Niulize chochote kuhusiana na biashara, masoko na mauzo

Niulize chochote kuhusiana na biashara, masoko na mauzo

Mkuu mimi nahitaji ushauri wa kipi nianzishe kwa Mkoa wa Kigoma. Nina mtaji wa laki mbili na nusu hivi. Nilikuwa na wazo la kuanzisha 1. Biashara ya mitumba je nitaipata wapi na faida inapatikanaje.
2. Kufungua duka la vipodozi ambalo linaanza na mtaji mdogo tu kama huo, je nikweli unapotaka kufungua duka hilo nilazima uende kusadili duka kwa mkemia anayehusia na mambo ya Afya.
 
Kwa anayejua biashara ya jumla ya vocha anieleweshe wanapataje kwa bei nafuu na kujumlisha. Faida yake iko vipi kwa duka la jumla?
 
Mkuu mimi nahitaji ushauri wa kipi nianzishe kwa Mkoa wa Kigoma. Nina mtaji wa laki mbili na nusu hivi. Nilikuwa na wazo la kuanzisha 1. Biashara ya mitumba je nitaipata wapi na faida inapatikanaje.
2. Kufungua duka la vipodozi ambalo linaanza na mtaji mdogo tu kama huo, je nikweli unapotaka kufungua duka hilo nilazima uende kusadili duka kwa mkemia anayehusia na mambo ya Afya.

biashara ya mitumba inasoko sana kigoma but kwa vijijini unakuja zako karume unachukua mitumba yako ya nguo moja buku ukifika huko unauza mpka elfu 4
 
Okey asante, ni posta maeneo gan? Kama unafaham mitaa tafadhal nisaidie pia naomba unisaidie kuuliza na bei zake kwa balo
dah sikushauri uingie kichwa kichwa unaweza kulia maana wengi wanaweka malonya ndani,tafuta mtu mzoefu wa kazi hizo
 
kwema mkuu,natafuta soko la bata maji,wa kawaida,bata pekin na bukini.napatikana dar mbezi beach.
 
Nauliza nitapataje Baloo lashati zile kali kabisa zamtumba navipi bei yabaloo
 
Okey asante, ni posta maeneo gan? Kama unafaham mitaa tafadhal nisaidie pia naomba unisaidie kuuliza na bei zake kwa balo
karibu na hii hoteli ya tamari, maeneo ya kitumbini, na maeneo ya kuzunguka hapo kuna maduka mengi,
 
Mkuu mim naomba kujua mahali ambapo ntapata maduka ya jumla yanayouza kemikali/madawa ya kutengeneza sabuni za maji na kipande
 
Kwa sigara tafadhali nenda kanunue kiwandani TCC wana mfumo wao wa kusajili wafanyabiashara kutokana na maeneo. Nakutafutia namba za simu za manager wa wilaya ya kinondoni atakusaidia. Tukumbushane Ila nikiipata sasa hv nakutumia
katika harakati zangu nilipita hapo tcc mwaka juzi wao wanasambaza sigara kwa agents wao waliopo sehemu mbalimbali hivyo na kuwa agent mpaka uwe na mtaji usiopungua milioni10....hapo inabidi akanunue kwa agent aliye karibu mfano kigamboni lazima kutakuwa na agent.

ni hayo mkuu
 
naanza na yule wa karanga, kampuni ya smart watengenezaji wa karanga za diamond karanga soko lao liko wazi na wananunua hadi tani 100 kwa mwezi wapigie kwa namba zao hizi 0658271110 na 0715578772 hua wanahitaji karanga nyeupe ziwe za kiwango cha juu yaani zisioze na ufunge kwenye kiroba cha kilo 20 kila kiroba nadhani ukiwapigia ni nzuri zaidi.
 
nafuata yule wa ng'ombe aina ya nyankole wale ng'ombe hufugwa uganda na rwanda na kwa Tanzania wanapatikana katika minada ya Ngara , rusahunga, katavi baadhi ya maeneo lakini huko nilipokutajia ni sehemu ambapo utapata kwa bei rahisi kuliko pugu itakua bei kubwa.
 
yule wa mbeya mwenye milioni moja , changamkia fursa msimu ndio huu kwa mbeya kuna mpunga , choroko, soya na ufuta kanunue vijijini halafu unaenda kuuza mbeya kwenye godowns za wabongo au wahindi na kwa mpunga kanunue vijijini unaenda kukoboa mjini unauza mchele pesa itazunguka nakusihi usifanye biashara ya mali kuoza kama ndizi, nyanya na vitunguu kama hauna uzoefu navyo, lakini pia unaweza kwenda kununua makoti ya lazer nakonde upande wa zambia na kuyauza pale sido , au kanunue mtumba hata belo 2 dar then kachane pale sido lkn kabla ya kufanya biashara fanya utafiti zaidi tafadhali.
 
Mkuu mim naomba kujua mahali ambapo ntapata maduka ya jumla yanayouza kemikali/madawa ya kutengeneza sabuni za maji na kipande
mtaa wa Somali na Kongo. nicheki kwa 0713039875 kama unataka home delivery
 
Mi ni mtaalam wa afya yangozi, ninayetoa ushauri bure juu ya matumizi ya vipodozi vya Asili kulingana na ngozi yake.mfano ngozi kavu lazima kipodozi chako kiwe na butter wakati ngozi ya mafuta lazima kipodozi chako kiwe na lemon. Pia tunatibu chunusi, MBA, fangasi, ngozi ziloathirika na vipodozi au metakelfin. Piga 0713-039875
 
Back
Top Bottom