Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
binafsi sipakubali kwasababu ya joto ila somehow pazur msimbati kule beach ipo vzrKwa sisi ambao tumetembea sehemu nyingi hii nchi,karibia Kila sehemu kunafanana fanana. Mabadiliko ni machache mno mkoa kwa mkoa. Na mtwara imepazidi sehemu nyingi tu siyo kubaya kihivyo.
Kuna dada yeye ametokea kuoachukia Dodoma vibaya mno. Ukimsikia anavyopaponda Dodoma unaweza sema huko mahali ni kuzimu na wanaoishi huko ni mashetani.
Ongea tu Chinga Wala Hakuna shida Mana najua mchana huu unaenda kufichama ule Chikandanga na mbaazi.Mzee au unataka niongee kilugha mm nimekaa sehemu nyingi
Sawa bhnaOngea tu Chinga Wala Hakuna shida Mana najua mchana huu unaenda kufichama ule Chikandanga na mbaazi.
Maadam umewakuta wengine wanaishi, nawe uta-adopt tu!Tangu nifike Mtwara miezi kadhaa iliyopita, mambo ninayokutana nayo sikuyategemea kabisa. Picha inaanza wakati nakuja kuripoti, ile nafika bus stand ya Mkanaredi naambiwa hapa ndiyo Manispaa ya Mikindani na ndiyo mjini.
Sikuamini! Mr. akanitia moyo na kuniambia nitazoea mazingira. Nikasema, "Sawa, maadam ni mjini, kitu cha msingi ni huduma."
Tukachukua lodge (na lodge zenyewe maji hayatoki, wanategemea maji ya mvua... yani ni tafrani tupu!). To cut a long story short, maisha ya Mtwara ni magumu kwenye nyanja zote! Maji ni shida, bei ya vitu iko juu sana kuliko hata Dar es Salaam, na miundombinu hafifu inafanya usafiri kuwa wa tabu.
Huduma za kifedha ni chache na ziko mbali, yani kulala au kushinda njaa ukiwa na hela mfukoni ni kitu cha kawaida sana hapa!
Ikifika saa 3 usiku, barabarani ni nyeupe kabisa—huoni mtu, na maduka yanafungwa mapema. Viwanja vipo, lakini The Shooters ndicho kiwanja pekee nilichoelewa, na nikiwa hapo najihisi kama niko Dar es Salaam.
Serikali ni kama imeususa kabisa huu mkoa!
Vipi umehamishiwa Lagula Hospital?Mambo mengine serikali inachangia sio wana
Mashamba makubwa unalima🤣
Hapazoeleki kule.Mimi naungana na shemeji kusema “utazoea tu”. Itakuchukua muda ila kuna siku utashangaa umeshapazoea kabisa.
Inategemea Dar sehemu gani, kuna sehemu Dar watu wanaishi kama wapo Beverly Hills.Mikoa yote inafanana Tu kama Akili yako umeipanga izoee mazingira utaweza kuishi popote
Unataka uishi kama upo DAR hapo ni kujidanganya, TANZANIA bado Sana hasa Huko mikoani hata hiyo DAR nayo imechoka sanaa sioni utofauti na mikoani tu
Maji ya bombani yana chumvi ukifulia nguo tu inapauka.Kila kukicha ni afadhari ya jana