Njia za kufuata ili kuachana na unywaji wa Pombe na Ulevi uliopitiliza

Njia za kufuata ili kuachana na unywaji wa Pombe na Ulevi uliopitiliza

Kila siku nilikuwa nakunywa bia sita na zaidi IPA Dogfish 90 (9% Alcohol) mpaka nikaanza kupata issues ndogo ndogo za kiafya. April mwaka huu rafiki yangu mmoja akanikokota kwenda kwenye retreat ya kilokole porini kwa siku tatu. Usiku ule wa kwanza tu mhubiri anasimama nikasikia "Wengine hapa ni walevi. Kwa jina la Yesu nakuhakikishia ukiondoka hapa hutakunywa pombe tena". Something clicked inside and I was touched. Nililia sana usiku ule in front of about 200 men. Basi nilizingirwa nikawekewa mikono nikaombewa mpaka nikawa hoi. Nilirudi home na kutupa bia zote zilizokuwa kwenye cooler. Halafu rafiki yangu mmoja akaniambia kuwa nikipata hamu ya pombe basi nile tikiti maji la baridi. Nilifanya hivyo na baada ya wiki mbili hamu yote ya pombe ikaisha na tangu mwezi wa nne 2015 sijaonja pombe tena. Gym, mboga mboga na matunda aisee nimerudi kwenye fomu balaa mpaka watu hawaamini. Huu ndo ushuhuda wangu wa kweli kuhusu kuacha pombe na sijui kama utakusaidia. Usikate tamaa na kama una nia ya kweli ya kuacha inawezekana hata kama ikibidi ni kupitia maombi na higher power. Good luck!
 
Jamani naomba msaada nina ndugu yangu ni mlevi sana mpaka anasahau kwenda kazini.

Naomba kwa anayejua dawa ya kuacha pombe anisaidie.

Ni seme ukweli nimecheka sana
Kusoma ujumbe huu. Hahaha dah samahani lakini.
 
Jamani naomba msaada nina ndugu yangu ni mlevi sana mpaka anasahau kwenda kazini.

Naomba kwa anayejua dawa ya kuacha pombe anisaidie.
Kama imani inaruhusu Mkuu nlisikia maziwa ya Noah old model a. k. a mbuzi katoliki vizia kinyaji chake mchanganyie humo hatokunywa pombe tena milele akisogelea pombe yeye ni kichefuchefu na akisubutu kusogezea pua yeye ni kutapika tuu. Yaani hamna namna ataacha tuu.
 
Changanya unywaji wa safari laga,kibo,serengeti,konyagi,kiroba alaf katiza mitaa ya manzese usiku,wakikugegeda utaacha
 
Mwaka 2010 mwezi Aprili nilipata matokeo yangu ya form 6. Nikanywa bia inaitwa Uhuru Peak Lager kusherehekea(Tangu siku hiyo sijawahi kuiona popote) Yaliyonikuta yalinifanya niape kwa miungu yote kutogusa pombe maishani mwangu! Mpaka leo sijawahi kutia kinywani kilevi chochote

Pombe ni shetani. Ukiamua kuacha unaacha tu wala haihitajiki kuwaza mara mbili. Acha tu basi... Simple !
 
Mimi niliacha pombe ghafla. ...nikashinda moyo sasa mwaka wa sita and am still counting
 
Mwaka 2010 mwezi Aprili nilipata matokeo yangu ya form 6. Nikanywa bia inaitwa Uhuru Peak Lager kusherehekea(Tangu siku hiyo sijawahi kuiona popote) Yaliyonikuta yalinifanya niape kwa miungu yote kutogusa pombe maishani mwangu! Mpaka leo sijawahi kutia kinywani kilevi chochote

Pombe ni shetani. Ukiamua kuacha unaacha tu wala haihitajiki kuwaza mara mbili. Acha tu basi... Simple !
Kwa wale alcoholic kabisa siyo rahisi kiasi hicho kwani kila kitu kinakuwa kimeathirika. Pombe ni uraibu kama yalivyo madawa mengine ya kulevya na kwa wengi kuachana nayo huwa siyo rahisi kihivyo. Wewe una bahati ulikunywa siku moja tu ukasepa. Ingekukolea sawasawa sidhani kama ungetumia neno simple. Yote kwa yote hatua ya kwanza ni kutambua kuwa una tatizo na kuweka dhamira ya kweli na will power ya kutaka kuacha. Mengine yatafuata baada ya hapo. Siyo simple lakini INAWEZEKANA!!!

Mimi niliacha pombe ghafla. ...nikashinda moyo sasa mwaka wa sita and am still counting
Hongera mkuu. Mimi huu mwezi wa saba and I am still going strong. Imebidi pia kuachana na marafiki wanywaji. Siku hizi jioni mi niko home nanyonya juice yangu ya matunda ninayotengeneza mwenyewe. Pombe ni utumwa na ukiponyoka unajiona mjinga kwa pesa, muda na afya uliyopoteza.
 
Pombe pia huleta umaskini ukisikia masimulizi ya pombe imeharibu vipi maisha ya watu utashangaa
 
Habari wana Jf,

Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu,

Naombeni msaada au kama kuna mtu yoyote anajuwa njia ya kuacha hivyo vitu aniambie,nimejikuta nakunywa pombe kila siku nikitoka kazini saa kumi lazima nipitie bar nianze kunywa bia na siku kama sina hela nakunywa makonyagi na nikiianza tu kunywa basi tarudi home saa sita na nikiwahi sana basi ni saa nne,yani kwa siku nakunywa bia zaidi ya 13 na sigara 40 sasa hali hii najaribu kuacha nashindwa yani nikiiona tu bar basi siwez kupita bila kuingia na hata nikipita natembea kama hatua kumi hiv narudi naenda bar.

Naombeni kama kuna mtu anajuwa dawa yoyote ila aniambie Tashukuru sana endapo tapata tiba
 
Duniani kote hamna dawa ya kuacha pombe wala sigara, dawa ni wewe mwenyewe kuamua kuacha.
 
Usihofu, kuna watu washauri nasaha humu watajaribu kukupa maushauri. Cha msingi ni imetambua kuwa ni tatizo, sasa ujishirikishe kuacha, fanya juu chini upate washauri na uweke pia juhudi binafsi.
Mimi NAMSHUKURU sana Mungu, sinywi hata kidogo, sivuti hata kidogo na ninapoona na kusikia watu kama wewe nahasika zaidi kutojiingiza ktk addiction yeyote ya harmful substances!
 
hakuna dawa ni maamuzi yako make nilikuwa nalala baa,sigara pakti kwa siku niliamua siku moja tu na kuacha
 
Hiyo kitu noma sana, kuna jamaa yangu alikua mlevi kinoma wazazi wake wakaangaika sana ili jamaa aache mitungi lakn patupu

Katika kuangaika ni pamoja na kumchanganyia maziwa ya binadamu na ya nguruwe katika pombe lakini bila bila hapo ni maamuzi binafsi
 
Back
Top Bottom