Njia za kupunguza gharama za ujenzi wa nyumba


Tuko pamoja mkuu, ule uzi wa solar siku hizi sioni update.
 

Naomba ufanunuzi kuhusu hizo unazoita nyumba za kawaida.
Zinajengwaje kwa makaratasi au?
 
Naomba ufanunuzi kuhusu hizo unazoita nyumba za kawaida.
Zinajengwaje kwa makaratasi au?

Nyumba za kawaida ni zile,
1.pesa ya ujenzi umekopa milion 7 taasisi za fedha unajenga nyumba inaisha unahamia na chenji ya kununulia bodaboda inabakia.
2.ujenzi hauangalii quality muhimu fundi kanjanja aifikishe nyumba palipokusudiwa maana mkopo ukiisha hakuna ujenzi tena.
 
Huu ni uchambuzi wa ujenzi wa kilocal sana,nyumba kama nyumba ujenzi wake husimamiwa na injinia mwanzo mwisho,hiyo ujenzi kusimamia mke wako labda unajenga kibanda cha mama lishe.

Si lazina awe engineer anaweza kuwa architect or Quantity Surveyor pia tena engineer awe structural engineer mana ma engineer wapo wengi hata IT na electrical wote engineer but hawana sifa za kusimamia
 
Si lazina awe engineer anaweza kuwa architect or Quantity Surveyor pia tena engineer awe structural engineer mana ma engineer wapo wengi hata IT na electrical wote engineer but hawana sifa za kusimamia

Ndo umeandika nini? Sisi tunazungumzia mimba wewe unatuletea vitambi.
 
Ndo umeandika nini? Sisi tunazungumzia mimba wewe unatuletea vitambi.

thanx kwa jibu lako mana nilikuwa sijui kama nia nikueleweshana mambo ya ujenzi ila kumbe ni taharabu, wewe ni mtoto wa kike?
 
Huu ni uchambuzi wa ujenzi wa kilocal sana,nyumba kama nyumba ujenzi wake husimamiwa na injinia mwanzo mwisho,hiyo ujenzi kusimamia mke wako labda unajenga kibanda cha mama lishe.

Hata kama unaye injinia kwa uzoefu wangu inabidi na wewe mwenyewe uwe makini. Nimeshajenga sana na nimeliwa pesa sana mpaka nilipoamua kuwa na ufuatiliaji wa karibu sana nikagundua mchezo mchafu unaofanywa na injinia na fundi. Fundi na injinia wanakupa bei ya cement, nondo, mbao, kokoto, mchanga n.k, ukizunguka mwenyewe unagundua ya kuwa kila mahali kuna 10%. Mwezi uliopita tu nilipewa mahesabu ya kokoto na fundi kwa kushirikiana na injinia, nikawaambia nitakuwepo mwenyewe kokoto ziitakaposhushwa. Nikagundua ya kuwa kokoto nilizolipia hazikuwa zilizoletwa, na pili nilipewa hesabu ya lori moja zaidi... Uzuri nilikuwa sijawapa pesa yao, na nikasimamia kuletewa kokoto sahihi na nikahesabu malori yaliyoshushwa. Sina haja ya kuwaeleza ukweli ulioniuma sana na niliokoa pesa sana. Nchi yetu ya 10% imani imekwisha!
 
Hapo ndo tunapokosea watanzania,
Kwako wewe nyumba ya kawaida ni ipi?
Unapompeleka site mke wako asie na ujuzi wa chochote kuhusu ujenzi ina maana gani?
Huyo haendi kusimamia ujenzi bali anaenda kumlinda fundi asiibe matirial yako ya kubangaiza.

----- mboyoyo
 
This is not not for everyone!
 
Umejieleza vizuri Na mi nakuongezea sample hizi ili uwe fundi ujenzi mwenye vielelezo Vya nyumba ulizotaja
 

Attachments

  • 1410756741017.jpg
    110.5 KB · Views: 467
Hongera sana Akohi kwa kutupa tips za kupunguza gharama za ujenzi...
 

Mwe! we si mtanzania wa kawaida niliyefikiri mnamuongelea hapa. Milango minne ya kwendea tu nje? hata mi napenda nyumba nzuri na unique lakini uwezo duni. Milango minne ni kati ya 1,600,000 - 2,000,000 kwa mbao nzuri standard hapa dar. Kwa hiyo nikiweka milango miwili nasevu nusu ya hiyo hela nafanyia kitu kingine. Kuwa na stoo jikoni pia kunamaanisha eneo kubwa zaidi na mlango tena na kadirisha. Mi sina hela na kiwanja changu kidogo. Hizo sockets nyingi tena nyingine za solar zingine za taanesko nazo hata mie ningependa sana kuwa nazo lakini hela sasa! Au nyie mnapata wapi hela? Mie mwalimu chaki haziuziki, natamani nifuge kuku lakini mwenye nyumba kakataa......basi nadunduliza na kukopa sakos. Hii nyumba itaisha leo kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…