Well uamuzi ni wako kaka...sisi tunakupa ushauri vile tunavyoona inafaa wewe uchukue alafu changanya na zako.Ila angalia kesho kutwa usije ukarudi unalia umekamatika sehemu maana akili yako haikua huru kuchagua kwa uangalifu...angalia tu usije ukaruka majivu na kukanyaga moto!!!Ni kweli usemayo lakini jamani hivi kweli mimi sina haki ya kuliwazwa katika magumu haya?!, mwenzangu ana ponda life yaani kanisahau kabisa, pia kuna suala la kimwili ambalo sijalisema hapa namimi ni mtu mzima niliyekamilika sana kijinsia navumilia kutopata haki hii kwa muda mrefu wakati nahisi mwenzangu anapata ndio maana hana tena shida na mimi.Nakula kwa kufanya vibarua vya kazi ndogo ndogo si kama mimi na mtoto tunamtegemea yeye keshatubwaga kabisa! hasa ukizingatia kuwa wa kwake yuko boarding.Pia tusisahau kuwa ajira zenyewe ni taabu siku hizi hata kwa wasomi wenye shahada zao kwangu nikisubiri kujijenga si nitazeeka manake inabidi nirudi shule ili nipate kazi.uamuzi wa kutafuta mwingine nimeufanya kwa mpangilio kwa mfano nilipojiunga na jf ilikuwa njia mojawapo ya kutafuta faraja kwa kubadilishana mawazo kama hivi, ndio maana utaona sikulisema hili mwanzo mpaka nilipoelewa utaratibu wa mada zinavyowasilishwa.kwa hiyo nitakayempata atajua nimekosa nini huko kwa awari na tutazungumzia uwezekano wa mapenzi ya dhati kabla ya kupiga hatua zaidi.
Kuna mada ulikuja nayo hapa ukisema kama nakumbuka vizuri uamini ndoa. Kuna siku nikakushauri umtokee yule mheshimiwa wa kawe kwani yeye ataka mtoto tu si kuolewa. Kuna nyingine ulisema nyie medical doctors mna ethics. Sasa hii unasema wewe ni std seven. Anyway michango ni muhimu kwa wale wenye situation kama hiyo.
Pole sana Mulama, mi nakusisitiza usikimbilie kumuacha mkeo,naomba utafute kazi au namna ya kujiendeleza. Ni rahisi sana watu kumuona huyo mwanamke mbaya lakini nikuhakikishie wanawake wengi hawatakuwa tofauti na huyo mama. Kama baba wa familia jitahidi nawe uingize kipato hata kama ni kidogo na pia kwenda kazini itakupunguzia stress unazopata sasa,atleast kule uta interact na watu,utakuwa na marafiki ambao kwa namna moja au nyingine watakuwa msaada kwako hata kama ni wa kisaikolojia. Nakutakia kila la kheri.
mkuu pole kama ni kweli
ningependa kujua hiyo nyumba mmepanga au ni yenu
vyovyote vile hama muage vizuri mtoto mhamishie kwa wazazi au nduguzo
hamia mkoa mwingine katafute kazi au anza biashara
kama ana chembe ya mapenzi atakutafuta
kama hana atajuta kumkosa houseboy na hiyo utaiona wakati mkiwasiliana
kwa yeye kukaa mwenyewe na wewe kuwa mwenyewe utaweza kuwa free thinking
usikimbilie kuoa kwanza tafuta pesa si unajua "ukitafuta wanawake utapoteza pesa ukitafuta pesa wanawake watakufuata"
ukikaa mwenyewe kwa miezi mitatu mpaka sita utajua ukweli ingawa hilo suala la kutoa mimba ina maana hapo future hakuna ila kaa mwenyewe kwa muda pata kazi wakati hujamuacha officially then ukitulia utakuwa na maamuzi ya busara
Kuna mada ulikuja nayo hapa ukisema kama nakumbuka vizuri uamini ndoa. Kuna siku nikakushauri umtokee yule mheshimiwa wa kawe kwani yeye ataka mtoto tu si kuolewa. Kuna nyingine ulisema nyie medical doctors mna ethics. Sasa hii unasema wewe ni std seven. Anyway michango ni muhimu kwa wale wenye situation kama hiyo.
DahhhhhhSante tajiri wangu..afrodenziuna akili mno hujui tu
The Boss malizia sentensi yako naona kama haijakamika.wanawake wakiwezeshwa ,kweli wanaweza.......................................
Thanx TBTahadhari ndugu mulama.
Usije chukia wanawake wote...
Wapo wengi wazuri wa tabia.
Pole saana aisee
Yaaaaani kaniudhi kweli huyu mama ambiliki, hata uso wa haya amekosa eeehalafu mwanamke kama huyu baadae mambo yako yanakuwa super ndio anaanza oohh mume wangu oohh cjui kitu gani na gani, bibadamu wengine utu hawana kabisa aise.
Ndugu zangu naombeni msaada kwenye kisa hiki cha kweli . nina mke tuliyefunga ndoa yapata miaka 11 iliyopita, mke wangu tulikutana kazini kwenye kiwanda cha kutengeneza biscuits ambapo yeye alikuwa teller mimi ni mwendesha mashine.
Baada ya kuoana nilimwendeleza kimasomo kwakuwa yeye alikuwa wa form IV nami ni darasa la saba, kwakuwa alifanya vizuri katika kozi zake alifanikiwa kupata kazi kwenye shirika moja la kimataifa kama administrative secretary.
Sisi huku kiwanda kilifungwa kutokana na biscuits kukosa masoko kutokana na ushindani uliopo hivyo nikalazimika kukaa nyumbani huku nikijitahidi kutafuta vibarua vya hapa na pale.
Issue ni kwamba mke wangu sasa amekuwa mbogo hataki kusaidia kitu chochote hapa nyumbani na ikitokea akatoa hela basi masimango yanatisha, tutaitwa majina ya kila aina mara poyoyo, mara Mario nk.
Wakati tunaoana kila mmoja alikuwa na mtoto na wote tulikuwa tunawalea kwa mapenzi bila ubaguzi, cha kushangaza yeye mtoto wake kampeleka international school wa kwangu amemwacha aendelee na hizi za kayumba!
Kinachonipa taabu sana ni kurudi usiku wa manane wakati mwingine akiwa amelewa nikimuuliza anasema walikuwa na kazi nyingi na mikutano inayoambatana na vinywaji, pia ana safari nyingi za kikazi na akifika huko huwa hataki nimpigie simu eti namsumbua!
Sasa je huyu bado anastahili kuwa mke wangu? Si kawa wa mataifa sasa niachane naye nikaoe mwingine?
Vikao vya wazee vimeshindwa kutoa ufumbuzi wanamuogopa au sijui ni kwamba anawakatia mkwanja mrefu?!
Nawasilisha
Ni tafakuri jadidi katika mkutadha huu, je wadau nyakati hizi tulizo nazo kuna haja ya kuoana? Ikiwa tendo la kuzaa na kuijaza dunia tuliloagizwa na maulana tunalitimiza kikamilifu nje ya utaratibu huu wa kuoana na imefikia mahala hata wengine hatutaki tena kujaza dunia tuna abort au kuua vi offspring vyetu kinyume na mpango wa mola!
Mimi naona mpaka hapo kuoana ni uchoyo tu wa kutaka mtu mmoja kushikilia mwenzie na kuwanyima fursa wengine kuongeza dunia hapohapo!
Mnasemaje wadau?