Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Wataalamu wetu mkishaanza kuleta habari za vyeti vingapi mnamiliki sie akina karume kenge inabidi tukae kimya.

Ishu sio vyeti ni knowledge tu , nilitegemea ungekuja na sababu za kunipinga kwa engine nilizokutajia hapo juu , ambazonni heavy duty na zina maisha marefu tu...
Umeniambia nifanye research-yaani maana yake ni kwamba sijui ninalozungumza, hukuja na comment wala kuuliza swali; halafu jibu langu hapo siyo kukuonyesha vyeti vya shule yangu bali nimesema nina leseni, yaani nimeidhinishwa na mamlaka za kiserikali kuwa nina ujuzi na uzoefu wa kutengeza magari ya watu binafsi. Sikuzungumzia utaalamu kutokana na "vyeti" ninavyomiliki, digrii nilizo nazo hazina uhusiano kabisa na magari kwa taarifa yako, na wala katika thread yote hii sijaingiza swala la taaluma yangu bali ninaongelea uzoefu wangu wa kutengeza magari tu. Kwa hiyo usijaribu kubadilisha topic kuwa ya taaluma

Nikirudi nyuma, katika introduction yangu nilieleza kuwa kuwa niulize chochote kuhusu injini za magari ya petroli; sikusema injini za dizeli au za umeme. Kila swali ninalijibu hapa nikijua linahusu injini za petroli; watu wote walioniuliza maswali yanayohusu injini za dizeli nimewajibu kuwa sina uzoefu nazo, ingawa ninaweza kuwa najua mambo kadhaa kuhusu injini hizo lakini sina uzoefu nazo na hivyo siwezi kutoa authoritative answer.

Usingenifundisha kufanya research, wewe ukauliza tu kuwa mbona kuna injini hizi zina ODD number ya cylinder, ningekujibu kabisa kuwa huenda hizo ni za dizeli au ni chache sana tena huenda ziko designed ama kwa ajili ya matumizi ya safari fupi fupi kama taxi. Nimeshashughulika na magari ya petroli kwa takribani miaka kumi na sita sasa na wala sijawahi ona gari ndogo yenye odd number ya cylinder; zilijaribiwa zamani lakini zikasitishwa.

Ziliopo chache ni mahsusi kwa magari maalum yasiyotegemewa kufanya safari ndefu za spidi kubwa kama zile zinazotengezwa maalumu kwa makampuni ya taxi. Hiyo ya huyo aliyeuliza swali hilo huenda ilikuwa kwa ajili ya taxi za Japan.
 
Inaezekana nilipokwambia ukafanye homework nilikukwaza !! Nisamehe bure kwa Hilo

Lakini bado kuna engine kibao za petrol , na cylinder 5 audi ,volvo etc na hizi zipo toka miaka mingi ya nyuma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaezekana nilipokwambia ukafanye homework nilikukwaza !! Nisamehe bure kwa Hilo

Lakini bado kuna engine kibao za petrol , na cylinder 5 audi ,volvo etc na hizi zipo toka miaka mingi ya nyuma

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni swala la communication skills; sijasema kuwa 5 cylinder hazipo, zilijaribiwa miaka ya nyuma lakini nyingi zikaondolewa zikabaki kwa ajili ya market ya Taxi na matumizi yasiyokuwa ya safari ndefu tu. Hizo unazosema wewe ambazo nyingi ziko Europe nina imani ni hizo za market ya makampuni ya Taxi na kwa safari fupi fupi kwa vile Europe hawatumii magari sana kwa usafiri wa mbali.
 
Mkuu Kichuguu asante sana kwa uzi huu.

Nina Nissan X-Trail ya mwaka 2002, nliinunua kwa mzee mmoja hivi. Ni namba B ila kiukweli mzee aliitunza vizuri sana. Sasa nlipoichukua nadhani nlii-abuse(maji ya Dawassa n.k), nikaitumia kama miezi mitatu ikaanza kuchemsha, nikaipeleka kwa washkaji wa uchochoroni wakaichokonoa mara kadhaa mpaka nlipojua nimeua injini...
Badili iyo throttle maana inaendeshwa na umeme

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni swala la communication skills; sijasema kuwa 5 cylinder hazipo, zilijaribiwa miaka ya nyuma lakini nyingi zikaondolewa zikabaki kwa ajili ya market ya Taxi na matumizi yasiyokuwa ya safari ndefu tu. Hizo unazosema wewe ambazo nyingi ziko Europe nina imani ni hizo za market ya makampuni ya Taxi na kwa safari fupi fupi kwa vile Europe hawatumii magari sana kwa usafiri wa mbali.
Naomba nisaidieni, gari yangu aina ya Toyota spacio old model, nimeipeleka car wash wakaiosha na engine pia baada ya pale imegoma kuwaka msaada tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba nisaidieni, gari yangu aina ya Toyota spacio old model, nimeipeleka car wash wakaiosha na engine pia baada ya pale imegoma kuwaka msaada tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
Iache ikauke; kama wameosha injini kwa maji basi inawezekana kuna maji yanakatisha njia za umeme unaonedesha gari. Acha maji hayo yakauke ndipo ujaribu tena; waambie wapulize injini nzima kwa upepo wa compressor kuondoa maji hayo.
 
Naomba nisaidieni, gari yangu aina ya Toyota spacio old model, nimeipeleka car wash wakaiosha na engine pia baada ya pale imegoma kuwaka msaada tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi hua mnaosha engine ili mpate nini mkuu?

Mimi nakaaga na gari tangu nainunua mpk naiuza sijawahi kuiosha engina hata siku 1 na sijawahi kupata tatizo lolote lile.
 
Hivi hua mnaosha engine ili mpate nini mkuu?

Mimi nakaaga na gari tangu nainunua mpk naiuza sijawahi kuiosha engina hata siku 1 na sijawahi kupata tatizo lolote lile.

Ni muhimu kusafisha injini yako mara kwa mara. Vumbi lina chemical inayoitwa silica ambayo huweza kuingiliana na njia za umeme wa gari lako na kulifanya lishindwe kufanya kazi zake sawasawa
 
Ni muhimu kusafisha injini yako mara kwa mara. Vumbi lina chemical inayoitwa silica ambayo huweza kuingiliana na njia za umeme wa gari lako na kulifanya lishindwe kufanya kazi zake sawasawa
So far nimeshaona hasara za kuiosha engine kuliko faida zake,zaidi ya kuipiga upepo engine siruhusu kitu kingine pale cha kuoshea(i.e maji/diesel/petrol).
 
So far nimeshaona hasara za kuiosha engine kuliko faida zake,zaidi ya kuipiga upepo engine siruhusu kitu kingine pale cha kuoshea(i.e maji/diesel/petrol).
"Kusafisha" injini haina maana ya "kuosha" injini: labda hukuinelewa. Hata hivyo kuna utaratibu mzuri sana wa kuosha injini, tafuta wataalamu wa detailing watakuambia namna ya kufanya hivo.
 
"Kusafisha" injini haina maana ya "kuosha" injini: labda hukuinelewa. Hata hivyo kuna utaratibu mzuri sana wa kuosha injini, tafuta wataalamu wa detailing watakuambia namna ya kufanya hivo.
Kiongozi mimi napiga upepo tu,hakuna kitu kingine kitagusa engine yangu sio steam cleaning/Pressure washing etc
 
"Kusafisha" injini haina maana ya "kuosha" injini: labda hukuinelewa. Hata hivyo kuna utaratibu mzuri sana wa kuosha injini, tafuta wataalamu wa detailing watakuambia namna ya kufanya hivo.
Mkuu kama kuna maujuzi ya jinsi ya kusafisha injini na sehemu zake zote hebu tuelekeze hapa maana maji ni shida sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kama kuna maujuzi ya jinsi ya kusafisha injini na sehemu zake zote hebu tuelekeze hapa maana maji ni shida sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Kusafisha injini ni process ndefu kidogo; inachukua karibu saa tatu hivi. Hii hufanyika zaidi pale mtu anapotaka kuuza gari lake. Ila kwa matumizi ya kawaida, safisha injini yako kwa kutumia upepo wa compressor tu.
 
Kusafisha injini ni process ndefu kidogo; inachukua karibu saa tatu hivi. Hii hufanyika zaidi pale mtu anapotaka kuuza gari lake. Ila kwa matumizi ya kawaida, safisha injini yako kwa kutumia upepo wa compressor tu.
kuna video za youtube za jamaa anajiita chrisfix. Jamaa anajitahidi kuelekeza
 
Mkuu Kichuguu na wadau wote.

Nin shida ya odometer kusoma speed kubwa ukiwa speed ndogo, yaani unaweza gundua upo speed 80km/hr ila itasoma 100km/hr.

Pia inakuwa haina nguvu kama awali na haibadili gear vizuri, muda mwingine Inabaki gear namba 3 hata ukanyage vipi.

Mlimani pia haina nguvu na haibadili gear kama kawaida.

Gari ni Rav4 kilitime.

Msaada jamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Kichuguu na wadau wote.

Nin shida ya odometer kusoma speed kubwa ukiwa speed ndogo, yaani unaweza gundua upo speed 80km/hr ila itasoma 100km/hr..

Sent using Jamii Forums mobile app
Labda umeweka matairi madogo kuliko saizi yake, au matairi yako hayana upepo wa kutosha.Kuhusu injini kukosa nguvu, inaweza kutokana na sababu mbili kubwa;
(1) Gearbox yako haina mafuta (ATF) ya kutosha au yashachafuta sana na filter imeanza kuziba.

(2) Fuel pump imechoka haipeleki mafuta ya kutosha kwenye injini

Baada ya hizo mbili kubwa nyingine ndogo ndogo ni pamoja na air filter kuwa chafu, fuel pressure regulator kuchoka, fuel filter (kama inayo- magari mengi ya kisasa fuel filter imejengewa kweye fuel pressure regulator) kuziba.

Senors mojawapo kutofanya kazi sawasawa (Air flow sensor, throttle position sensor kutofanya kazi sawasawa, Manifold temperature sensor kutofanya kazi sawasawa, na nyinginezo; Injini za siku hizi zina sensor nyingi tu. Ila kabla ya kuanza kuhangaika na hizo sensor, angalia hizo kuu mbili nilizotaja hapo juu, labda na Air filter
 
5W40 ni nzito kuliko 5w30; kwa hiyo inapopenya kwenye sehemu ambazo inatakiwa ilainishe inabananisha zaidi vyuma husika badala ya kuvilaninish, na hivyo kuweka stress (mzigo mkubwa sana kwenye injini yako), jambo ambalo litaua sehemu nyingine za injini kutokana na kuelemewa na mzigo. Fikiria kama unatembea kwenye bwawa leye matope, utapita kwa urahisi katika bwawa ambalo tope lake ni laini kuliko bwawa ambalo tope lake ni kama udongo wa mfinyanzi.
Kichuguu gari yangu imetembea km 186000 oil gani nzuri Mimi nilitumia s40 je nataka nibadilishe
 
Miaka siyo kigezo cha uchakavu wa gari coz ndani ya miaka nane magari mawili tofauti yanaweza yakawa yametembea km tofauti kabisa
Nimezungumzia matumizi ya kawaida ya gari kufuatia viwango vinavyokubalika na makampuni ya Bima. Kama gari haituimiki kabisa, yaani iko ndani siku zote, au au kama inakuwa abused sana hiyo ni kesi nyingine kabisa;

kwa kawaid gari inayotumiwa vizuri kila siku, baada ya miaka minane itakuwa imetembea kiasi cha km 130,000 hivi, lakini kama inakuwa abused sana si ajabu kuikuta na zaidi ya km 200,000, na ile inayotunzwa kama yai la kwanza itnaweza kuwa na km 40,000 tu. Nikizungumzia miaka, ninakuwa nafuata matumzi ya kawaida.
 
Back
Top Bottom