Nipeni Urais wa Tanzania muone namna gani CCM wametuchelewesha!

Nipeni Urais wa Tanzania muone namna gani CCM wametuchelewesha!

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Nitafanya mambo matano muhimu.

1. Kuufanya Arusha kuwa Mji wa Taasisi za Kimataifa Afrika ambapo Taasisi zote za kimataifa zitapewa maeneo ya kujenga Ofisi zao na Makazi ya Wafanyakazi wao Arusha- Kupitia hili nina uhakika wa kuingiza fedha nyingi sana za kigeni pamoja na kutengeneza ajira za uhakika kwa Watanzania wengi sana.

2. Kuifanya Dar es Salaam kuwa Mji wa Biashara kweli na Dodoma Ofisi na Makazi ya Serikali tu. Kwenye hili kila kitu cha Kibiashara na maeneo makubwa mazuri ya starehe yatajengwa Dar.

Dodoma kutakuwa na Ofisi za Wizara, Ikulu, Bunge na Mahakama tu. Hakuna taasisi itakuwa na Ofisi Dodoma bali Ofisi za Taasisi zitagawanywa mikoa mbalimbali ikiwemo Dar, Mwanza, Mbeya, Kigoma, Lindi, Iringa, Kilimanjaro, Tanga na Njombe ili kuleta uwiano katika vichocheo vya maendeleo sehemu mbalimbali.

3. Kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha usafirishaji kuelekea kusini, katikati na kaskazini mwa Afrika kupitia Bandari zake na reli. Hapa nitaweka miondombinu ya uhakika ya reli za umeme na barabara za uhakika kwenye njia zote za mipaka ya kuingia na kutoka Tanzania.

4. Kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha Utalii na Uwekezaji Afrika. Kila kivutio cha utalii kinachopaswa kuwepo Tanzania kitawekwa.

Mwisho nitaivunja Wizara ya Ardhi na kuajiri vijana wapya ambao watafanya zoezi na kuipima na kuipanga nchi nzima.

Kabla ya yote haya nitaanza na Katiba Mpya.

Mungu nisaidie!
 
Tangu nili makamba kawa mngoni?

anyway, kwenye uraisi wako bado sijaona kutoboa kwani umeishia kwenye mipango ile ile ya kuendeleza arusha, dar kama haww wa sasa hivi tu, lkn vp khs mkoa mzima wa mbeya na eneo lote la nyanda za juu kusini mpaka songea? vp khs mtwara, lindi na kusini yote? vp khs tanga na bandari yake? vp khs rift valley the most fertile region in afrika inapita manyara mpaka kusini, vp khs kagera, musoma na mara kwa ujumla? vp khs visiwa vyetu kama mafia ungekuwa na mipango gani navyo? nasikitika kusema uraisi wako usingekuwa tofauti sana na awamu ya 4 …
 
anyway, kwenye uraisi wako bado sijaona kutoboa kwani umeishia kwenye mipango ile ile ya kuendeleza arusha, dar kama haww wa sasa hivi tu, bp khs mkoa mzima wa mbeya na eneo lote la nyanda za juu kusini mpaka songea? vp khs mtwara, lindi na kusini yote? vp khs tanga na bandari yake? vp khs rift valley the most fertile region in afrika inapita manyara mpaka kusini, vp khs kagera, musoma na mara kwa ujumla? nasikitika kusema uraisi wako hsutakuwa kuwa tofauti sana na awamu ya 4 …
Maeneo yote hayo mengine yataguswa kwenye vipaumbele vya utalii na miondombinu mingine ya kuingia nchi jirani bila kusahau uwekezaj mkubwa na viwanda na uzalishaji mkubwa wa vyakula ( kilimo)
 
Nitafanya mambo matano muhimu.

1. Kuufanya Arusha kuwa Mji wa Taasisi za Kimataifa Afrika ambapo Taasisi zote za kimataifa zitapewa maeneo ya kujenga Ofisi zao na Makazi ya Wafanyakazi wao Arusha- Kupitia hili nina uhakika wa kuingiza fedha nyingi sana za kigeni pamoja na kutengeneza ajira za uhakika kwa Watanzania wengi sana.

2. Kuifanya Dar es Salaam kuwa Mji wa Biashara kweli na Dodoma Ofisi na Makazi ya Serikali tu. Kwenye hili kila kitu cha Kibiashara na maeneo makubwa mazuri ya starehe yatajengwa Dar.

Dodoma kutakuwa na Ofisi za Wizara, Ikulu, Bunge na Mahakama tu. Hakuna taasisi itakuwa na Ofisi Dodoma bali Ofisi za Taasisi zitagawanywa mikoa mbalimbali ikiwemo Dar, Mwanza, Mbeya, Kigoma, Lindi, Iringa, Kilimanjaro, Tanga na Njombe ili kuleta uwiano katika vichocheo vya maendeleo sehemu mbalimbali.

3. Kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha usafirishaji kuelekea kusini, katikati na kaskazini mwa Afrika kupitia Bandari zake na reli. Hapa nitaweka miondombinu ya uhakika ya reli za umeme na barabara za uhakika kwenye njia zote za mipaka ya kuingia na kutoka Tanzania.

4. Kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha Utalii na Uwekezaji Afrika. Kila kivutio cha utalii kinachopaswa kuwepo Tanzania kitawekwa.

Mwisho nitaivunja Wizara ya Ardhi na kuajiri vijana wapya ambao watafanya zoezi na kuipima na kuipanga nchi nzima.

Kabla ya yote haya nitaanza na Katiba Mpya.

Mungu nisaidie!
Urais wa ccm hata Baba Levo anaweza kuongpza. As long as Kamati kuu imempitisha au nguvu nyingine yoyote ikimpitisha ndani ya chama.
 
Itakuaje kila rais akataka kuendeleza hiyo mikoa tu

Jaribuni kufikiria na vijijini kupaendeleza .

Ile Sera ya umeme wa elfu 27 ilikuwa nzuri Sana .

DSM inahitaji kurekebisha na kujengwa barabara za kupita juu na chini, kupunguza msongamono .


Ila ukiwa rais hakikisha mnaboresha na vijijini pia na sio DSM pekee.
 
Back
Top Bottom