Njia za kufuata ili kuachana na unywaji wa Pombe na Ulevi uliopitiliza

Njia za kufuata ili kuachana na unywaji wa Pombe na Ulevi uliopitiliza

Hiyo kitu noma sana, kuna jamaa yangu alikua mlevi kinoma wazazi wake wakaangaika sana ili jamaa aache mitungi lakn patupu

Katika kuangaika ni pamoja na kumchanganyia maziwa ya binadamu na ya nguruwe katika pombe lakini bila bila hapo ni maamuzi binafsi

aiseee asante kwa kuushauri
 
Usihofu, kuna watu washauri nasaha humu watajaribu kukupa maushauri. Cha msingi ni imetambua kuwa ni tatizo, sasa ujishirikishe kuacha, fanya juu chini upate washauri na uweke pia juhudi binafsi.
Mimi NAMSHUKURU sana Mungu, sinywi hata kidogo, sivuti hata kidogo na ninapoona na kusikia watu kama wewe nahasika zaidi kutojiingiza ktk addiction yeyote ya harmful substances!

bora kama hutumii na usije ukasubutu hata kuonja maana mimi nilionja mara mbili tu nikawa nikinywa naona kali ila baadaye inakuwa tamu kweli.
 
Habari wana Jf,

Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu,

Naombeni msaada au kama kuna mtu yoyote anajuwa njia ya kuacha hivyo vitu aniambie,nimejikuta nakunywa pombe kila siku nikitoka kazini saa kumi lazima nipitie bar nianze kunywa bia na siku kama sina hela nakunywa makonyagi na nikiianza tu kunywa basi tarudi home saa sita na nikiwahi sana basi ni saa nne,yani kwa siku nakunywa bia zaidi ya 13 na sigara 40 sasa hali hii najaribu kuacha nashindwa yani nikiiona tu bar basi siwez kupita bila kuingia na hata nikipita natembea kama hatua kumi hiv narudi naenda bar.

Naombeni kama kuna mtu anajuwa dawa yoyote ila aniambie Tashukuru sana endapo tapata tiba

Kuacha kunywa nini?
 
Ukitaka kuweza cku huna pesa ya bia usinywe konyagi wala usikopo bia. Pia jifunze kupunguza idadi ya chupa za bia kuacha kwa njia ya kusema leo naacha huwezi punguza idadi taratibu utajikuta unaacha ila kama cyo za kulogezewa au za kurithi.
 
Kumbe nina mwenzangu. Tatizo mimi nataka kuacha sana, ila napenda ile feeling nayoipata. Kumbe hii ndio maana ya addiction nilikua sijui na sikudhani nitakuja kuwa addicted na kitu ila ni mateso.
 
Halafu mimi napenda kunywa mwenyeweee. Au na rafiki mmoja au wawili kwa nadra sana.
 
Wanadai ukichanganyiwa maziwa ya mama anayenyonyesha kwenye bia ukinywa utatapika na kuacha bia kabisa na viroba. Pia waone wataalamu
 
Nikweli ukichanganyiwa hayo maziwa ya mama mixer na Noah (kitimoto) unatapika sana ila inakua kama umeflash tu,,, unaweza kaa wiki bila kugonga chupa cku ukichukua moja utajikuta unapiga kreti...
 
13x2000x30=780000.je wewe unapata mshahara kiasi gani hapo bado sigara.we cha msingi kuanzia leo acha
 
Image result for how to quit alcohol
Can I cut back on my drinking or do I need to stop drinking completely?
Set a drinking goal.
Choose a limit for how much you will drink. ...
Keep a "diary" of your drinking.
To help you reach your goal, keep a "diary" of your drinking. ...
Watch it at home. ...
Drink slowly. ...
Take a break from alcohol.
 
Ukiona unashindwa kuacha kwa hiyari. ..ISHIWA uone kama hata ndani utatoka
 
....... nianze kunywa bia na siku kama sina hela nakunywa makonyagi na nikiianza tu kunywa basi tarudi home saa sita na nikiwahi sana basi ni saa nne,yani kwa siku nakunywa bia zaidi ya 13 na sigara 40

Naombeni kama kuna mtu anajuwa dawa yoyote ila aniambie Tashukuru sana endapo tapata tiba

Ninakunywa ila nimepunguza sana na ninaelekea kuacha kama wewe unavyodhamiria. Cha msingi ni wewe mwenyewe kuendelea na dhamira yako na kama umeoa mke wako ni muhimu sana kwani ana nafasi ya kukusaidia. Mimi nilikuwa nakunywa kuanzia asubuhi, na wakati mwingine nilikuwa naenda kazini nishapiga Bavaria 8.6 kama tatu hivi, na jioni usiseme....akina Black label na wenzake chupa ilikuwa inaisha...ila baada ya kuamua kutaka kuacha nilipewa technique na wataalam ambazo nyingine naona wadau wameshazisema. Naomba nikupe experience yangu!
1. Acha kabisa kunywa Whysky na Konyagi...endelea na bia tu
2. Anza kupunguza idadi ya bia unazokunywa kwa siku...
3. Anza kuruka siku moja moja bila kunywa bia, siku ambazo hunywi kunywa maji mengi sana....endelea hivyo mpaka ifike mara moja kwa wiki n.k
4.Ukishindwa na hata ukujikuta umeanza huo mpango halafu hapo katikati ukauvuriga kwa kutwanga creti nzima uzife moyo, uanze tena huo mpango, Usiondoke kweye DHAMIRA YAKO YA KUACH...
5. Niliamua kumpa mke wangu ashie pesa zangu ili kufanikisha hayo, na kwa kweli mke wangu alinisaidia kwani mshahara ukiingia au nikipata posho yoyote ya safari ndio shida ilikuwepo hapo, niliamua kuwa mkweli na kubaki na pesa za mambo ya kawaida tu na zikiisha basi, mambo yote ya pesa ni mke wangu tu alikuwa anayafanya na kunijulisha...hili niliamua mwenyewe baada ya kuona nimekuwa mlevi wa kupindukia.....
6. Nilmuomba sana Mungu anisaidie kuniondolea ile hamu ya pombe, kweli huwa siendi sana kanisani ila ninasali mwenyewe hasa usiku, imenisaidia sana na kunijenga...
7. Sasa ni kama mwaka umepita baada ya kuanza mpango huo wa hiyari na kwa kweli nimepunguza sana na kwa mwezi ninaweza kunywa bia si zaidi ya sita tu, na nikizikosa hainisumbui kabisa.....na sasa naweza kuwa na pesa na wala nisinunue bia kabisa....Namshukuru Mungu sana na mke wangu.
 
Image result for how to quit alcohol
Can I cut back on my drinking or do I need to stop drinking completely?
Set a drinking goal.
Choose a limit for how much you will drink. ...
Keep a "diary" of your drinking.
To help you reach your goal, keep a "diary" of your drinking. ...
Watch it at home. ...
Drink slowly. ...
Take a break from alcohol.

msisahau na kuacha kubet h ktu never forget
 
Nilipoteza kama dollar 1000 kwenye wallet nikiwa nimelewa kesho yake nikajilaumu sana kwa uzembe wa hovyo nikasema huu ni ujinga pombe sasa basi ni zaidi ya week tatu sasa na bado naendelea kuhesabu pombe inaweza kupelekea ukafanya vitu vya hovyo ukafifisha hata ndoto zako
 
Jamani naomba msaada nina ndugu yangu ni mlevi sana mpaka anasahau kwenda kazini.

Naomba kwa anayejua dawa ya kuacha pombe anisaidie.

ni PM nikuelekeze if ua serious na utakuja kushuhudia hapa kaacha pombe
 
Back
Top Bottom