Nitajie Rais wa Africa aliyefanikiwa kudhibiti nchi kwa kuwa mlaini/mpole mpole (polite)

Nitajie Rais wa Africa aliyefanikiwa kudhibiti nchi kwa kuwa mlaini/mpole mpole (polite)

Nchi kama China,Russia,Germany hazikuendelea kwa kubembelezana,Josep Stallin,Mao Zedong,Adolf Hitle,huwezi kuacha kuwataja hawa watu ukiongelea maendeleo ya hizo nchi 3 nilizozitaja,

But Dunia imebadilika,kiongozi yeyote yule aongoze kwa mujibu wa sheria na atakayepatikana na hatia ahukumiwe kwa mujibu wa sheria na kusiwe na ile kubembelezana,wahujumu uchumi,wala rushwa,Wezi na makosa mengine makubwa wahukumiwe adhabu kali.
 
Hata Lincoln, A hakuwa mpole. Kwa taarifa yako ndiye aliyeendesha vita dhidi ya waliotaka kuitenga Amerika na akafanikiwa akiwa na Kamanda wake General Grant!
Vita ni uamuzi wa kitaifa dhidi ya waasi wanaotaka kuligawa taifa (uhaini). Usilinganishe na uamuzi binafsi wa kuzuia uhuru wa habari, demokrasia na kuwa na vikundi vya wasiojulikana kuteka, kutesa na kuua wakosoaji nje ya mfumo wa katiba na sheria za nchi.
 
Tunajua upole ni sifa ambayo kila mmoja anapaswa kuwa nayo pale inapostahili. Chochote kinachofanyika kinapaswa kuwa na kiasi.

Swali langu ni je, ni kiongozi gani wa nchi za kiafrika alieweza kudhibiti nchi kwa kuwa mpole?
Tuanze na Nyerere, Mandela. Kenyata nk. Je, walikuwa na haiba zipi ktk kudhibiti nchi kisiasa, kiuchumi, kijamii nk
Ramaphosa
 
Tunajua upole ni sifa ambayo kila mmoja anapaswa kuwa nayo pale inapostahili. Chochote kinachofanyika kinapaswa kuwa na kiasi.

Swali langu ni je, ni kiongozi gani wa nchi za kiafrika alieweza kudhibiti nchi kwa kuwa mpole?
Tuanze na Nyerere, Mandela. Kenyata nk. Je, walikuwa na haiba zipi ktk kudhibiti nchi kisiasa, kiuchumi, kijamii nk
Una maana gani unaposema mpole?. Maana ukali unaweza kumaanisha ukosefu wa hekima. Ukali unaweza kumaanisha kutaka kuwa juu ya wasaidizi wako muda wote hata katika masuala ya weledi ambayo wameyasomea na wanayafahamu kukuzidi.

Ukali unaweza kumaanisha maamuzi ya pupa tu yanayoitia hasara nchi yako kwa maana ya matumizi mabaya ya kodi ya wananchi yanayoambatana na hicho unachoamua.

Ukali unaweza kukosa hekima na ukataka kila mtu afikirie kama unavyofikiria, Upole ukizidi ni mbaya kwa hao wanaoongozwa lakini ukali unaambatana na dhuluma, udhalimu, uonevu na mabaya mengine ya viwango hivyo.
 
Africa Africa tu hapa mnaleta uzungu tu Africa kumejaa na kunanuka rushwa na ubinafsi utendaji mbooovu inahitajika nguvu kubwa kutawala Africa
 
Kwani kufoka ndo uongozi?
Mandela hakuwahi kufokafoka..
Wala Botswana haijawahi pata kiongozi anaefokafoka...
Mauritius unajua wametuacha kiasi gani Kwa Maendeleo?hawana Viongozi wanao foka foka..
Kufoka foka ni dalili ya kutokuwa na majawabu na kutupia lawama watu wa chini yako ..
Hata Mwingi hakuwa anafoka foka .
Mkapa ndo kabisa alikuwa anafanya overhaul maeneo Tele bila hata kufoka foka
Pia kufoka ni dalili ya matatizo binafsi ya rais husika. Kutaka kuogopwa kunaambatana na hiyo tabia.

Ni inferiority complex ya tangu utotoni anayokuwa nayo huyo rais. Wengine wanakuwa na unyonge kwa maprofesa na wanajeshi na ni unyonge wa huko walipokulia.
 
Vita ni uamuzi wa kitaifa dhidi ya waasi wanaotaka kuligawa taifa (uhaini). Usilinganishe na uamuzi binafsi wa kuzuia uhuru wa habari, demokrasia na kuwa na vikundi vya wasiojulikana kuteka, kutesa na kuua wakosoaji nje ya mfumo wa katiba na sheria za nchi.
Ahahahahah!
 
Kweli nianze kugoogle taifa moja baada ya jingine na viongozi wake?
Ungeweka hapa wasifu wake itasaidia na wengine pia wenye kuhitaji majibu!

Huyo kiongozi alitumia mbinu gani?
Aliwezaje kudhibiti uhalifu wa kisiasa, kijamii nk? Aliwezaje kuwafanya walio chini kuwa waadilifu wakati wote? Aliwezaje kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma? Hilo taifa lina idadi gani ya watu? Wana kipato kipi?
Wanaendeshaje uchumi wao? Walianzia wapi?
Kudhibiti uhalifu wa kisiasa na kijamii kunahitaji kuwa na mifumo inayofanya kazi hakuhitaji mtu anayetumia nguvu kubwa na wakati huo huo akiumiza tabaka la watu wa upande mwingine bila ya sababu ya msingi.

Rais ni wa wote na busara ya kawaida tu inapaswa imkumbushe kuwa ni mtumishi wa kila mtu akianza kupendelea kundi fulani kwa makusudi anakuwa analiumiza kundi lingine kwa makusudi hiyo hiyo.
 
Tunajua upole ni sifa ambayo kila mmoja anapaswa kuwa nayo pale inapostahili. Chochote kinachofanyika kinapaswa kuwa na kiasi.

Swali langu ni je, ni kiongozi gani wa nchi za kiafrika alieweza kudhibiti nchi kwa kuwa mpole?
Tuanze na Nyerere, Mandela. Kenyata nk. Je, walikuwa na haiba zipi ktk kudhibiti nchi kisiasa, kiuchumi, kijamii nk
Unamaanisha kudhibiti ni kufanyaje, kuua? Kudhulumu watu mali zao, kuwa Rais mkatili kama Magufuli?
 
Tunajua upole ni sifa ambayo kila mmoja anapaswa kuwa nayo pale inapostahili. Chochote kinachofanyika kinapaswa kuwa na kiasi.

Swali langu ni je, ni kiongozi gani wa nchi za kiafrika alieweza kudhibiti nchi kwa kuwa mpole?
Tuanze na Nyerere, Mandela. Kenyata nk. Je, walikuwa na haiba zipi ktk kudhibiti nchi kisiasa, kiuchumi, kijamii nk
Ukali unasaidia pale ambapo mhusika anakuwa mtenda haki asiye mwizi. Mf nyerere. Usimlete yule2 jambazi muuaji hapa,. The nightmare of tz
 
Kwani kufoka ndo uongozi?
Mandela hakuwahi kufokafoka..
Wala Botswana haijawahi pata kiongozi anaefokafoka...
Mauritius unajua wametuacha kiasi gani Kwa Maendeleo?hawana Viongozi wanao foka foka..
Kufoka foka ni dalili ya kutokuwa na majawabu na kutupia lawama watu wa chini yako ..
Hata Mwingi hakuwa anafoka foka .
Mkapa ndo kabisa alikuwa anafanya overhaul maeneo Tele bila hata kufoka foka

Mwingi amewahi ongoza nchi gani Afrika?
 
South Africa wana katiba nzuri sana, lakini rais wao yuko kwenye skandali za ufisadi karibu kila mwaka, hiyo katiba yako inasaidiaje hapo?
Kenya wana katiba nzuri, lakini wamechagua rais aliye na tuhuma za ufisadi wa kutisha, hiyo katiba yako inasaidiaje hapo?
Hizo ni katiba nzuri kwa jinsi walivyoona wao sio lazima ifae kwetu.ila pia inawezekana kupitia katiba hizo ndizo zilizopelekea wewe kujua kuna huo ufisadi.Ni mjinga peke yake ndiye atakayeogopa nchi kua na katiba bora itakayowajibisha na kujisimamia.
 
Wewe nchi ni kubwa na ina watendaji wengi lazima wote wajue msimamo wako kwamba ukizingua kwenye taasisi yako au shirika unatimuliwa kwa aibu lazima tu waogope...mtoa mada hakuna rais mpole atakayefanikiwa africa Mungu ametupa mfano bora wa magufuli kazi kwetu
Kibaki alikua mkali? Mbona Kenya ilipaa kiuchumi kuliko hata utawala wa dikteta Moi
 
Mbona Bashite na Sabaya hawakutimuliwa kwa aibu??
Wewe nchi ni kubwa na ina watendaji wengi lazima wote wajue msimamo wako kwamba ukizingua kwenye taasisi yako au shirika unatimuliwa kwa aibu lazima tu waogope...mtoa mada hakuna rais mpole atakayefanikiwa africa Mungu ametupa mfano bora wa magufuli kazi kwetu
 
Back
Top Bottom