Niuluze chochote kuhusu utapeli

Niuluze chochote kuhusu utapeli

Kama ilivyo kwa makampuni binafsi, mashirika, na taasisi, pamoja na watu binafsi, wanaweza kuwa katika hatari ya udanganyifu wakati wa kununua bidhaa kutoka nje ya nchi (mtandaoni). Hali kadhalika, kwa wafanyabiashara waendao China, wanapokagua mizigo vizuri wakati wa kupakia kwenye kontena, wanaweza kubadilishiwa bidhaa au kukumbwa na udanganyifu wakati wa malipo mtandaoni. Kabla ya kupokea email kutoka kwa real manufature, then unapokea a same spam email kutoka kwa (hacker)mwizi, na hivyo kusababisha malipo kufanyika kwa taasisi isiyo sahihi. Je, hali hii inaweza kutokea pia serikali, kwa mfano, katika manunuzi ya ndege au SGR, au tenda, au bidhaa nyingine, na kusababisha hasara kutokana na tamaa ya kupata unafuu fulani? Na kama kuna mifano halisi, tafadhali nipe.
 
Mkuu vp kuhusu Utapeli wa Deci,Kalinda na Vikoba huu nao unakuwaje ??
 
Mkuu vp kuhusu Utapeli wa Deci,Kalinda na Vikoba huu nao unakuwaje ??
Huu ni utapeli unaotumia mfumo wa pembe tatu inayo angalia juu kama piramidi, ili kuanza mradi wa utapeli huu itabidi uwe na kianzio kidogo hata milioni 500 hivi ili kuwahadaa kenge pori wanaopenda hela za bure.

Kwahiyo utaweka vifurushi mf. Mtu akiweka laki 1 atapata 5000 kila siku, akiweka milioni 1 atapata elfu 50 kila siku, akialika mtu atapata kamisheni.

Kile kianzio chako unakitumia kama chambo, na watakao jiunga mwanzo watapiga hela kweli na watashawishika kuwaalika watu wengi zaidi, kadiri watu wanavyoalikwa utarudisha pesa yako na kupata faida hata mara 50, faida ikitosha unazuia watu kutoa fedha.

Unaweka tangazo kuwa waendelee kujiunga wakati mnashughulikia tatizo la kiufundi, ndo wamepigwa hivyo.
 
Kama ilivyo kwa makampuni binafsi, mashirika, na taasisi, pamoja na watu binafsi, wanaweza kuwa katika hatari ya udanganyifu wakati wa kununua bidhaa kutoka nje ya nchi (mtandaoni)...
Inawezekana, fedha nyingi ambazo hupotea bila maelezo serikalini ni kutokana na wataalamu kutapeliwa, ila wanaogopa kusema, si ulisikia TTCL wanadai mabilioni ya pesa ila hawajui wanaye mdai? Si ulishuhudia vichwa vya treni kuokotwa bandarini? Huo ni utapeli.
 
Boss la DP World niko hapa kujibu maswali yako. Nimekunja 4 hapa kwenye ofisi yangu ya kifahari najizungusha zungusha kwenye kiti changu wakati nikifikiri kuhusiana na michongo ya kuongeza ukwasi wangu kupitia watu wa Africa na rasilimali zao.

Karibuni.

Wewe kama Boss wa DP World mipango yenu ni ipi kuongeza ufanisi?

Mtazuiaje madawa ya kulevya, silaha, au nyara za serikali kusafirishwa nje?

Mna mpango wa kuwatimua wafanyakazi wote wazawa?
 
Back
Top Bottom