Nawaamkua nyote
Tarehe 17 Novemba 2024, Waziri Mkuu akiwa eneo la Kariakoo kukagua zoezi linaloeneelea la uokoaji wa waliokwama chini ya kifusi cha ghorofa iliyoanguka. Alitoa maagizo kwa jeshi la polisi kumkamata Mtanzania aitwaye Niffer ambaye kupitia mitabdaoni alitoa taarifa kuwa amechangisha pesa za za kuwahani wahanga wa ajali ya ghorofa. kuna mambo kadhaa ya kuangazia hapa
- Niffer ametoa taarifa ya kuchangisha na kuelezea kiwango alichokikusanya
- Waziri Mkuu ameipokea taarifa ya Niffer kama vile anapokea briefings za kiuchunguzi
- Waziri Mkuu anatoa agizo la kukamatwa na kuhojiwa Niffer ili aeleze nani kamruhusu kuchangisha tarehe 17 Novemba 2024
- Tarehe 18 Novemba 2024, waziri Mkuu anaelekeza polisi wamhoji mmiliki wa jengo lililoanguka. Agizo hilo limekuja baada ya wananchi kuhoji alipo mmiliki wa jengo na kama hajakamatwa tangu siku ya jengo kuanguka.
- Jengo limeanguka ahsubuhi saa tatu halafu Mkuu wa Mkoa na vikosi vya uokozi wanafika eneo la tukio saa nane mchana. Hilo jambo halijamkera Waziri Mkuu
Naomba kufahamu, sheria gani imevunjwa ama kukiukwa na Niffer kuchangisha fedha ambapo si mara ya kwanza kuchangisha na kuwasilisha kwa walengwa?
Naomba kufahamu. Ni michango gani ya wahanga iliyolusanywa kupitia serikali na ikawasilishwa kwa walengwa? Nakumbuka michango ya tetemeko la ardhi Kagera ilikusanywa na walengwa hawwkuambulia senti. Vivyo hivyo mafuriko Morogoro wahanga waliishia kusikia redioni michango ambayo haikuwafikia.
Waziri Mkuu atueleze. Matumizi ya fedha za dharurq na majanga chini ya ofisi yake zimetumikqje tangu aingie ofisini?
Kweli ITATUWEKA HURU
WaTz hata hamuelewi, nimesoma comment za baadhi ya watu humu mitandaoni yaani waTz hebu tuache upuuzi na tuelewe sheria[emoji34]
eti wengine mnahoji eti mbona harusi sjui msiba au sherehe tunachanga? iweje hili wakataze?
ngoja niongelee hili la kawaida nisiende serikali issues.
1- hivi kuna michango unayoletewa bila mpangilio au kibali? sizungumzii kibali cha serikali. Kama ni mchango wa harusi, kikao cha kamati hukaa na kuandaa utaratibu michango ikusanywe kwa namna gani. Atachaguliwa mtu , iwe mwenyekiti au katibu kwa ajili.ya kupokea na kuhakiki michango, after that wakae tena kama kikao kuletewa taarifa ya michango iliokusanywa, majina ya waliochangia, kilichopelea nk, then wanapanga maandalizi yote from the exactly total amount iliopatikana. Sjui.sasacwatachagua ukumbi, mziki, chakula, vinyaj nk, BUT KILA KITU KILIENDA KWA RECORD.
Haya huyo binti, alikua na account gani? ambayo inahakikiwa? na nani? nani atahakikisha imepatikana kiasi gani? kifanyiwe nini? au kiwasilishwe wapi? - just auditing
before litiliwe mashaka jambo lake hadi PM alipoongelea na yeye kujifanya sasa kwenda vodacom na tigo wamprintie transaction list sababu ameshaona janga, bila kubumburuka angetoa hio list? kwa nani? je angeonesha whole list na amount received na imetumikaje?
mf tu. Ana followers 1.7M, kila followet akachanga Tsh 100 tu, angekua na smount.kubwa sana. Je nani angehakiki hiko alichokikusanya kupitia janga ambalo limeumiza watu zaidi ya yeye kutumia kama fursa ya kujipatia kinyume na sheria kwa kiwaibia watu kwa kusema ni msaada?
hivi serikali ikisema iruhusu huu utaratibu wa kijinga wa watu kuchangisha kwenye majanga mskubwa ya kitaifa itakuaje? si itakua vurugu nchini? watu wana followers wangapi huko insta? si kila mtu angechangisha? tuache utoto na upumbavu