Njia za kupunguza gharama za ujenzi wa nyumba

Njia za kupunguza gharama za ujenzi wa nyumba

Naunga hoja mkono nimejifunza mawili matatu. Hasa pale unaposema uanze na mashimo ya choo. Ni kweli shimo udogo kwa maeneo ambayo maji mi tatizo unaweza pia ikatumika kuhifadhia maji kwa ajili ya ujenzi.

Yes lile dogo utahifadhia maji lakin baadhi ya maeneo utapata water table hasa kwa lile kubwa, so utakuwa umeokoa gharama kubwa za maji
 
Makamee i guess some thing is not right to you upstairs.

Kama hujui sio lazima uchangie.

We ndo wale umerithi kila kitu hata bei ya kiwanja, tofari, cement hujui, na huna kitu tangible cha kujivunia kama mpambananaji.

Niliamua kuchimba shimo la choo kubwa ili kwanza niachane na karaha ya kila mwezi au miwili unaleta gari la kufyonza uchafu maana shimo limejaa, pili ili nipate mawe na kifusi cha kutosha.
Na kulijenga hilo shimo ililazim tuweke concrete beam toka chini then juu tuka suka beam zungine mbili kwa umbo la alama ya kujumilisha, mwisho ndo tukamwaga zege la kufunika eneo lote.

Unqposema choo cha kata ndo umedhirisha kwa 100% ya ku copy na ku paste vitu, mpaka leo huwa sielewi kwanini watu tuna standise ukubwa wa mashimo ya vyoo? Why? Na ndo maana kila kukicha vinajaa na inakuwa kero.

Mimi kwa ujenzi wangu mambi mengi niliamua kurekebisha makosa ya wengi.

Shimo la choo cha nyumba la mita 12 kwa mita 15? Aisee acha fix hilo ni shimo kubwa sana.
 
Vipimo ni futi sio mita, nimerekebisha
 
Kwa wale wenye ardhi ya kichanga basi mchanga utakao tolewa shimoni ndo utaanza nao kwenye ujenzi na wengine unakuta anapata bahati ya maji pia so unauwa ndege wawili kwa jiwe moja

Kwa akili mlazo kama zako unajua jiografia ya maeneo yote unaweza kuchimba na kupata matirial ya kujengea,
Kama hujui maeneo kama Arusha udongo wake haufai kwa chochote hata uchimbe mita 200 kwenda chini,na baadhi ya maeneo inakulazimu uhamishe udongo na ulete udongo mpya ili uweze kujenga.
 
Makame jifunze kuwa positive na ku appreciate, unapoona mtu kakosea ni vizuri kukosoa ili mambo yaende lakin sio kejeri ambazo hazina tija

Hata kukalili ni sehemu ya kujifunza unless hutambui maana halisi ya jf.

Jiulize wewe binafsi toka umejiunga jf ume add value ipi?
 
Kwa akili mlazo kama zako unajua jiografia ya maeneo yote unaweza kuchimba na kupata matirial ya kujengea,
Kama hujui maeneo kama Arusha udongo wake haufai kwa chochote hata uchimbe mita 200 kwenda chini,na baadhi ya maeneo inakulazimu uhamishe udongo na ulete udongo mpya ili uweze kujenga.

Hilo nimelielezea hapo juu
 
Makame jifunze kuwa positive na ku appreciate, unapoona mtu kakosea ni vizuri kukosoa ili mambo yaende lakin sio kejeri ambazo hazina tija

Hata kukalili ni sehemu ya kujifunza unless hutambui maana halisi ya jf.

Jiulize wewe binafsi toka umejiunga jf ume add value ipi?

Kosa moja goli 3
 
•Naungana na Makamee kwenye usimamizi ni muhimu kumuweka msimamizi mwenye ufahamu kuhusu ujenzi(Foreman) mkumbuke hawa mafundi wanalipwa kulingana na tofali anazojenga so huwa wanaenda fasta ili mradi ajenge tofali nyingi kwahiyo utaratibu wa ujenzi kama kutumia kamba au pima maji kwa ajili ya kunyoosha ukuta uwa hatumii au anatumia kiubabaishaji kama mtu sio mtaalamu wa hayo mambo hauwezi kuona kwahiyo ni vizuri kumuweka msimamizi ambaye unaweza kumlipa hata sh 20000 kwa siku mbali ya kumuweka wife/ndugu kwa ajili ya kusimamia materials yasiibiwe na mafundi.
•Gharama za kuchimba kisima ni kubwa sana zaidi ya 3m na ujenzi pia wa nyumba kuanzia chini hadi juu haizidi week mbili kwa nyumba hizi zetu za kawaida na kwa siku ukitumia maji ya elfu 20 kwa wiki 2 ni maji ya 280,000/= hizo 2.72m utafanyia mambo mengine
•Kupunguza gharama za ujenzi basi jitahidi kununua materials kwa agent wakubwa kama bulk na huwa wanaleta hadi site,kama kununua cement mifuko 200 na nondo tani kazaa kwa pamoja,tofali nunua moja kwa moja site hapa utasave mda kuna site nyingine wana gari la kukubebea free nunua karibu na unapojenga sio site hipo kivule tofali unanunua mbagala.
 
Nakupongeza kwa ubunifu Akhoi. Tumekuwa tunachimba mashimo ya maji taka bila kujiuliza kwanini vipimo viwe hivyo.

Nina maswali mawili. Kwanini usipende kabati jikoni badala ya kabati kwenye stoo. Au vitu huweki kabatini kabisa?
Ila mkeo ni mpole sana. Hajadai makabati jikoni?

Swali la pili linahusu hizo sockets mbilimbili za tanesco na za sola. Si ungepunguza gharama kwa kuweka changeover switch? Nawakilisha.
 
Nimekuelewa nita copy na kumodifying idea yako ili nitoe kitu cha maana big up

Mara ntaomba urejeshe modifications utakazikuwa umefanya ili nasisi tujifunze
 
Augustine.
Kabati jikoni zinapunguza space.

Ukiweka change over inamaana unatumia system moja ya wiring lakin mimi nimetumia wiring ya tanesco na solar kila moja inajitegemea na ndi maana hata socket ziko tofauti kwa sababu kila system moja ina wire zake zinazojitegemea
 
Sawa King Kong ila matumizi ya maji ni endelevu si ukichimba utaendelea na kumaliza ujenzi lakin matumizi ya maji hayakomi mf kwangu mimepanda miti mingi sana kiasi watu wanapaita pale penye miti mingi hahaha na niliweza kuikuza kwasababu ya maji na hata kumwagilia kuta na zege ili ikomae inakuwa rahisi tofauti na maji ya kununua maana ijulikane kuwa cement haiitaji joto wala jua kali, inahitaji ubaridi ili ikomae na kukauka vizuri, ikipata joto inaungua na ndo maana kuta zinabanduka au kupata nyufa
 
Nakubaliana na mleta mada kwa baadhi ya maeneo, lakini kwa maeneo mengine makubaliana na Makamee pamoja na King Kong. Suala la fundi pamoja na msimamizi ni la kuzingatiwa sana, inatakiwa wawe ni watu wenye uelewa mpana katika hii fani ya ujenzi, hasa msimamizi. Binafsi nimekwisha kumbana na mafundi wengi tena kwa kuelekezwa na mtu kwamba anaye fundi mzuri kumbe hamna kitu, ni fundi wa kupanga tofali na kupiga plaster. Mafundi wengi hawajui masuala ya "ratio" wengi hawajui vipimo vya zege, fundi anakwambia ununue nondo za 12mm kwa ajili ya kusuka colum au beam, na anatumia nondo 3 bila kuweka rings za kushikilia hizo nondo. Ushauri wangu, kama hauna uelewa na mambo ya ujenzi mtafute mtaalamu wa ujenzi akupe ushauri, siyo lazima asimamie unaweza kumtumi kukupa ushauri tu. Kumbuka unaweza kukwepa gharama lakini baada ya muda mfupi ukaingia gharama kubwa kuliko za mwanzo, kv msingi na kuta kupata nyufa au rangi ukutani kupata fangasi.
 
Last edited by a moderator:
Mwenye kuelewa, ameelewa..
Mungu akubariki, mleta mada..!
 
Ni sawa kabisa Kyenju ila hapa nilimaanisha wale watu ambao wana a, b, c za ujenzi ila hawana muda wa kusimamia na ndo maana nikashauri uweke mtu wa karibu ili akae pale toka asubuhi then wewe muhusika unaenda jion kureview mf mimi ilitokea unarudi jion unakuta kuta au beam imepinda na ililazim baadhi ya kuta kuzivunja na tukaanza upya. Au unakuta kona haina square ila kwa ambae hana muda kabisa basi ni vizuri aweke na apate msimamizi mwenye uelewa.
Kimsing hapa changamoto ni mbili.

Kuibiwa vifaa na ubora wa ujenzi
 
Sawa King Kong ila matumizi ya maji ni endelevu si ukichimba utaendelea na kumaliza ujenzi lakin matumizi ya maji hayakomi mf kwangu mimepanda miti mingi sana kiasi watu wanapaita pale penye miti mingi hahaha na niliweza kuikuza kwasababu ya maji na hata kumwagilia kuta na zege ili ikomae inakuwa rahisi tofauti na maji ya kununua maana ijulikane kuwa cement haiitaji joto wala jua kali, inahitaji ubaridi ili ikomae na kukauka vizuri, ikipata joto inaungua na ndo maana kuta zinabanduka au kupata nyufa

Lengo ni kupunguza gharama za ujenzi ndio maana swala la kuchimba kisima kwa mwanzo litaongeza cost unaweza kuchimba baada ya kumaliza,Swala la miti ni safi maana linaleta kivuli,wewe umejenga maeneo yapi huko tuje tuone mfano?
 
Nakubaliana na mleta mada kwa baadhi ya maeneo, lakini kwa maeneo mengine makubaliana na Makamee pamoja na King Kong. Suala la fundi pamoja na msimamizi ni la kuzingatiwa sana, inatakiwa wawe ni watu wenye uelewa mpana katika hii fani ya ujenzi, hasa msimamizi. Binafsi nimekwisha kumbana na mafundi wengi tena kwa kuelekezwa na mtu kwamba anaye fundi mzuri kumbe hamna kitu, ni fundi wa kupanga tofali na kupiga plaster. Mafundi wengi hawajui masuala ya "ratio" wengi hawajui vipimo vya zege, fundi anakwambia ununue nondo za 12mm kwa ajili ya kusuka colum au beam, na anatumia nondo 3 bila kuweka rings za kushikilia hizo nondo. Ushauri wangu, kama hauna uelewa na mambo ya ujenzi mtafute mtaalamu wa ujenzi akupe ushauri, siyo lazima asimamie unaweza kumtumi kukupa ushauri tu. Kumbuka unaweza kukwepa gharama lakini baada ya muda mfupi ukaingia gharama kubwa kuliko za mwanzo, kv msingi na kuta kupata nyufa au rangi ukutani kupata fangasi.

Well said msimamizi mtaalamu ni mtu muhimu sana maana yeye kazi yake ni kumkosoa fundi na kumrekebisha ukimuacha fundi peke yake lazima ule hasara yeye fundi anakimbiza kazi tu jioni ahesabu matofali mangapi kajenga aingize chake.
 
Last edited by a moderator:
Huu ni uchambuzi wa ujenzi wa kilocal sana,nyumba kama nyumba ujenzi wake husimamiwa na injinia mwanzo mwisho,hiyo ujenzi kusimamia mke wako labda unajenga kibanda cha mama lishe.

We umewahi kujenga?
 
We umewahi kujenga?

Nikikwambia swali lako lina utata utabisha?
Kama unamaanisha kujenga ya ufundi mimi sio fundi,
Kama una maanisha kujenga ya kumiliki jengo jibu lake ndio.
 
Back
Top Bottom