Njama za kuifukuza Sahara Magharibi zinasukwa. Tanzania inahusika?

Njama za kuifukuza Sahara Magharibi zinasukwa. Tanzania inahusika?

Zitto

Former MP Kigoma Urban
Joined
Mar 2, 2007
Posts
1,562
Reaction score
10,888
Kuna mkakati wa kuifukuza POLISARIO nchini.

Serikali ya Tanzania: POLISARIO ni Chama cha Ukombozi ambacho kilipewa hadhi ya Serikali na uanachama wa Umoja wa Afrika tangu 1982. Suala hili limeanza kuleta utata wa kisheria Katika Umoja wa Afrika na Katika duru za Kimataifa.

ACT Wazalendo: Huu ni Mkakati unaosukwa kuifukuza POLISARIO kwenye Umoja wa Afrika na tulionya hili mapema sana wa kampeni za kuirudisha Morocco AU. Serikali ya Tanzania kuweka sentensi hii kwenye Hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje Mwaka 2018 ni mkakati wa kutuandaa kisaikolojia kuifukuza POLISARIO.

Msimamo wetu ni kuwa Jamhuri ya SAHRAWI (Sahara Magharibi) ni Taifa huru lililovamiwa na Morocco. Ubalozi uliopo nchini ni ubalozi wa SAHRAWI na sio wa POLISARIO na kiti cha AU ni kiti cha Jamhuri ya SAHRAWI.

Tunaitaka Serikali ya Tanzania iache ujanja ujanja kwenye suala hili na itumie nafasi yake ya urafiki na Morocco kuhakikisha Maazimio ya UN yanatekelezwa ili watu wa Sahara wawe Huru wajenge nchi yao.

Zitto Kabwe

24/5/2018
 
Huyu jamaa awe mwandishi wa vitabu tuu kwa sasa, maana hana focus ya jambo lolote akaliaimamia mpka mwisho.
Vitabu andika wewe. Ambaye hana focus ni wewe kusoma ambayo huyapendi au kucomment ujinga.
Jadili hoja zilizotolewa, usifanye personal attack.

Na ujumbe ni kutoka ACT - wazalendo sio MTU mmoja, kama kuna kosa katika walichokiandika tuma malalamiko yako kwa msajili wa vyama vya siasa.

Vijana wa kitanzania tunakuwa wapumbavu wapumbavu. Kama hoja huna uelewa nayo, inakuzidi uwezo pita kimya, sio kuhara hapa. Shame on you.
 
Tanzania first, kama hatupati faida yoyote watimuliwe mbali, huu ni wakati wa kuiweka Tanzania kwenye uchumi, tunataka Tanzania yenye uchumi[/QUOTE]
Uchumi wa nchi unajengwa na Watanzania wenyewe ...umfukuze mtu ama usimfukuze kama wananchi hawapo tayari kuijenga nchi yao haisaidii chochote
 
Itapendeza zaidi kama hiyo Hotuba utaiweka hapa pia, ili tuchangie kwa facts, sio hisia.
 
Acha na wao wapambane na hali yao kama sisi tunavyopambana na yetu. Wao ni ndugu wakubaliane sisi tujenge yetu.

Tumesaidia wengi wengine wametusahau kama SA hata kwenye msiba wa Mandela walitutenga mpaka JK akawakumbusha kwamba Mzee alisahau na Viatu vyake tz.

AU ndio walitaka kabisa kuondoa picha ya Nyerere tumshukuru Mugabe alipiga mkwara ndio watu wakanywea
 
Back
Top Bottom