Nisaidieni: Namnyofoaje baba yangu kwenye Shirika kabla Rais Samia hajamuwajibisha?

sifi leo

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2012
Posts
5,182
Reaction score
8,948
Nipeni ushauri, mshua wangu ni miongoni mwa vikonge vilivyosalia kwenye shirika X, na juzi usiku tukiwa mezani tunakula Kwa mbali nilimwona presha imempanda nilivyomuuliza kisa nini akadai anawaza ile kauli aliyoitoa Rais Dr Samia kuhusu mashirika yasiyo na faida.

Mzee anadai hawezi nyofoka lazima apelekewe moto, sasa anaomba msaada nini tufanye kumsuru, na Mzee mwenyewe ni konyo alivyopanda juu alipanda na ngazi yake hakutaka wengine wapande Ili nyakati kama hizo waimbe palapanda pamoja.

Wadau mwenye uzoefu anisaidie kuhusu mrungura usijali tupo pamoja.
 
Mwambie ajiuzulu, kwani ni lazima awe kiongozi wa hiyo taasisi ?
 
Weka mzigo wa kutosha mezani ili nimtengenezee mshua wako dawa ya kibabe ya kumpumbaza Mama.
Nipo pande za Kwa Msisi huku Handeni, Tanga. 😇
 
Baba yako wakati anapewa hiyo kazi ulikuwepo?
Mwache aendelea kubaki kwenye kiti anyolewe mavyuzii yake yeye hafanyi kazi anakula pesa za umma bure..!!!
 
Na Wizi na uporaji wote alioufanya anahofu nini wakati ni jitu tajiri?
 
Sifi leo! Mwambie babako akaombe kazi DP World kwani hadi sasa bado hawajapata Mkurugenzi Mkuu hapa TZ!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…