Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Ukiwasha gari asubuh silencer haikai inazima mpaka uwashe mara 2 au mara 3, halafu ukitembea baada ya muda inawasha check engine...sema check engine kuna siku inawaka na siku nyingine haiwak kabisa aua inawaka na kupotea...ila mpaka uendeshe gari kwa muda flan hiv
Peleka gari ichekiwa kwa computer kabla hujalipia matengezo. Sehemu kubwa ya tatizo lako ni sensor fulani inaitwa MAF (Manifold Air Flow) imekufa; kama hiyo ni nzima basi manifold air pressure (MAP) sensor inaweza kuwa imekufa. Sehemu kubwa ya matatizo yako inaelekea kuwa injini haipati hewa ya kutosha wakati unaanza.

Vitu vingine ambavyo mimi sivipi uzito sana ni pamoja na betri kuwa haina nguvu ya kutosha au gari kuwa na oil iliyochoka au nzito sana (hili linawezekana sana Tanzania kwa vile watu wengi wanatumia SAE40 na SAE50 kwenye injini ndogo). Check betri yako na oil kabla ya kupeleka gari kwenye computer scan. kama gari yako ina geji ya betri na geji ya oil basi unategemea kuwa unaona geji hizo zikisoma zaid ya nusu.
 
Peleka gari ichekiwa kwa computer kabla hujalipia matengezo. Sehemu kubwa ya tatizo lako ni sensor fulani inaitwa MAF (Manifold Air Flow) imekufa; kama hiyo ni nzima basi manifold air pressure (MAP) sensor inaweza kuwa imekufa. Sehemu kubwa ya matatizo yako inaelekea kuwa injini haipati hewa ya kutosha wakati unaanza. Vitu vingine ambavyo mimi sivipi uzito sana ni pamoja na betri kuwa haina nguvu ya kutosha au gari kuwa na oil iliyochoka au nzito sana (hili linawezekana sana Tanzania kwa vile watu wengi wanatumia SAE40 na SAE50 kwenye injini ndogo). Check betri yako na oil kabla ya kupeleka gari kwenye computer scan. kama gari yako ina geji ya betri na geji ya oil basi unategemea kuwa unaona geji hizo zikisoma zaid ya nusu.

computer scan ndo ilinipa error ya SYSTEM TOO LEAN
 
computer scan ndo ilinipa error ya SYSTEM TOO LEAN
Badilisha Air flow sensor na air pressure sensor; kuna magari mengine yana air flow sensor tu na kuna magari yana air flow sensor na air pressure sensor kwa pamoja. Angalia gari lako vizuri.

Ngoja nikueleze, ni kuwa mojawapo ya sensor hizo zinadanganya computer ya gari kuwa kuna hewa ya kutosha kumbe zinapeleka ama hewa nyingi sana kupita kiasi kwenye injini au kidogo kuliko mahitaji ya injini.

Sasa mafuta huungua tu iwapo kuna uwiano fulani wa mafuta na hewa; hewa ikiwa nyingi sana mafuta hayaungui na vile vile hewa ikiwa kidogo sana hayaungui vizuri na husababisha injini kutikisika kwa nguvu kufanya vibration sensors za injini kuzima computer na injini yote na gari kuzimika.

Hii ya hewa kuwa kidogo husababisha injini isiwake tena kwa muda fulani, wakati ile ya hewa nyingi unaweza kujaribu mara kadhaa kuanzisha injini. Madereva wengine wanakuwa wanapiga ufunguo na kuchezesha accelerator ili kubalance mafuta na hewa, lakini magari ya kisasa yanatumia computer kufanya hivyo, kwa hiyo hata ukipiga pedal la accelerator haliwezi kuweka tofauti yoyote
 
Badilisha Air flow sensor na air pressure sensor; kuna magari mengine yana air flow sensor tu na kuna magari yana air flow sensor na air pressure sensor kwa pamoja. Angalia gari lako vizuri...

Asante sana mkuu kwa ushauri.....gari ni VITS RS ENGINE 1Nz. Sasa cjui itakua na sensor zote hizo ulizotaja hapo juu au vp
 
Asante sana mkuu kwa ushauri.....gari ni VITS RS ENGINE 1Nz. Sasa cjui itakua na sensor zote hizo ulizotaja hapo juu au vp
Tatizo ni kuwa magari mengi yaliyoko Tanzania hayapo hapa nilipo, kwa hiyo mpaka nitafute model ya kimarekani inayofanana na gari lako. Nipe muda hadi kesho.
 
Tatizo ni kuwa magari mengi yaliyoko Tanzania hayapo hapa nilipo, kwa hiyo mpaka nitafute model ya kimarekani inayofanana na gari lako. Nipe muda hadi kesho.

Asante sana mkuu...ila engine kutikisika inatikisika kwel mkuu tena sana na ukiwasha a.c ndo kabisa
 
Mkuu pole na majukum , inawezekana ushatolea ufafanuzi lakin naomba ikikupendeza nisadie pia, Nimeagiza gari haina ya Nissan dualis inatumia engine MR20 naomba kujua oil gani inafaa kwa haina hii ya engine au ikikupendeza naomba uchambuzi kidogo wa gari hii ?
225063_image06%20(1).jpg
 
Asante sana mkuu...ila engine kutikisika inatikisika kwel mkuu tena sana na ukiwasha a.c ndo kabisa
Niambie model ya Injini yake; hapa USA kuna gari ilizwa kama Toyota Echo kati ya mwaka 2000 na 2005 hivi, na hiyo ilikuwa Mass Air Flow (MAF) sensor tu
 
Mkuu pole na majukum , inawezekana ushatolea ufafanuzi lakin naomba ikikupendeza nisadie pia, Nimeagiza gari haina ya Nissan dualis inatumia engine MR20 naomba kujua oil gani inafaa kwa haina hii ya engine au ikikupendeza naomba uchambuzi kidogo wa gari hii ?View attachment 1462130
Hii ni kati ya magari ambyo nimeshatolea majibu yake; kuna mwanachama mmoja hapa anaitwa kingjohn255 anauza oil Dar na anazijua vizuri oil za magari; wasiliana naye atakusaidia. Unatakiwa kutumia ama 5W-30 au 10W-30 na usiweke oil yoyote yenye namba 40 au zaidi ndani yake. Utafaidi sana gari lako kwwa muda mrefu sana.
 
Thanks mkuu.
Kusafisha injini ni process ndefu kidogo; inachukua karibu saa tatu hivi. Hii hufanyika zaidi pale mtu anapotaka kuuza gari lake. Ila kwa matumizi ya kawaida, safisha injini yako kwa kutumia upepo wa compressor tu.
 
Hii ni kati ya magari ambyo nimeshatolea majibu yake; kuna mwanachams mmoja anaitwa kingjohn hapa anauza oil Dar na anazijua vizuri za magri; wasiliana naye atakusaidia. Unatakiwa kutumia ama 5W-30 au 10-W30 na usiwekr oil yoyote yenye namba 40 au zaidi ndani yake. Utafaidi sana gari lako.
Ahsante sana mkuu
 
Rudi kwenye oil yake- tumia 10W-30 au SAE30 kama inapatikana, tena utashangaa injini yako itakavyotulia. Bado hujachelewa sana
Mkuu natumia SAE 5w-30 full synthetic-Atlantic kwenye 2NZ engine. Je ni oil sahihi? Alafu napaswa kubadili baada ya kilometer ngapi? Maana fundi aliniambia niwe nabadili after every 5000km. Odometer inasoma 70,900km.
 
Mkuu natumia SAE 5w-30 full synthetic-Atlantic kwenye 2NZ engine. Je ni oil sahihi? Alafu napaswa kubadili baada ya kilometer ngapi? Maana fundi aliniambia niwe nabadili after every 5000km. Odometer inasoma 70,900km.
Hiyo 5W-30 ni oil sahihi kabisa, ila itategemea unaendesha muda gani kabla ya gari kusimama. Kama uneendesha jijini tu unaweza kubadilisha baada ya kuanzia km 5,000 mpaka 8,000 kama unatumia oil ya hali ya juu na filter yako ni nzuri. Kuna magari huwa tunabadilisha ouli baada ya kama km 13,000; ila sasa inategemea na oil unayotumia na filter yake. Kama gari lako linapiga ruti ndefu tu, unaweza kubadilisha oili baada ya km13,000. (Of course kutegema kuwa una filter nzuri, na vile vile unatumia oil nzuri)
 
Nashukuru mkuu. Natumia jijini tu so nitakuwa nabadili after 5000 ili kuipa injini maisha marefu. Naomba pia kujua nitumie gearbox oil ya aina gani kwa gari hiyo. Maana sijawahi ibadili tangu gari iingie nchini mwez january thou nikiiangalia deep stick naona oil iko vzuri tatizo sijui aliekuwa anaitumia aliibadili lini so nataka niibadili niwe na uhakika zaidi.
Hiyo 5W-30 ni oil sahihi kabisa, ila itategemea unaendesha muda gani kabla ya gari kusimama. Kama uneendesha jijini tu unaweza kubadilisha baada ya kuanzia km 5,000 mpaka 8,000 kama unatumia oil ya hali ya juu na filter yako ni nzuri. Kuna magari huwa tunabadilisha ouli baada ya kama km 13,000; ila sasa inategemea na oil unayotumia na filter yake. Kama gari lako linapiga ruti ndefu tu, unaweza kubadilisha oili baada ya km13,000. (Of course kutegema kuwa una filter nzuri, na vile vile unatumia oil nzuri)
 
Nashukuru mkuu. Natumia jijini tu so nitakuwa nabadili after 5000 ili kuipa injini maisha marefu. Naomba pia kujua nitumie gearbox oil ya aina gani kwa gari hiyo. Maana sijawahi ibadili tangu gari iingie nchini mwez january thou nikiiangalia deep stick naona oil iko vzuri tatizo sijui aliekuwa anaitumia aliibadili lini so nataka niibadili niwe na uhakika zaidi.
Kama ni gearbox ya mkono tumia 80w-90 ila gearbox automatic lazima usome kitabu cha gari; ATF hjazifanani hata kwa gari za aina moja..
 
hahah!
Kichuguu sasa ndugu yangu aliyekuambia gari zetu za mjapan zinakujga na vitabu nani?
Hata kama huna kitabu, kwa Tanzania wewe tumia 10W-30; hutakuwa matatizoni hata siku moja, ingawa Makambako bado nitawashauri wafikirie5W-30. Usiingine kwenye oil yenye namba ya 40 au zaidi
 
TOYOTA ATF TYPE-IV kaa humo
Nashukuru mkuu. Natumia jijini tu so nitakuwa nabadili after 5000 ili kuipa injini maisha marefu. Naomba pia kujua nitumie gearbox oil ya aina gani kwa gari hiyo. Maana sijawahi ibadili tangu gari iingie nchini mwez january thou nikiiangalia deep stick naona oil iko vzuri tatizo sijui aliekuwa anaitumia aliibadili lini so nataka niibadili niwe na uhakika zaidi.
 
Back
Top Bottom