Nini tofauti kati ya Maruhani, Mapepo, Mashetani na Majini?

Nini tofauti kati ya Maruhani, Mapepo, Mashetani na Majini?

Kichwa kinajieleza. Mwenye ulewa afafanue. Utasikia mtu ana maruhani au ana mapepo au ana mashetani au ana majini. Tofauti yake ni nini?


Maruhani ndiyo mapepo ndiyo yale yanayowashika sana akina mama, utasikia watu wakisema; mama fulani kapandisha maruhani wake na kwakuwa ni athari zinazowashika watu hasa kina mama na huwashika kichwani bila watu wa nje kuziona hizo athari na hata muathirika naye hufanya matendo fulani bila kujitambua basi watu wakayaita kwa jina la "majini" --- jini ni umoja wa neno majini, maana yake ya moja kwa moja ni kitu chochote kisichoonekana kwa macho ya kawaida (naked eyes), jini au jinn ni neno la kiarabu lenye maana hiyo ya asili.--- shetani ni kitu chochote kiovu chenye uhai, awe mtu, mnyama, nyoka nk, anapokuwavni muovu au mtenda uhalifu huyo anabeba jina la shetani.
 
Kichwa kinajieleza. Mwenye ulewa afafanue. Utasikia mtu ana maruhani au ana mapepo au ana mashetani au ana majini. Tofauti yake ni nini?


Mzee Yusuph Makamba anaweza kuwa na jibu zuri sana, amezungumza katika dakika ya 5:35 na kuendelea SIKILIZA HII
 
Maruhani ndiyo mapepo ndiyo yale yanayowashika sana akina mama, utasikia watu wakisema; mama fulani kapandisha maruhani wake na kwakuwa ni athari zinazowashika watu hasa kina mama na huwashika kichwani bila watu wa nje kuziona hizo athari na hata muathirika naye hufanya matendo fulani bila kujitambua basi watu wakayaita kwa jina la "majini" --- jini ni umoja wa neno majini, maana yake ya moja kwa moja ni kitu chochote kisichoonekana kwa macho ya kawaida (naked eyes), jini au jinn ni neno la kiarabu lenye maana hiyo ya asili.--- shetani ni kitu chochote kiovu chenye uhai, awe mtu, mnyama, nyoka nk, anapokuwavni muovu au mtenda uhalifu huyo anabeba jina la shetani.


Kimsingi, majina yote kasoro moja yametokana na maneno ya kiarabu, maruhani (ruhani) kwa kiarabu ni روح حن yaani roho yenye tamaa kubwa ya kitu fulani ambayo ndiyo mapepo yanayowashika kina mama zaidi wengine huyaita kwa jina la majini (jinn) kwa kiarabu الجن ambalo ni neno lilitokana na kitenzi جن yaani kuficha/ kutoonekana kwa macho ya kawaida, kwakuwa akina mama wanaopatwa na hayo mapepo yasiyoonekana kwa macho ndipo waarabu wakayaita kwa jina "majini"-- lakini huo ni ugonjwa miongoni mwa magonjwa ya akili na kitaalamu ugonjwa huo unaitwa "Hysteria", wala hakuna kiumbe au viumbe vinavyotoka nje na vikamwingia mtu kichwani kama jinsi watu wengi wanavyoamini na kuaminishwa. Naam, katika lugha ya kiarabu inaruhusiwa bakteria wote (microscopic organism) kuitwa kwa kutumia jina "majini" kwa sababu tu ya sifa yao ya kutoonekana kirahisi, na baadhi ya maandiko ya kiarabu fasaha cha kale (clasic arabic) neno hilo limetumika kwa mnasaba huo.

Neno shetani kwa kiarabu ni شيطان (shaitwaan), ni kiumbe chochote kiovu chenye uhai.
 
Hakuna tofauti hapo ndugu, ni sawa na kusema Zero na Sifuri


Mind u; hakujawajahi na hakutawahi kuwepo ma jini Mazuri kama wanavyoamini ndugu zetu
 
1.Jini ni kiumbe kama alivyo binadamu,kuna majini wema wachamungu na waovu watenda dhambi.

2. Shetani ni ile hali au tabia ya kushawishi maovu/dhambi kwahiyo shetani anaweza kuwa jini au binadamu mwenye tabia ya kushawishi katika maovu.

2. Maruhani ni aina ya jini muovu anayemuingia mtu na kujifanya kumwamrisha mema kumbe ni mbaya tu hana lolote.

3. Mapepo ni hayo hayo majini waovu yanayompanda binadamu.

Naomba kuwasilisha.
 
Shetani ni kiumbe tofauti kabisa na jini. Mashetani ni wale malaika walioasi wakageuka mashetani. Mashetani ndio wanaotawala utendaji kazi wa majini kupitia wachawi, waganga na wale wote wanaohusika na nguvu za giza (mfano freemason, wanga, waabudu shetani, mizimu na kadhalika). Majini ambao kwa jina lingine huitwa mapepo yanatokana na uhusiano wa kingono kati shetani na binadamu kwa hivyo yanazaliwa kama binadamu, na kufa pia. Yapo kwenye koo/kabila mbalimbali nyingi sana kama vibwengo, jini sharifu, jini ruhani, jini bahari n.k. Wapo watu wanaofuga majini (exactly kama mifugo mingine na kuwalisha), na hayo majini yanatumwa na walioyafuga yaende kufanya uovu fulani (kwa mfano kusababisha ajali, kumtia mtu ugonjwa n.k.). Mmiliki wa jini husika analipwa kwa kumtuma huyo jini. Majini pia yana majina kulingana na kazi wanazofanya. Kwa mfano kuna jini maiti (ambaye anaweza kuwa ni ukoo labda wa sharifu au ruhani n.k.), na kazi yake ni kuua (kumuua mtu au hata kuua mafanikio yake). Kuna jini mahaba (ambaye anamvamia mwanamke na kuwa analala naye kama mume wake. Anaota anafanya tendo la ndoa na mtu fulani kumbe ameingiliwa na jini mahaba. Huyu jini mahaba anamtenga kabisa mke na mume wake wa ndoa. Wapo pia jini mahaba wa kike wanaojioza kwa mwanaume kwa nguvu). Yapo pia majini ambayo watu wa ukoo fulani wamekubaliana nayo wawe wanaishi nayo mwilini. Hayo yakienda kwa mganga yanakabidhiwa kwa huyo mtu yamlinde. Mambo ni mengi sa-a-a-na kwa hiyo sio rahisi kuyaelezea kwa kifupi katika andiko kama hili.
 
1.Jini ni kiumbe kama alivyo binadamu,kuna majini wema wachamungu na waovu watenda dhambi.

2. Shetani ni ile hali au tabia ya kushawishi maovu/dhambi kwahiyo shetani anaweza kuwa jini au binadamu mwenye tabia ya kushawishi katika maovu.

2. Maruhani ni aina ya jini muovu anayemuingia mtu na kujifanya kumwamrisha mema kumbe ni mbaya tu hana lolote.

3. Mapepo ni hayo hayo majini waovu yanayompanda binadamu.

Naomba kuwasilisha.
Laiti watu wangejua, kuwa hakuna majini wema na wala haitakaa itokee hiyo, jini liwe na wema.. Never ever... Laiti watu wangejua..
 
Kichwa kinajieleza. Mwenye ulewa afafanue. Utasikia mtu ana maruhani au ana mapepo au ana mashetani au ana majini. Tofauti yake ni nini?
Vyote hivi ni viumbe roho... Lakini vikiongozwa na shetani... Huyu ndie asili kuu ya hivi vingine vyote....
Maruhani hayana tofauti kubwa na mapepo wala majini..... Ni sawa tu unaposema mbogamboga au aina za matunda ama aina za wanyama
Mizimu haitokei mpaka mwili utengane na roho
Majini ni viumbe roho walioumbwa kwa moto hawana asili na binadamu.. Wanajitegemea...
Mapepo ni viumbe roho wanaotangatanga wanaobeba utambulisho fulani kama pepo la ngono, uchawi, husuda, rohombaya, madeni nknk....
 
Laiti watu wangejua, kuwa hakuna majini wema na wala haitakaa itokee hiyo, jini liwe na wema.. Never ever... Laiti watu wangejua..
Wewe ndo hujui hebu jikalie kimya. Jini ni kiumbe mwenye sifa ya kutoonekana na mwanadamu (invisible) ingawa tunaishi katika ulimwengu huu huu. Wao wanatuona lakn sisi hatuwaoni,sasa jiulize majini wote wangekuwa waovu nani angebaki na kuendelea kuishi katika wanadamu juu ya ardhi hii?
 
Back
Top Bottom