Nini tofauti kati ya Maruhani, Mapepo, Mashetani na Majini?

Nini tofauti kati ya Maruhani, Mapepo, Mashetani na Majini?

Kichwa kinajieleza. Mwenye ulewa afafanue. Utasikia mtu ana maruhani au ana mapepo au ana mashetani au ana majini. Tofauti yake ni nini?
Pamoja na ufafanuzi utakaotolewa hapa, jambo moja muhimu ni kwamba; Hizi zote ni kazi za ufalme wa giza ila kwa ngazi tofaututofauti. Na Ufalme wa Nuru hufukuza kila aina ya giza, bila kujali ngazi husika!.
 
Mkuu mie sitaki kukupinga ila najaribu kupambanisha kati ya unachoeleza na kinachotokea kwenye uhalisia,huko mwanzo ulikuwa unasema njia ya kutuliza hiyo hali inapompata mgonjwa ni mkuliwaza kama kumuimbia(japo tunaona makanisani wanakemea) sasa hapa nimekutajia hiyo njia ya kumnusisha mafuta umekubaliana hiyo dawa kisa tu unasema inapita puani na kuingia kwenye ubongo ila hujari hayo mafuta yametengenezwa kwa kutumia nini hadi ikawa dawa yenye kuhusika na huo ugonjwa wa akili.

Binafsi sitaka matatizo mengine kama haya ni magonjwa ya akili tu ila kusema yote haya ni magonjwa tu ya akili na si vinginevyo hapo ndio palipo na tatizo.


Mkuu, Labda mimi sielewi unachosema na mimi hunielewi ninachosema, nasema hivi mapepo au maruhani au majini yanayowashika hasa kina mama na kina dada ni ugonjwa unaoathiri ubongo, kwakuwa unathiri ubongo ni lazima tuuite kwa jina jingine "ugonjwa wa akili" (mental disease) na kwa kitaalamu unaitwa Hysteria, waarabu wanaita Ruhani au jinn, unaitwa hivyo kwasababu muathirika huwa anafanya mambo ya ajabu bila kujitambua au bila ridhaa yake, mfano anaweza kupagawa kwa kujirusha na kuongea maneno ya ajabu au akaongea lugha mpya na maneno yasiyokuwa na mpangilio (ravings) kiasi kwamba inaonekana kana kwamba kuna nguvu isiyoonekana imo ndani ya huyo muthirika ndiyo inayomsukuma kufanya hayo matendo na ndipo waarabu wakaita (Ruhani au jinn)---- Ruhani ni "Roho" yenye tamaa au tashwishwi na jinn ni kitu kisichoonekana kwa macho.

Mimi nilikuwa nasema dawa nilizoshuhudia zikitumika kuwatuliza wagonjwa hao kwamba ni kuwaliwaza kwa muziki au sauti nyororo kama jinsi dua zinavyosomwa na kuwashika sikio au kwenye paji la uso kwa kufanya hivyo mganga anafanya kazi ya kurejesha akili ya mgonjwa, sikio na paji ni mahali palipo karibu na ubongo ambao kwa muda huo ndiyo uliokuwa affected kwa maana hiyo inakuwa ni njia rahisi ya mawasiliano ya karibu
kati ya ubongo na hivyo viungo, hii inafanana kwa kiasi fulani na "acupuncture" ya Wachina ambapo wao hutumia sindano kutoboatoboa sehemu yenye ugonjwa.

Wewe umezungumzia juu ya dawa ya kunusa, mimi naafiki na zipo nyingine zaidi ya hizo tulizozitaja.

Ugonjwa huo unajulikana kama Hysteria na unawapata wanawake zaidi duniani pote, Wazungu, waarabu, waswahili nk,.

HUO NI UGONJWA WA AKILI, KWA SABABU UNAATHIRI UBONGO TU KATIKA MWILI WA BINADAMU.
 
Mkuu, Labda mimi sielewi unachosema na mimi hunielewi ninachosema, nasema hivi mapepo au maruhani au majini yanayowashika hasa kina mama na kina dada ni ugonjwa unaoathiri ubongo, kwakuwa unathiri ubongo ni lazima tuuite kwa jina jingine "ugonjwa wa akili" (mental disease) na kwa kitaalamu unaitwa Hysteria, waarabu wanaita Ruhani au jinn, unaitwa hivyo kwasababu muathirika huwa anafanya mambo ya ajabu bila kujitambua au bila ridhaa yake, mfano anaweza kupagawa kwa kujirusha na kuongea maneno ya ajabu au akaongea lugha mpya na maneno yasiyokuwa na mpangilio (ravings) kiasi kwamba inaonekana kana kwamba kuna nguvu isiyoonekana imo ndani ya huyo muthirika ndiyo inayomsukuma kufanya hayo matendo na ndipo waarabu wakaita (Ruhani au jinn)---- Ruhani ni "Roho" yenye tamaa au tashwishwi na jinn ni kitu kisichoonekana kwa macho.
Mimi nilikuwa nasema dawa nilizoshuhudia zikitumika kuwatuliza wagonjwa hao kwamba ni kuwaliwaza kwa muziki au sauti nyororo kama jinsi dua zinavyosomwa na kuwashika sikio au kwenye paji la uso kwa kufanya hivyo mganga anafanya kazi ya kurejesha akili ya mgonjwa, sikio na paji ni mahali palipo karibu na ubongo ambao kwa muda huo ndiyo uliokuwa affected kwa maana hiyo inakuwa ni njia rahisi ya mawasiliano ya karibu kati ya ubongo na hivyo viungo, hii inafanana kwa kiasi fulani na "acupuncture" ya Wachina ambapo wao hutumia sindano kutoboatoboa sehemu yenye ugonjwa.
Wewe umezungumzia juu ya dawa ya kunusa, mimi naafiki na zipo nyingine zaidi ya hizo tulizozitaja.
Ugonjwa huo unajulikana kama Hysteria na unawapata wanawake zaidi duniani pote, Wazungu, waarabu, waswahili nk,.
HUO NI UGONJWA WA AKILI, KWA SABABU UNAATHIRI UBONGO TU KATIKA MWILI WA BINADAMU.
Nia yangu ni kujifunza.

Hebu niambie kitaalamu kumwimbia nyimbo au kumshika kichwa huyo mgonjwa kunaponeshaje/kutuliza vp hiyo hali ya mgonjwa?
 
Nia yangu ni kujifunza.

Hebu niambie kitaalamu kumwimbia nyimbo au kumshika kichwa huyo mgonjwa kunaponeshaje/kutuliza vp hiyo hali ya mgonjwa?


Mkuu dawa "hasa" hapo ni kumshika kichwani tu (kwa maoni yangu). Hiyo inafanana kwa kiasi fulani na "acupuncture" ya kichina, yaani ni tiba inayogusa moja kwa moja au karibu sana na eneo husika.

Paji-- kugusa, sikio---kumuimbia/kumsikilizisha na pua---kumnusisha dawa, hizo zote ni njia za kujaribu "kugusa" ubongo ambao kwa wakati huo ndiyo unakuwa umeathirika, na hata kama inawezekana kumnawisha maji ya baridi usoni/machoni hiyo nayo inaweza ikawa njia ya kumponya kwa wakati huo kwasababu macho ni sehemu ya ubongo zaidi kuliko hata sikio na pua.(hayo ni maoni yangu).
 
Mkuu dawa "hasa" hapo ni kumshika kichwani tu (kwa maoni yangu). Hiyo inafanana kwa kiasi fulani na "acupuncture" ya kichina, yaani ni tiba inayogusa moja kwa moja au karibu sana na eneo husika.
Paji-- kugusa, sikio---kumuimbia/kumsikilizisha na pua---kumnusisha dawa, hizo zote ni njia za kujaribu "kugusa" ubongo ambao kwa wakati huo ndiyo unakuwa umeathirika, na hata kama inawezekana kumnawisha maji ya baridi usoni/machoni hiyo nayo inaweza ikawa njia ya kumponya kwa wakati huo kwasababu macho ni sehemu ya ubongo zaidi kuliko hata sikio na pua.(hayo ni maoni yangu).
Sawa mkuu ikama ulivyosema hayo ni mawazo yako naulishasema wewe sio mtaalamu,ila ningepata maelezo ya kitaalamu ningefurahi sana ila labda tutapata mtaalamu humu aje kueleza kitaalamu maana nina shauku ya kutaka kujua mahusiano ya huo ugonjwa na kumuimbia tu na ugonjwa ukatulia.
 
Sawa mkuu ikama ulivyosema hayo ni mawazo yako naulishasema wewe sio mtaalamu,ila ningepata maelezo ya kitaalamu ningefurahi sana ila labda tutapata mtaalamu humu aje kueleza kitaalamu maana nina shauku ya kutaka kujua mahusiano ya huo ugonjwa na kumuimbia tu na ugonjwa ukatulia.


Siyo kumuimbia tu, bali pamoja na kumshika sikio au kichwani kwenye paji vitendo hivyo vifanyike kwa pamoja.

Ni kwa namna gani hiyo tiba inaingia ndani ya ubongo ni rahisi kusema kwamba pua, sikio na macho ni viungo vyenye "nerves" zinazokwenda kwenye ubongo.

Ni kwa namna gani ponyo hilo hufanyika ndani ya ubongo kweli hapo tusubiri wataalamu.
 
Siyo kumuimbia tu, bali pamoja na kumshika sikio au kichwani kwenye paji vitendo hivyo vifanyike kwa pamoja.
Ni kwa namna gani hiyo tiba inaingia ndani ya ubongo ni rahisi kusema kwamba pua, sikio na macho ni viungo vyenye "nerves" zinazokwenda kwenye ubongo.
Ni kwa namna gani ponyo hilo hufanyika ndani ya ubongo kweli hapo tusubiri wataalamu.
Ndio maana nikasema bora tusubiri mtaalamu kama maana sie wenyewe hatutoweza kuelewa,kwa sababu mkuu wakati mwengine usomaji Qur'an kwa mgonjwa(unaita kuimba kwa kumliwaza) hupelekea maumivu kwa mgonjwa,ukifuatilia haya masuala kuna wakati mgonjwa anasikilizishwa Qur'an bila kushikwa popote na humletea maumivu mwili.

Kwa wenye kuamini kuwa huo ugonjwa ni kuingiwa na jini basi huamini kuwa hivyo visomo vya Qur'an kitu chenye kumuadhibu huyo jini na si kumliwaza mgonjwa na ndiyo maana utaona makanisani hukemea kwa ukali kabisa kuamuru pepo atoke na si kumliwaza mgonjwa ili hiyo hali ipoe. Na ndiyo maana wakati mwengine mtu mwenye kujulikana na hilo tatizo hata pale anapokuwa kwenye hali ya kawaida basi usomaji wa Qur'an unaweza kutumika kupandisha hilo jini(kwa wenye kuamini hivyo)na kuanza kuongea nalo kwa kuamini kuwa hicho kisomo kinamuadhibu huyo jini.
Hivyo mambo haya ni mengi mkuu na yana nichanganya inahitajika mtaalamu aeleze vizuri kuhuaiana na huu ugonjwa maana niliwahi kumsikiliza kidogo mtaalamu mmoja akielezea huu ugonjwa aliwataja hadi manabii na hawa wachungaji kuwa nao wana huu ugonjwa wa akili.
 
Ndio maana nikasema bora tusubiri mtaalamu kama maana sie wenyewe hatutoweza kuelewa,kwa sababu mkuu wakati mwengine usomaji Qur'an kwa mgonjwa(unaita kuimba kwa kumliwaza) hupelekea maumivu kwa mgonjwa,ukifuatilia haya masuala kuna wakati mgonjwa anasikilizishwa Qur'an bila kushikwa popote na humletea maumivu mwili.

Kwa wenye kuamini kuwa huo ugonjwa ni kuingiwa na jini basi huamini kuwa hivyo visomo vya Qur'an kitu chenye kumuadhibu huyo jini na si kumliwaza mgonjwa na ndiyo maana utaona makanisani hukemea kwa ukali kabisa kuamuru pepo atoke na si kumliwaza mgonjwa ili hiyo hali ipoe. Na ndiyo maana wakati mwengine mtu mwenye kujulikana na hilo tatizo hata pale anapokuwa kwenye hali ya kawaida basi usomaji wa Qur'an unaweza kutumika kupandisha hilo jini(kwa wenye kuamini hivyo)na kuanza kuongea nalo kwa kuamini kuwa hicho kisomo kinamuadhibu huyo jini.
Hivyo mambo haya ni mengi mkuu na yana nichanganya inahitajika mtaalamu aeleze vizuri kuhuaiana na huu ugonjwa maana niliwahi kumsikiliza kidogo mtaalamu mmoja akielezea huu ugonjwa aliwataja hadi manabii na hawa wachungaji kuwa nao wana huu ugonjwa wa akili.

Labda nikuulize jambo moja, je wewe binafsi unaamini huo ugonjwa ni kitu gani au uliambiwa ni nini??

Pili wewe ni dini gani??
 
Labda nikuulize jambo moja, je wewe binafsi unaamini huo ugonjwa ni kitu gani au uliambiwa ni nini??
Pili wewe ni dini gani??
Mimi binafsi naamini huo ugonjwa kama wengi wanavyoamini kuwa ni majini/mapepo ila pia naamini kuwepo magonjwa ya akili.
 
Mimi binafsi naamini huo ugonjwa kama wengi wanavyoamini kuwa ni majini/mapepo ila pia naamini kuwepo magonjwa ya akili.


Majini/mapepo, unaweza kuyaelezea jjinsi unavyoyajua??
 
ZEE LA HEKIMA Kidogo wewe ndio umeonyesha kufafanua vizuri kidogo endeleza uzi au tukuulize maswali: haya hao majini wanaotumwa kwenda kuleta pesa na kumletea mhusika ni maruhani au majini na pesa hizo huwa wanazichukua wapi maana Benki huwa wanashindwa kuingia inamaana huwa wana ulinzi mwingine ambao unawazuia kuingia.
Shetani ni kiumbe tofauti kabisa na jini. Mashetani ni wale malaika walioasi wakageuka mashetani. Mashetani ndio wanaotawala utendaji kazi wa majini kupitia wachawi, waganga na wale wote wanaohusika na nguvu za giza (mfano freemason, wanga, waabudu shetani, mizimu na kadhalika). Majini ambao kwa jina lingine huitwa mapepo yanatokana na uhusiano wa kingono kati shetani na binadamu kwa hivyo yanazaliwa kama binadamu, na kufa pia. Yapo kwenye koo/kabila mbalimbali nyingi sana kama vibwengo, jini sharifu, jini ruhani, jini bahari n.k. Wapo watu wanaofuga majini (exactly kama mifugo mingine na kuwalisha), na hayo majini yanatumwa na walioyafuga yaende kufanya uovu fulani (kwa mfano kusababisha ajali, kumtia mtu ugonjwa n.k.). Mmiliki wa jini husika analipwa kwa kumtuma huyo jini. Majini pia yana majina kulingana na kazi wanazofanya. Kwa mfano kuna jini maiti (ambaye anaweza kuwa ni ukoo labda wa sharifu au ruhani n.k.), na kazi yake ni kuua (kumuua mtu au hata kuua mafanikio yake). Kuna jini mahaba (ambaye anamvamia mwanamke na kuwa analala naye kama mume wake. Anaota anafanya tendo la ndoa na mtu fulani kumbe ameingiliwa na jini mahaba. Huyu jini mahaba anamtenga kabisa mke na mume wake wa ndoa. Wapo pia jini mahaba wa kike wanaojioza kwa mwanaume kwa nguvu). Yapo pia majini ambayo watu wa ukoo fulani wamekubaliana nayo wawe wanaishi nayo mwilini. Hayo yakienda kwa mganga yanakabidhiwa kwa huyo mtu yamlinde. Mambo ni mengi sa-a-a-na kwa hiyo sio rahisi kuyaelezea kwa kifupi katika andiko kama hili.
 
Tafadhali, Na mimi nijulishe jinsi hivyo unavyowajua wewe na wengineo.
Kama nilivyosema sina ujuzi na hawa viumbe ninachojua wana sifa ya kutokuonekana na wana uwezo na ujuzi wa vitu vingi tofauti na binaadamu.
 
Hakuna tofauti hapo ndugu, ni sawa na kusema Zero na Sifuri


Mind u; hakujawajahi na hakutawahi kuwepo ma jini Mazuri kama wanavyoamini ndugu zetu
Nini ilikuwa nia ya Mungu kuyaumba mapepo/majini?
 
Mfano wana uwezo wa kujigeuza maumbile tofauti tofauti kama wanyama ndege na hata binadamu,kitu ambacho sie hatuwezi.


Wewe umewahi kushuhudia jinni akijigeuza hivyo usemavyo???
 
Back
Top Bottom