Nini Sababu: Mume amehama ghafla na kwenda kupanga bila ugomvi wala maelezo yoyote

Nini Sababu: Mume amehama ghafla na kwenda kupanga bila ugomvi wala maelezo yoyote

Kuna kutofautiana malezi, ujue kuna wengine kwenye circle yao ya makuzi hawana kampani ya aina fulani ya watu ambao kidogo wana uhuni. Ujue ukiwa na wana ambao ni wahuni, kwenye situation kama hizo, huwaga wanaplay vizuri tu kukushauri. Sasa utakuta circle yake aliokuwa nao karibu tokea utoto ni design ya wale wanaojiita "wapendwa",hawajui kuchepuka.
😂😂😂 sasa hapa mkuu kuchepuka kunaingiaje lakin!?
 
😂😂😂 sasa hapa mkuu kuchepuka kunaingiaje lakin!?
Ukiwa na wana then wakakuona mke anakuzingua,wanakutafutia pisi tena kali. Ila ukiwa mpendwa sana,kwenye circle yako hauna mwana hata mmoja ambae mzee wa chini,shughuli unayo.

Mimi kuna wanangu lazima watakuwekea kikao kabisa,wakikuona hueleweki sababu ya kuzinguliwa na nwanamke.
 
Ilaa wanawake bhanaa ss mtu kakuambia mwache Kwanzaa akili ikae sawa atarudii nyumbani ,na umefatilia umemkuta Hana michepuko ,ww unaanza Tena kumvurugaa kwenda Hadi ustawi wa jamii unazidi kumfukuza zaidi Kwa kumchanganyaaa😄😄
Hata mimi nimemshangaa huyo Mwanamke! Baada ya kutatua tatizo anaongeza tatizo! Bila shaka yeye ndio tatizo anatafuta sapoti ya kujihami!
 
Hii ni hali ngumu sana, na inaonyesha kwamba mume huyo ana jambo zito anapitia, lakini hataki kulieleza kwa mtu yeyote.

Kama ameweza hata kumtukana askofu na kukaidi wazazi, huenda hakuna mtu ambaye anamheshimu vya kutosha kumshauri.

Tafuta mtu mmoja ambaye unahisi anaweza kumvuta sikio na kusikilizwa (rafiki wa karibu, mkubwa wake kazini, au mtu anayeaminiwa sana na familia yake

Kama ameanza ujenzi wa nyumba mpya, huenda ameshaamua kuanza maisha mapya mbali na familia yake.

Badala ya kumlazimisha kurudi, jaribu kumpa nafasi ya kueleza nia yake halisi kwa njia isiyo ya kumshinikiza.

Kuhusu kukaa na mke wa mtu

Umefanya jambo la utu kwa kumsaidia mke wa jirani yako, lakini kwa upande wa maadili, ni vyema kutafuta njia mbadala ili asikae kwako kwa muda mrefu. Pengine washirikishe ndugu wa karibu wa mkewe ili wamsaidie kwenye kipindi hiki kigumu.

Mkewe anaonekana kuwa kwenye hali mbaya ya msongo wa mawazo. Tafuta namna ya kumshauri akapate ushauri wa kitaalamu kwa sababu hali hii inaweza kuathiri afya yake kwa kiwango kikubwa.

MWISHO JAPO SI KWA UMUHIMU HUYO MWANAMKE ANAJUA KWANINI MUME WAKE HAATKI KURUDI NYUMBANI, AU KAMA HAJUI HUYO MWANUME HUENDA KUNA MAAGANO AMEINGIA YA KISHETANI HIVYO AKATAKIWA ASIKAE NA MWANAMKE
Ntauzingatia Ushauri huu, sante Sana mkuu
 
Kukosa akili tu. Why sasa anamtesa mtoto wa watu na vituko kama mtoto mdogo?

Ina maana ameshindwa hata kumwambia ukweli au shida ni ipi ili mtoto wa watu ajue shida ni nini?

Kama umeamua kuachana na mtu fanya kwa kufuata taratibu sio unaondoka kama kichaa bila maelezo yoyote yale unaishia kumfanya mtu anaweweseka na pengine akavurugikiwa kiakili na kuwa kichaa kabisa.
 
Ndoa ni aina fulani ya kifungo,kuna jamaa yangu kaoa,huyu mke wake amekuwa msumbufu,simu kila mara,kuulizia mshahara kama umetoka,mara uko wapi? Mara mbona hujanipigia,mara luku imeisha,mara napanua biashara,mara kumanyoko zake,yaani jamaa naona amekuwa stressful, kataeni ndoa wakuu,ila mimi naoa mwakani
 
Kukosa akili tu. Why sasa anamtesa mtoto wa watu na vituko kama mtoto mdogo?

Ina maana ameshindwa hata kumwambia ukweli au shida ni ipi ili mtoto wa watu ajue shida ni nini?

Kama umeamua kuachana na mtu fanya kwa kufuata taratibu sio unaondoka kama kichaa bila maelezo yoyote yale unaishia kumfanya mtu anaweweseka na pengine akavurugikiwa kiakili na kuwa kichaa kabisa.
Mwanamke anaweza akakufanyia ubaya mkubwa kwa siri na bado akiwa public ana play victim na kulia na kugala gala kabisa......hata siku moja usiyaamini machozi ya mwanamke utaangamia.......

Kwa kuwa ni jambo la faragha lakini naamini litakuwa zito na huyo mwanamke anajua labda anaogopa kuliweka wazi pengine ni jambo la aibu kwake kutokana na taswira yake kwenye jamii......

Hata siku moja usimlie yamini mwanadamu kwenye masuala ya faragha mwanadamu anafanya mengi sana na mengine ukiyashuhudia huwezi kuamini......
 
Mwanamke anaweza akakufanyia ubaya mkubwa kwa siri na bado akiwa public ana play victim na kulia na kugala gala kabisa......hata siku moja usiyaamini machozi ya mwanamke utaangamia.......

Kwa kuwa ni jambo la faragha lakini naamini litakuwa zito na huyo mwanamke anajua labda anaogopa kuliweka wazi pengine ni jambo la aibu kwake kutokana na taswira yake kwenye jamii......

Hata siku moja usimlie yamini mwanadamu kwenye masuala ya faragha mwanadamu anafanya mengi sana na mengine ukiyashuhudia huwezi kuamini......
Nakuunga mkono. Ila ni vema angesema wazi tu hatima na asiwe na mambo mengi. Sio lazima kusema aseme kilichotokea sababu inaweza kuwa ni jambo la fedheha kusema. Ila angebainisha hata kwa watu baki kuwa mwanamke amemkosea sana na hataweza msamehe.

Kwasababu kuna watu huwa wanakuwa na hizi shida za kukengeuka katikati ya mahusiano na kugeuka wenzao kwasababu zao binafsi na sio kukosewa.
 
Kila mara nimejaribu kumkubushia mkewe anavoteseka kuukosa uwepo wake nyumbani, jamaa Wala haoneshi kujali, miezi 6 sasa inakatika, jamaa hana mahusiano yoyote nje, kuoa mke mwingine Wala Hana mpango wowote WA kurejea nyumbani kwake.
Labda anataka kuwa padre mkuu. Siku ukikutana naye uje umdadisi kuhusu hilo. Huenda amepata wito wa kumtumikia Mungu kupitia upadre.
 
Aliporuhusiwa ikabd ahamie kwangu mpk atakapokaa sawa maana watoto wao wote wamesharud mashuleni, jamaa nilimtaarifu Hilo ili atoe ruksa mkewe augulie kwangu, kasema sawa Haina shida. Ni Mwezi Sasa mkewe anashinda,kula na kulala nyumbani kwangu. Jamaa Hana Hata wasiwasi.
Ila tu usije ukampapasa mkuu. Ukimgusa tu utamjaza mimba na lawama zote zitahamia kwako.
 
Mkewe tangu jamaa ahame, saivi Kawa Kama kuchanganyikiwa , simuelewi elewi kabisa. Hata anachoumwa Hata hakieleweki, nahisi ni stress za ndoa zake.
Naweza kupata contact zake mkuu?
 
Pole sana kwake.
Kila mtu ana namna yake ya kujitibu anapopata changamoto.

Hapo chanzo kikubwa ni huyo aliyekimbiwa.
 
Kuna group lingine la wanaume waokaa bar na wale wanaopenda kushinda kazini,kurudi makwao ni night kali nao wana mengi ya kusema ndio hivyo wameamua kumezea ila ndani wanaumia japo hawasemi.

Wale wanaoshinda bar unaweza sema ni wanavizia malaya kumbe anatuliza maumivu, ambayo pombe ikiisha yanarudi tena.
Kweli Kabisa
 
Kilasiku tunawaimbia humu kwamba ndoa ni ukatili, hamtusikii...🤣
 
Back
Top Bottom