"Nitakufanyia Umafia" Nini maana ya neno Mafia? Kwanini Mafia?

"Nitakufanyia Umafia" Nini maana ya neno Mafia? Kwanini Mafia?

scatter

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2013
Posts
1,667
Reaction score
926
Wakuu habari zenu,

Kichwa cha habari kinajieleza. Ningependa kufahamishwa kwa nini mtu akitaka kufanya jambo baya utasikia akisema NITAKUFANYIA UMAFIA au utasikia akisema MIMI NI MAFIA NITAKUUA!

Je, kuna uhusiano wowote na kisiwa cha Mafia?

Mwenye kujua kiini cha neno hili ningefurahi kufahamishwa kwani nina trip ya kwenda Mafia so nikikumbuka maneno hayo juu naishiwa hamu kabisa ya safari.

Kama kuna uhusiano na watu wa Mafia chanzo kilikuwa nini?


======


Jumong S says;
Hili ni kundi lililosikika na linalosikika sana duniani na ni maarufu sana nchi za Ulaya hasa Italy, visiwa vya Cicily. Inasemekana jamaa ni wavumbuzi wakubwa wa mbinu za kijasusi, mauaji na ulinzi. Kuna ukweli kuwa wana mbinu nyingi ambazo wakati mwingine hata vyombo vya usalama hawajawahi kuzijua.

Huko kuna kila aina ya practice au mafunzo ya kujifua ikiwa ni pamoja na Martial Art, Karate, Kung Fu, Kick Boxing n.k. Pia hujifunza kwa ustadi mkubwa matumizi ya silaha zote uzijuazo!

Jamaa hubadilika kadri tekinolojia inavyobadilika. Ni vigumu kujua kiongozi wao ni yupi maana mara nyingi hugawanyika ktk vikundi vidogo vidogo ambavyo huwa na uongozi na members huaminishwa kuwa ndo uongozi wa MAFIA japo orders nyingine za kundi hutoka from unknown sources!

Anayewajua zaidi atuelezee maana hivi karibuni serikali ya Italy ilitangaza kuwakamata viongozi wakubwa wa Mafia na kusema kundi linasambaratika!

Je, kuna ukweli kuwa kundi lina association na Kanisa?
 
Mafia ina maana ya kumfanyia adui yako mambo yasiyofaa na yenye kuzidi ukatili wa mtu wa kawaida
 
ref HITLER story n.k. lilikuwa jina la vikundi vya kikatili enzi hizo
 
A mafia is a type of organized crime syndicate whose primary activities are protection racketeering, the arbitration of disputes between criminals, and the organizing and oversight of illegal agreements and transactions. Secondary activities may be practiced such as drug-trafficking, loan sharking and fraud.
 
Asili ya Umafia ni Italy
haina uhusiano na kisiwa cha mafia cha Tanzania...

Umafia wa Italy unahusisha makundi ya kihalifu
yaliyokuwa yanafanya shughuli zake kama kundi
shughuli hizo zinafanana na za kiserikali lakini sio kihalali za kisheria

mfano serikali ina arrest kupitia police...mafia wana teka nyara
serikali ina hukumu kifo thru mahakama..mafia wanatoa hukumu ya kifo na unauwawa na hitmen..
inaitwa 'organized crime'
 
mafia pako salama mkuu...safari njema

Kihistoria Mafia ilikuwa mahali pa miji ya kale ya utamaduni wa Waswahili kama vile miji ya Chole na Kua. Baada ya kuondoka kwa Wareno ilikuwa chini ya Sultani wa Omani baadaye ya Zanzibar.

Mwaka 1892 Wajerumani walinunua Mafia kutoka Sultani ya Zanzibar ikawa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. 1915 Waingereza waliteka kisiwa wakishambulia manowari ya Kijerumani ya SMS Königsberg mdomoni wa mto Rufiji kutoka Mafia. Baada ya mwisho wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Mafia imekuwa sehemu ya Tanganyika sio tena Zanzibar.
 
Mafia kwa asili si kikundi kimoja. Asili ya jina ni mji mdogo uliopo Sicily Italy, katika karne ya 19 kuna Waitaly kutoka eneo hilo walihamia Marekani na wengi wao kujihusisha na biashara haramu kama madanguro na magendo.

Baadaye kadri vikundi vilipokua vikaanzisha magenge ya uhalifu na ulipizaji kisasi. Ilifikia hatua mpaka baadhi ya Wanasiasa wakawa bribed ili shughuli zao ziendelee.
 
kumfanyia mtu umafia maana yake ni kumdhuru mtu bila kuacha ushahidi
 
Asili ya Umafia ni Italy
haina uhusiano na kisiwa cha mafia cha Tanzania...

Umafia wa Italy unahusisha makundi ya kihalifu
yaliyokuwa yanafanya shughuli zake kama kundi
shughuli hizo zinafanana na za kiserikali lakini sio kihalali za kisheria

mfano serikali ina arrest kupitia police...mafia wana teka nyara
serikali ina hukumu kifo thru mahakama..mafia wanatoa hukumu ya kifo na unauwawa na hitmen..
inaitwa 'organized crime'
Nimekuelewa mkuu
 
Kuna watu walinidanganya kuwa kisiwa cha mafia kuna watu wanakula nyama za watu ...pia kuna uchawi wa kutisha
 
Umafia inashabihana na lahaja kama kubonyezwa kizenji ni maneno tu ww nenda Mafia usiogope yakheee ila kuna mambo ukiyakuta yaache kulekule sawa yakheee
 
Umafia inashabihana na lahaja kama kubonyezwa kizenji ni maneno tu ww nenda Mafia usiogope yakheee ila kuna mambo ukiyakuta yaache kulekule sawa yakheee
Mambo gani tena .


Wanalima mihogo nn
 
kumfanyia mtu umafia maana yake ni kumdhuru mtu bila kuacha ushahidi

Mkuu wewe ndio umetoa maana halisi ya kumfanyia mtu "Umafia". Mafia wakitaka kukuua hawatakuonyesha dalili hata siku moja. Watajifanya wajinga ili uwadharau na kudhani kuwa hawawezi kukudhuru. Tena kama ni mtu wa karibu watajifanya marafiki zako kweli kweli.

Siku ambayo huitegemei kabisa ndio utashangaa anakuja mmoja anakualika mwende mkale chakula cha jioni ukipanda kwenye gari utakuta kuna mtu kakaa siti ya nyuma, utatambulishwa kuwa huyo ni cousin wa huyo aliyekualika dinner. Mkifika sehemu ambayo imekaa vizuri na wewe ume-relax ndio utashitukia kamba ipo shingoni, jamaa aliyekaa siti ya nyuma anakunyonga mpaka unakufa.

Wakishakuuwa wana jinsi yao ya kupoteza mwili wako usipatikane tena; Wanaweza kuweka mwili wako kwenye pipa wakalijaza zege kisha wakaenda kulitupa baharini, wanaweza kuweka mwili wako kwenye gari bovu kisha wakalipeleka kwenye compacter, mashine ambayo italisaga na kuliminya hilo gari mpaka liwe dogo kama box, wanaweza kukukatakata kisha wakatumbukiza vipande vya mwili wako kwenye acid na nyingine nyingi ambazo huzitumia kuhakikisha mwili wako haupatikani tena. Huo ndio "Umafia".
 
Back
Top Bottom