Njoo tuelekezane jinsi ya kupiga hela Burundi

Njoo tuelekezane jinsi ya kupiga hela Burundi

CRDB Bank wana tawi Burundi. Jaribu kupata taarifa kama unaweza kuhamisha faranga kwenda Tsh na vice versa.

Kuhusu ujambazi inategemeana na mitaa unayopiga mishe na kuishi
Hii haiwezekani mkuu huwezi kuhamisha pesa kutoka faranga kwenda shilingi, kinachotumika hapa ni dola kwa dola

Yaani kama una faranga unaibadiri kule kule iwe dola ndio unaidepost kisha unakuja kuwithdraw huku
 
Sasa mkuu watu wanafanya biashara mashariki mwa Congo, ambako hata bank ni shida, sembuse Burundi, ambako bank zipo?
Hapo cha kufanya ni hizo pesa za Burundi unakwenda sehemu za kubadirishia(bank) kwani burundi kwenye kubadirisha pesa ni wakali sana, wana taka uende sehemu rasmi, tatizo lao sasa ni rate za chini sana!!!

Utapata dola,
Burundi kuna CRDB anakwama wapi??
 
Tanzania ilivyo kubwa na fursa kibao ya nini kwenda burundi kufanya umachinga.kama unaenda Burundi fine ila uende kama muwekezaji na mtajii wa maana sio chinga,k wanza usalama mdogo na ni masikini kuliko sisi,
Akili ndogo sana hii na sio akili ya biashara, nenda TPA ukaulize miongoni mwa nchi zinazotuchangia kwenye bandari yetu ya Dar Burundi ni miongoni, au kaa barabarani uone kwa siku yanakatiza malori mangapi ya Burundi

Lkn sisi Tanzania na China tunalingana kama mtu kutoka China anakuja kufanya umachinga Tanzania why sisi tusiende Burundi? Tajiri anamtegemea sana masikini kwenye biashara lkn pia kosa sio lako fanya siku moja ukatembee tu Bujumbura kisha urudi kusema Burundi ni masikini
 
Akili ndogo sana hii na sio akili ya biashara, nenda TPA ukaulize miongoni mwa nchi zinazotuchangia kwenye bandari yetu ya Dar Burundi ni miongoni, au kaa barabarani uone kwa siku yanakatiza malori mangapi ya Burundi

Lkn sisi Tanzania na China tunalingana kama mtu kutoka China anakuja kufanya umachinga Tanzania why sisi tusiende Burundi? Tajiri anamtegemea sana masikini kwenye biashara lkn pia kosa sio lako fanya siku moja ukatembee tu Bujumbura kisha urudi kusema Burundi ni masikini
Kuna sehemu nakuelewa ila kubali tu burundi ni masikini east africa nzima
 
Ushahidi upo mkuu. Ukitaka nenda Kananga ngara kaa pale utajionea
Chifu, nimefanya kazi boda ya Tz na Burundi miaka sita,Nchi ya Burundi nimetembea mikoa takribani nane, hivyo naielewa vilivyo, Ndio maana nakuuliza km Una ushahidi.
 
Kuna sehemu nakuelewa ila kubali tu burundi ni masikini east africa nzima
Nadhani ni duniani, lakini siyo sababu. Ukiwa unafanya kazi/biashara na masikini ni rahisi zaidi kufanikiwa kuliko kufanya na matajiri au watu wanaojielewa, mana wanaojielewa wataichunguza sana bidhaa yako na kuitoa kasoro wakati masikini hawajui hata imetengenezwaje. Refer Bakhresa na Mo.
 
Chifu, nimefanya kazi boda ya Tz na Burundi miaka sita,Nchi ya Burundi nimetembea mikoa takribani nane, hivyo naielewa vilivyo, Ndio maana nakuuliza km Una ushahidi.
Ahaa. Basi kama ni mwenyeji nafahamu pia utakuwa na uelewa mpana juu ya warundi kuliko Mimi. Ila jamaa ni watata sana.
Anyway nipe ramani chifu.
 
CRDB ipo bado lkn pia KCB ipo vile vile changamoto benki ya taifa (BRB) imezuia miamara ya kimataifa kwa sarafu ya BIF (faranga)

Hivyo ili ufanye miamara kimataifa ukiwa Burundi unatakiwa uwe na akaunti ya dola CRDB wanayo na KCB pia wanayo, ukiwa Burundi unaweza kudepost na kuwithdraw kwa dola kupitia akaunti yako hiyo hiyo hiyo
Hapo kwenye exchange rates zao sasa, ndio balaa!!na ole wako ukamatwe una badirishia vichochoroni kwenye rates nzuri!!
 
Hii haiwezekani mkuu huwezi kuhamisha pesa kutoka faranga kwenda shilingi, kinachotumika hapa ni dola kwa dola

Yaani kama una faranga unaibadiri kule kule iwe dola ndio unaidepost kisha unakuja kuwithdraw huku
Haya ni maelezo ya CRDB au ni ufahamu wako?
 
Burundi kwa sasa matumizi ya dola sio kama zamani, kwa sasa hadi uagizaji wa mafuta umekuwa wa kusua sua mimi nina jamaa zangu wengi tuu wanahusika na malori na mara kwa mara wananipa update ya huko ikoje kwa sasa,

jana tuu nilikuwa naongea na dereva mmoja ambaye nlitaka aniletee sabuni za nyota nne nikamuuliza kama hali ya kukosekana kwa mafuta bado kupo na akanieleza bado yanasumbua,

na sababu kubwa ni waagizaji wa mafuta hawaruhusiwi kuuza kwa dola wanatakiwa watumie faranga kitu ambacho wao kwenye soko la dunia kuniwapa wakati mgumu kwenye manunuzi.

Na kuhusu benki CRDB najua bado ipo nakumbuka panaitwa buyenzi ndio tawi lipo hapo na usalama upo si kama baadhi ya watu wanavyosema hapa maana ingekuwa si hivyo madereva wetu wangesema tuu hali ikoje.

Mkuu fanya kutembelea eneo husika usiogope sana kujifunza mimi mwenyewe natarajia kwenda huko ndani ya miezi mitatu ijayo nataka nifanye biashara ya mazao na hizo sabuni.

Ila pamoja na umasikini wa Burundi bado mafuta kwao ni bei rahisi kuliko kwetu na mafuta yao kwa asilimia kubwa yanapitia kwetu.

Miji iliyochangamka ni Gitega,Ngozi, Muyinga na Bujumbura yenyewe na kwa hakika ukifnikiwa kupata bidhaa zako zikaenda sawa sawa mafanikio utayaona tuu.

Japo na watu wa kule wengi ni wabishi na majasiri sababu ya vita vita na baadhi walishaingia msituni lakini si kitu cha kukutisha sana cha msingi ishi na watu vizuri upate kufanya biashara zako kwa amani kabisa...

twende zetu buja mkuu tuache uoga watanzania.
 
Burundi kwa sasa matumizi ya dola sio kama zamani, kwa sasa hadi uagizaji wa mafuta umekuwa wa kusua sua mimi nina jamaa zangu wengi tuu wanahusika na malori na mara kwa mara wananipa update ya huko ikoje kwa sasa,

jana tuu nilikuwa naongea na dereva mmoja ambaye nlitaka aniletee sabuni za nyota nne nikamuuliza kama hali ya kukosekana kwa mafuta bado kupo na akanieleza bado yanasumbua,

na sababu kubwa ni waagizaji wa mafuta hawaruhusiwi kuuza kwa dola wanatakiwa watumie faranga kitu ambacho wao kwenye soko la dunia kuniwapa wakati mgumu kwenye manunuzi.

Na kuhusu benki CRDB najua bado ipo nakumbuka panaitwa buyenzi ndio tawi lipo hapo na usalama upo si kama baadhi ya watu wanavyosema hapa maana ingekuwa si hivyo madereva wetu wangesema tuu hali ikoje.

Mkuu fanya kutembelea eneo husika usiogope sana kujifunza mimi mwenyewe natarajia kwenda huko ndani ya miezi mitatu ijayo nataka nifanye biashara ya mazao na hizo sabuni.

Ila pamoja na umasikini wa Burundi bado mafuta kwao ni bei rahisi kuliko kwetu na mafuta yao kwa asilimia kubwa yanapitia kwetu.

Miji iliyochangamka ni Gitega,Ngozi, Muyinga na Bujumbura yenyewe na kwa hakika ukifnikiwa kupata bidhaa zako zikaenda sawa sawa mafanikio utayaona tuu.

Japo na watu wa kule wengi ni wabishi na majasiri sababu ya vita vita na baadhi walishaingia msituni lakini si kitu cha kukutisha sana cha msingi ishi na watu vizuri upate kufanya biashara zako kwa amani kabisa...

twende zetu buja mkuu tuache uoga watanzania.
Mwanangu unaenda lini na mi niunge body?
 
Haya ni maelezo ya CRDB au ni ufahamu wako?
Ni maelezo ya CRDB wa kule kule Burundi, mkuu hii ni benki moja lkn ipo chini ya usimamizi tofauti

Huku kwetu Tz CRDB wapo chini ya BOT (kumbuka BOT wana utaratibu wao) na kule CRDB wapo chini ya BRB (hivyo hivyo BRB wana utaratibu wao)

Mfano huku Tz unaweza kutuma pesa Burundi kupitia mobile banking (M-pesa, Tigopesa nk) lkn mitandao ya kule EcoCash na LumiCash hairuhusiwi kutuma pesa nje wao wanafanya local transfer pekeee

Nimetoka Burundi tarehe 23 January nimefuatilia hii nikiwa huko haiwezekani! BIF inafanya transaction locally ukitaka kufanya transaction internationally ukiwa Burundi ni lazima uwe na dola

Western Uniun na Moneygram nao pia wanapokea dola pekeee BIF hawatumi
 
Tafuta sehemu nyingine yakwenda kufanya biashara lakini sio Burundi .....Mimi nipo Kigoma na Burundi tunaenda mara kwa mara lakini sio sehemu salama kabisa na warundi Wana maisha magumu sana asikwambie mtu
 
Back
Top Bottom