New ID l
JF-Expert Member
- Apr 3, 2017
- 248
- 480
- Thread starter
- #261
ThanksTooth Brush ukiweka part 4 iendeleze hukuhuku usifungulie thread nyingine,ni ushaur tyu!!
aibo,aibo,aibo hahahahahaha....
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
ThanksTooth Brush ukiweka part 4 iendeleze hukuhuku usifungulie thread nyingine,ni ushaur tyu!!
aibo,aibo,aibo hahahahahaha....
Amiin!!Umetumia busara sana rafiki , mungu akubaliki.
Iko wapi[HASHTAG]#part[/HASHTAG] 3 IPO UBAONI guys!
Mkuuu mbn part four haikuj?Dah!...hakika nilivulugwa sana2,
taratibu..niliokota begi langu...
nikimtazama yule mkaka tuliyekutana nae pale nchini Zambia..nikamuona kwa mbali
anajifanya yuko busy na simu yake...,
Nikatazama yale mazingila..
nikagundua kuna kamchezo kamechezeka........*
Sasa tuendelee................¥
Nilipoona kuwa yule B'mkubwa
anaanza kutekwa akili na yule brother...ya kutotaka nisikiliza,
palepale *mizimu* ya babu yangu kijijini yalinipanda kichwani.....hahaha....lol,
Nilimfuata kwa kasi ya ajabu yule B'mkubwa, na kumshika mkono kwanguvu...then
nikamchana makavu live..!
Nikamwambia...,
B'mkubwa skiliza bhana,
huyu bro' yeye ndio aliyenipanga mimi kuja huku South Africa..na wala haikuwa dhamira yangu mimi kuja huku,
ispokuwa ni yeye ndio aliyenishawishi kuja hapa
South Africa......Sasa nashangaa kwa yeye kunigeuka hapa nchini!.....kwa nini???
Istoshe..." alinidhihirishia kwenye simu yake yakwamba,,
tukifika hapa wewe B'mkubwa ndiye utakae tupokea....,
Sasa nashangaa tena baada ya kukuona wewe tu" ananikataa,
na mimi hapa nchini...sina ndugu wala rafiki hata jamaa pia sina ataniachaje kwenye mazingila km haya....???.
Muda wote huo.....,,,
Yule brother, anamsisitiza B'mkubwa aachane na mimi watimke.....na yule mkaka nikamuona kama anampa signal huyu brother,, yakwamba aendelee kunikataa...kwakweli nikafahamu tu' kuwa walisha kula njama ya kunitelekeza..ili yule mkaka apate kuniibia vitu vyangu then aniache kwenye mataa.
Dah!...yule B'mkubwa baada ya kuyasikia yale..."
Akaniuliza: sasa tutafanyaje..?
Nakumbuka ile mizigo ilishaingizwa ndani ya gari *Taxi*
BaC' alipouliza lile swali...kwa upande wangu' nilimjibu swali lake huku nafungua mlango wa ile *Taxi*...na kusema:
b'mkubwa' wewe twende nyumbani kwanza tutakwenda kujua hukohuko tukishafika!
B'mkubwa na yule kijana wake
*brother* walivuta pumzi, maana hawakujuwa wafanye nini...na mimi tayali nimeshaingia ndani ya ile *Taxi*
Kisha wote wawili waliingia ndani ya ile *Taxi* ingawa yule brother alikuwa na hasira kweli.
Ndani ya ile *Tax* nilimkuta mdada flani ni *mtanzania*pia
alikuwa ameketi siti ya mbele,
akiwemo na dereva wa ile Tax*
Lakini..katika tukio lote lililotokea pale, yule mdada wala hakutoka nje ya ile *Taxi* nafikili maamuzi yake yalifikia hapo maybe.......!
BaC'....mimi, yule brother na B'mkubwa sote watatu tuliketi siti za nyuma, siti za mbele' alikuwepo dereva na yule mdada.
Huyu mdada...nafikili alikuwa ni mtoto wa hiyari wa yule B'mkubwa... __not sure!
Hivyo' niliketi katikati mwa ile siti
ya nyuma, kuliani kwangu..aliketi
B'mkubwa, kushotoni kwangu aliketi yule brother....huku kushoto..ndio upande aliosimama yule mkaka tuliyekutana nae pale Zambia,
hivyo" nilishindwa kumkodolea macho yule mkaka, kwa kumuhofia huyu adui yangu *brother* aliyeketi huku kushotoni kwangu.
Kwakuwa macho hayana pazia, nilipepesa macho kidogo kumcheck yule mkaka *Zambia*
live...nilimuona akijilaumu yeye mwanyewe huku ameiweka mikono yake miwili kichwani kwake, kwa kuona kuwa lengo lake limefeli... *maybe*.
Baada ya sisi sote wa tano..
namaanisha mimi, yule bro,
b'mkubwa, yule mdada na dereva, kukamilika ndani ya ile
Taxi..gari iliwashwa' tayari kwa kuiyanza safari ya kuelekea home............
Nakumbuka...yule brother, baada ya kuona kuwa nimemzidi nguvu katika lile tukio,
ndani ya ile *Taxi* hakupata tena
nguvu au chance ya kuzungumza lolote, hivyo' alikaa kimya......
Wakati gari yetu inaendelea kukata mataa ndani ya jiji la Johannesburg...,B'mkubwa akasema: kumwambia yule mdada wa mbele.....
Wee *fulani*, ebu mchukue huyu kijana na uende nae huko nyumbani kwako!
Akaendelea kwa kusema:
ni rafiki wa huyu kijana wangu" wala hana tabu yoyote huyu!
Yule B'mkubwa, kumbe haishi kwenye ule mji *Johannesburg*
Bali anaishi kwenye mji mwengine uitwao *Swaziland*
{ si mahalapake kuuelezea huu mji...kumradhi *wajuaji* } jxt jok.
Yule mdada akaitikia: sawa haina shida!
Na safari iliendelea mpaka kwenye stand ya gari za kuelekea huko Swaziland etC!
Wao wawili yule brother na B'mkubwa, wakateremka na kuondoka huko *Swaziland*
Mimi na yule mdada, tukaelekea kwenye soko la palepale centre..
tulipofika pale sokoni, tukaachana na ile *Taxi*...na kutafuta vitu husika *spice etC*
Kusema kweli yule mdada, kwa namna moja ama nyengine alikuwa anatisha kimtindo..haha lol....
Sasa akawa ananiambia...:
Uwe makini huku mdogo wangu,
vinginevyo watakutoboa macho muda wowote !umesikia?
Duh!...Nikamuitikia:
Ndio *dada komando* hahaha..
JUST JOKE..
Kwakweli niliogopa sana kutokana na yale maneno yake
ya kwamba niwe makini...
Kwani hata mimi mwenyewe nikiyatizama tu' yale mazingila na history ya lifestyle yao, nikajua tu' kuwa hapa natakiwa niwe makini.
Pia alinisisitiza nifanye hivyo kwani hata yeye anatembea na pilipili iliopo kwenye kichupa kidogo cha plastic *spray*
Wahenga mutanisaidia kinaitwaje hicho kichupa ( ?!? )
Anasema hiyo pilipili ndio km silaha yake.
Aaah! nikajipa moyo, na kusema mimi baalia bhana...
Pia kwa kiasi flani stress za kufikilia nita lala wapi, zilipungua.
Hadi kwenye mishale ya saa
12 :30- 50 ya jioni tulitimba nyumbani kwa yule mdada..
Wala hapakuwa mbali na lile soko......
Kufika...nikawakuta *wabongo*
kama 7 iv' wameketi wakigonga mkojo wa shetani...hahaha....
samahani, walikuwa wanagonga
Bia....nikawapa Hi'
walifulahi kuniona japo wengine walinilaumu...eti kwanini nimekuja South.A. nalhali wao wanataka kuludi Bongo...
na kusema eti South.A. hakuna issue.......< wakatishaji tamaa >
kila kona [HASHTAG]#wapo[/HASHTAG]...jamani!
Nashukulu....walinipokea kwa bashasha pale,...ndani ya dakika kama 5...nikaletewa mpunga wa maana juu yake zilisheni mipaja ya kuku aisee
hadi nikaona noma kula.....
Nakumbuka nilikula kidogo tu'
si unajua tena uso umeumbwa na *HAYA*...!
Ndugu yangu ukijiona wewe huna *HAYA* basi wewe ni
[HASHTAG]#mfu[/HASHTAG]!......sorry.
Ikumbukwe kuwa..huyu mdada anamiliki restaurant *mgahawa*
hapa nilipofikia, na hata makazi yake huyu mdada, yako hapahapa mjengoni.....
Alichokifanya huyu mdada, ni kuongea na yule mmiliki wa ule mjengo...yakwamba ile sehemu ya parking...ndio afanyie biashala yake hiyo ya Restaurant.....
Pia ifahamike mmiliki wa ule mjengo ni *mzawa*.
BaC' baada ya masaa kadhaa kupita, hatimae wale wabongo wengine walisepa makwao...
hata nikabaki mimi na yule mdada pamoja na some guys wanaoishi mulemule mjengoni
akiwemo na dogo flani ni
*mtanzania* pia. Huyu dogo'
ni mfanya kazi wa yule mdada.
Baada ya kumaliza kazi zake yule dogo, akanifuata pale nilipoketi mimi...then akaniuliza maswali machache kuhusu Tz^
etC.......
Kwakweli aliweza kuonesha upendo juu yangu na hata uwepo wangu pia.
Kwakuwa maisha ya South .A.
ni maisha ya kibahalia...
alafu hatujuani, wala hawakuona shida kunilaza palepale kwenye sofa la kukalia customers *wateja*....
Na mimi wala sijamind bali nilichukulia poa2 na kuona kuwa msaada ule ni mzuri, kuliko kulala nje kabisa...
Kwakuwa ile sehemu ilikuwa na geti kubwa imala...njozi zilikuwa si mbaya sana.
WAHENGA" pale niliposema kuwa: walinilaza kwenye sofa..
MUSITAFSIRI TOFAUTI...hah
Asubuhi kulipokucha...alfajir"
yule dogo alishuka kutoka juu..
coZ' wao wanalala juu *ghorofani* na mgahawa upo kwa chini..sO' aliharakisha kila kinacho husika mahala pale..
Nami nikatoa shukrani zangu kwa kumsaidia zile kazi nilizoziweza...pia ilikuwa ni sehemu yangu ya kujipendekeza kwao, na nilihakikisha nafanya juu chini
ili nijiaminishe kwao...
Na hakika nilifanya hivyo!
Ilipotimu saa 7 :40 - 8 am...
kilakitu kilikuwa byee...na wateja nao walianza kutia maguu...
For sure..uwepo wangu ulileta tija kiasi flani, hata yule mdada alipokuja na yeye, aliona kuwa kuna umuhimu wa mimi kuwepo pale....ingawa hawakuniamini kwa %.kwani wapemba hujuana kwa virema bhana..hahaha...
Hatimae office ilipofungwa km mas'hara iv' nikalipwa Rand 30.
Na kuahidiwa kuwa nitakuwa msaidizi wa pale mgahawani..
Japo haikuwa pesa nyingi niliyolipwa..lkn niliona kuwa ule ni mwanzo wa kupata kingi zaidi.
Kama kawaida yangu mzee!
niliupiga usingizi palepale kwenye sofa la customers,
Ndani ya wiki moja tayari..nilishaanza kuzoeleka pale mgahawani....Na kazi zilienda vyema2.....
Ingawa geto langu, kitanda changu ilikuwa ni palepe kwa siku zote.
Wiki iliyofuata nilitembezwa kwenye baadhi ya mitaa ya palepale town na yule dogo.
Ifahamike kuwa...hapo nilipofikia, palikuwa ni centre
Kama vile K\ KOO au POSTA
*Tanzania*
Ndani ya wiki hii ya pili...
Nilimwambia yule mdada kuwa anifanyie mchakato wa passport yangu ikagongwe *Visa* kwani visa yangu..ilisha expire..ilikuwa ni ya 7 days...Sikumwambia lolote juu ya dhamira yangu kuhusu harakati zangu za kutaka kusonga mbele zaidi.
Akasema: poa...ila wanagonga na pesa ukiwa hapahapa home
Otherwise...uende mwenyewe border....
Nikamuuliza: ni njia ipi ambayo ni rahisi kati ya hizo mbili?
yaani...kutoa pesa au kwenda border...?
Akanijibu: ni heri ukatoa pesa tu,
kwani itakugharimu kiasi cha Rand 500! kuliko kwenda border alafu wewe ni mgeni!
Kwakuwa na mimi sikukaa kizembe, nikachomoa Rand 500
kisha nikampa yule mdada,
Lakini..akaniuliza:
Kwanini unataka kuharibu pesa zako nalhali sisi wenzako wote tunaishi tu bila hata ya kutumia hizo passport ??
Akaendelea kwa kusema:
wenzako huwa tunagonga tukitaka kurudi *Bongo*
So' wewe achana nayo tu!
Kwakuwa mimi nilikuwa na malengo yangu kichwani,
nikamsihi afanye vile ninavyotaka....
Kwakweli ilimstua ile hali ya mimi kung'ang'ania kugongewa ile passport...ilimbidi tu afanye hivyo..kwa kuwa haikuwa pesa yake bali ni pesa zangu!
Kesho yake..yule mdada akampigia simu jamaa flani anayeishi jiji la *Pretolia...
Huyu jamaa..inasadikika yeye mishe zake ni za kuvuka border mara kwa mara, hivyo' hubeba na passports za watu wengine kwaajili ya kuwagongea *Visa*
kwa malipo!.
Ilichukuwa kama siku tatu ndipo yule jamaa wa *pretolia* akaja.
Alipofika, alikabidhiwa ile passport na pesa..kisha akatimka zake....
Na maisha yaliendelea.....
Zilipita km wiki 2 pasina kumuona yule jamaa *Pretolia*
na nakumbuka aliahidi kuileta ndani ya siku 3..tangu alipoichukuwa ile passport.
Nikamuuliza yule mdada.... kuhusu ma passport...
Akasema: subili ataileta kesho kwani nimempigia simu na ameahidi hivyo!
Nikaona sio kesi'...
nikasubili kesho na kesho ikapita.. nikasubili tena na tena na tena.....
Nilipoona kuwa kila siku napewa ahadi..,
Nikamwendea online..yuleee'
baalia wangu wa kitaani *Tz*
on fB.
Tukawa tunachart....ndani ya story' nikamuelezea yote yanayoendelea pale *Johburg*
Ushauri wake huyu baalia wangu, wala haukuwa mbaya sana, ila tu kila mtu anafikra zake ktk hii dunia,
Yeye alinishauri kuwa niendelee kukomaa palepale na kusema mwanzo mgumu, hivyo' niachane na masuala ya passport......
BaC' siku zilikatika...pia roho ilikuwa inaniuma ninapoona kuwa, napika na kuosha vyombo vya wabongo wenzangu ambao wao wakishapiga mishe zao huja pale restaurant na kupiga msosi
Haswa wanapohesabu mipesa zao,; Pumbavvvv! alafu eti mimi nalipwa Rand 30..sawa na bei ya sahani ya *ubwabwa*.
Kwakweli sikuridhika na ile hali.
Kilichofuata ni kupeleleza lifestyle na jiji la Capetown namna lilivyo, ingawa kabla ya kuingi ndani ya nchi ya
South Africa, nilikuwa ni mwenye kuchunguza vizuri maisha ya hili jiji la Capetown,
kwakutumia simu, laptop, pc nK.
Sasa hapa ni kutaka kuhakikisha
kwamba, vile nilivyoona kwenye media...ndivyo hivyo hivyo ilivyo?!?
Majibu niliyoyapata...yakawa tofauti tofauti...kwani wengine wanasema: kuna baridi kali sana huko na hata wengine hufa kwa baridi kali, wengine wanasema: maisha ya huko ni very expensive *ghali mno*,
wengine wanasema: hakuna mishemishe kama hapa Johannesburg, yaani kila mtu analakwake na wengine husema: jiji la Capetown ni kama Europe lifestyle yake.
Kwa upande wangu, nilivutiwa na huu msemo:
Maisha ya Capetown ni very expensive na Maisha ya Capetown ni kama Europe...
na hayo mengine wala sikujali kwa kweli.
Kadri siku zinavyokwenda, ndivyo nilivyozidi kumchukia yule mdada...maana nilihisi ananipotezea muda kwakweli,
pia kadri siku zinavyoyoyoma ndivyo uadui ulivyozidi baina yangu na yule mdada, na hata lile sofa nililokuwa nalalia...,halikuwa langu tena maana kuna jamaa km watatu..
waliongezeka mule ndani
*restaurant*...hivyo' nikawa nalala juu ya *pultebo* mwanzo mwisho!
Kadri siku zinavyojongea, ndivyo nilikuwa mfunguaji geti, it means..wakitoka kupiga mishe zao <_____> [HASHTAG]#ujangili[/HASHTAG].....
*akina fulani*
Siku nyengine napewa Rand..
5-10, Siku nyengine namfungulia mtu geti haliyakuwa anavuja damu eti kapigwa *shaba* dah!...yaani
kero tupu aisee!
Siku nyengine tunatimuliwa na maaskari yani dah!.
Ilipotimia kama miezi miwili baadae, siku hiyo nikaona kama mbwai na iwe mbwai2,
Nikamchana makavu live!
Nikamwambia...aisee wee mwanamke usiponipa leo passport yangu utakiona cha mtema kuni...
Alipanic na mimi pia nikapanic..
Likawa bonge la timbwili aisee!
Nikawaona waZulu wanashangaa shangaa....
AIBO,AIBO,AIBO...
nikawaambia: kwendeni mbele huko na AIBO zenu...hapa
KAZI TU ! pumbavvvv.
Kwa bahati nzuri wale wabongo wenzetu...walikuwepo palepale,
So' walituepusha na yule *Satan
Hakika issue ilikuwa kabambe, na kazi yenyewe nikaiachilia mbali...nikaona kuwa anataka anifuge pale na 30 zake...
Kasheshe kwangu sasa baada ya kuacha kazi..nikawa sijui nitakula vp, nitalala vp..kwa maana tayari nimeshamkolofisha mother house....mtihani!
Kwakweli tulikolofishana sana2
Hata nikaambiwa malufuku kukanyaga pale mjengoni...
Akadai kuwasiliana na yule B'mkubwa kuhusu kilichotokea pale.....sasa sijajua kwakweli B'mkubwa alijibu nini!
Kumbuka,,, begi langu liko kwake wakati huo wote.
Na mimi nikamwambia: sichukui burg hadi unipe my passport!
Nilifanya hivyo, ili kuepusha upotevu wa lile begi.
Kwa bahati yengine....
Yule dogo ambae ni msaidizi wa yule mdada, yeye alikuwa na rafiki yake yupo km mtaa wa 3 kutoka pale mjengoni, So' kwa siri alinipeleka hapo na akamuelezea full story kilichonitokea mimi pale mjengoni....
Nashukulu,, nilipokelewa kibaalia...na hata kuniambia nisiwe na wasi wasi......
Nakumbuka huyu rafiki...ambae ni rafiki wa yule dogo, alikuwa anaishi na friends zake wa2 *Tanzanians* all of them geto
moja. So pale jumla yao walikuwa wa 3...baada ya kuongezeka mimi tukawa wa 4,
geto moja.
Nililala pale wiki moja wakati nasubilia passport yangu...
Aisee nilipopata jina lake ambalo analitumia on fb...
yule aliyepewa ile passport..
Tulitukanana sana on fb..
Tukatishana sana on fb...
Ndani ya sikumbili zijazo nikaitwa pale mjengoni nikachukue passport yangu..
Ajabu ni kwamba yule jamaa mwenyewe ambae aliyepewa ile passport wala hakuja pale mjengoni...ila passport niliikuta.
Nikafahamu kuwa passport ilikuwepo ndani ila yule mdada alikuwa anataka kunifuga tu pale mjengoni......
Kesho yake baada ya kuipata ile passport...yule dogo alini kama Rand 100...pia kuna demu flani *mtanzania* yeye alinipa Rand 200...
Wale friends wa yule dogo...,wao walinisindikiza kwenye kituo cha daladala..
kwenda jiji la Capetown...
Kumbuka..., hapa kuna usafili wa aina mbalimbali...sO' inategemea na pesa yako..
Mimi nilichaguwa usafili wa kibaalia hahaha.......hhaha
Nilichaguwa usafili wa
*roli* mabaalia wengi wanaufahamu huu usafili %.
Niliingia ndani ya *daladala*
safari kuelekea sehemu moja panaitwa #Engine_garage...!
Kama lisali moja au kasoro iv"
Tulifika hapo Engine garage..
Kumbuka wale friends' wao walirejea pale tu' nilipoingia ndani ya ile *daladala*
Hakika nilizikuta roli kama 4...zinaelekea huko Capetown,
Mimi nikalipoint roli flani na nikapatana nae yule dereva..
Mishale ya saa 4- 5
Roli lilianza kuingia ndani ya
high way...tayari kwa kuiyanza safari.....
Je' unajua kilichonikuta njiani?
Je' unahisi nilifika huko CapeT?
Kumbuka...Visa yangu ilisha expired.....
Gonga likes nyingi....
Then tukutane [HASHTAG]#part[/HASHTAG] 4..
Tooth Brush
#$$$
Ujinga kuquote thread ndefu hivo unashindwa kuandika bila kuquote kitu kirefu ivo mnatupa shida bwanaaaaMkuuu mbn part four haikuj?