Noah inazingua sana (linamiss na kuwaka taa ya check engine) naombeni msaada

Noah inazingua sana (linamiss na kuwaka taa ya check engine) naombeni msaada

Point yako ya mwisho sikubaliani nayo. Nunua mashine ya kufanya diagnosis, halafu ikiwaka check engine, ichomeke na usome uone tatizo nini (haihitaji uwe fundi kufanya diagnosis). ukishajua, mpelekee fundi wa kitaa tu wa kawaida, halafu mwambie akutengezee jambo flani (kwa mujibu wa kodi uliopata). Atakutengenezea tu na itakuwa fresh...

Hoja yako naipinga,ni vizuri kupeleka gari kwa competent mechanics mwenye diagnos tools, though mwenye gari kua na OBD-2 yake mwenyewe ni kitu kizuri lkn nakuhakikisha wewe kama ni layman kwny hio field utaenda chaka sana tu na utanunua spare mpya kwa sana tu.

Kwa mfano OBD-2 reader yako ikisoma codes P0171 (Lean Exhaust Bank 1) na P0174 (Lean Exhaust Bank 2) utakimbilia kunua Oxygen Sensors wkt unaweza kukuta kuna vacuum leak na possibly haujabadilisha Fuelt filter kwa muda mrefu saana,unanunua zako fuel filter mpya mchezo umeisha wkt sababu ulisoma codes mwenyewe bila kua na utaalam husika ungenunua Oxygen Sensors.

Unaweza kusoma codes za P0401(insuficcient EGR) ukakimbilia fasta kununua EGR Valve mpya wkt inaweza kua ni EGR control solenoids au sababu ni exhaust hose imepasuka.

So ni vizuri kupeleka gari kwa wataalam husika.
 
Hoja yako naipinga,ni vizuri kupeleka gari kwa competent mechanics mwenye diagnos tools, though mwenye gari kua na OBD-2 yake mwenyewe ni kitu kizuri lkn nakuhakikisha wewe kama ni layman kwny hio field utaenda chaka sana tu na utanunua spare mpya kwa sana tu...
Sasa huoni kama unarudia yale yale ya mafundi wa kitaa basi?

Tizama alivopendekezewa mleta mada ikiwa gari ina miss an tuliopost hapa sote hatukutoka na diagnosis kwenda kuitizama hio gari ila ni from knowledge na uzoefu tu, kuna vitu A B C vichekiwe na hizo code ulizoleta ndio ivo ivo vitu kuna vitu A B C. Nikiona Gari inachemsha, natizama Radiator, hoses zake, water pump, fan, thermostat na head gasket, hii bila kuhitaji diagnosis kwa sababu najua mfumo wa upozaji gari. Kwa mfano, nikiona code inanambia engine overheating, najua nianzie wapi.

Kwaio hata mtu wa kawaida, akifanya diagnosis, ukifanya google search tu ya hizo codes unapata maelezo, unachukua maelezo unaenda kwa fundi na kumwambia, haya hebu ncheki kitu flani kinafanya kazi? kitu flani je, mpaka unapopata mzizi wa fitna.

kuna codes kwenye diagnosis, hizo huwa ni direct, hazina sijui ucheki hichi na hichi kabla ya hichi. O2 sensor codes mfano ikikujia, itakuwa kama ni sensor 1 bank 2, ushajua kama ni ya kwanza kwenye upande wa 2 exhaust manifold. Hii ni kuibadilisha tu moja kwa moja na sio kutizama chengine chochote labda iwe hamna umeme hapo.
 
Sasa huoni kama unarudia yale yale ya mafundi wa kitaa basi?

Tizama alivopendekezewa mleta mada ikiwa gari ina miss an tuliopost hapa sote hatukutoka na diagnosis kwenda kuitizama hio gari ila ni from knowledge na uzoefu tu, kuna vitu A B C vichekiwe na hizo code ulizoleta ndio ivo ivo vitu kuna vitu A B C...

'kuna codes kwenye diagnosis, hizo huwa ni direct, hazina sijui ucheki hichi na hichi kabla ya hichi. O2 sensor codes mfano ikikujia, itakuwa kama ni sensor 1 bank 2, ushajua kama ni ya kwanza kwenye upande wa 2 exhaust manifold. Hii ni kuibadilisha tu moja kwa moja na sio kutizama chengine chochote labda iwe hamna umeme hapo.'

Daah hapa napoteza muda wangu tu aisee,haya all the best.
 
Tatizo ni kwamba ukiwasha gari yako inaanza na cold start badala ya warm start coz engine asubuhi inakua ya baridi na inahitaji warm start ili ifanye kazi sawia. Kwa cold start ndo maana unapata tatizo la miss...

You have a point.
 
Nibadili pressure sensor. Ikatulia sana.
Screenshot_20200521-095738_Chrome.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
kali linux,
LEGE alivokuuliza hajakosea.

System ya kuingiza hewa kwenye gari ni MAF sensor, hii hupima kiasi cha hewa kinachoingia ndani ya engine ambayo inaipa taarifa ECU kiasi gani cha mafuta iweke kwenye engine. Hii haina uhusiano na temperature ya engine. Temperature ya engine inatizamwa na thermostat ambayo ina regulate temperature ya gari...

Inategemea mkuu. MAF zinatofautiana, kuna MAF zina pin 3 zingine zina pin 4 wakati zingine zina mpaka pin 5. Ukiikuta MAF ina pin 5 basi ndani ya hiyo MAF wamemount IAT sensor.
 
Fundi asiye na diagnosis tools hagusi gari yangu,period.

Labda yawe haya matatizo ya pancha,kubadili oil na mambo mengine kama hayo lkn nje ya hapo mambo ya Trial&errors sio kabisa.


Bado diagnosis tool itakuambia kuna shida kwenye mfumo fulani. Huo mfumo na wenyewe una vitu vingi. Hivyo bado mtu ataanza kuhangaika na kitu kimoja kimoja.

Ndio maana kuna diagnosis tool ya 100k na kuna zingine za 5M.
 
kali linux,
Unaona sasa boss toyota noah na turbocharg wapi na wapi ???.acha kutoa ushauri mwingi wa kupoteza unachokiongelea hakipo kabisa kwanza unaleta maelezo ya gari ya disel sijui baridi hiyo kitu haipo in short tatizo lake lipo hivi...

Thermostat ina uhusiano gani na EFI?
 
Tatizo la gari kumiss;

Check coil kama zinafanya kazi, njia moja ya kucheki coil yenye tatizo, washa gari yako, anza kuchomoa moja moja na utizame gari itabadilika mlio, ukiona umechomoa coil na kuona mlio wa gari haubadiliki ujue hapo ndio kwenye tatizo, sasa kumake sure kama ni coil ibadilishe weka kwenye cylinder nyengine halafu urudie process, ukiona kwenye coil hio hio mlio haubadiliki, basi tatizo ni hio coil, na kama mlio unabadilika basi pale ulipoitoa kuna tatizo la plug...
Sawa kabisa, nami wiki mbili zilizopita nilipata tatizo kama hilo,nikampelekea fundi wangu akabadilisha coil plug zote kwani mbili zilikuwa zimekufa yaani hazifanyi kazi na zimeingia maji baada ya kuosha engine
 
Sasa huoni kama unarudia yale yale ya mafundi wa kitaa basi?

Tizama alivopendekezewa mleta mada ikiwa gari ina miss an tuliopost hapa sote hatukutoka na diagnosis kwenda kuitizama hio gari ila ni from knowledge na uzoefu tu, kuna vitu A B C vichekiwe na hizo code ulizoleta ndio ivo ivo vitu kuna vitu A B C. Nikiona Gari inachemsha, natizama Radiator, hoses zake, water pump, fan, thermostat na head gasket, hii bila kuhitaji diagnosis kwa sababu najua mfumo wa upozaji gari. Kwa mfano, nikiona code inanambia engine overheating, najua nianzie wapi...

Hahah umetaja vitu vingi sana hapo kwenye engine overheating lakini naona hujagusa vitu kama ECT. nakuapia unaweza kubadili hivyo vyote ulivyoandika hapo na bado gari ikaendelea kuoverheat.
 
Thermostat ina uhusiano gani na EFI?
Mkuu hapo kwanza unazungumzia kitu kimoja na mfumo..

EFI ni electronic fuel injection..huu ni mfumo update wa cabureter..

Thermostat hii hufungwa kwenye njia ya maji kazi yake ni kama switch,automatic switch inafanya kazi kwa kutegemeana na joto la maji..maji yakiwa ya moto kufikia joto husika inafungua na kuruhusu maji kwenda kwenye rejeta kupoozwa..

Gari yenye mfumo wa EFI lazima iwe na thermostat lkn sio lazima gari yenye thermostart iwe na EFI sijui nimekujibu au laa kama bado uliza kwa namna utakavyo nitakujibu
 
Mkuu hapo kwanza unazungumzia kitu kimoja na mfumo..

EFI ni electronic fuel injection..huu ni mfumo update wa cabureter...

Bado hujanijibu swali langu. Au labda ngoja niulize hivi. Kuondoa thermostat kuaathiri vipi mfumo wa mafuta?
 
Hahah umetaja vitu vingi sana hapo kwenye engine overheating lakini naona hujagusa vitu kama ECT. nakuapia unaweza kubadili hivyo vyote ulivyoandika hapo na bado gari ikaendelea kuoverheat.
Unazungumzia kitu kinaitwa Electronic Control Transmission? Transmission unajua kama ni tofauti na engine?
 
Inategemea mkuu. MAF zinatofautiana, kuna MAF zina pin 3 zingine zina pin 4 wakati zingine zina mpaka pin 5. Ukiikuta MAF ina pin 5 basi ndani ya hiyo MAF wamemount IAT sensor.
Mass Air Flow Sensor, ndugu, hebu check hio jina ya hio sensor. Inahusiana na hewa tu inayokwenda kwenye combustion chambers. Hata kama ina pini 50, itapima hewa inayoingia kwenye engine ni kiasi gani, na temperature ya HEWA sio engine ni kiasi gani.

Chomoa MAF sensor kwenye gari, halafu niletee mrejesho kama unapata tatizo la overheating kwenye engine. Halafu chomoa Thermostat kwenye gari, Toka magomeni mpaka kariakoo unipe mrejesho, ndio utaelewa nazungumza nini.
 
'kuna codes kwenye diagnosis, hizo huwa ni direct, hazina sijui ucheki hichi na hichi kabla ya hichi. O2 sensor codes mfano ikikujia, itakuwa kama ni sensor 1 bank 2, ushajua kama ni ya kwanza kwenye upande wa 2 exhaust manifold. Hii ni kuibadilisha tu moja kwa moja na sio kutizama chengine chochote labda iwe hamna umeme hapo.'

Daah hapa napoteza muda wangu tu aisee,haya all the best.
Unapinga kuwa code ya O2 sensor sivyo nnavosema au?
 
Unazungumzia kitu kinaitwa Electronic Control Transmission? Transmission unajua kama ni tofauti na engine?

Ukitaja ECT kwenye gari unazungumzia Engine coolant temperature sensor. Na siyo hicho ulichotaja wewe.
 
Mass Air Flow Sensor, ndugu, hebu check hio jina ya hio sensor. Inahusiana na hewa tu inayokwenda kwenye combustion chambers. Hata kama ina pini 50, itapima hewa inayoingia kwenye engine ni kiasi gani, na temperature ya HEWA sio engine ni kiasi gani. Chomoa MAF sensor kwenye gari, halafu niletee mrejesho kama unapata tatizo la overheating kwenye engine. Halafu chomoa Thermostat kwenye gari, Toka magomeni mpaka kariakoo unipe mrejesho, ndio utaelewa nazungumza nini.

Halafu mbona kwenye maelezo yangu mimi hamna sehemu nimetaja thermostat wala mambo ya overhitting? Nimetaja intake arr temperature sensor ambayo badala ya kuiweka separate kwenye magari mengine huwa wanaamua kuiweka ndani ya MAF ambapo ndio wanaongeza hizo pin.

Halafu hiyo MAF yenye pin 50 mimi ndio naisikia kwako leo.

Halafu umesema ukiondoa thermostat gari ina overhit? Kwani thermostat inafanya kazi gani kwenye gari?
 
Tatizo watu wanazungumza vitu vikubwa ili waonekane wanajua mambo, nimefatilia kwa makini nini alitaka kusaidiwa mleta uzi nikaona kuna tofauti kubwa sana na anachojibiwa, kila mtu analipuka na lake ili mladi tu aonekane anajua tena kwa kutaja matatizo makubwa makubwa wakat mwenye gar miss zikitokea anaendelea na maisha yake sasa kama matatizo ni makubwa kiasi hicho si angepaki gar!!?

Mafundi mnazingua ndiyo maana huwa mnaharibu magar ya watu kwa kukimbilia kuwaza matatizo makubwa hata kama gar lina tatizo dogo, mm nimeshawahi kusumbuliwa na gar kwa sababu tu betri linacheza yaan halichaji vizur gari ikawa inamis na kusoma check injini lakin kwa kwa mafundi naambiwa tatizo kubwa nikakaa na gari langu mpaka nikaja kuligundua tatizo mwenyewe na maisha yanaendelea, Mleta uzi nakushauri usipende kuwaamini sana mafundi hasa wanaotengeneza kwa kutumia uzoefu hawa hujaribu jaribu kama waganga wa kienyeji watakuharibia gari mkuu.

Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom