chofachogenda
Senior Member
- Oct 6, 2016
- 107
- 199
Ebwana mwenye nyimbo yoyote ya eleven stars
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Asha nambie kweli ni wimbo wa Jagwa Music chini Simba baba J ambaye alikuja kufia jela,wakati huo dogo Jack hajulikani bado yupo kwao Mwembesongo kule Moro towm.Na hiyo nyingine inaitwa "Kondakta" (Marumbano na zogo kubwa katika basi lile,kati Kondakta na bwana mgambo yule),nyimbo hii wenyewe ni bendi inayoitwa CHAUKUCHA FAMILY(watoto wadogo waliokomaa vichwa) kutoka Mwananyamala kwa Kopa.Humo kuna watu kama akina Aigosh ambao ni maprofesheno waliojitoa Jagwa baada ya kurumbana.Ashaaaa niambie ukweli kama hunitaki usinitapeli... ilikua balaaa
kondakta kaja juu akasema haiwezekani kupanda bure imeruhusiwa jeshi la polisi..
mnanda [emoji119][emoji119][emoji119] sema tu hawauelewi
Btw Asha imeimbwa na jack simela au
hatari mkuu..kuna mtu pia alikuwa anaitwa ali tasha aka tasha boyKamongo Manjalino,huni ni miongoni mwa maprofesheno wa Jagwa Music,yeye alikua anagusa kinanda(njia).
mkuu kumbe baba j kafia jela.. ilikuwaje mkuu?Asha nambie kweli ni wimbo wa Jagwa Music chini Simba baba J ambaye alikuja kufia jela,wakati huo dogo Jack hajulikani bado yupo kwao Mwembesongo kule Moro towm.Na hiyo nyingine inaitwa "Kondakta" (Marumbano na zogo kubwa katika basi lile,kati Kondakta na bwana mgambo yule),nyimbo hii wenyewe ni bendi inayoitwa CHAUKUCHA FAMILY(watoto wadogo waliokomaa vichwa) kutoka Mwananyamala kwa Kopa.Humo kuna watu kama akina Aigosh ambao ni maprofesheno waliojitoa Jagwa baada ya kurumbana.
Nashukuru mkuuHizo ni zama za chakacha,za bendi kama Dar nyota,Night Star ya akina Haidary Kessy na nyinginezo.Hizi hupatikanaji wake umekua ni watabu sana,lakini wacha nikupekulie maabara.
Yaah,nyakati hizo ndio Jagwa wamepamba moto kuurudisha mziki wao wa mnanda ambao tayari ulishatekwa na watoto wa Temeke kama akina,Omary Omary(Atomic),Chuna(Kombora)IssaKiyange(Buti kubwa/Uraibu),Mwina(Miami Beach)na Matajiri watoto (Seven Survivor).hatari mkuu..kuna mtu pia alikuwa anaitwa ali tasha aka tasha boy
Unajua wadau waliokua wanajihusisha na mziki wa mnanda/mchriki wengi walikua ni watoto wa uswahilini wenye maisha ya kihuni.Kwahiyo kwao jela ingia toka ni kawaida tu,so tilipu ya mwisho yalimbana maradhi hukohuko jela na ukampata umauti.mkuu kumbe baba j kafia jela.. ilikuwaje mkuu?
Embu niwekee hapo mdau nikusikilize nautafuta sana siupatiBendi ni Jagwa na muimbaji ni Jack Simela.
Mziki una ushabiki kama unavyoona timu za mpira,hao uliowataja wote ni mafundi na kila mmoja ana radha na mashabiki wake hivyo kwenye kuamua nani mkali kila mtu ana sababu zake.Kwa upande wangu mm Juma Mpogo au General Lupozi anajua ingawa wote nawapenda.nani mkali kati ya omary omary, baba j na generali juma mpogo???
Poa mdauNirushie namba zako DM nikutumie kwa what's up.
ni kweli mkuu..ila wote ni marehemu kwa sasa na wameondoka na mchiriku ndio kwisha habari yake!Mziki una ushabiki kama unavyoona timu za mpira,hao uliowataja wote ni mafundi na kila mmoja ana radha na mashabiki wake hivyo kwenye kuamua nani mkali kila mtu ana sababu zake.Kwa upande wangu mm Juma Mpogo au General Lupozi anajua ingawa wote nawapenda.