Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais
kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu
kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa
kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais
ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi
cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya
40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka
Rais atapendekeza jina la mtu atakae kuwa Makamu wa Rais na
uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua
asilimia hamsini ya Wabunge wote.
Lakini kuhusu awamu au kugombea tena katiba iko wazi kabisa
Endapo makamu wa raisi atakaa madarakani kwa muda wa miaka chini ya mitatu anaruhusiwa kugombea anaruhusiwa kugombea mara mbili lakini endapo atashika kwa zaidi ya miaka zaidi ya mitatu ataruhusiwa kugombea mara moja tu.