Nipo Dar, nahitaji hustler mmoja anipe idea ya kuwekeza 400k then nipate Angalau faida ya 20k kwa siku

Nipo Dar, nahitaji hustler mmoja anipe idea ya kuwekeza 400k then nipate Angalau faida ya 20k kwa siku

Huyo hustler ntampa 70k Kama Asante

NB hii idea before ajanipa Nampa hiyo 70k kwanza sitaki ujanja ujanja
Nipo dsm

Nb Mm Ni hustler na nimeshatapeliwa Sana so endapo nikikupa hiyo 70k ukapotea utakuwa unataka kunifanya niendelee kukaa kwa shemeji tu.
Mi nakupa ushauri wa bureee nenda Goba kwenye mnada wa mbuzi tafuta banda anza kuuza bia tafuta mdada mzurii Ijumaa na Jumapili hukosi laki3 kwa hizo siku mbili siku zingine za wiki wengine watakupa mawazo
 
Kwamba in a week umake( faida) laki na 40 ila MTAJI NI LAKKI 4[emoji1787][emoji119]

Hela yoyote ile inaweza kuwa ni ndogo au kubwa sana inapopimwa kwenye aina ya biashara ambayo itaenda kuingizwa na mazingira ya biashara yenyewe, kwamfano kupata faida ya 20K kwenye biashara ya hardware itahitaji uwe na mtaji mkubwa sana zaidi ya hiyo 400K, ila kuipata hiyo 20K kwenye mgahawa hiyo 400K(ikiwa kama operating capital) inawezekana na kuzidi kabisaa.

Mama lishe mzuri wa maeneo ya mogodi iliyochangamka ukimpa 400K aiingize kwenye biashara anao uwezo wa kukunja hata 50K kama faida kwa siku (nikiongea kwa uzoefu kabisa na wanaotembea huko watasema hapa), plate mnayonunua huku town 2000 kule ni 4000-4500 na watu ni wengi balaa, 20K kitu gani??

Kuna jamaa yangu pale Mwanza anauza ugali na samaki tu (samaki fulani wanaitwa mumi) yule ukipita pale nyomi analojaza ni mpaka raia zina simama, sehemu kama ile operating capital ya 400K ni kubwa sana tukitoa fixed cost, na 20K ni hela ndogo sana kuiingiza.

Tofauti na hivyo nilivysema hapo, kuna vibiashara ambavyo ni vya KIJINGA na vya AIBU sana kwa macho yenu, ila ndio vyenye hela, na watu wengi huanzia huko.

Kukataa kuwa haiwezekani kuzalisha 20K kutoka kwenye 400K ni kukosa akili na mawazo ya kijasiriamali.

MSIKARIRI MAISHA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wamekariri biashara za vitabuni, kila kitu wanaona hakiwezekani wakiapply zile formular zao[emoji23][emoji23][emoji23].


Sent using Jamii Forums mobile app

Hapo KWA hiyo hela anaongeza 20k anapata mifuko buku/bundle la Pp bags Kg 100 kuna masoko mengi ya mazao Nchini .. na mifuko unatembea Kasi ya 4g a day unaweza uza mpaka mifuko 5000 mara 20???



Tatizo kukariri kama ulivyosema mkuu
 
Mtaji wa 400k unatosha kabisa. Ila kabla ya yote unatakiwa uumize akili vya kutosha hata mwili pia. Biashara ya huo mtaji inabidi kujitoa mhanga na muda wote uwepo kimwili na kiakili. Ni mtaji ambao hauhitaji kabisa ule uswahili wa kusema "mwanzo mgumu", "binadamu sio wakamilifu tunafanya makosa", nk. Huo mtaji unahitaji discpline ya hatari maana kosa kidogo tu mtaji umefia mbali. Ungekuwa una subira na una mchina huko China ungeagiza 100pcs za viatu vya Tsh 2000 ambazo unaweza kuuza TZ kwa Tsh 10,000 hadi 15,000/=. Ni subira ya mwezi hadi mwezi na nusu.
 

Attachments

  • IMG-20221006-WA0000.jpg
    IMG-20221006-WA0000.jpg
    71.7 KB · Views: 14
Huyo hustler ntampa 70k kama Asante.

NB hii idea before ajanipa Nampa hiyo 70k kwanza sitaki ujanja ujanja. Nipo DSM.

NB: Mimi ni hustler na nimeshatapeliwa Sana so endapo nikikupa hiyo 70k ukapotea utakuwa unataka kunifanya niendelee kukaa kwa shemeji tu.
Wazo lazima lifanyike hapo ?
 
Mtaji wa 400k unatosha kabisa. Ila kabla ya yote unatakiwa uumize akili vya kutosha hata mwili pia. Biashara ya huo mtaji inabidi kujitoa mhanga na muda wote uwepo kimwili na kiakili. Ni mtaji ambao hauhitaji kabisa ule uswahili wa kusema "mwanzo mgumu", "binadamu sio wakamilifu tunafanya makosa", nk. Huo mtaji unahitaji discpline ya hatari maana kosa kidogo tu mtaji umefia mbali. Ungekuwa una subira na una mchina huko China ungeagiza 100pcs za viatu vya Tsh 2000 ambazo unaweza kuuza TZ kwa Tsh 10,000 hadi 15,000/=. Ni subira ya mwezi hadi mwezi na nusu.
Mkuu hizo raba nazipatia wapi?
 
Hiyo labda tuuze nyama choma ya mbwa
 
Back
Top Bottom