SoC01 Njia pekee ya kuelekea Mafanikio ni kufanya uwekezaji katika Ubongo wako Vijana

SoC01 Njia pekee ya kuelekea Mafanikio ni kufanya uwekezaji katika Ubongo wako Vijana

Stories of Change - 2021 Competition

muafi

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2015
Posts
2,557
Reaction score
6,128
images.jpeg


Miaka kadhaa iliyopita nilipohitimu elimu ya Chuo Baba yangu yangu mzazi aliniita akaniuliza nikikupa milioni moja unaweza ukaifanyia nini ili uache kusubiri ajira!

kwaweli nilikosa jibu kwa muda ule nilikaa nimemuangalia tu, kisha nikamuomba anipe muda wa kutosha nimpe jibu, nilimwambia anipe siku mbili tu nifikirie nini cha kufanya then nitampa jibu akakubali,

nilitumia hizo siku mbili kwa kuwaza na kuwazua, nikaomba mawazo ya watu wengine wananiambia uza viatu wengine uza mazao wengine uza dagaa yaani ilikua ni mvurugano

Mwisho wa siku nikaona ili nionekane sijashindwa ngoja nimpelekee jibu, nikamwambia mzee naomba hiyo pesa nikaanzishe Bihashara ya duka nmepata fremu sehemu flani, ,

Mzee aliniangalia akacheka akauliza unauhakika utaifanya hiyo biashara? nikasema ndiyo,

mzigo ukaingizwa benk 1M, nikasema hapa nimeula, nikaaanza nikakodi fremu ya elfu 50 nikalipia miezi mitatu 150,
nikaweka mbao za dukani kwa elfu 90 nikaunua na muzani wa mawe na mavitu vitu mengine kabla ya kununua bidhaa za kuanza kuuza tayari nilikua nimebakiza laki nne tu mkononi, nikaanza kuchanganyikiwa, ile nimeanza kuleta gunia la unga gunia la sukari na vitu vidogo sana hela ikaisha mkononi na bidhaa hazikutosha kabisa dukani.

Kilichofuata ilikuwa nakula pesa hizo hizo ambazo nauza ile biashara ilikaa miezi minne tu nikaifunga (nikafilisika)

Nilipofunga Biashara niliona hata aibu mbele ya aliyenipa mtaji nikaanza kujiuliza huwenda hata ningenunua kiwanja ningekua nina kitu cha kuonyesha mbele ya watu,

Kuna Rafiki yangu mmoja yeye tuliachana baada ya yeye kumaliza kidato cha nne hakuendelea zaidi na masomo alijikita kwenye biashara( ya kuuza chakula mgahawa) yeye kupitia biashara zake hizo nilikuta tayari ana nyumba ya vyumba viwili na sebule na anamke na mtoto na bado anaendelea na biashara yake hiyo hiyo aliniambia alianza na mtaji wa shilingi za kitanzania laki moja na elfu themanini na sita.

Hapo ndipo nilikaa nikajifikiria sana nikaona kumbe tatizo sio mtaji wala tatizo sio Biashara tatizo ni uwekezaji nilioufanya ndani ya ubongo wangu mimi,

Ili ufanikiwe kimaisha ni lazima ufanye kwanza uwekezaji ndani ya ubongo wako ndipo uanze kuchukia hatua za kusonga mbele,

Je, Ubongo wako umeulisha nini?

Je ubongo wako umeuaminisha nini?

Je, unautumia ubongo wako sawasawa?

Leo hii akija mtu akakwambia nakupa milioni kumi sasahivi niambie utazifanyia biashara ipi utamjibuje?

Mimi nina uhakika tukikaa watu watatu tukapewa milioni sita sita kati yetu kuna ambaye ataenda kuziwekeza vizuri zilete faida na kuna ambaye ataanza kuomba ushauri kwa watu azifanyie biashara gani? anauliza si kwamba haoni biashara za kufanya ni kwamba bado hajautune ubongo wake uwe tayari kwa biashara,

SIKILIZA

Katika zama hizi ni kwamba mambo yamebadilika kwa kiasi kikubwa sana, Tupo kwenye ulimwengu wa Tatizo la ajira dunia nzima, na katika hali ya kawaida hasa kwa vijana huu ndio wakati mahususi wa kuhangaika sana kabla nguvu tulizo nazo hazijaisha,

je, Tutawezaje?

Nitakupa njia chache miongoni mwa nyingi sana, njia hizi ni kwaajili ya kuuandaa ubongo wako uwe tayari kukabiliana na changamoto zinazotuzunguka,

NJIA ZA KUFANYA UWEKEZAJI KATIKA UBONGO WAKO,

ninapozungumzia uwekezaji katika ubongo maana yake namaanisha kuujaza ubongo wako vitu vya muhimu sana yaani kuulisha material ya kukusaidia kuendana na mazingira yoyote yale,

Mungu katupa utajili kupitia akili kazi ni kwetu tu kuigeuza hiyo akili izae utajili,

IELEWE NASFI YAKO/AKILI INAWAZA NINI na inaweza nini

Kuna kitu kinaitwa akili ya asili, mbali na kwemda shule kupata madegree na ma PHD lakini siku zote kitu kinachoongoza maisha huwa ni ile akili ya asili aliyotuumbia Mungu kila mmoja anayo,
hii sasa ndio huwa ya kuitumia katika maisha ndio maana unaweza kukuta mtu wa darasa la nne anaendesha biashara vizuri sana lakini mtu wa PHD hawezi kujiajili, utofauti ni kuwa huyu wa darasa la nne ana akili ya asili ndiyo inamuongoza,

Kufanya kitu/biashara bila kujua akili yako inawaza nini, inaamini nini au inakuongoza vipi huo ni upotezaji wa muda na upotezaji wa Pesa utaishia kufirisika na kusema umelogwa,

Wakati nimemaliza masomo yangu nikapewa mtaji wa 1M nilikurupuka nikatembea na mawazo ya watu sikupata msukumo wa akili yangu kuniongoza nifanye nini maana yake nilikua nafanya kitu nisichokijua matokeo yake nikajikuta nafeli vibaya mno.

Hapa jambo kubwa la msingi ni kuangalia akili yako inaweza nini? Mbali na elimu na ujuzi uliofundishwa je, akili yako inaweza nini kingine? Unaweza kufanya biashara ipi unayoweza kuimudu?

Je, unao msukumo wa ndani au wa nje wa kufanya hicho unachotaka kukifanya?
je? Akili yako imetulia sawasawa kukabiliana na changamoto za hicho unachokitaka kukifanya? Unataka kufungua tution center halafu akili yako asilimia kubwa inawaza ngono, utaweza kuwamudu wateja?


USIISHI KATIKA NADHARIA/MAZOEA/KUKALILI

Hapa sasa ndio tunafeli kwa kiasi kikubwa sana, Vijana tumekua na nadharia tumekalili, imefika hatua mtu akifika chuo akapata degree baadhi ya kazi/biashara anaona sio hadhi yake, haya ni mazoea yaliyopitwa na wakati,

hapa tuamue kubadilika kulingana na wakati, ubongo wako inabidi uufanye uache kuishi kwa mazoea na nadhalia, ndio maana mpaka sasa unakuta graduates wa vyuo tunaangaika sana mtaani kuliko ndugu zetu tunaoona ni wenye elimu za kawaida,

Tunaishi kwa kupambana sana tuingie soko la ajira tuajiliwe lakini hatupambani sana kujiajiri wenyewe, hii ni kwasababu ubongo wetu tumeisha uaminisha ili ufanikiwe kimaisha ni lazima uajiliwe,

Hii imetufanya kuchelewa sana katika mafanikio ya maisha, ni wakati sasa wa kuacha mazoea na nadharia za kukalili tuamue kujivua elimu za kufundishwa na tuongozwe na akili zetu alizotupa Mungu,
siunajua ili uishi vyema lazima utafute hela? siunajua hela zinakotafutwa? sasa basi vua joho usitafute kazi tafuta pesa,
boresha maarifa yako ya kutafuta Pesa haimaanishi kwamba ukajiendeleze kielimu upate degree au PhD

hapa ni kuuongezea ubongo maarifa yaani uwe na ufahamu wa vitu vingi, kuna tofauti kati ya kuwa na elimu na maarifa, unaweza kuwa na elimu ila huna maarifa, na unaweza kuwa huna elimu kubwa ila una maarifa makubwa,

tujifunze kusoma article mbali mbali za kutuongezea maarifa ya nini tunataka tufanye mfano mimi nahitaji kufanya ufugaji wa kuku lazima niende kwa wafugaji na kusoma article za ufugaji lazima nikajifunze zaidi kupata ujuzi, lazima niiaminishe akili yangu kwamba naweza na nitafanikiwa

UTHUBUTU

hapa ndipo penye Busara , kati ya vitu vinavyotufelisha sana ni kuogopa kuthubutu,

Tumekua waoga na wenye aibu kupindukia,
Mafanikio sio kitu unachopata bila kuweka juhudi, hata hivyo ni mawazo ambayo lazima uchukue maamuzi kutimiza malengo yako na inahitaji uthubutu kwakuwa ni kazi ngumu

wengi tumeshindwa kabisa kabisa kwa kuogopa kujaribu, unaogopa kufanya biashara kwakuwa unaogopa hasara,

unaogopa kuhangaika na kushinda juani hivyo unasubiri uajiliwe iliukae kwenye kiyoyozi,

ndugu zangu mawazo yako yote bila kuthubutu nikazi bure, vua aibu zote na uoga wote vaa ujasiri jikane nafsi yako, fanya kile unachoamini kitakuletea faida,

tafuta pesa, tafuta pesa, tafuta pesa kwa nguvu zote ukiwa bado ni kijana maana ndiyo umri wako sasa,

wengi tukiamua kuthubutu, tutafanikiwa kiasi kikubwa na tutaishi maisha ya raha,

Fanya uwekezaji mkubwa katika ubongo wako, ili uendane na hali ya sasa,

maisha ni maamuzi!

TRY YOU CAN DO!
 
Upvote 3
[emoji122][emoji122][emoji122] BE BLESSED [emoji120][emoji120][emoji120]
 
Biashara ni nidhamu na uvumilivu
Usikute biashara yenye pesa nyingi faida yake kiduchu
 
Hakika umenena vyema...

Biashara ni Imani na inachukua muda kukuletea matarajio unayotaka...
Muhimu ni kua mvumilivu mwenye nidhani na msimamo...
 
Back
Top Bottom