BakalemwaTz
Senior Member
- Jul 14, 2017
- 120
- 125
Karibu katika andiko hili muhimu juu ya utatuzi wa tatizo kubwa la ukosefu wa ajira kwa vijana nchini Tanzania. Andiko hili pia limejumuhisha takwimu muhimu za ajira nchini, sababu za ukosefu wa ajira kwa vijana, athari za ukosefu wa ajira kwa vijana na njia muhimu za kutatua tatizo la ajira nchini.
Taswira ya ajira kwa vijana nchini Tanzania
Kwa Mujibu wa takwimu za ajira nchini kutoka National Bureau of Statistics (NBS), Kiwango cha ajira nchini kilipanda kutoka asilimia 10.1 mwaka 2015 Mpaka 9.6% Mwaka 2019.Kwa mujibu wa ripoti hii ni watanzania million 22.5 wenye ajira rasmi na zisizo rasmi nchini. Ajira hizi ni pamoja na ajira kutoka serikalini, mashirika, taasisi na makampuni binafsi. Ripoti ya NBS ya mwaka 2016 iliyotelewa mwaka 2018 inaeleza kuwa ajira rasmi nchini Tanzania ni zaidi ya milioni 2.5.
Chanzo: NBS ( National Bureau of Statistics)
Nchini Tanzania kijana ni yule mwenye umri wa miaka 15-35. Mamlaka ya Takwimu (NBS) inakadilia kuwa ifikapo mwaka 2035 Tanzania itakuwa na vijana takribani milioni 35.4. Kufikia Mwaka 2020 Tanzania ilikua na vijana wapatao milioni 22.5.
Ripoti ya Shirika la wafanyakazi dunia (ILO) ya mwaka 2020, inasema ni asilimia 3.6 % ya vijana wa kitanzania wenye kazi rasimi.
Ni asilimia 10% ya vinaja wanaopata kazi rasimi kati ya 800,000 ya vijana wanoingia kwenye soko la ajira kila mwaka kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya dunia ya Mwaka 2016.
Sababu kuu 5 za ukosefu wa ajira kwa vijana nchini Tanzania
Pamoja na serikali ya Tanzania kutoa fursa ya ajira kwa vijana, bado kumeendelea kuwa na wimbi kubwa la vijana wasio na kazi nchini. Zifuatazo ni sababu zinazopelekea kuwepo na tatizo la ajira nchini.Mitaala na Sera za elimu Nchini
Mfumo wa elimu umekua ni chanzo kikubwa cha ukosefu wa ajira kwa vijana. Katika ulimwengu wa sasa mashirika, makampuni na watu binafsi huajiri watu wenye ujuzi na uweredi kuliko sifa na ufahulu wa vyeti. Mitaala na sera za elimu ya nchi haziwaandai vijana kuingia katika soko la ajira za ushindani kwani elimu yetu hutolewa kwa nadharia sana (theory) kuliko vitendo .Ukosefu wa ujuzi, Ubunifu na elimu ya ujasiriamali
Vijana wengi wahitimu huwa wanapofika kwenye soko la ajira, hugundua kuwa hawana ustadi sahihi wa kutosheleza soko la kazi la leo. Hii ni kwa sababu mitaala ya Vyuo vingi haitoshelezi soko la ajira kwa sasa lenye kuhitaji waajiri wenye ustadi, ubunifu na uweredi. Mitaara yetu pia haitoi miongozo yenye kuwaandaa vijana kuweza kujiajiri kupitia kuanzisha miradi na shughuli za kibiashara zenye kuwaingizia kipato.Uchumi na Bajeti ya Nchi
Ni wazi kwamba serikali haiwezi kuwaajiri watu wote. Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazoendelea (developing country) hivyo Kipato cha nchi hakiwezi kutosheleza kuwaajiri vijana wote. Kwa mujibu wa bajeti ya nchi ya mwaka wa fedha 2021/22 ni zaidi ya ajira 40,000 zitakazotolewa na serikali.Kasi ya Mabadiliko ya tekinolojia.
Ukuaji wa tekinologia umepelekea wingu kubwa la ukosefu wa ajira nchini. Ufanisi wa kazi katika ulimwengu wa tekinolojia huitaji watu wenye ujuzi wa hali ya juu na uweredi katika kuhimili kasi ya mabadiliko kwa kubuni njia mpya za kutatua changamoto katika jamii. Matumizi ya sayansi na tekinolojia nchini imekua changamoto kubwa na chanzo cha ukosefu wa ajira kwa vijana hususani soko la ajira nje ya mipaka ya Tanzania.Ongezeko Kubwa la Watu.
Kuongezeka kwa idadi ya watu kunafuatana na kuongezeka kwa nguvu kazi ya jamii ambayo inasababisha idadi kubwa ya watu kukosa ajira, kwani watu wengi hushindania fursa chache zilizopo katika jamii.ATHARI ZA UKOSEFU WA AJIRA KWA VIJANA
Athari za ukosefu wa ajira kwa vijana wa kitanzania ni nyingi. Athari hizi zinaweza kuwa za kibinafsi, kifamilia, kijamii na hata kitaifa. Zifuatazo ni athari za ukosefu wa ajira kwa vinaja.- Kuongezeka kwa matendo ya uharifu:- mfano, wizi
- Ugumu wa maisha na umasikini
- Kupungua kwa pato la taifa na familia kwani kundi kubwa ni tegemezi
- Msongo wa mawazo unaopelekea magonjwa kama kisukari, presha, na kichaa
NJIA 5 BORA ZA KUTATUA TATIZO KUBWA LA AJIRA KWA VIJANA NCHINI TANZANIA
Ukweli ni kwamba serikali na mashirika binafisi haviwezi kutoa ajira kwa vijana wote kwani ongezeko la vijana waliohitimu katika vyuo mbalimbali huongezeka kila mwaka, kwa takwimu za TCU zinaonyesha kiwango cha vijana wanaojiunga na vyuo vikuu hufikia zaidi ya elfu 50 kwa wastani kutoka mwaka 2015-2020. Vivyo hivyo kiwango kikubwa cha vijana huitimu elimu ngazi ya cheti na diploma.Chanzo: tovuti ya vyuo vikuu TCU
Njia zifuatazo zinafaa kuchuliwa hatua kali ili kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2035 idadi kubwa ya vijana waweze kuwa na ujuzi, uweredi na umahili utakaowafanya kuajirika na kuajiriwa ili kukuza uchumi wa nchi yetu.
Kuanzisha Programu za ujuzi, elimu na mafunzo (Practical and skill-based programs)
Ili kuweza kutatua tatizo sugu la ajira Tanzania kwa sasa na usoni, serikali inatakiwa kuanzisha mitaara maalumu itakayoweza kutumika mashuleni kuanzia ngazi ya msingi mpaka vyuo vya kati na juu. Mitaara hii inatakiwa kuwaandaa vijana kupata ujuzi na si kwa nadharia.Kuwapatia Vijana Mitaji na Elimu ya Ujasiriamali
Kama taifa tunatakiwa kuanzisha majukwaa maalum yenye kulenga kuwawezesha vijana kufikia ndoto zao. Serikali, Mashirika, wadau na makampuni mbalimbali vinatakiwa kwa pamoja kuunda sera na majukwaa maalumu ya kuwezesha vijana kufikia ndoto zao. Hii itawawezesha vijana kujiajiri na kuongeza uzalishaji wa tija kwa uchumi wa taifaKuboresha na Kukuza Sekta ya Sayansi na Tekinolojia.
Nchi zilizoendeleah uweka jicho lao katika tasnia ya sayansi na tekinolojia, hii ni kutokana na jinsi tekinolojia ilivyoweza kutatua kero na changamoto za jamii yetu. Zaidi ya 70% asilimia ya changamoto zilizopo katika jamii yetu utatuzi wake hutegemea maendeleo ya tekinolojia.Hivyo, vijana wafunzwe ujuzi mbalimbali wa kubuni, kutengeneza na kutumia vifaa au programu zenye kulenga kutatua kero za kijamii. Hii inafaa kuazishwa ngazi ya msingi mpaka vyuoni. Ufanisi na ukuaji wa tekinolojia utahitaji pia kupunguza gharama na sheria za matumizi ya mitandao kwani kuna maelfu ya ajira kwa vijana wamejiari na kuendesha maisha yao kupitia mitandao.
Kuanzisha Mashindao ya Ubunifu Kwa Vijina na Kuwawezesha Mawazo Yao Kufanikiwa
Story of Change, ni moja ya shindano muhimu ambalo huibua hisia na uwezo kwa vijana katika kutatua changamoto za jamii. Mashindano ya kibunifu yanatakiwa kupewa kipaumbele ili kuwezesha vijana wabunifu kutumia majukwaa (platform) yao kutatua matatizo ya jamii. Hii pia itasaidia kuongeza hamasa kwa vijana wengi waliopoteza mwelekeo kuanzisha malengo muhimu na kujikwamua kiuchumi.Uboreshaji wa sera za uwekezaji wa ndani
Mwaka 2017, Hayati Prof Vicent Kihiyo, aliyekuwa Mkuu wa chuo kikuu SEKOMU aliwahi kusema ili nchi iweze kukua kiuchumi inatakiwa kuruhusu uwekezaji mkubwa wa sekta binafsi ilikuruhusu mzunguko wa pesa katika jamii. Hii ni pamoja na kuweka sera nzuri za uwekezaji wenye tija kwa kufuata trickle Down Theory (Kuruhusu uwekezaji mkubwa kwa kupunguza kiwango cha kodi) hii itasaidia sekta binafsi kuajiri kundi kubwa la vijana na kuongeza tija kwa wawekezaji wapya ambao ni “vijana”.Mwisho, Niombe watanzania wote kwa ujumla, makampuni, mashirika na wadau wa sekta binafsi tushikamane kwa pamoja na serikali kuijenga Tanzania moja yenye lengo moja na kuwa na taifa lenye vijana mahiri katika kuinua taifa na si vijana tegemezi. Vijana pia ni vyema kufunza ujuzi tofauti ili kuweza kujiajri na kuajirika ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.
Upvote
102