Nini Sababu: Mume amehama ghafla na kwenda kupanga bila ugomvi wala maelezo yoyote

Nini Sababu: Mume amehama ghafla na kwenda kupanga bila ugomvi wala maelezo yoyote

Kuna point hapo, kiukweli jamaa ni mkavu Kama Hana kilichotokea, juz TU hapa katoka kuwalipia wanae wote ada bila wasiwasi kabisa.
Achaa afanye kile kwake anachoona ni sahihi Kwa wakatii huu ,mpk pale atakapokaa sawaa šŸ˜„
 
Hayo mambo Yao ya ndani mimi siyajui.....lakini tambua kuwa nje ya vifungo vya kiimani na kuiogopa hukumu ya mola wake..... mwanadamu hawezi kuishinda tamaa na vishawishi...... unaweza ukampikia mwanao pilau ili afaidi akakataa alafu unamkuta anagombania ugali na dagaa la chuku chuku nyumba ya jirani
Huwezi linganisha ndoa na tabia za watoto, ndoa zina mambo magumu sana mtu akiongea utashangaa huyu si huwa yupo happy muda wote , kumbe huko ndani kwake ni sarakasi za kutosha
 
Mzee sio kila wakat na sio kwa kila mtu. Tunakutana na kuoana na watu ambao background check zao hatuna kiundani.
Kwakifupi kuna mambo mengi sana ,japo huwa tunayaona ila tunayapuuzia mpaka pale yatutokee puani ndio tunaanzaga kuunga unga dots, sasa bora ushtuke mapema. Saa zngine unashtuka too late
Ujue umenifumbua kitu flani hivi, na mchepuko wangu mmoja hivi, kipind nnachokua nmegombana nae Kila mtu kivyake, ndo kipind Ile miradi viporo niliyoitelekeza napata Ela na akili ya kuifufua. Na kweli Huwa inafufuka.

Tukirudiana TU, naanza upya kutelekeza miradi
 
Ujue umenifumbua kitu flani hivi, na mchepuko wangu mmoja hivi, kipind nnachokua nmegombana nae Kila mtu kivyake, ndo kipind Ile miradi viporo niliyoitelekeza napata Ela na akili ya kuifufua. Na kweli Huwa inafufuka.

Tukirudiana TU, naanza upya kutelekeza miradi
Akili mtu wangu. Haya mambo haya bwana we acha tu
 
Huwezi linganisha ndoa na tabia za watoto, ndoa zina mambo magumu sana mtu akiongea utashangaa huyu si huwa yupo happy muda wote , kumbe huko ndani kwake ni sarakasi za kutosha
Nimeweka mfano wa watoto alama ya nafsi isiyoridhika baada ya kukosa udhibiti.......

Wale walioamua au kuchagua kuishi na mwenza sio kama wamefungwa matamanio bali wamefanikiwa kuyadhibiti matamanio
 
Kwamba askofu kamla mkewe, mbn Kama haiingii akilini mkuu, MKE WA jamaa mlokole na anajiheshim Sana yule.
Hao hao wanaojiheshimu behind the scene utakimbia

Trust me hapo pana ishu kubwa sana ya usaliti,si kawaida kwa mwanaume kufanya maamuzi magumu kiasi hicho

Kama ukitaka kujua ukweli wa hilo,mwambie mkeo afanye kazi ya ziada aongee na mwanamke mwenzake ukweli utajulikana tu
 
Anasema keshapeleka kesi Kwa wazazi pande zote mbili, mumewe anadai hamna tatzo, Kuna mambo anayaweka sawa, yakikaa sawa atarudi nyumbani,wala Hana tatzo nae.

Kavumilia Sana Ila haoni dalili yoyote mumewe kurudi. Anadai keshapeleka kesi kanisani, mumewe alishaitwa Sana kagoma kwenda na Kuna siku kapigiwa kamtukana Hadi askofu.

Kwa red hapo.......
Labda anafanya mipango ahamie upande wa pili...
 
Binafsi nachoona kwanza Jamaa ni wale watu wasiri sana, wenye hulka ya upole na ukimya. Mtu wa aina hyo sio rahisi kufungua kifua chake kujua aloyaficha.
Kikubwa inakubidi kwanza ww msuluhishi uwe na uwezo wa kusoma Saikolojia ya mtu, unamuhoji na kuongea naye je unavyomuona anayoongea yanatoka moyoni (ya ukweli)?, au anaongea ili tuu uridhike mada iishe? Ukizingatia hilo utajua nn kinaendelea.
*
Mke angekuwa muelewa na mvumilivu angekausha asubiri huo muda ambao jamaa kasema atarudi akimalza mambo yake, ikiwa jamaa haachi kupeleka matumizi home basi bdo anaipenda familia yke, angekuwa hawataki asingepokea simu na mawasiliano na wala matumizi asingepeleka home. Mke huenda anapanik kwa kukosa haki yke ya ndoa, basi angefnya utaratibu na mumewe awe hta anaenda kupeana huko jamaa alipo, huku mke akisubiri muda wa jamaa kurejea home.
*
Tumia njia ya kufanya mawasiliano na wazaz wake kuwachimba kiundan lazma kawaambia lengo lake ama yale yanayomsibu, ila ww anashndwa kukweleza Coz ww n rafiki tuu na upo karibu na mkewe huenda siri yke itafika asipotaka ifike.
*
Mtumie mkeo kumdadisi kiundan mke w jamaa, huenda kuna dalili jamaa aliziona kwa mkewe (kiusaliti, shirikina n.k) ambazo jamaa hajazipenda na kwakuwa dini yke haimtaki kuachana mpaka kifo anaona hyo ndo njia sahih ya kukaa mbali na mkewe.
*
Mwisho; ukiona ktk hayo bdo hupati muelekeo, kaa kimya usiendelee kumuuliza jamaa kuhusu hilo suala maana huenda ukawa wamkera na baadae mkaja kutia dosari urafiki wenu.
 
Huyo jamaa ni kama mimi tu, siwezi kumwambia mtu yoyote upuuzi wa mke wangu, nikishasema tu sioni sababu ya kuendelea kuishi nae na nikisha achana na wife sioni bababu ya kuongea chochote.

Huyo mwanamke anajua sababu kwanini hadi kaachwa ila hataki kusema yeye anataka eti aliyekuwa mume wake ndo aseme.
 
Wakuu,
Huyu jamaa ni jirani yangu haswa, yaani tunashare upande mmoja WA ukuta wa fensi,shughuli nyingi za kifamilia Huwa anashiriki vizuri Sana, migogoro pia anakuja kusuluhisa na kunishauri pia.

Japo Kwa ndoa yake niliamini Ni ndoa iliyokamilika haswa maana tangu miaka yote tuishi hapa sijawahi kusikia kagombana na mkewe Hata siku moja, hivyo Huwa nawaheshimu sn.

Kuna siku mkewe alileta malalamiko kwangu kua mmewe kahama nyumbani kwake ghafla,

Anasema siku ya mwisho kuonekana NYUMBANI, aliaga Kama kawaida anaenda kazini kwake asbh na MAPEMA na ndo hakurudi mazima mpaka Leo hii.

Anadai hakubeba chochote kile nyumbani, Kila kitu Kiko Kama kilivyo kua, hawajagombana na wala hajaambiwa kipi kamkosea.

Anadai Mume wake tangu ahame matumizi ya Kila siku anatoa vzur Ila haifiki kabisa nyumbani. anapewa boda ndo apeleke.

Anasema mumewe akipigiwa simu anapokea anadai atarudi TU Ila kavumilia Sana anaona haioni dalili yoyote ya mumewe kurudi nyumbani.

Anasema alishapeleleza Sana hadi kujua anapoishi, kaenda Sana pale (Hadi mida ya usiku sn) labda Kuna mwanamke anaishi nae pale Ila kathibitisha mumewe anaishi peke yake TU na haijawai kuleta mwanamke yeyote pale Hata siku moja.

Anasema keshapeleka kesi Kwa wazazi pande zote mbili, mumewe anadai hamna tatzo, Kuna mambo anayaweka sawa, yakikaa sawa atarudi nyumbani,wala Hana tatzo nae.

Kavumilia Sana Ila haoni dalili yoyote mumewe kurudi. Anadai keshapeleka kesi kanisani, mumewe alishaitwa Sana kagoma kwenda na Kuna siku kapigiwa kamtukana Hadi askofu.

Anasema ilivyofika miezi 3 haoni dalili yoyote akajaribu kwenda ustawi WA jamii kumfungulia kesi ya kutelekeza familia (labda atapata hofu ya serikali), mumewe alivotoka uko ndo kamchukia kabisa na kamblock kwenye mawasiliano yake yote na pesa za matumizi ya familia Kwa Sasa anachukulia ustawi WA jamii.

Jamaa nimejaribu kumdadisi tatzo Nini,hataki kabisa kufunguka, anadai hana tatzo lolote na mkewe, Kuna mambo yake kadhaa anayaweka sawa, punde tu atarejea home nisijali.

Kila mara nimejaribu kumkubushia mkewe anavoteseka kuukosa uwepo wake nyumbani, jamaa Wala haoneshi kujali, miezi 6 sasa inakatika, jamaa hana mahusiano yoyote nje, kuoa mke mwingine Wala Hana mpango wowote WA kurejea nyumbani kwake.

Watoto wao wote sahv wamerejea mashuleni, mkewe juzi kati kaumwa sn mpk kalazwa, jamaa kataarifiwa Ila katuma pesa TU Hata hajakanyaga hospital Wala kumpiga simu kumjulia hali.

Aliporuhusiwa ikabd ahamie kwangu mpk atakapokaa sawa maana watoto wao wote wamesharud mashuleni, jamaa nilimtaarifu Hilo ili atoe ruksa mkewe augulie kwangu, kasema sawa Haina shida. Ni Mwezi Sasa mkewe anashinda,kula na kulala nyumbani kwangu. Jamaa Hana Hata wasiwasi.

Juzi kati kanunua kiwanja nje ya mji, kaniita nimsainie Kama shahidi na kashaanza msingi anasema hapa ndo anajenga makazi yake mapya.

Namuuliza hii inamaanisha Nini khs hatma ya familia yake, anasema haihusiani kbs na familia yake, na Wala nisije thubutu kumwambia chochote mkewe khs hili suala TUTAGOMBANA. Nkamwambia sawa Haina shida.

Hebu wakuu,
Huenda mi sio nzur kwny mambo kusuluhisha migogoro ya ndoa za watu.

Najua humu mna mawazo mazur sn na wataalam tele WA ishu hizi za ndoa.

Hebu nipeni mawazo mawili matatu niweze kuinusuru hii ndoa ya Hawa jirani zangu.

Mkewe tangu jamaa ahame, saivi Kawa Kama kuchanganyikiwa , simuelewi elewi kabisa. Hata anachoumwa Hata hakieleweki, nahisi ni stress za ndoa zake.

Pia, KUISHI NA MKE WA MTU NYUMBANI KWANGU, KIUKWELI binafsi nijistukia kua kimaadili HAIKAI VIZURI kabisa.

Nawasilisha wakuušŸ™
Ameamua kujipa likizo kwa muda ila nadhani mkewe atakua anajua ndio maana anapata presha presha za hapa na pale, kama alichat na akasahau kufuta now kimemramba... Wengine hawana muda na drama za mapenzi.
 
Pia, KUISHI NA MKE WA MTU NYUMBANI KWANGU, KIUKWELI binafsi nijistukia kua kimaadili HAIKAI VIZURI kabisa.

Mpeleke kwa wazazi wake au ndugu zake. Siku akitokewa na mengine huku labda pia ndio muda wa kutolewa kafwalwa basi yatakukuta wewe msamaria mwema, jirani mwema.
 
Back
Top Bottom