Nini tofauti kati ya Maruhani, Mapepo, Mashetani na Majini?

Kichwa kinajieleza. Mwenye ulewa afafanue. Utasikia mtu ana maruhani au ana mapepo au ana mashetani au ana majini. Tofauti yake ni nini?
maruhani na majini yameanzzia uarabuni,hufugwa na watu wa dini fulani ili kuuwa watu, haya hufugwa sana sehemu za uswahilini na mwambao, sitazitaja
 
Nini ilikuwa nia ya Mungu kuyaumba mapepo/majini?
[/QUOTE
Majini ni wafuasi waliokuwa wakimuunga mkono Lusifa alipokuwa ndiye Malaika mkuu. Sasa alipoasi alikuwa na wafuasi, ndio hao majini
 
Kwa maelezo yako unataka kutuaminisha kua hata virusi wa UKIMWI, maleria, nk wanaweza kuitwa (jin) kwasababu hawaonekani..?
 
Kwa maelezo yako unataka kutuaminisha kua hata virusi wa UKIMWI, maleria, nk wanaweza kuitwa (jin) kwasababu hawaonekani..?


Sawa kabisa, matumizi ya neno jinn katika kiarabu kwa ajili ya hivyo viumbe inaruhusiwa kabisa.

Kuna simulizi moja kutoka kwa mtukufu mtume Muhammad (saw), alipata kuwaonya waarabu katika zama zake waache kutumia vinyesi vikavu vya ngamia na mifupa ya wanyama kujichambia baada ya kwenda haja kama jinsi leo watu wanavyotumia toilet paper, mtume (saw) aliwaambia vitu hivyo ni vyakula vya majinni, ikumbukwe katika zama hizo Mtume (saw) aliwakuta warabu katika lindi la ushenzi mkubwa hivyo ilibidi kwanza awafundishe "ustaarabu/ adabu" (civilization/manners ) kulingana na mafundisho ya kiislamu na hivyo akawaambia badala yake watumei maji.

Katika zama hizo (takriban miaka 1400) iliyopita Waarabu hawakujua kwamba vinyesi na mifupa ya wanyama inaweza kuwa ni chakula cha Bakteria hivyo kuvitumia kujichambia wangeweza kujisababshia maambukizi katika sehemu za siri, lakini Mungu alimjulisha mtume wake juu ya jambo hilo na mtume (saw) akawatahadharisha wafuasi wake.

Leo kutokana na maendeleo ya elimu ya sayansi inawezekana kuwaona hao bakteria katika vinyesi kwa kutumia vifaa, bakteria hao wanakula kwa njia ya kuozesha (decaying).

Hivyo hao majinni aliowataja mtume (saw) ndiyo hao majinn.

Kuna simulizi lingine mtume (saw) alituasa tusome dua tunapoingia chooni ili kujikinga na majinni wanaoishi humo, majinn wanaoishi humo chooni sio viumbe wengine bali ni wadudu wadowadogo wa maradhi (microbes) wanaopatikana katika vinyesi vyetu sisi binadamu, mfano, wadudu wa kipindupindu, kuhara damu, wadudu wa kichocho nk, hao ndio majinn waishio chooni na wala hakuna eti jinn makata wala jinn Subiani au jinn mahaba tunaoaminishwa tuwakubali, huo i ujinga mtu na hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kukubali hadithi hizo za uongo.
 
Kwahiyo hayo yote uliyoyasema kuhusu majinni umesikia tu??

"Na pale Shet'ani alipo wapambia vitendo vyao, na akawaambia: Hapana watu wa kukushindeni hii leo, na hali mimi ni mlinzi wenu. Yalipo onana majeshi mawili, akarudi nyuma, na akasema: Mimi si pamoja nanyi. Mimi naona msiyo yaona. Mimi namwogopa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu." Qur'an Anfal 48
 


Tunazungumzia juu ya majinn na sio juu ya Shaitwaani (shetani).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…