Nitaishangaa serikali kama kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 haitatoa chakula cha mchana bure kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari nchini.

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari zenu viongozi!
Ni dhahiri Tanzania inakwenda kuwa serikali tajiri. Serikali ambayo haitakuwa tegemezi kwa namna yoyote ile.
Kuna changamoto nyingi nchini katika sekta za afya, elimu, na uchumi.
Nikianzia sekta ya elimu , serikali itoe chakula cha mchana bure mashuleni. Huku msingi na sekondari ndiko wanakoandaliwa watumishi wa umma. Serikali ikizembea huku shule za msingi na sekondari itajikuta ina watumishi wenye uwezo mdogo na wasio wazalendo. Itavuna raia wenye ufahamu mdogo na wenye kukosa uzalendo.
Serikali iende mbali zaidi kwa kuondoa au kuwalipia ada wanafunzi wote wa vyuo vikuu.
Hizi kodi za uzalendo tunazokatwa kwa lazima zitatosha kufanya haya na mengine mengi.
 
Nyerere na ujamaa wake ulitufundisha sana kuoenda vya bure hakika sasa mkuu wew mtoto wako unataka serikali imlishe bure wew ukifanya nini ? Hebu beba majukumu lisha watoto wako kwa kutoa michango ya chakula shulen na si kutegemea serikali kuleta vya bure maana kwa tulipofikia hicho kitu ni almost impossible an

Nb.
Kodi zilizo ongezwa tayar wamesema watapo zipeleka
 
Mimi najiweza. Naweza ku accommodate mahitaji yangu yote muhimu pamoja na familia yangu. Sio mbinafsi kama wewe.
Nikizungumza jambo simaanishi mimi na familia yangu ndio walengwa. Nazungumzia maisha ya Watanzania.
 
Mimi najiweza. Naweza ku accommodate mahitaji yangu yote muhimu pamoja na familia yangu. Sio mbinafsi kama wewe.
Nikizungumza jambo simaanishi mimi na familia yangu ndio walengwa. Nazungumzia maisha ya Watanzania.
huko ni kuwalemaza watu. mpaka na sosi mashuleni serikali ikulishie watoto? i get it maybe ww unauwezo kama ulivyosema. but that is a bad idea
 
huko ni kuwalemaza watu. mpaka na sosi mashuleni serikali ikulishie watoto? i get it maybe ww unauwezo kama ulivyosema. but that is a bad idea
HAPANA
Ungesoma shule za msingi tulizosoma sisi zamani ungeelewa concept yangu.
Tulikuwa tukienda shule asubuhi kila mapumziko tuliyatumia kucheza mpira tu. Nyumbani mbali na wengine nyumbani karibu ila wakirudi wanaishia kutwanga mihogo mikavu(makopa) ndipo wale.
 
Kwani ilani ya chama inasemaje
 
huko ni kuwalemaza watu. mpaka na sosi mashuleni serikali ikulishie watoto? i get it maybe ww unauwezo kama ulivyosema. but that is a bad idea
Umesoma shule gani mkuu?? Labda umesoma mijini humu ambako changamoto ya elimu si kubwa sana.
Kuna mahali mtoto anatoka km nyingi ili afike shule, na kuna muda wa kwenda kula na kurud shule aendelee na msomo, wenzie wakitoka ye inabidi abaki bila kula chochote. Aisee ni huruma man.

Kitu kingine apa naona watz wengi wakitusua huwa wanaona ambao hawajatusua ni wazembe na wavivu, tukiondoa hiyo mindset itasaidia kusaidiana.
 
Ubinafsi na roho mbaya ya kiibilisi.
Hivi mtu kama huyu anayepinga mwanafunzi kupewa chakula shuleni ana akili na utu kichwani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…