Mdogo ake the BOLD
JF-Expert Member
- Mar 30, 2018
- 510
- 871
Kama injini ina nguvu kama kawaida basi Intake manifold inaweza kuwa inavuja; yaani baada kupita kwenye air flow sensor kuna hewa nyingine inaingia kwenye injini bila kupimwa na air flow sensor. Kama injini haina nguvu, basi huenda injector zako hazifanyi kazi vizuri kwa hiyo haziingizi mafuta ya kutosha kwenye injini. Vinginevyo inawezekana oxygen sensor yako imekufa, inapeleka namba mbaya kwenye computer
Haina madhara immediately, ila in the long run inaweza kuharibu brake booster yako ukakosa brake, na vile vile inaweza kuvunja pistor rings. Unaweza kuendesha na hilo leak kwa muda hata miezi sita au zaidi bila matatizo yoyote lakini siku moja utapata madhara kama hayo niliyokutajia.Engine ina nguvu kama kawida na je inawezekana ikaleta shida kwenye engine???
Haina madhara immediately, ila in the long run inaweza kuharibu brake booster yako ukakosa brake, na vile vile inaweza kuvunja pistor rings. Unaweza kuendesha na hilo leak kwa muda hata miezi sita au zaidi bila matatizo yoyote lakini siku moja utapata madhara kama hayo niliyokutajia.
Mkuu ....nimebadili air filter sensor japo ilikuwa nzima,nimebadili air filter nayo, naomba msaada hapaNiambie vitu ambavyo umeshabaidilisha bila mafanikio
Usishangae kuhusu utambulisho huu. Mimi sasa ni ASE Certified Service Consultant wa magari madogo yanayotumia petroli hasa ya Ford, GM, na Chrysler....
Usishangae kuhusu utambulisho huu. Mimi sasa ni ASE Certified Service Consultant wa magari madogo yanayotumia petroli hasa ya Ford, GM, na Chrysler.
Nimepata license yangu hivi majuzi tu mwaka huu baada ya kuitafuta kwa muda kidogo through part-time activities kwani hiyo siyo kazi yangu kuu.
Certification hiyo inahitaji siyo tu kufaulu mtihani wake, lakini pia uwe na uzoefu wa kutosha kwenye auto-repair shop.
Nimekamilisha experience hiyo inayotakiwa mwaka huu na kupata license yangu.
Kwa vile injini nyingi za petroli zinafanana katika utendaji, jisikie free kuniuliza swali lolote kuhusu matatizo ya injini ya gari yako model yoyote inayotumia mafuta ya petroli.
Siahidi kuwa majibu yangu yote yatakuwa ni sahihi, lakini sehemu kubwa itakuwa ni sahihi, na hata yale ambayo hayatakuwa sahihi yanaweza kukusadia kujua wapi pa kuanzia.
Ina kilometa ngapi. kwani kuanzia mwaka 2003 sasa hivi ina umri wa miaka 17, lakini zaidi inategemea imeshetembea umbali gani. Kama bado iko chini ya KM 250,000 utatakiwa utumie 10W-30 tu, ila kama imeshazidi hapo basi unaweza kutumia 10W-40 au SAE40. Usitumie 20W-50 au SAE50 kwenye gari hilo kwa namna yoyote ile iwayo.Habari mkuu! Naomba kujua ni Engine oil yenye grade gani inafaa kwenye Toyota harrier ya mwaka 2003 Engine 2AZ-FE 2400cc inayotumia petrol na inatumika hapa dar es salaam,maana nimeona mkanganyiko sana wengine wanasema 10W40 wengine 5W30 wengine 20W50,tupe muongozo wako kitaalam.Natanguliza shukrani
Swali lako sikulielewa vizrui, tafadhari tumia PM kusudi tuweze kueleweshana tatizo lenyewe kabla ya kutafuta ufumbuzi wake.Nimekuwa nafuatilia sana elimu unayotoa mdogo wangu for sure am inspired, mpaka nikajiuliza nilikuwa wapi kusomea mambo kama haya, ukweli you deserve to be a lecturer somewhere, umenitoa mbali kwa elimu ya magari nakufuatilia sana.
Anyway nahitaji elimu zaidi maana ndugu yako namiliki subaru forester, iliwahi kuingia maji nikafanya kosa la kuiwasha niitoe ikashindikana, kilichotokea niliomba breakdown ikaichukua mpaka 0-60 garage magwiji wa subaru wanasema hawatengenezi gari aina nyingine, baada ya kuchunguza mfumo wake ni wa umeme wakabaini control box na stering reck zimeungua, wakabadirisha, lakini haikuisha hata miezi minne kurudi service gari ilikuwa inagonga wakasema stering reck imeharibika na ina gharama nikawastukia kuna mmoja akasema ataifanyia engineering itaendelea kutumika nikaogopa, NIMEPATA MSHAURI HAPA NAKAZIA ILI UNISHAURI POA, ANANIAMBIA MAFUNDI WENGI HUWA HAWAPENDI KUSEMA UKWELI, NI KWAMBA HIZI GARI HUWA ZIKIINGIA ILI ZIDUMU WANABADILISHA STERING RECK NA KUWEKA YA HYDRAURIC NA SIO YA UMEME ILIYOKUWEPO, Nipe weledi ndugu yangu niepukane na vishoka japo wana majina makubwa kwenye garage zao.
Ina kilometa ngapi. kwani kuanzia mwaka 2003 sasa hivi ina umri wa miaka 17, lakini zaidi inategemea imeshetembea umbali gani. Kama bado iko chini ya KM 250,000 utatakiwa utumie 10W-30 tu, ila kama imeshazidi hapo basi unaweza kutumia 10W-40 au SAE40. Usitumie 20W-50 au SAE50 kwenye gari hilo kwa namna yoyote ile iwayo.
Sio mara zote piston ring husababisha gari kukosanguvu katika piston ringi kuna kama shanga za aina tatu kuna moja inahusika na oil amachokwambia fundi kinaweza kuwa na ukweliHabari mkuu Kichuguu m nna ist c.c 1490 ni ya mwaka 2004 kuna kipindi nilifanya service nkaweka oil ya liquilmoly 5w-30 nkaenda moshi-dar kurudi oil ikawa imepungua sana yaan iko chini ya nusu baada ya kwenda kwa fundi akasema gari ina kilometer nyingi akabadil oil akaweka castorl 20w-50 then nkaenda dom-dar kurudi tatizo limejirudia tena oil imepungua sana shida inaweza kuwa nn??
Na je oil niliyitumia ni sahihi?? Nilimuuliza je shida inaweza kuwa piston ring akasema ingekua inatoa moshi na kupoteza nguvu....msaada hapo mkuu
Oil ya mwanzo ya liquimoly ndio iliyokua sahihi hiyo ya 20w50 sio sahihi kwa gari hiyo na hapo kutakuana tatizo kubwa la kiufundi pengine Kuna leakage sehemu ambayo inapitisha oil, kwa gari hiyo oil inayoshauriwa kutumiwa ni 5w30, 10w30 na sio 20w50 hii ni oil nzito SanaHabari mkuu Kichuguu m nna ist c.c 1490 ni ya mwaka 2004 kuna kipindi nilifanya service nkaweka oil ya liquilmoly 5w-30 nkaenda moshi-dar kurudi oil ikawa imepungua sana yaan iko chini ya nusu baada ya kwenda kwa fundi akasema gari ina kilometer nyingi akabadil oil akaweka castorl 20w-50 then nkaenda dom-dar kurudi tatizo limejirudia tena oil imepungua sana shida inaweza kuwa nn??
Na je oil niliyitumia ni sahihi?? Nilimuuliza je shida inaweza kuwa piston ring akasema ingekua inatoa moshi na kupoteza nguvu....msaada hapo mkuu
Mshale wa joto unategemea na aina ya maji unayotumia kama coolant na joto la nje la sehemu ulipo. Tumia coolant ambayo iko recommended (ya kijani au ya machungwa) na usijali umetembea umbali gani kabla mshale haujafika katikaki. Tatizo ni pale tu ambapo joto linapozidi kiwango hicho. Kwa mfano ukiwasha gari ukaliacha kwenye silence kwa muda kabla hujaanza safari unaweza kuanza safari yako wakati joto limeshapanda, lakini hiyo haimaaninishi tatizo lolote kwenye injini yako.Salama Mdau. ndugu nijuze kwa kawaida gari ianatakiwa kufikisha KM ngapi mshale wa joto la njini kuwa kaiwada? maana gari yangu km 3 joto linafika kati kati kwa maana la kaiwada
Unaponunua gari used, sheria kuu ni kufanya service zote kikamilifu. badilisha oil zote, yaani kwenye injini, gearbox an kwenye diff. Halafu badilisha coolant yote. Ila kama gari hiyo inatumia autotransimission unaweza kubadili ATF yote, lakini hapa inahitaji kuwa na mtu anayejua kufanya hivyo kwani ukikosea kubadili ATF basi utapeleka gari hilo kwenye jalalaNaomba kufahamu, ukiingiza used car kutoka japan, ni muhimu kufanya service zp? Na je unaweza kutumia oil ya gear box uliyoikuta na ukabadili ya engine tu?