu ya malipo yako yaliochelewa kisha uone utadumu muda gani katika hiko kiti!
Watu kama Zitto na Mbowe ni wajanja wajanja sana. Wanaijua mamlaka ya Rais wa Tanzania vizuri.

Ndio maana sometimes Zitto huwa anapata mihemko anaandisha harsh sana mtandaoni, halafu baada ya dakika 2 unakuta kafuta.

Ukishampa mtu madaraka hata akiwa chizi, ndio imetoka hiyo. Lazima utumie busara sana.

Ni sawa na mtu kwenye nchi yenye madereva wasiotii sheria za barabarani kutembea kwa madoido katikati ya zebra ukijua una haki zote.

Ukigongwa ukafa au ukavunjwa miguu, hata wakileta traffic police 3,000 wakapima na kuonesha umeonewa na dereva ndio mkosaji, wewe miguu yako au uhai hauwezi kurudi.

Zitabaki stori tu.
 
Watu kama Zitto na Mbowe ni wajanja wajanja sana. Wanaijua mamlaka ya Rais wa Tanzania vizuri.

Ndio sometimes Zitto huwa anapata mihemko anaandisha harsh sana mtandaoni, halafu baada ya dakika 2 unakuta kafuta.

Ukishampa mtu madaraka hata akiwa chizi, ndio imetoka hiyo. Lazima utumie busara sana.

Ni sawa na mtu kwenye nchi yenye madereva wasiotii sheria za barabarani kutembea kwa madoido katikati ya zebra ukijua una haki zote.

Ukigongwa ukafa au ukavunjwa miguu, hata wakileta traffic police 3,000 wakapima na kuonesha umeonewa na dereva ndio mkosaji, wewe miguu yako au uhai hauwezi kurudi.

Zitabaki stori tu.
Yeah nobody care ushaumizwa kesi inamalizwa chap chap inabaki story!
 
Wanasema eti kuuliza si ujinga! Wakati ujinga ni hali ya kutojua kitu au jambo fulani.

Sasa kama kitu unakijua au jambo unalijua, unauliza ili iweje sasa?

Baadhi ya hii misemo ya Kiswahili ukiichambua kwa undani utabaini haina mantiki kabisa.

Ah! Hayo ya misemo ya Kiswahili tuyaache kwa leo maana nina ujinga wa mambo kadha wa kadha na ningependa niufute.

Haya twende kazi:

Hivi, hili suala la katiba mpya ni suala la fadhila ya Rais aliyepo madarakani au?

Nauliza hivyo kwa sababu tokea hili vuguvugu lianze tena baada ya kifo cha Rais Magufuli, kumekuwepo na maombi kwa Rais Samia kuwa aurejeshe tena mchakato wa katiba mpya.

Mara kadhaa sasa yeye Rais Samia keshasema suala hilo lisubiri [kidogo/ kwanza] maana anataka aisimamishe kwanza nchi kiuchumi.

Ni kama sielewi elewi vile inakuwaje suala muhimu kama hilo kuhusu mustabali wa taifa liwe ni suala la hisani ya mtu mmoja ilhali taifa linakadiriwa kuwa idadi ya watu takriban milioni 60.

Jingine ambalo silielewi elewi ni hili suala la huyu jamaa wa CHADEMA aitwaye Mdude Nyagali.

Hivi hilo ‘Mdude’ ni jina lake kweli? [emoji848]

Baada ya kutoa kauli yake ya hivi karibuni kwamba kimsingi ataendelea kuanzia palepale alipoishia kabla ya kwenda jela kipindi Rais Magufuli akiwa hai, kumekuwepo na maneno maneno ya kwamba auchunge mdomo wake kuhusu anayoyasema dhidi ya Rais Samia kwa sababu yeye Mama Samia ndo kamtoa huko jela alikokuwa.

Ina maana Tanzania mtu kuwa jela au kuwa huru kunaweza kutegemea hila ama fadhila za Rais aliyepo madarakani na si sheria za nchi?

Madai ni kwamba Mdude alibambikiwa kesi na utawala wa Magufuli. Lakini utawala wa Samia umeamua kumwachia huru [emoji2357].

Rais Magufuli alipiga marufuku wanasiasa kufanya shughuli za kisiasa nchini. Akasema eti wanaruhusiwa tu kufanya shughuli hizo kwenye majimbo yao.

Ajabu kweli kweli maana Tanzania ni nchi iliyo huru na nijuavyo Mtanzania yeyote yule ana haki ya kufanya kazi sehemu yoyote iliyo nchini mwake.

Kaja Rais Samia naye anaendelea na uamuzi huo huo wa kupiga marufuku shughuli za kisiasa kwa wanasiasa nje ya majimbo yao isipokuwa kwa CCM tu.

Ni wazi kabisa kuwa hii amri ni ukiukwaji wa katiba maana shughuli za kisiasa ni haki kwa mujibu wa katiba.

Sielewi kwa nini wanasiasa wa upinzani hawaikaidi hiyo amri maana sheria ipo upande wao.

Kwani kwa mfano wakiamua kuzifanya hizo shughuli za kisiasa nchi nzima, nini kitawatokea?

Watakamatwa na polisi na kufungwa jela? Watashitakiwa na serikali kwa kosa/ makosa gani?

Watafikishwa mahakamani na kushitakiwa kutenda kosa/ makosa gani?

Kama wanachokifanya ni haki yao kikatiba, ni mahakama gani itayowapata na hatia ya kuitumia haki yao ya kikatiba?

Hii nchi bana…imejaa watu wa ajabu kweli!
Umerudishiwa akili zako mkuu!!
 
Katiba na Sheria!
Suala hili liliishafikia hatua ya kupiga kura kwa mujibu wa sheria? je tupige kura ?au tuanze upya na rasimu ya Warioba tuiache rasimu ya Sita? Na je tuliisha kubaliana nini kuhusu Muundo wa serikali mbili au tatu? Kama taifa kwa vile viongozi wa siasa hapo ndipo kwenye mvutano mkubwa. Hatutapoteza fedha za wananchi kwa kuanzisha mchakato usio na tija. Tuwe wazi kama sheria zinatuongoza turejee maswali haya muhimu
 
Back
Top Bottom